FALLY IPUPA "CADENAS"

 

Walipooondoka akina Suzuki enzi hizo ile timu ya Koffi ilitabiriwa kuwa ingekuwa ni muda wa Koffi kutamba kwenye anga za muziki wa Kongo.

Alipohojiwa na Canal France International (CFI) – Koffi alisema kuwa Quartier Latin ni Dream Team (akiifananisha na timu ya taifa ya mpira wa kikapu ya Marekani) kwani pale vinapikwa vipaji na kuvipa nafasi ila alisisitiza kuwa wale watakao jifunza kwa nidhamu na nidhamu ya Quartier Latin  ni kujali wapenzi zaidi kujua wanataka nini na ukawapa wanachokitaka basi utadumu kwenye soko, hiki ndicho alichotoka nacho Fally Ipupa kwa Koffi, kwa kweli kwenye hichi kizazi cha tano cha wanamuziki wa Congo jamaa yuko juu na anajitahidi sana kuwakamata mashabiki huku akittengeneza video zake kimataifa zaidi tofauti na zile Video za Ki Congo tulizozoea.

Papaa Julie We Eston, Papaa Sisco na Kati ya Kwetu Saloon Bana Congolee wa Kigamboni. tuko pamoja na jumapili kama kawa Bonanza la Diamond Musica ndani ya Chadibwa Beach- Kigamboni.

Sikiliza hili Rhumba kisha nipe maoni yako unamtabiria nini kwa mwaka huu kijana Fally Ipupa.

Ijumaa Kareem.

2 Responses to FALLY IPUPA "CADENAS"

  1. Edwin Ndaki says:

    hii imekaa vema Pius..soon nitakuwa bongo lazima nipite anga hizo..long time saana:)

  2. Anonymous says:

    Hivi ARSENAL IKINYUKWA kama ilivyochezea KICHAPO hapo juzi toka kwa Mashetani Wekundu wekundu unakuwaga huna kimbelembele cha ku-POST habari za LIGI KUU ZA ENGLAND? TEEEH! TEHE! TEHE!

Leave a comment