Ukinitajia mwanamuziki Lady Jay Dee kwangu ninayojinsi ninavyomuangalia mwanadada huyu. Napenda sana ubunifu alionao na jinsi anavyoimba kwa kutumia sauti asilia ambayo inaandikika kimuziki, nikiwa namaana kuwa muziki wake uko kwenye Note za kimuziki hasa na hivyo kutompa kazi prodyuza yeyote au wapiga vyombo wake.
Nilipopata nafasi ya kuongea na Maneno Uvuruge (Gonga hapa usome mahojiano naye)ambaye kwa wakati fulani aliwahi kufanya kazi na Machozi Band yake Lady Jay Dee anasema kuwa kati ya watu alifanya kazi nao basi hatomsahau Lady Jay Dee kwani walikuwa wakiongea lugha moja “unajua kama mtu anayeimba anaimba kwenye note hupati taabu mpiga ala, ila kama muimbaji anatoka nje ya note anakupa taabu wewe kumfunika ili washabiki wasielewe, alisema Uvuruge ambaye anapiga Solo kwenye Band ya Kilimanjaro Connection inayopiga muziki nchini Malaysia kwa sasa.
Kwangu mimi Lady Jay Dee ni zaidi ya Mwanamuziki.
Hivi karibuni mwanamuziki huyu alitembelea huko mikoa ya kusini na kugawa Vyandarua kwa ajili ya kampeni ya kutokomeza Malaria na huko alikutana na Mwanamuziki maarufu Barani Africa Balozi wa Malaria Afrika Princess Vyone Chaka Chaka.
Lady Jay Dee akisalimiana na Waziri Mkuu Mizengo Pinda huko Ntwara.
Akichangia jambo pamoja na Waziri Mkuu na Yvone Chaka Chaka Kulia.
akiwa Hospitali na kugawa Vyandarau kwa akina mama wajawazito
Sikiliza kibao cha Siwema toka kwake Lady Jay Dee anayepiga gitaa mwanzo kulia ni Maneno Uvuruge.
“…Kwa kutazama kwako vipindi vya Maisha Plus, kusoma habari zinazolihusu shindano na kutoa maoni, moja kwa moja ulikuwa sehemu ya Maisha Plus. Timu nzima ya Maisha Plus inakushukuru wewe kwa kuchukua muda wako na kulifuatilia shindano hili, hii ndiyo ilikuwa sehemu kubwa ya mafanikio yetu kwa kuwa tulikulenga wewe. Kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili umekuwa nasi bega kwa bega kutuunga mkono katika hili, tunautambua mchango wako kwa kuwa wewe ni sehemu ya shindano hili. Tunamshukuru mungu kwa kuweza kulifanya shindano hili kuwa kubwa na lenye mafanikio na zaidi ya yote limekuwa sehemu ya kuwajenga na kuwaburudisha Watanzania. Mwisho wa msimu huu ndio mwanzo wa maandalizi ya shindano la msimu ujao, tunaamini utakuwa na subira ukiwa na imani na sisi kuwa tukuandalia kitu kingine kizuri na chenye manufaa. Mungu akubariki kwa sehemu ya mafanikio ya Maisha Plus. regards” Julieth Kulangwa
Mwanamuziki Justin Timberlake na Rapper Fiasco Lupe wataungana na muimbaji Kenna katika kampeni ya Maji safi kwa kupanda Mlima Kilimanjaro.
Nia ya kupanda mlima kilimanjaro ni kuchangia mradi ambao ulianzishwa na Kenna ambaye ni mzaliwa wa Ethipia, ikumbukwe kuwa nyingi ya nchi za Africa bado suala la Maji safi ni kitendawili.
Justin amesema kuwa anakuwa akifanya mazoezi mara mbili kwa wiki ili kuzoeza mapafu yake kwa ajili ya kubeba hewa ya Oksijeni ya kutosha ambayo inahitajika sana wakati wa kupanda mlima huo wenye urefu wa M 5800.
Tutapanda kwa wiki nzima huku tukiwa na mzigo wa paundi karibu 30 mgongoni, kazi ni kubwa mbele yetu alisema Timberlake akiongea na GQ.
Naye Kenna alisema ”Baba yangu nusura afariki kwa ajili ya tatizo la maji miaka hiyo…” nina marafiki wengi sana ambao wako tayari kusaidia kampeni hii hivyo ni lazima tuifanikishe alisema Kenna.
Kwa mujibu wa mtandao wa gazeti la Guardian wastani wa wapandaji 10 hufariki kila mwaka katika harakati za kuupanda mlima huo mrefu kuliko yote Barani Afrika.
Waandaaji wamepanga upandaji ufanyike kipindi hiki cha majira ya kipupwe.
Nakuacha na kibao Whats Goes Around Comes Around toka kwake Justin Timberlake!!
Eto’o has scored 32 goals in 42 games so far this season
Klabu ya Manchester City imefanya mazungumzo na Klabu ya Barcelona juu ya mchezaji Samuel Eto’o BBC imeripoti.
Etoo ambaye kwa sasa ameingiza kimiani magoli 32 kwenye mechi 42 alizocheza msimu huu ameonyesha kiwango kizuri hasa baada ya kupona ambapo kulikuwa na hati hati ya majaliwa yake.
Katika pitapita zangu jumapili nikaingia Mid Valley Mega Mall nikiwa na rafiki yangu Yatie Mwaki, nilikutana na hii Fashion Show iliyokuwa imeandaliwa na Elle Fashion, nikaona si vibaya kama nitashare na wadau wangu walao picha mbili tatu, Mamaa Shamim upoo?. Maonyesho haya yalikuwa kwa ajili ya kuonyesha nguo mpya na kulikuwa na punguzo kubwa la beo 30% to 70% kwa waliohitaji kufanya biashara karibuni Malaysia.
Weekend ndio hiyo kama kawaida nakuacha na kibao Liberez kibao hiki ni maalum kwa washkaji zangu Mama Sophia Kessy, Le Suvereign Maghambo, Mukulu Ling’ande (mna nini bwana?), Jeff Msangi, Robbie Mzee Wa Upang, Rasheed na Danny, Muafirika hehehe Mutu ya Mbeya, Mukubwa Six, Mgosi Tameem na Abel, Mamaa Ghaty, Mamaa Joy Mwaisa na wengine wooooote!! Weekend njema Chakuchoma kwa sana, nawamiss kinoma washkaji!!
Huku akishangiliwa na mashabiki zaidi ya 6000 waliofurika kwenye Eneo la SunWay Lagoon, Mwanamuziki chipukizi na mshindi wa shindano la American Idol kwa mwaka jana David Archuleta hivi karibuni alifanya ziara nchini Malaysia, Ziara ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu na iliisha kwa lawama kwani maelfu kwa mamia ya mashabiki walikosa Tiketi za kumuona kijana huyu ambaye aliistaajabisha watu kwa jinsi ilivyokuwa kazi kwa Polisi kumtoa uwanja wa Ndege wa KLIA mara alipowasili, Shukrani kwa Blogger na Rafiki yangu Tian kwa habari na picha kama alivyonasa kwa Camera yake.
Picha na Story na Tian Chad, Blogger na Mwanafunzi mwenzangu, Shukran za Kipekee kwako, Xie Xie, Terima Kasih, Thank you, Asante sana, Merci !!
Archuleta akiwa katika vazi la kimalay maarufu kama Barju
David katika vazi la Barju
Akivikwa Barju
It was only 1:30PM
Saw the crowd inside ?!
They are giving us theDIGI Cheering Tube
A nice view of Sunway Lagoon Amphitheatre
Basically almost all seats has been taken except the VIP seats is still empty
VIP can come late ha! >.<
The Rtm “Terminator” Video Crew is recording
People were shouting
While we are waiting, what are we doing?
Playing Nintendo DS Lite?
Cam-whoring?
Chatting?
Yawning?
Meditating??
David Archuleta has a bunch of YOUNG fans 🙂
Guess how young they are?
Even the Caucasian came here to see David 🙂
The crowd will shout every time the spot light was switch on.
Such a good catalyst to bring up the ambience !
Almost 3PM
The crowd is still coming in
It is humid + hot inside…
I was sitting beside a group of youngster which reach here since 10.30AM!!
They only manage to get inside here after 12:30 PM the gate opened.Imagine they are all waiting under the sun…
Impressed with their David’s spirit!
Lucky enough to get a space beside them ha! XD
Waiting waiting……
They let us have practice on how to sing David’s Song
This girl is one of the great supporter 🙂
After 3.30PM ++ JJ and EAN from hitz.FM came out giving free gifts by asking simple questions
They are good :)This little girl really know how to sing his song!
Impressed + salute
The performance started
Everyone thought David is coming out but “Nobody Knows” Hao Ren @ 朱浩仁
came outWhat a great start with a great song name! Haha!
People were actually booing at him because all come here to see David ar
Luckily he get some cheers when he perform the dance.
Luckily!
Then the finale of “One In A Million” came here all the way from National Service
Just to perform to us and see David at the same time.
His name = _______
(need ur help ^@^”)
Later on Danell Lee came out
People shouted, ” We want David!”
Danell replied, “Yes. David? Danell here!”Such a good reply to avoid being embarrassed
I like the Chinese Version of Mimpi
I still remember when I was working in TOYCITY
I was able to sell TWO Remote Control Aeroplanes in one shot after keep listening to this song.
You will get some positive energy when listen to the right song 🙂
AT LAST, David Archuleta is showing up!!
He is just 19 years old and already have a good achievement!
Looking forward to be as success as he is!
(Not a singer la ;p)
“A Little Too Not Over You”
“Don’t Let Go”
My favourite shot far away from the stage! 🙂
“Crush”
Many Arch Angel had a crush on him
How many video recorder here?? ;p
For just a while, David is going to MIA
The performance is so so short!
Everyone was standing and now even the VIP Seats are ALL full!
The VIPs are so nice sitting enjoying their best view ar
Luckily no terrorist inside.
In the end sure he came back la 🙂
(A tactic to make people want more)“A Thousand Miles”
I really like this one
“Angel”
The last song he performed!
When this end
Most people complaining it was too short and they want more!Unfortunately that is the end…
Imagine you have start to wait since early in the morning just to see David not more than 30 minutes…~
I think David is “hiding” inside a car and wait for the crowd to go off before taking a group photo with his VIP fans 🙂
There were bunch of people taking photo with EAN
He has too many requests to decline
And JJ look shocked with the crowd too XD
Some people able to get poster for themselves.
And some people able to get the BIG Banner for themselves!!
Just a moment before she did what she did ;p
When you going out from the Amphitheatre, you will see all the David’s banner disappeared except DIGI Banner!
Haha! What a hardcore fans of David
Shindano la Maisha Plus linafikia tamati Jumapili, ambapo mshindi ataondoka na kitita cha shilingi milioni 10 papo hapo baada kudumu kwa siku 56.
Shindano hilo lililoanza Machi 1,2009 linafikia tamati ikiwa ni sehemu ya kwanza na ya pekee katika historia ya mashindano ya uhalisia( Reality Shows) nchini Tanzania.
Mratibu wa shindano hilo, David Sevuri anasema shindano hilo linamalizika huku malengo yakiwa yamefikiwa kwa kiasi kikubwa.
“Tulilenga kuwawezesha vijana kujitambua,Kuwapa ujuzi kwa kuwafundisha vitu mbalimbali, Kuendeleza vipaji vyao,kuwapa mtazamo chanya wa maisha watazamaji na washiriki,kubadilishana utamaduni na kuburudisha watazamaji, tunajivunia kusema kuwa tumeweza kufanikisha yote haya” alisema.
‘Eviction’ ya aina yake kufanyika Jumapili
Shindano limebakiwa na washiriki 10 ambao mmoja kati yao ndiye atakayechukua zawadi hiyo kubwa hapo kesho.
Mtoano utaanza kuonyeshwa kupitia TBC1 Jumapili saa tatu asubuhi ambapo kwa kuanza saa nne kamili asubuhi washiriki wawili wataaga na baadae washiriki wengine wataaga saa saba kamili mchana.
Mtoano wa mwisho utafanyika saa mbili na nusu usiku ambapo shindano litakuwa limebakiwa na washiriki watatu tu.
Mpigie kura mshiriki umtakaye ashinde
Miloni kumi imetengengwa kwa mshindi lakini uamuzi wa kumpa mshindi upo kwa mashabiki ambao ndio waamuzi katika shindano hili.
Maulid 33, Hamis 15, Moshy 19, Abdul 32, Charles 11, Steve 14, Upendo 18, Boniface 20, Teddy 36 na Modesta 37.
Unaweza kupiga kura kwenye mtandao ambao ni maishaplus.g5click.com au kwa njia ya simu kwenda 15522.
Maisha Plus kurudi tena
Ni miezi miwili imepita tangu shindano hilo lianze, kutokana na uhalisia wa shindano hilo kureflect maisha ya Watanzania wengi wameomba liendelee kuwepo,kwa mujibu wa waandaaji shindano hilo litarejea baada ya mapumziko ya muda mfupi.
Mraribu wa shindano hilo David Sevuri ameliambia Starehe kuwa kutokana na maoni ya watu wengi shindano hilo litakuwa tena TBC1 baada ya timu ya shindano hilo kijipanga upya.
“Tutarudi tena tukiwa tumeliboresha zaidi shindano hili, lakini watazamaji bado watakuwa na vitu vingi vya kutazama kwa wakati wote ambao hatutakuwepo kijijini kwa kuwa tuna vitu vingi havijaonyeshwa” alisema.
Sevuri alisema kipindi cha Maisha Plus cha Jumapili kitaendelea kama kawaida kwa muda wote wakati ‘season’ II ikisubiriwa.
Michael Essien wa Chelsea akiwa na Mama yake mzazi huko nyumbani kwao Accra Ghana.
Mama mzazi wa mchezaji mahiri wa Chelsea na Timu ya Taifa ya Ghana Michael Essien, Aba Djanode amesema kuwa mwanaye ambaye ana miaka 26 sasa asingekuwa hapo alipo kama asingepata tiba maalum kwa ajili ya ugonjwa wa malaria unaogharimu maisha ya binadamu kila uchao na takwimu zinaonyesha kwa wastani mtu mmoja kwa kila sekunde 30 hufariki kwa Malaria.
Mama Djanode ameanzisha kampeni ya kutokomeza Malaria huko Ghana akishirikiana na mwanaye ambao kwa pamoja wanasaidia kugawa vyandarua kwa wanachi wanaohitaji na kusaidia kampeni tya kutokomeza mazalia ya Mbu.
“…Michael alipata Malaria akiwa na miezi kumi na baadaye tena akiwa na miaka saba” alisema Mama Djanode alipoongea na gazeti la The Sun kupitia kwa mkarimani wake.
Wachezaji wa Everton wakishangilia baada ya mchezaji wao Tim Howard kupachika kimiani bao la Penati ambayo ilihitimisha kiama cha Mancheter United hapo jana kwenye mtanange kati yao, matokeo ambayo yanaipeleka Everton Fainali baada ya kufika hatua hiyo mara ya mwisho mwaka 1995.
Mchezo ulienda dakika za nyongeza na kuamuliwa kupiga Penalti ambapo mchezaji wa Man U wa kwanza kupiga alikosa Penalti baada ya mchezaji wa Everton naye Kupaisha. Everton walikuwa wa kwanza kupiga.
Mchezo huu ulichezwa kwenye uwanja wa Wembley Stadium na ulihudhuriwa na mashabiki wapatao 88,141.
Wachezaji wa Man U wakimuangalia mwenzao akienda kupiga Penati katika mchezo wa jana ambapo mashabiki walimlaumu kocha wao Fergie kwa kuchezesha kikosi B, Pole wadau wa Man U, Michael Otieno Opar, Dr. Kiiza, M-jay, Simple X, bila kumsahau mshabiki No. 1 wa Arsenal Batty Wills na PDG Ling’ande, Mnanini bwana.
Dogo akiwa haamini kilichotokea baada ya Man U kupoteza mchezo na Everton hapo jana.
Waswahili wanasema Njaa kipimo cha akili, Kila kukicha watu wanazidi kubuni namna ya kukabiriana na maisha ya kila siku, na hii imekuwa changamoto kwani maisha ya kutegemea kuajiriwa kwa sasa hakuna na kila mmoja anatakiwa kuwaza jinsi gani atajiajiri. Changamoto hii ndio matunda ya vitu kama Maisha Plus.
Maisha Plus ni nini?
Ni shindano la uhalisia ( Reality Show) ambayo halijawahi kufanyika barani Afrika, ni shindalo linalo ‘reflect’maisha halisi ya Mtanzania hasa vijana. Shindano hili lilianza kuonyeshwa kupitia kituo cha TBC1 March 1,2009, Mchakato wa kuwatafuta washiriki 18 ulianza Novemba mwaka 2008 katika kanda nane za Tanzania bara na Visiwani.
Lengo la Maisha Plus ni nini?
Kuwawezesha vijana kujitambua
Kuwapa ujuzi kwa kuwafundisha vitu mbalimbali kupitia semina na mafunzo mbalimbali wanayopewa.
Kuendeleza vipaji vyao
Kuwapa mtazamo chanya wa maisha watazamaji na washiriki.
Kubadilishana utamaduni
Kuburudisha watazamaji.
Malengo ya badae ya Maisha Plus
Mwezi wa saba season II ya shindano hili itaanza na safari hii usaili utafanyika katika mikoa yote ya Tanzania. Season III ya shindano hili itajumuisha nchi zote za Afrika Mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi n.k. Waandaaji wa shindano hili ni kampuni ya dmb Inc inayomilikiwa na Masoud Kipanya, Fransis Bonda na David Sevuri. Kipindi hutengenezwa na kampuni ya True Vision Production.
Regards Julieth Kulangwa Media Coordinator 0717 551355
Washiriki 10 tayari wamebakia kwenye mtanange wa Fainali ambapo hapo mmoja ndio ataibuka kidedea kwenye kinyang’anyiro cha Reality Show ya Maisha Plus.
Pamoja na vigezo vingine kura yako ndio itatoa mshindi hivyo shime piga kura sasa.
Namba za kupiga kura ni hizo hapo chini ikiambatana jina na namba ya mshiriki.
Usikose kuangalia hapa kujua nini kitatokea na kusoma maoni toka kwa wadau wetu ambao wanachangia sana Bonyeza hapa!! kusoma habari na story zote za Maisha Plus humu.
Baada ya kutegeshewa kinasa sauti ambacho kwa kiasi kikubwa kimewezesha kujua uhalisia wa watu wakiwa mbali na Camera nini kitafuata?
Usikose kuangalia Maisha Plus TBC 1 na kusoma Spoti starehe kila uchao kwa habari motomto.
Moja ya habari ambazo mashabiki wa mpira hasa wa timu ya MAnchester United imekuwa ikiwapa wasiwasi ni kuhusu kuondoka kwa mchezaji wao hodari Christian Ronaldo.
Ronaldo ambaye toka amekuwa na Klabu ya Manchester United amekuwa na mafanikio makubwa na kuibuka kama mchezaji bora na mafungaji bora mara kadhaa amekuwa akidaka vichwa vya habari kila uchao na habari za hivi karibuni zinasema kuwa Ronaldo anatarajiwa kwenda Spain msimu ukiisha.
Kwa timu ya Manchester United si jambo geni kuondokewa na watu wenye majina makubwa kwani kocha FErguson amekuwa ni mwalimu wa watu ambao ama waling’ara au wanang’ara leo hii kama mnakumbuka watu kama Eric Cantona, David Beckham, Roy Kean, Rud Van Nistelrooy, Paul Scholes, Rio Fednand na wengineo ambao kwa sababu moja au nyingine wapo ama hawako kwa sasa.
Katika kipindi chake akiwa na klabu ya MAnchester amekuwa hatishwi na mchezaji kuondoka na wakati mwingine aliuza mchezaji hata kama bado yuko kwenye chati.
Fergie alimuuza Bekham akiwa bado kwenye kiwango cha juu kabisa, mtu kama Roy Kean mwenyewe Ferguson anasema ni mchezaji bora ambaye hajawahi kufundisha, na Mc Grath anamchukulia kama defender bora kucheza Uingereza, sio huyo tuu akimuongelea Van Nisterooy Fergie anamsema kama ni mmoja wa washambuliaji bora kabisa.
Ama kwa hakika hakuna anayeweza kumlaumu kocha huyu kwa kuuza ama kuachia majina makubwa yaende.
Akiongea na Televisheni ya Portugees Agent wa Ronaldo alikaririwa akisema kuwa Mchezaji wake amekukuwa hatetewi na marefa uwanjani na kusema kuwa hiyo imeharibu morali wa mchezo uwanjani kwani binafsi anachukulia marefa kama wanamkomoa.
Muonekano wa nje wa wanja la Nelson Mandela bay multipurpose stadium huko jijini Port Elizabeth ukiwa ni mmoja wa viwanja vitakavyotumika kwenye mtanange wa Kombe la Dunia ,mwaka kesho 2010. Afrika kusini iko kwenye maandalizi ya mwisho ya kukamilisha kupokea timu kwa ajili ya mashindano hayo.
Chelsea are through to the semi finals of the Champions League following a spectacular 4-4 draw with arch rivals Liverpool on Tuesday. The Londoners had won the first leg 3-1.
Liverpool had a great first half hour at Stamford Bridge. Fabio Aurelio took a free kick from the right wing and while all expected for him to cross in, the ball sailed into the goal at the first post with keeper Petr Cech only able to watch.
RT @CarolNdosi: “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na k… 2 months ago
RT @CarolNdosi: Ninasadiki kwa Mungu mmoja..baba mwenyezi Muumba wa Dunia...na kwa Yesu Kristu..mzaliwa pekee..Mungu Mwana.. 2 months ago
@CarolNdosi Most of them wanataka followers n to become famous whil seating somewhere akingoja atumiwe na ya kutolea. 2 months ago
RT @CarolNdosi: “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na k… 2 months ago
RT @CarolNdosi: Ninasadiki kwa Mungu mmoja..baba mwenyezi Muumba wa Dunia...na kwa Yesu Kristu..mzaliwa pekee..Mungu Mwana.. 2 months ago
RT @GeezGrill: Hii ni Combo Platter ya 1/2Kg Ribs na 4pcs Russian Sauasages inakuja na Ndizi 2 na Kachumbari kwa 15,000/- tuu toa order yak… 6 months ago