Vijana tuamke tuwe wabunifu kwenye biashara – Mange
Kampuni ya Kizalendo imezindua bidhaa za urembo kwa ajili ya kina dada. Kampuni hiyo ambayo inajishughulisha na bidhaa za nywele kwa akina dada ilifanya uzinduzi uliofana kwenye Hotel ya Kempisk tarehe 11 July na kuhudhuriwa wageni wengi waalikwa ambapo bendi ya Machozi ilitumbuiza.
Aidha akiongea na Spoti na Starehe Mmiliki wa Bidhaa hizo Mange Kimambi amesema kuwa kwa sasa bidhaa hizo za Malkia anatengenezea China ila mipango iliyopo ni kuhamishia kiwanda Tanzania si tu kwa soko la ndani bali hata soko la nchi jirani pia, Pia Mange aliwashauri vijana kuzichangamkia nafasi za biashara zilizopo nchini kwani Tanzania ni nchi changa ambayo ina nafasi nyingi za kujikwamua kwa wajasiriamali, “Kwa sasa tanzania kuna opportunities nyingi sana kwa vijana, ni kwasisi wenyewe tu kuamka,kuziona na kuzifanyia kazi” alisema Mange.
Pia nilimuuliza nini kilichompelekea kuamua kujikita kwenye biashara hii “…Mimi binafsi huwa nakuwa disappointed napoona kila dada anaefungua biashara anaamua tu kumuiga mtu na kufungua boutique, lazma tuwe creative ili tuendelee”
”…Kilichoniingiza kwenye biashara hii ni mapenzi yangu kwenye urembo wa mwanamke ha hususan nywele,napenda sana nywele, na niliona nataka kuleta nywele zenye quality bora zaidi kwa bei ya chini zaidi ili kuwapa wanawake wote Tanzania nafasi ya kujihisi kama MALKIA, ndo maana na nywele zinaitwa MALKIA” Alimalizia.
Spoti na Starehe inachukua nafasi hii kumpongeza mjasiriamali na kumtakia kila la heri kwenye maendeleo ya biashara.
Baadhi ya watu waliohudhuria sherehe hiyo ni Miriam Odemba, Lisa Jensen, Basila Mwanukuzi, Lady Jay Dee na Machozi walitumbuiza, Gadna Habash, Chiz Benz, Ali Remtula, Khadija MWanamboka na wengineo wengi kwenye mizania ya urembo na burudani au Spoti na Starehe.
Pata habari kwa Picha juu ya yaliyojiri kwenye uzinduzi huo.
Wanadada Mamodel wakiwa kwenye Mstari wakati wakionyesha kwa waalikwa mitindo mbali mbali ya nywele za Malkia
Mmiliki wa Malkia akiongea Machache Kwenye Uzinduzi huo
Ma model wa Malkia wakiwa tayari kwa ajili ya kupita mbele ya waalikwa wakati wa uzinduzi huo.
Chid Benzi alikuwepo pia
Akina dada toka Fanaka EVents wakiuza bidhaa za Malkia kwenye Uzinduzi huo kwenye Hotel ya Kempisk
Machozi Band waliburudisha uzinduzi huo.
wageni mbali mbali walialikwa kwenye usiku wa uzinduzi huo ambao alifana vilivyo.
Model akipita Jukwaani wakati wa uzinduzi wa Malkia Kempisk
ONYO: Picha zote kwa hisani ya Malkia, Hairuhusiwi kutumia picha hizi bila idhini ya Malkia.