Ngoma Africa Band na Nyimbo za masimulizi!
Bendi maarufu ya mziki wa dansi the Ngoma Africa Band,inayoongozwa na mwanamziki
maarufu Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Ebby Makunja “Bw.Kichwa Ngumu”
Imeibua zogo la gumzo lingine kwa kufyatua wimbo wao uliobeba jina la “Baba wa kambo”
wimbo huo umefyatuliwa wakati CD yao “Apache wacha Pombe” inawasha moto mkali wa kimataifa !
wimbo wao huo wa “Baba wa Kambo” ulifyatuliwa katika kuadhimisha sikuu ya watoto dunian! wimbo huo unawakilisha kilio cha mamilion ya watoto wanao teseka katika utwala wa kidikteta wa kina “Baba wa Kambo” ni utunzi wake tena kiongozi na mwimbaji wa bendi
Ebrahim Makunja.
Katika wimbo huo Ras Makunja amemrushia lawama(madongo) “Baba wa kambo” na kikosi
cha Ngoma Africa kikimsindikiza kwa kumzomea !baba wa kambo tunakushikia bango!
Kindumbwe Ndumbwe Charia ! na Nguo! kaitia moto!
Bendi hiyo maarufu inayopeperusha bendera ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa,
imefanikiwa kuliachia song hilo ambalo linamshitaki “Baba wa kambo” Kwa Jamii!
na jamii pamoja na tahasisi zake zifanye kila njia kutupia jicho swala la maelezi ya watoto
ambao ulelewa na kina baba wa kufikia maarufu kwa jina la “Baba wa Kambo”
madongo hayo ya Ras Makunja na kikosi chake The Ngoma Africa hayakuishia hapo tu
bali lawama nazo zimerushiwa kwa kwa MAMA ALIYELEWA MAPENZI na kumshau mwanae akiteswa na “Baba wa Kambo”
Mzozo huo katika ya Baba wa kambo na The Ngoma Africa band utapelekwa kwa jamii hili
upatikane uhamuzi nani ?mwenye makosa Baba wa Kambo! au Mama Aliyelewa Mapenzi!
au Ngoma Africa Band waliomzomea baba wa kambo na kuweka mateso yake yote uwanjani yajadaliwe na jamii?
Baadhi ya Malalamiko ya ngoma africa kuwa “Baba wa Kambo” anamfanyishwa YATIMA kazi ya kutafuta kuni !wakati watoto wengine wapo shuleni! anamnyima ELimu yatima!
wakati Elimu ni ufunguo wa maisha,anampa KISAGO CHA MOTO yatima,anamlaza chumba cha Uwani karibu na chooni !kula na kulala kwa shida!
Baba wa Kambo naye labda atalalamika kuwa kiongozi wa bendi hiyo ni mwanamziki mwenye GUBU! kawashawishi wenziwe kumzomea wakati mila zinasema usimzomehe mkubwa!