Najua weekend ndio imekwisha tena na tunajiandaa kuingia maofisini kesho malawira, Naomba nikumburudishe na Kibao Rangi ya Chungwa toka kwao wana Kilimanjaro Connections Band. Kaka Beny Wisa upoo? Mukulu Kiiza, Le Suveree Maghambo, Mukubwa Baty na Six bila kumsahau Suveree Ling;ande, mnanini bwana. pateni burudani unilelee mwanangu Juma na Dula. hehehehe
Tyson afiwa na mwanaye!!
May 31, 2009 Mtoto wa bingwa wa zamani wa masumbwi Mike Tyson amefariki hospitalini baada ya kuanguka na kuburuzwa na mkanda wa mashine ya kufanyia mazoezi(Treadmill) iliyomo kwenye chumba chake cha kufanyia mazoezi nyumbani kwao Phoenix huko Marekani tarehe 26 May 2009.
Awali mtoto Exodus alikutwa na kaka yake mwenye miaka 7 akiwa amebanwa shingo na mkanda kwenye mashine hiyo ndipo alipokimbizwa hospital lakini alifariki siku moja baadaye.
Feisal Ismail na Baby Madaha wazindua kwa shangwe!!
May 31, 2009. Wanamuziki Feisal Ismail na mwenzake Baby Madaha majuzi wamezindua albamu zai chini ya Kampuni ya Pilipili Entertainments.
Katika uzinduzi huo ambao ulifanya kwa aina yake na kuhudhuriwa na Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo George Mkuchika pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara mama Marry Nagu, pia Ritah Paulsen alikuwepo Mkurugenzi wa kampuni ya Bench Mark Production waandaaji wa Bongo Star Search ambao msanii Feisal aliibuliwa huko.
Baby Madaha akithibitisha ubora wake jukwaani wakati wa Uzinduzi wa Video yake, Picha na Full Shangwe.
Kutoka kulia ni Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo George Mkuchika, Mwanamuziki Feisal Ismail maadam Ritah Paulsen Mkurugenzi wa Benchimark Production kampuni, ambayo pia inaandaa Bongo Star Search na Waziri wa Viwanda na Biashara mama Marry Nagu wakiwa katika picha ya pamoja, Feisal aliibuliwa na Bongo Star Search mpaka hapo alipofikia katika mafanikio yake.
Illuminata aulamba u Miss Universal
May 31, 2009iluminata james usiku wa kuamkia leo ametangazwa kuwa mshindi wa miss universe tz 2009, baada ya kuwabwaga wenzake kadhaa kwenye mtanange ambao ulikuwa na burudani lukuki.
Mashindano hayo ambayo yalifanyika katika ukumbi mpya wa Mlimani City Hall na kuhudhuria na mamia ya wapenzi wa burudani hasa sanaa ya urembo. Wanamuziki kadhaa walitumbuiza ikiwepo pamoja na AY, Wahuu toka nchini Kenya ambaye alibamba vilivyo, Diamond Musica ambao walimwaga Sebene la kufa mtu pamoja na kikundi machachari cha Ngoma cha Albino na kuufanya usiku huo kuwa wa aina yake.
Mbali na Illuminata mshindi wa pili ni evelyn almasi na hidaya maeda ambaye ni mshindi wa tatu.
Tano bora ya mtanange huo, Picha zote na Muhidini Issa Michuzi, habari na Robert William Mwafrica aka Mwafirombe.
Caouany nyota mpya kwenye ulimwengu wa Ubunifu
May 31, 2009 Mkurugenzi na Mbunifu wa mavazi kutoka kampuni ya Carpuany and Design Mamaa Grace Sinamwita kulia akipozi katika picha na Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Ritah Paulsen wakati wa uzinduzi wa kampuni ya Pilipili Entertainment uliofanyika jana sambamba na uzinduzi wa Video mbili za wanamuziki Baby Madaha na Faisal Ismail kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski. Capuany alikuwa Class mate wangu High School, hongera sana dadaa.
Queen Suzy avishwa pete ya Uchumba!!
May 29, 2009Mnenguaji wa FM Academia Queen Suzy ambaye kwa sasa yuko Malaysia ziarani na Bendi ya The Kilimanjaro Connections amepata mchumba ambaye anatarajia kufunga naye ndoa baadaye mwaka huu. Suzy ambaye amevalishwa pete ya uchumba na Mchumba wake huyo raia wa Uingereza anayeishi na kufanya kazi nchini Malaysia.
Awali Queen Suzy alivalishwa pete hiyo kwenye sherehe ndogo iliyofanyika kwenye Jengo la KLCC na kuhudhuriwa na baadhi ya Wanamuziki na marafiki wa karibu wa pande zote.
Suzy anatarajia kurejea nyumbani baadaye mwezi ujao baada ya mkataba wao kumalizia na amesema mchumba wake pia anatarajia kwenda Tanzania mwezi July ambapo taratibu nyingine zitafuatwa.
Suzy ambaye yuko Malaysia tangu mwezi wa december mwaka jana akiambatana na wana mkorogo, pia amepiga mafanikio kwenye sekta nzima ya muziki kwani kwa sasa pamoja na kucheza pia ameanza kuimba chini ya gwiji muimbaji mkufunzi Delphinus Mununga (mdogo wa marehemu Kasheba), “kwakweli nafurahi mafanikio yangu kimuziki ningependelea kuimba zaidi kwani sasa nakiona kipaji changu cha muziki” alisema Suzy alipokuwa akiongea nami katika kiota chao cha Rum Jungle.
Queen Suzy akiwa na mpenzi wake kisiwani Lang’kawi-Malaysia.
Akamatwa na Polisi kwa kushinda Bahati nasibu ya Man U na Barcelona.
May 28, 2009 Mtu mmoja mwenye asili ya kimalay amekamatwa na polisi leo asubuhi baada ya kushinda bahati nasibu ya mpira kwa kutabiri matokeo kati ya Manchester United na Barcelona ambapo Barcelona waliibuka kidedea.
Mtu huyo ambaye jina lake halijatajwa amekamatwa leo asubuhi majira ya saa tatu kutokana na Kucheza bahati nasibu ambayo hairuhusiwi kwa Wamalay sheria ambayo imo kwenye dini ya Kiislamu ambayo Serikali ya Malaysia inaifata.
Kwa mujibu wa mashuhuda jamaa huyo alishinda gari aina ya Myvi yenye thamani ya Malysia Ringit 47,000 sawa na dola 13000 za kimarekani. Inasemekana mtu huyo alipinga na mwenzake katika klabu moja maarufu kwa kuangalia mpira maeneo ya kati ya jiji la Kuala Lumpur.
Kwa mujibu wa sheria ya Malaysia, jamii ya Wamalay waislamu (Bumi Putra) hawaruhusiwi kucheza aina yeyote ya michezo ya kubahatisha. Malaysia inajamii ya aina tatu, Wamalay walio wengi, Wachina na Wahindi.
wengine walia wengine wacheka! Barcelona bwana we acha tuu.
May 28, 2009 Kwa kweli mpira umekwisha na mashabiki wangu kama kawaida hawakosi cha kuongea. Nawafurahia sana mashabiki wa Man U kila mara, wakishindwa wanasema, wakishinda wanasemaa. Hii ni baada ya kupoteza mchezo wa leo ambao wamechapwa 2-0, mabao ambayo yamefungwa na Etoo na Messi dakika ya 10 na ya 70 ya mchezo na kuzimisha mbwembwe za Mabingwa hao wa kandanda.
nilikuwa nacheka tuu kila ninaposoma status kwenye facebook toka kwa marafiki zangu kila pembe ya dunia kila mtu alikuwa na lake, kuna waliopongezwa na kupongezeka, si vibaya ukazisoma hisia zao hehehehee
Sirleem Kikeke The best team won. The longest 3 hour flight…..
Hamis Mwinjuma damn futbol..siku nikiangalia tu lazima man ifungwe,pu****u!
Adil Abdallah Alnahhdy MAN U FANS POLENI!AS PEOPLE ALWAYS SAY THAT THERE IS ALWAYS A NEXT TIME
Athuman Idd Machuppa Gaucho NILIPOZUNGUMZIA HUWEZI KUMFUNDISHA SAMAKI KUOGELEA WENGI HAWAKUJUA NINI NAMAANISHA LAKINI KILE KILICHOTOKEA ROME NDIO MAANA YANGU!!!!! THANKS BARCA WE ARE HAPPY NOW!!!man utd mechi mmeicheza sana mdomoni barca wametuonyesha kandanda swafi kabisa hakuna ubishi haya ronaldo wenu leo ndio alikuwa anamkaba PUYOL!!!!!!
Mashabiki wa Man U tawi la Tanzania ambao uzinduzi wao uliingia dosari.
Mazaza Mtawali Man U lost, I know it is a bitter pill to swallow! Clearly Barca were the better team tonite in Rome. I am moving on but I cant help to mention that Man U has played 24 games in the Champions League without defeat, until of course tonite in Rome. It is a new UCL record. Congratulations to Barca and see u next year as the gaffer promised, WE WILL BE BACK EVEN STRONGER!!
Andrew Maf Laughing at d proud arrogant ManU players….. we saw d real world best in action tonyt – Lionel Messi Houston sorry, congrats Chima.
Mashabiki wa Barcelona wakisherehekea baada ya ushindi
Benson Mokiwa sorry y’all ManU fans!Lakini y’all knew that itatokea hivyo?au mnataka mniambie mlifikiri Ronaldo atamshinda Messi??ooh never ever
Okta Nurika Man United’s loss was caused by arrogance before the match. The player said "Barca is stronger but we’re better". Man United’s youngsters now must learn from their mentors of being humble before the match. Please look at how Schmeichel respected Munich in ’99 final and look at how gentle Solskjaer and Beckham were!
Amal Mohd Viva la Barcelona…. yipee they freakin did it!! Ronaldo sulk urself to death!!! hahha
Edgar Benson Easy mathematics…Simply 90 mnts…!!!…. one has to be a winner..! yaahaaa today Yahoooo n Tomorrow Google…! or Microsoft against Macintosh..! they ar both big head…hahahah.!!! … hey Manu fans… take it easy..!! lah..!
Fatma Senkoro "oooh barca wadogo zetu,….au mlifikiri TAIFA CUP?
Luke Jackson and Thiery ”Chogo” Henry is officially tundika-ring them Darugaz..
David Ngilangwa Kama hukubali kushindwa kwanini unashindana sasa?
Mahmoud Mohamedali Rehmtulla END OF SEASON RESULTS: BARCELONA ARE TREBLE CHAMPIONS MANUTD ARE TREBLE CHAMPIONS ASS-ANAL ARE ZERO CHAMPIONS LIVERFOOLS ARE ZERO CHAMPIONS CHELSEA WANGOJA 30TH KIKOMBE CHA UJI Dohhh kwani timu mbili zachukua kila kitu?
Mashabiki wa Barcelona wakifanya fujo katika kusherehekea ushindi huko Barcelona.
Farzana Seif Al-rumhy Congrats to BERCELONA n pole sana to MAN U FANS!!!NEXT TIME BETTER CHOOSE THE RIGHT TEAM TO SUPPORT!!!!TENA NEXT TIME MAKE BETTER FORMATION YA LEO SUCKED!
Dimple Zambetakis Wahenga walisema.."Mapua Funuuu" ndo hayo Man U!!!
Shaima Majeed wewee .. I’m The First to Congratulate You All… Barca .. Barca Ya madallal ( Henery+ MissY = Winnning For Sure 😉
Pius Micky Man U, mkulima kala mbegu!! Nilidhani maneno ndio yanacheza maana mlisema sanaaaaa!! Poleni mwayego.
Kitanda kitalalika hiki?
May 27, 2009Kitanda hiki kinaweza kuwa kitamu au kichungu inategemea na matokeo ya masaa machache yajayo ambayo yatashuhudia miamba miwili ikimenyana kwenye mtanange wa Klabu bingwa. Hii inafuatia timu ya Manchester kushinda kiikombe cha ligi ya nyumbani na kutawazwa mabingwa hata kabla ligi kuisha halikadhalika na Barcelona nao.
Je nani kulia na nani kucheka masaa machache yajayo? Tega sikio najua wadau wangu Ben Twisa, Mukulu Edgar Kiiza na Mamaa ndani ya Kabul, Mh. Balozi, Kanku Kelly na wengineo kiroho kinawadunda sana wakati huu.
Muhula wa Pili wa WaPi Zanzibar umewadia….
May 27, 2009WaPi ni tamasha la sanaa linalofanyika kila mwezi. Tukio hili linakusudia kutoa nafasi kwa wasanii wanaochipukia kushiriki na kuthibitisha vipaji vyao.Katika Muhula huu tunakusudia kuanza kulipeleka tuko hili katika baadhi ya shule ili kuchochea ushiriki wa wanafunzi zaidi katika mijadala na sanaa.
Tunatarajia pia kushirikiana na baadhi ya taasisi mbalimbali ili kutoa nafasi za kujiendeleza kitaaluma na kisanii kwa wale watakaoonyesha juhudi na mwelekeo mzuri.
Tukio jingine jipya katika muhula huu ambalo litawezeshwa kama kawaida na BRITISH COUNCIL ni ubunifu na usanifu mitindo.
Mada ya safari hii katika WaPi ni ANGUKO LA UCHUMI DUNIANI…. Tunatarajia kushirikisha wadau mbalimbali katika kujadili athari za mtikisiko wa uchumi hapa kwetu. Pia hii ni nafasi muhimu ya kuangalia ni kwa jinsi gani jamii ina uelewa katika tatizo hili na namna ya kukabiliana nalo.
PROGRAMU ITASHIRIKISHA:
Waongozaji wa tukio kutoka WaPi Zanzibar
DJ Cool Para
Jukwaa la sanaa za Mikono
Mwl Muchi kutoka Nyumba ya Sanaa Zanzibar atasimamia warsha fupi juu ya sanaa ya uchoraji kwenye Kona ya MAARIFA
NEW GENERATION katika uchezaji na sarakasi
Mjadala wa mada
USHINDANI WA MAEMSII
Kimanumanu Kidumbak
Wamo Sanaa group katika Ngoma asilia
Pamoja na wasanii anaokuja juu katika Hip Hop Zanzibar..Chaby Six na Mr Mvuto
Mengineyo ni pamoja na Tenzi, Upambaji, Uchezaji na upigaji wa ala mbalimbali…MAHALI NI NGOME KONGWEAlhamisi tarehe 28-05-2009 kuanzia saa 9 alasiri hadi 2 usiku
Hamna kiingilio
African Day – yafana Kuala,Malaysia
May 26, 2009Kwa mara nyingine tena Jumuiya ya Mabalozi toka Africa walioko Malaysia wamefanikisha ile siku ya African Day katika Hotel ya Marriott hapa Kuala Lumpur Malaysia, ni siku ambayo inakutanisha waafrica walioko Malaysia na kusherehekea na kubadilishana mawazo. Balozi wa Tanzania Mh. Abdul Sisco Mtiro hakuhudhuria sherehe hizo kwani yuko nchini Cambodia alikokwenda kuwakilisha hati zake za utambulisho wa Ubalozi kwani Mh. Sinco anawakilisha Malaysia, Singapore, Cambodia, Laos, Philipines na Indonesia.
Kulikuwa na maonyesho ya vitu tofauti tofauti na nchi mbali mbali zilikuwa na meza zao ambapo walitambulisha nchi zao ama kwa utamaduni au kwa vivutio vya aina mbali mbali.
Si mchezo kusimama hapo naimani hata Obama alianzia chini kama hivi ipo siku!! Mdau Pius wa Spoti na Starehe Blog akiwa kwenye sherehe hizo.
Friends and Staff from Tanzania High Commission – Kuala Lumpur.
Watanzania Yusra toka Zanzibar na Salim wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye usiku huo ambao hufanyika mara moja kwa mwaka.
Pius na mtoto wa Balozi wa Swaziland ambao walitia fora kwa mavazi yao.
A.F.R.I.C.A
Waafrica toka kila pembe walikuwepo.
Yusra, Noel na Iyah wakiwakilisha Tanzania.
Mdau akiwa na Balozi wa Swaziland Malaysia akiwa na mkewe na mwanaye kwenye sherehe hiyo.
Mikonoz kama kawa.
Mr Paul: Finaly I am back to Music
May 25, 2009 Mwanamuziki mtanzania Paul Mbena aka Mr Paul amerudi kwenye uringo wa muziki kama alivyoahidi nilipofanya mahojiano naye mara ya mwisho.
Paul ambaye kwa sasa anaishi na kufanya shughuli zake za kimuziki nchini Australia kwenye jiji la Melbourne anasema kuwa ameshakamilisha nyimbo mbili ((Nakutamani na Malaika wa Moyo wangu) ambazo ziko kwenye mtindo wa Afro Funk style, nyimbo hizi ndizo zitakuwepo kwenye mradi wa Multicultural Art Victoria Visible CD, mradi ambao unajumuisha wanamuziki wa mataifa na mitindo mbalimbali (Gonga hapa kusoma zaidi.) angalia page ya mwisho utaona nafasi ya Paul Mbena ambaye kwenye mradi huu ametambulishwa kama Project Officer.
Awali aliongelea zaidi kuhusu mradi huu Mr Paul alisema “Nitarecord nyimbo mbili nyimbo zitapatikana World wide through eMusic, Amazon MP3 amd Nokia Music store worldwide, Si unajua music wa Zouk ni wa mapenzi, nyimbo hizo nazo zinamguso wa kimapenzi zaidi,
Pia Mr Paul aliongeza “Hii CD itatoka katikati ya mwaka huu. nadhani utakuwa ndio mwanzo wa safari yangu ya kimuziki hapa ughaibuni kwani tayari wanamuziki wengine wameanza kuonyesha interest ya kujiunga nami kuanzisha band. nitaendele kukupa info as things are proceeding.
Mr PAul ni mmoja wa wanamuziki ambao wamefanikiwa kimaisha kupitia Muziki ambapo alijisomesha na kwa sasa ameajiriwa na kufanya kazi nchini Australia akiwa anasimamia mradi wa kuelimisha rika wa Snake Condom. Tuliwahi kufanya naye mahojiano gonga hapa usome.
Ras Makunja aka Bw.Kichwa Ngumu vidole machoni na "Mzee Kizabi zabina"!
May 25, 2009 Ras Makunja aka Bw.Kichwa Ngumu vidole machoni na "Mzee Kizabi zabina"!
Hii kali ya mwaka ! wakati mjadala unaendelea kuhusu vekesheni ya balozi wa nanihino ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Tageta.
Kaka braza kakimbilia studio kufyatua wimbo mpya uliobeba jina la "Kizabi Zabina" si mtu Mwema! Kizabi zabina huyo alitajwa kwa jina la Mzee pazi, analalamikiwa na kiongozi wa bendi ya ngoma africa ras makunja kwa kuigombanisha jamii nakuwa sumu ndani jamii.
Wadaku walioshuhudia madongo makali yalikuwa yakirushwa na mwanamziki huyo katika studio huko ughaibuni.wamebaki midomo wazi kutokana na uzito wa madongo na hoja zilizojaa ukweli ukweli kuhusu "Kizabi Zabina" huyo aka Mzee Pazi.
Kiongozi wa Ngoma Africa Ras Makunja kamshitaki kwa jamii "Kizabi Zabina" kwa kosa la kuichonganisha jamii, tena kampa Shua kwa kumwambia "atafute la kufanya" na "kuwekeza muda mwingi katika maendeleo".
Watafiti wa mambo wanadai kuwa Ras makunja na kitu kipya hiko "Kizabi Zabina" kinaifanya bendi ya The Ngoma Africa yenye maskani ughaibuni kuonekana kuwa karibu sana na jamii ya Uswahilini kwa tungo zake ambazo mara nyingi zina elimisha,au kuishauri jamii ,wakati mwingine ni mwaliko wa malumbano ya hoja.
‘Bikira’ iliyouzwa kwa mnada yapata mnunuzi!
May 24, 2009Ni kwa ajili ya kufadhili masomo na kuikimu familia.
Alina Percea
Alina Percea toka Romania hatimaye amefanikiwa kupata mteja wa Bikira yake kwa dau la euro 10,000.
Alina Percea mwenye umri wa miaka 18 aliinadi bikira yake kwenye tovuti moja nchini Ujerumani miezi michache iliyopita.Alina alipanga kuzitumia fedha atakazopata baada ya kuuza bikira yake kwaajili ya kujisomeshea chuo kikuu na kuisaidia familia yake masikini iliyopo nchini Romania.
Alina ambaye kabla ya mnada huo alipimwa bikira yake, ilimbidi afanyiwe majaribio kwa mara ya pili kuthibitisha bikira yake.Daktari aliyemfanyia majaribio hayo alitangaza katika kikao na waandishi wa habari kwamba "Alina kweli ni bikira na hajawahi kufanya mapenzi".
“Sijui ni lini au wapi nitakutana na mshindi wangu, lakini nafurahia kusafiri iwapo atalipia gharama za usafiri"."Tutaenda hotelini katika wiki chache zijazo na tutatumia usiku mmoja pamoja, na kama tukipendana tunaweza tukakaa pamoja na usiku wa pili"."Tunaweza tukatumia kondomu au kama atafanyiwa vipimo vya magonjwa ya zinaa niko tayari kumeza vidonge vya kuzuia mimba"."Natumaini jamaa ataelewa kuwa mimi ni bikira hivyo atanihudumia vizuri" alimalizia kusema Alina.
Habari hii ni kwa mujibu wa Mzee wa Full shangwe ambaye ameiandika kwa kirefu, Gonga hapa uisome habari hii. Wabheja mwanawane.
Iran wapiga marufuku mtandao wa Facebook
May 24, 2009 Serikali ya Iran imeufunga mtandao wa Facebook kabla ya uchaguzi mkuu mwezi ujao, kwa mujibu wa habari zilizorushwa na shirika la utangazaji la BBC likikariri habari ya IRNA imesema kuwa serikali imefikia hatua hiyo baada ya mgombea Mousavi mmoja kujizolea washabiki kupitia mtandao huo.
Mir Hossein Mousavi (pichani juu) ambaye anawafuasi wengi na anatazamiwa kuleta marekebisho si tu kwa uchumi bali pia kwa style ya maisha ya wananchi wengi wa Iran ndiye mlengwa wa mkasa huo. Facebook umekuwa mtandao wa karibuni kukubwa na mkasa huu kwani mitandao kama Flickr, YouTube, MySpace na Blogger wengi wameshafungiwa na hairuhusiwi nchini Iran.
Kwa sasa mtandao wa Facebook haupatikani nchini Iran na haijulikani kama lini utarejea au ndio utakuwa haupatikani kabisa.
Jana niliandika kuhusu shura ya maimamu wa Indonesia ambao walipitisha azimio la kuufunga mtandao huo azimia ambalo likipitishwa na serikali litafanya mimilioni ya watumiaji wa mtandao huo kuathirika, telemka chini utaona habari hiyo.
“hakuna uhuru wa habari nchini kwangu, watu hawako huru kusema chochote dhidi ya serikali. alisema rafiki yangu tuliyeko shule na darasa moja Aidin ambaye anatokea Iran.
Wanaijoo waja tena na Fall in Love!!
May 24, 2009Uko kwenye Chart za juu MTV
Walikuja juu kwenye ulimwengu wa Sinema na kuiteka karibia Afrika yote kila nchi ukipita wanapenda na kuangalia sinema za Kinigeria. Sasa wamekuja kivingine na kuiteka Afrika kama si dunia kwa miziki yao.
Leo hii nakuletea video ya wimbo unaitwa Fall in Love toka kwake D’banj aka The KOKO Master akimshirikisha Don Jazzy.
Wimbo huu umeshika kila kona na unapigwa sana hata club, wao wanasema wana angalia soko la nje zaidi, basi kwa mpenzi yeyote wa muziki ataupenda muziki huu iwe kwa kuusikiliza au kwa kuucheza. Wimbo huu fall in love uko kwenye chart za juu za Radio na TElevisheni mbali mbali ikiwemo MTV.
Si maneno tuu hata video ya wimbo huu ni ya hali ya juu ingawa hii iliyoko hapa quality yake si nzuri sana pia Napenda kuusikiliza kutokana na lugha wanayotumia mfano anaposema my sweet portatoo, i wanna make u my wifoo, ur the love of my lifoo, i cant deny oooooo!!
Pata burudani na jumapili njema.
Kaka awakatisha tamaa Chelsea
May 23, 2009Mchezaji Wa AC Milan Mbraziri Kaka amesema kuwa hawezi kuondoka klabu yake ya AC Milan na kujiunga na Chelsea kama inavyosemwa. Kaka aliyasema hayo alipoongea na gazeti moja la michezo nchini Italy jana.
Kaka ambaye ana mkataba na timu yake ya AC Milan hadi mwaka 2013 amesema bado anaona Milan ni klabu yenye manufaa na inayomfaa kwa sasa. Siku za karibuni klabu ya Chelsea ilionyesha nia ya dhati ya kumsajili mchezaji huyu mkongwe kwenye kikosi chake ambaye pia alikuwa akitolewa macho na Manchester City.
BBCKuchambua Premier Ligi leo!
May 23, 2009Mlinzi Ferdinand hakucheza dhidi ya Arsenal kutokana na jeraha lakini atapambana na Barcelona katika ligi ya Ulaya ya klabu bingwa
Idhaa ya Kiswahili ya BBC ikishirikiana na redio washirika, Jumamosi ijayo, tarehe 23 mwezi Mei 2009, watazungumzia kuhusu msimu wa ligi kuu ya Premier, mwaka 2008 – 2009, na ambao mabingwa watetezi, Man U, wameweza kuhifadhi ubingwa.
Ikiwa una pongezi kwa timu yako, au hata ungelipenda kulaumu au kuikosoa timu yako, tunayakaribisha maoni yako.
Hata hivyo kumbuka bado kuna mechi kadha za kumalizia ligi.
-
Jumapili, tarehe 24 Mei 2009
Arsenal v Stoke, 18:00
Aston Villa v Newcastle, 18:00
Blackburn v West Brom, 18:00
Fulham v Everton, 18:00
Hull v Man Utd, 18:00
Liverpool v Tottenham, 18:00
Man City v Bolton, 18:00
Sunderland v Chelsea, 18:00
West Ham v Middlesbrough, 18:00
Wigan v Portsmouth, 18:00
Unaweza kutoa maoni yako kwenye BBC Ulimwengu wa Soka kwa kutuandikia ujumbe mfupi wa maandishi, yaani text message au sms, ukitumia nambari hii: + 44 7786 202 005.