Thursday, June 26, 2008

June 26, 2008

Ngoma Africa Band na Nyimbo za masimulizi!

*Ras Makunja kamrushia madongo Baba wa Kambo!?

Bendi maarufu ya mziki wa dansi the Ngoma Africa Band,inayoongozwa na mwanamziki

maarufu Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Ebby Makunja “Bw.Kichwa Ngumu”

Imeibua zogo la gumzo lingine kwa kufyatua wimbo wao uliobeba jina la “Baba wa kambo”

wimbo huo umefyatuliwa wakati CD yao “Apache wacha Pombe” inawasha moto mkali wa kimataifa !

wimbo wao huo wa “Baba wa Kambo” ulifyatuliwa katika kuadhimisha sikuu ya watoto dunian! wimbo huo unawakilisha kilio cha mamilion ya watoto wanao teseka katika utwala wa kidikteta wa kina “Baba wa Kambo” ni utunzi wake tena kiongozi na mwimbaji wa bendi

Ebrahim Makunja.

Katika wimbo huo Ras Makunja amemrushia lawama(madongo) “Baba wa kambo” na kikosi

cha Ngoma Africa kikimsindikiza kwa kumzomea !baba wa kambo tunakushikia bango!

Kindumbwe Ndumbwe Charia ! na Nguo! kaitia moto!

Bendi hiyo maarufu inayopeperusha bendera ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa,

imefanikiwa kuliachia song hilo ambalo linamshitaki “Baba wa kambo” Kwa Jamii!

na jamii pamoja na tahasisi zake zifanye kila njia kutupia jicho swala la maelezi ya watoto

ambao ulelewa na kina baba wa kufikia maarufu kwa jina la “Baba wa Kambo”

madongo hayo ya Ras Makunja na kikosi chake The Ngoma Africa hayakuishia hapo tu

bali lawama nazo zimerushiwa kwa kwa MAMA ALIYELEWA MAPENZI na kumshau mwanae akiteswa na “Baba wa Kambo”

Mzozo huo katika ya Baba wa kambo na The Ngoma Africa band utapelekwa kwa jamii hili

upatikane uhamuzi nani ?mwenye makosa Baba wa Kambo! au Mama Aliyelewa Mapenzi!

au Ngoma Africa Band waliomzomea baba wa kambo na kuweka mateso yake yote uwanjani yajadaliwe na jamii?

Baadhi ya Malalamiko ya ngoma africa kuwa “Baba wa Kambo” anamfanyishwa YATIMA kazi ya kutafuta kuni !wakati watoto wengine wapo shuleni! anamnyima ELimu yatima!

wakati Elimu ni ufunguo wa maisha,anampa KISAGO CHA MOTO yatima,anamlaza chumba cha Uwani karibu na chooni !kula na kulala kwa shida!

Baba wa Kambo naye labda atalalamika kuwa kiongozi wa bendi hiyo ni mwanamziki mwenye GUBU! kawashawishi wenziwe kumzomea wakati mila zinasema usimzomehe mkubwa!

hatujui Jamii itamuhua nini? au nani mwenye makosa


Werasson: Niko tayari kupiga na JB Mpiana Tanzania

June 26, 2008
Pichani ni Rais wa Kongo RDC Joseph Kabila akiwa na timu ya Wanamuziki akiwemo Marehemu Madilu System alipokutana nao na kuwapatanisha baadhi yao akiwemo JB Mpiana na Werasson mwaka juzi.
MWANAMUZIKI hodari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ngiama Makanda ‘Werrason’ amewasili Dar es Salaam na kusema yupo tayari kupiga pamoja na Jean Bedel Mpiana ‘JB Mpiana’ endapo atapatikana promota wa kuwaleta Tanzania kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania.Msanii huyo aliwasili juzi jioni akitokea Jamhuri ya Kongo ambapo na kundi la wanamuziki 24, anatarajiwa kutoa burudani kesho kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza kabla ya kupiga Arusha Jumapili kwenye Hoteli ya Naura Springs.

Endapo ‘Werrason’ atapiga pamoja na ‘JB’ Mpiana itakuwa ni historia baada ya nyota hao kuingia katika mzozo mkubwa ulioibua vita kati yao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Makanda alisema atafurahi kupiga pamoja na Mpiana ambaye inadaiwa ni wapinzani na chanzo cha kuvunjika kwa kundi maarufu la Wenge BCBG lililowahi kutamba Afrika.

“Sina matatizo na Mpiana ni rafiki yangu napenda siku moja nije naye hapa tufanye onesho la pamoja nipo tayari hata sasa cha msingi apatikane promota mwenye uwezo nitamwambia lakini naomba nipate uhakika kama mnatuhitaji kabla ya mwaka huu kumalizika,” alisema Makanda.

Makanda alisema anapenda kuona muziki wa Tanzania unapiga hatua kama ilivyo Jamhuri ya Kongo na kuongeza kuwa endapo atapata fursa ya kuzungumza nao atawashawishi watengeneze albamu ya pamoja.

Msanii huyo alisema alishindwa kutoa burudani mwaka jana kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake na alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi Watanzania kutokana na tukio hilo.

Alisema amejiandaa kuacha historia kwa kupiga nyimbo zake mfululizo ili kukata kiu ya mashabiki wa burudani ambao walikuwa na shauku kubwa ya kumuona nyota huyo akiwa jukwaani katika ardhi ya Tanzania.

Ziara ya mwanamuziki huyo imedhaminiwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya Embassy kwa kushirikiana na Club E.


JB Mpiana alipofanya kweli Ufaransa

June 26, 2008

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

Kama kawaida Ziara ya JB Mpiana ilihitimishwa Ndani ya Bataclan Paris, Ufaransa tarehe 22 mwezi huu na mambo yalikuwa moto, JB Mpiana anayetamba na Albamu yake Mpya Ya Quel Est Ton Probleme? Aliwaburudisha mashabiki walijaza ukumbi kwa nyimbo za zamani na zikichanganyika na mpya, Kama Zadio Congolo, Mtindo wa Lopele pia mashabiki walilipuka nao kinoma, Kali ni pale kibao matata cha Liberez kilipoanza kuimbwa, Wimbo huu umo kwenye Albamm yake mpya na umetokea kupendwa sana. Liberez ni utunzi wa mwanamuziki mpiga Bass gitaa wa Wenge BCBG Sunda Bass. Onyesho limesifiwa kwa kuwa na Sound System nzuri na Jb alitumia muda vizuri na muda wote mashabiki walifurahi.