Yuko wapi Allain Konkou?

June 11, 2012

Unamkumbuka Alain Kounkou alivyowasha moto Africa nzima 1992 na hii kitu ?? wewe ulikuwa wapi wakati huo na unakumbuka nini ukisikiliza hili Generique la ukweli????

Sijui yuko wapi huyu mtu alikua na masebene ya ukweli.


Foundation Solomon Kalou, Thank you..

June 11, 2012

Huwa nasikia raha sana ninapoona mtu mweusi anapata mafanikio katika shughuli zake halafu anaamua kurudisha sehemu ya kile alichokipata kwa watu wake. Leo tumtizame mwanandinga Solomon Kalou wa timu ya soka ya Chelsea ya Uingereza anapoamua kushare kile alichokipata kupitia kipaji chake na watu wake wa nyumbani kwao alikozaliwa Ivory Coast kwa kuzindua Foundation yake kwa ajili ya watu wa Ivory Coast.

Hafla ya uzinduzi wa foundation hiyo ilifanyika katika jiji la Abidjan na kuhudhuriwa na watu mbali mbali mashughuli wa Ivory Coast ambapo ulikua ni usiku mzuri sana uliombatana na burudani kibao… pata picha ya kilichojiri kwa uchache na hii iwe ni changamoto kwa watu wote wa hapa nyumbani wanapopata mafanikio makubwa ya kimaisha na kiuchumi kujaribu ku share mafanikio yao hayo na jamii inayowazunguka..


Foundation Solomon Kalou, Thank you..

June 11, 2012

Huwa nasikia raha sana ninapoona mtu mweusi anapata mafanikio katika shughuli zake halafu anaamua kurudisha sehemu ya kile alichokipata kwa watu wake. Leo tumtizame mwanandinga Solomon Kalou wa timu ya soka ya Chelsea ya Uingereza anapoamua kushare kile alichokipata kupitia kipaji chake na watu wake wa nyumbani kwao alikozaliwa Ivory Coast kwa kuzindua Foundation yake kwa ajili ya watu wa Ivory Coast.

Hafla ya uzinduzi wa foundation hiyo ilifanyika katika jiji la Abidjan na kuhudhuriwa na watu mbali mbali mashughuli wa Ivory Coast ambapo ulikua ni usiku mzuri sana uliombatana na burudani kibao… pata picha ya kilichojiri kwa uchache na hii iwe ni changamoto kwa watu wote wa hapa nyumbani wanapopata mafanikio makubwa ya kimaisha na kiuchumi kujaribu ku share mafanikio yao hayo na jamii inayowazunguka..