Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri aja kivingine July

June 3, 2008

.

.

Solo thang akiwa na Mtoto wake Yassir nyumbani kwake, huko UK

Muziki ni safari, Kwa wanaokumbuka enzi hizo ukilitaja jina Solo Thang kila mtu mpenda Muziki anasisimuka, kwani ni mmoja wa wanamuziki wa Kizazi kipya ambao kwa kiasi kikubwa “walipigana vita ya msituni” kufanya muziki huu ukubalike kwa jamii. Kwa sasa Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri anaishi Uingereza akiwa ameoa na mtoto mmoja anayeitwa YASSIR na Mama yake anaitwa YASMIN.
Kwa muda sasa mwanamuziki Solo Thang amekuwa kimya kutaka kujua yuko wapi Spoti Starehe tumefanya mahojiano naye kutaka kujua machache toka kwake na maisha yake hasa ya kisanii kwenye sanaa nzima ya Muziki.

Spoti na Starehe (S na S): Mara ya mwisho nilisoma Interview yako Bongo5 ile Albamu uliyofanyia huku ughaibuni ilitoka kaka nataka mawili matatu kaka.

Solo: okee,bado ndo naiweka sawa kakakuna mambo mengi na shule ilinibana mkuu.

S na S: Jina ni bado lile lile la Albamu?

Solo: Yaa inaitwa TRAVELLER, ndio jina waliokuwa wananita enzi nasoma jitegemee….99

S na S: oooh poa sana, sasa unategemea kuimaliza lini, i mean itakuwa sokoni?

Solo: Kama nilivyo Kwambia kuna mambo namalizia ila Inshallah Hivi karibuni nitaanza na Single

Akiwa pamoja na Dj lee flex, na mdau baraka, DJ Lee ni mmoja wa Madj ambao wanaitangaza Bongo Flava Nje.

S na S: Vipi Maisha kwa ujumla nasikia ulikuwa unasoma, Je zaidi kumaliza Chuo cha Diplomasia pale Kurasini kuna chochote tena?

Solo : Shule kama kawa kaka haina mwisho,we learn new things daily ..nilishamaliza baadhi ya courses na nitaendelea na buku.kwa sasa napiga mzigo nakuiweka sawa family!


S na S: oooh safi sana mkuu kila la heri, Je unaionaje game kaka na ujio wa vijana wapya ukilinganisha na enzi zenu? nani mpya unamfeel sana?

Solo: Mmh well vijana wanatisha wanajitahidi ila FID Q yuko poa, CHIDI mwanangu yuko bomba

S na S: Je hufikirii kufanya kolabo na wanamuziki tofauti na wa nyumbani ili uende kimataifa zadi unalizungumziaje hili mkuu?

Solo: hicho ndio kilichonifanya niwe kimya kidogo,kunavitu vingi nilikuwa nafikiria jinsi kuviboresha ikiwa na kuliingilia soko la kimataifa babu, natarajia kutoa single mwezi july tarehe nitaitangaza baadae kaka

S na S: Single hiyo umemshirikisha nani babu? ni ya kiswahili au?

Solo: Nyimbo nitakazo toa kuanzia sasa zitakuwa na version mbili moja ya kiswahili na remix ambayo itakuwa ya kiingereza

S na S: Je mkubwa unazungumziaje wanamuziki wa Kenya ukilinganisha na wenzao wa Tanzania ambapo wengi wa Kenya wanapata shoo nyigi za nje, je hii ni kusema Genge inakubalika zaidi ya Bongo Flava kaka?

Solo hakuna babu,show ni connections na jinsi gani wasanii wanajiuza,inabidi wabongo tutumie sana mitandao katika kunadi kazi zetu…..kwa hiyo matumizi ya computer ni muhimu sana katika kujitangaza babu na nijukumu la wabongo walio nje ya nch kusupport vipaji vya home,kama Uk wapo baadhi ya maDj wakibongo wanajitahidi sana katika kuutangaza mziki wetu kuna jamaa wanajiita bongo flavour familly,Dj Jimmy blanks,kina Dj habib,Dj lee flex…..etc, ni jukumu la wabongo walio na michongo kumegeana babu

S na S: Kuna upande mwingine hata wewe uliupigia kelele sana kuhusu Wasambazaji kule nyumbani Bongo ambao bado ni hao hao kuna jinsi kweli ya kuepukana nao “wadosi” kama ipo kwa jinsi gani?

Solo: ipo dawa ni kuwa na umoja na kuwatosa,pia tunaweza kuuza kazi zetu kwa njia ya mtandao….kama itunes, beta record na store nyingine nyngi tu za muziki

S na S: Hapo utakuwa unalizungumzia soko la nje je kwa mikoani ambapo kazi zenu zinanunuliwa zaidi na jijini ambapo ndio kuna soko kubwa lakini ni rahisi kupata nyimbo za mwanamuziki kwa mtu ku burn CD tena toka kwa wanamuziki unasemaje kwa haya mawili?

Solo:ndo maana nikasema umoja muhimu!naamini wanamuziki sisi ndio waathirika wa hili,kama tutakuwa na msimamo kwa pamoja si kazi kupata suluhisho la hil, kama wadosi watakataa kubadilika ni kususia kuuza kazi zetu kwao naaamini watajitokeza tuwatu wa kununua kazi zetu,au tunaweza kuweka utaratibu wa kuuza wenyewe vyote inawezekana muhimu ni kujipanga….nakumbuka Mr Two alishawahi kukomaa na kusambaza mwenyewe na Kilimanjaro band kama sikusei

its all possible..pia wabongo waelimishwe umuhimu wa kununua nakala halisi na si zakukopy,ili kusupport vipaji vya nyumbani,la sivyo itabaki majina tu yanavuma mifuko imetoboka

.

.

“Traveller” Mitaani ughaibuni.

S na S: Je umewahi kuwaza kuwa na Chama chenu ili muwe na sauti moja? unafikiri hili linawezekana?

Solo: unajua tatizo njaa babu kwenye njaa hakuna msimamo…..vyama huwa vinaanzisha ila havidumu na huwa havina nguvu…..sababu mnaweza kupanga hili,baadhi wakazunguka! sauti moja ndo inatakiwa ya wasanii nchi nzima. Tukae chini na wadosi watueleze tatizo nini?kazi zinavuka mpaka mipaka hakuna mjadala wa hilo!, pia nimeanzisha blog yangu ili kuwapa latest mashabiki zangu pamoja na habari zingine za burudani ndani na nje ya bongo http://www.solothang.blogspot.com.

S na S: Elimu na usanii haviingiliani ila vinategemeana pia je kuna mabadiliko yeyote unayahisi kwa kipindi kile na sasa baada ya vidato kadhaa kimuziki?

Solo: makubwa kaka,am grown up now ha ha with wife and son,kuishi ngambo pia kunakupa experience kubwa kila ninachokiwaza na kwa faida yangu na family, which means siwazi kunyonywa tena.
S na S: Hongera sana kwa hilo!! Kila mtu anafikiria kuwekeza kwenye Studio na kwa sasa kila kona kuna Studio Dar hadi limekaa njema hili mkuu?
Solo: Studio kila kona poa muhimu kama zitakuwa na viwango tu babu,pia inaleta ushindani na ni mzuri kibiashara.

.

.

“when it comes to Mic,Rhyme!! man am baaad..”

S na S: Je una lolote la kuwaeleza MAshabiki, Wanamuziki wenzio, au hata wadau wa Muziki hata “wadosi”?

Solo; Mashabiki kwanza nawaomba msamaha kwa ukimya,pili wakae mkao wa kula soon tunaanzia July kwa washkaji ni muhimu kuwa na plan B,wasitegemee tu mziki kama kitega uchumi,wa Invest pesa wanayoipata ili kuwa na nyenzo nyingine ya kuingiza kipato,maisha mchakamchaka, fani yetu haina pension,so we need to work hard for the future,na nawatakia kila la kheri

S na S: Asante kaka kwa muda wako kila la heri kwenye shughuli zako

Solo: Asante sana kaka nawe pia.

Pata burudani ya Solo thang na Q Chilla kwa kubofya hapa