Mkurugenzi wa Arsenal Stan Kroenke (pichani) amepiga hatua moja zaidi ambapo anaweza kujitolea kununua hisa zote za club hio.
Tajiri huyo wa Kimarekani amenunua hisa kumi zaidi kwa pauni £8,500 kila moja na kupandisha mchango wake katika hisa kufikia asili mia 28.9%.
Hiyo ina maana kwamba Bw. Kroenke ndiye mwenye hisa nyingi zaidi ya wengine, akimshinda tajiri kutoka Uzbekistan Alisher Usmanov, mwenye asili mia 24%. Bw. Kroenke anakaribia kiwango cha juu cha 29.99% ambapo itambidi atangaze nia ya kununua hisa zilizosalia.
Hata hivyo hisa zilizosalia zinashikiliwa na Wakurugenzi wanaozishikilia kwa mkono wa chuma. Bw.Kroenke anayemiliki club ya NBA huko Marekani Denver Nuggets amekua akinunua hisa za club ya Arsenal taratibu mwaka huu akidokoa kila fursa inayojitokeza kutoka kwa wanaotaka kuuza.
Pamoja na Bw.Kroenke, wengine wenye kifua katika kumiliki hisa kubwa ni Bw.Usmanov, Danny Fiszman na Lady Bracewell Smith. Hata hivyo haijaeleweka kama Bw.Kroenke ana nia ya kununua hisa zilizosalia kwa nia ya kuimiliki club nzima ya Arsenal au amenunua hisa hizo kwa ajili ya faida ya uwekezaji wa mda mrefu.