WASANII WAKONGWE WAMTEMBELEA JK IKULU.
December 21, 2012
Picha juu Rais jakaya kikwete akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaaam leo.
Rais jakaya kikwete akimshukuru Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa Dansi nchini King Kiki
Mr Waziri Ally kutoka bendi ya kilimanjaro Band wana Njenje akitoa salaam za shukrani na pongezi kwa niamba ya ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu uliomtembelea Ikulu jijini Dar es salaaam leo — in Dar es Salaam.
Rais Jakaya kikwete akijadiliana jambo na Mwanamuziki Mkongwe kutoka Bendi ya Kilimanjaro Band Wana Njenje Bw Waziri Ally Muda mfupi baada ya ujumbe wa wasanii wakongwe wa muziki wa dansi pamoja na filamu kumtembelea Ikulu jijini Dar es salaaam leo — in Dar es Salaam.
Picha zote na Ikulu
Habari njema kwa Mashabiki wa Werasson
December 18, 2012Habari njema kwa mashabiki wa Werason, Igwee anatarajia kuja nchini karibuni, bado mipango ya awali ndio iko mbioni,, usia wangu tu kwa wanaotaka kumleta msituwekee na Local Bands kwani hawa wanamuziki wanajitosheleza wenyewe acheni tule burudani ya kutosha hata ikiwa ni masaa mawili tu, kwani sisi tunakwenda kumuona yeye na si Local Bands, hizi tunaziona kila siku.
Tutaendelea kufahamishana hapa hapa kuhusu ujio huu mambo yakiwa tayari.
“@
Koffi awasha moto Dar
December 16, 2012
Quadra Kora Man Le Grand Fororo Koffi akiwa jukwaani katika tamasha la Tusker Carnival usiku wa kiamkia leo.
Koffi akienda Sambamba na Cindy na warembo wake

Mashabiki wamekaa wakifatilia show. Ferre Gola aliwahi kukataa na kuomba viti vitolewe akisema anataka watu wacheze sio wakae ye hafanyi maigizo.
Stage
Picha zote kwa hisani kubwa kabisa ya Mzee wa Jiachie.
Fally Ipupa asherehekea Birthday yake leo kwa kuzindua Wimbo Mpya “Sweet Life”
December 14, 2012Ni Mmoja wa vijana wa Koffi Olomide ambaye amefanikiwa sana kwa sasa na ana portion yake kwa mashabiki na kwenye soko la muziki wa Dansi ulimwenguni.
Leo tarehe 14 December ndio siku ya kuzaliwa ya mwanamuziki Fally Ipupa huku akiizindua Single yake inayokwenda kwa jina la Sweet Life. Fally ni mmoja ya wanamuziki ambao wametoka mbali sana kwenye soko la Muziki huku nyota yake ikianza kung’ara kwenye kundi la Quartier Latin lakwake Koffi Olomide akisikika vizuri kwenye wimbo kama Sylivie na nyinginezo.
Mahadhi ya wimbo huu hayako kwenye Bolingo kama tulivyozoea ila uko kwenye mahadhi fulani kama R n B, Fally alisema nia yake ni kuupeleka muziki wa Congo kwenye level nyingine kabisa, na sasa tunaona hata aina ya muziki anayopiga, haya yanaweza kuwa mageuzi kwenye hiki kinachojulikana kama kizazi cha tano kwani hata Ferre Gola naye anatoa nyimbo akiwashirikisha magwiji kama Celine Deon na Rick Rossy.
Ikumbukwe pia Fally alishawahi kufanya interview Kwa JB Mpiana wakati bendi ikiundwa upya lakini bado alikuwa na ndoto ya kutoka kivyake kwani alikataa mpango wa kusaini mkataba wa muda mrefu. Leo hii tunashuhudia Fally akiwa na mashabiki lukuki huku akizindua albamu na zote zikiwa na nyimbo nzuri.