Kim and The Boys azikwa

December 17, 2009

kim

Marehemu Abdulhakim Magomelo aka Kim  Pichani wakati wa uhai wake.

Picha hii ilipigwa mwaka 1991 wakati wa harusi yake.

image

DJ maarufu nchini aliyewahi kutamba katika medani ya muziki jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla, Abdulhalim Magomelo ‘Kim & The Boys,’ hatimaye amezikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar Es Salaam jioni hii.

Kim ambaye alifariki majuzi kwa maradhi ya moyo. alijizolea umaarufu jijini na nchini kwa ujumla.

Wapenzi na mashabiki wa burudani, wataukumbuka mchango wake katika muziki na ucheshi wake, Kim ni Dj aliyewika vilivyo kwa umahiri wa kazi yake katika madisko mbalimbali jijini Dar es Salaam kama Mbowe Disco, na Silver Sands Disco. Vile vile Kim ni muasisi wa shindano la Yo-rap Bonanza.

Kwenye mazishi na shughuli nzima ya msiba watoto wote wa mjini walikuwepo, vijana wazamani, kuanzia wanamuziki wa kizazi kipya, ma Dj wa zamani na wapenda burudani wote.

Kim ndiye aliyeyatoa majina kama Black Moses (RIP), Ommy Sidney , Othman DigaDiga, Saleh Jabir, II Proud (Sugu / Mr II) pamoja na wengine wengi.

Kim ameacha mke na watoto watatu.

Ma DJ wa zamani wakiwa katika picha ya pamoja mara mbaada ya mazishi ya DJ mwenzao Abdulhakhim Magomelo DJ Kim and the Boy katika makaburi ya kisutu jijini Dare es salaam mazishi hayo yamefanyika saa kumi jioni na yamehudhuriwa na watu maarufu mbalimbali.

Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi. Amina.

Picha zote na Full Shangwe


Mambo ya Sweet Easy

December 17, 2009

image


Nonini alipokuwa Malaysia ….

December 16, 2009

Mwanamuziki Nonini toka kenya hivi karibuni alifanya onyesho mwanana Jijini Kuala Lumpuer nchini Malaysia na kuhudhuriwa na mamia ya mashabiki.

Nonini ni mwanamuziki wa pili toka Africa Mashariki kufanya Onyesho nchini Malaysia, wa kwanza alikuwa mtanzania Ambwene Yessaya aka AY.

Aidha Nonini alitembelea chuo kikuu cha Limkokwing na kutunikiwa heshima ya Balozi wa Vijana.

image

image

image

image

image

Picha zote na Walter Rweyemamu wa Limkokwing University Malaysia.


Timu nzima ya Eritrea yaingia mitini Kenya

December 15, 2009

image Maafisa wa shirikisho la soka nchini Kenya wanasema kuwa wameanzisha uchunguzi kwa madai kuwa timu nzima ya soka ya Eritrea imetoweka.

Tovuti ya chama cha upinzani nchini Eritrea imechapisha habari kuwa timu hiyo ilitoweka baada ya kucheza mechi yao ya robo fainali ya kombe la mataifa ya Afrika Mashariki na kati CECAFA jijini Nairobi.

Imearifiwa kuwa kati ya timu nzima ya Eritrea iliyokwenda Nairobi ni kocha pekee Negash Teklit na kanali wa kijeshi anaehusika na michezo ndio wamerejea nchini Eritrea.

Timu ya Eritrea ilipata matokeo mazuri katika mechi za awali hata kufaulu kuingia robo fainali . Hata hivyo wachezaji walitoroka baada ya kucheza mechi yao ya mwisho dhidi ya Tanzania bara.

Ubalozi wa Eritrea nchini Kenya umepuuza madai hayo kama ni propaganda tupu.

Na BBC


Wenger: Arsenal yarejea kuusaka ubingwa

December 15, 2009

image

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger anamatumaini timu yake imerejea katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya soka baada ya maajabu waliyoonesha walipoilaza Liverpool.

Gunners kama wanavyojulikana, kwa sasa wapo pointi sita nyuma ya vinara wa ligi hiyo Chelsea baada ya bao la ushindi la Andrey Arshavin kipindi cha pili kuwahakikishia pointi tatu muhimu.

Wenger wakati wa kipindi cha mapumziko alikuwa amewakasirikia wachezaji wake kupindukia na nahodha wa timu hiyo Cesc Fabregas akaeleza tangu amfahamu Wenger hajawahi kumuona katika hali hiyo.

Alipoulizwa iwapo timu yake imerejea katika mbio za kuusaka ubingwa, Wenger alisema kimahesabu ndio na kimawazo inawezekana.

Nahodha Fabregas aliongeza kusema wakati wa mapumziko ukali wa Wenger ulisaidia na akamtaka awe mkali mara kwa mara na ikiwezekana zaidi.

Siku ya Jumamosi Chelsea walilazimishwa sare ya mabao 3-3 na Everton huku Manchester United nao wakikubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Aston Villa pale Old Trafford hali iliyoongeza ushindani katika pambano la Jumapili baina ya Liverpool na Arsenal nao wakiwania ubingwa.


Gamboot dance; Muziki ulioasisiwa na watumwa migodini!!

December 15, 2009

Unapozungumzia muziki wa Afrika utaongelea Muziki wa Kongo ambao kwa kiasi kikubwa umefanikiwa kutoka nje ya bara hili lakini ukiwauliza wenyewe hasa watakwambia Muziki wa Kusini mwa Afrika ndio hasa unawakilisha bara la Afrika kutokana kuenzi utamaduni wa muafrika.

Leo tutaangalia Gamboot Dance toka kusini mwa Afrika.

Gumboot dance ni aina ya muziki ambayo ni maarufu sana kusini mwa Africa, ikiwa imejizolea umaarufu huku Afrika ya Kusini, Botswana na hata Zimbabwe.

Gumboot ilianzia Africa ta kusini kwenye machimbo ya Dhahabu miaka hiyo kukiwa na utumwa ambapo waafrika walilundikwa kwenda kufanya kazi machimboni, Kutokana na hali ya machimboni walikuwa walivaa Boot miguuni ili kujikinga na matope, inasemekana walikuwa wakipewa muda mchache sana wa kupumzika na katika muda huu ambao walikuwa wakiutumia kupata chochote watumwa hao wa migodini walitumia kujisahaulisha machungu ya kazi ngumu kwa kucheza na kuimba na walicheza huku wakiwa wamevaa boot zao miguuni, katika kucheza huku boot zile zilitoa mlio wa aina yake na kufanya huo kuwa mrindimo wa Muziki ule.

Wapo wanaosema kuwa katika Machimbo yale watumwa hawa hawakurugusiwa kuongea na hivyo kuwa wakiwasiliana kwa kutumia ishara kwa kupiga boot zao na hiyo kuwa chanzo cha aina hii ya dance.

Wapo wanamuziki wengi ambao walishafanya hata maonyesho Ulaya akiwamo Culture and Spears toka Botswana. Ambapo yeye ameongeza vionjo kama kinanda na ala nyinginezo na kuunogesha zaidi muziki huu.

Mandhari inayotumiwa mara nyingi ni kuonyesha maisha halisi ya mtu wa kawaida kabisa, na hata nyimbo zenyewe zina reflect utamaduni zaidi wa Muafrika. Kwenye nyimbo hizi mara nyingi ni majigambo ya kuonyesha ni jinsi gani utamaduni wetu unanguvu na kujivunia hilo.

Pamoja na ukweli kuwa aina hii ya muziki imenogeshwa na vyombo vya kisasa bado uchezaji wake unafuata misingi ya gamboot hata kama wachezaji hawajavaa boot na utamaduni ndio huzingatiwa ikiwa ni kuvaa kitamaduni na nyimbo zake huwa zinakusudiwa kufundisha zaidi kwani zina story fupi fupi.

Upangaji wa sauti na uchezaji wa kiustadi ndio vinavutia katika kuangalia video hizi ambapo mipigi yake imepoa na kutoa nafasi kwa sauti kutawala zaidi, aina hii ya Gumboot dance imekuwa maarufu zaidi huko Botswana ambako ni maarufu kama Tseswana Dance ambapo wao wamechukua zaidi uchezaji na kuongeza ala za muziki na kuimba zaidi, Wabotswana wanajulikana kwa mauombo yao mazuri (maumbo ya kiafrika) na hivyo kunogesha zaidi uchezaji wao (angalia video ya pili) ilihali kwa Wazuru wa Afrika ya kusini wao bado ni rhythim ya boot inatawala zaidi.

Pata kionjo hapa hii nakwenda pia kwa mwanangu kipenzi Baby Glory anawapenda sana hawa.


HOLD ON ya Mr II kiwango!

December 15, 2009

Kwa mtu anayejua muziki wa Bongo Flava ulipoanzia atakubaliana na mimi hii ndio ilikuwa Style yake hasa kabla “wadhamini” na wenye Radio zao hawajabadilisha muziki na kuwalazimisha watu kama Juma Nature na Prof Jay kuimba.

Nadhani unaelewa namaanisha nini ila hili lina muda wake na siku yake ambapo tutaangalia kwa mapama mapinduzi mazima ya muziki huu kwani hivi karibuni Spoti na Starehe ilifanya mahojiano na mwanamuziki Juma Kasim aka Sir NAture na katika alilolizungumzia sana ni kuhusu mabadiliko mazima na kulazimishwa kuimba kitu ambacho sio identity yake eti tu style yake haiuzi!!.


KINGS AND QUEENS-AY‏, Video inayokuja kwenye Ubora wa kimataifa.

December 14, 2009

 

image

King and Queen, kama unakumbuka The King of zamunda basi ngoja uone Video hii ya Mwanamuziki AY ndio utakubali kuwa kijana kajipanga.

Hizi ni baadhi ya picha  zilizochukuliwa katika video  mpya inayoitwa KINGS AND QUEENS niliyomshirikisha JOKATE & AMANI kutoka KENYA.Wimbo umetayarishwa na na Super Producer HERMY B ndani ya Studio ya B.Hitz Music Group na kufanyiwa video na OGOPA DEE JAYS toka Kenya.Video ilifanyika Jijini Nairobi na itaanza kuruka wiki ijayo MTV BASE na vituo vingine ndani ya Afrika Mashariki.

image

“Wimbo huu nimejaribu kufikisha fikra zangu kuwa MWANAMKE WA KIAFRIKA NDIE BORA KABISA NA NAJISIKIA FAHARI SANA KUZALIWA NAO NDANI YA BARA MOJA” alisema AY kwenye taarifa yake kwenda kwa wanahabari na Ma blogger mbali mbali ikiwemo Spoti Starehe.

image

“Kama nilivyosema TUNAUFUNGA MWAKA NA KUUFUNGUA NA MZEE WA COMMERCIAL basi subirini mambo makubwa toka kwa MZEE WA COMMERCIAL AMBWENE YESSAYAH MWENYE KIU YA KUWAKILISHA TANZANIA NA AFRIKA YA MASHARIKI KWA UJUMLA KATIKA ANGA ZA MBALI…” Aliongeza AY

Binafsi namkubali sana kijana AY kwa ubishi anaoonyesha kwenye game, wapo walioanza na waliishia njia na wapo walioanza na wapo kwenye safari, Muziki ni Jihadi, unatakiwa kujitolea na endapo utaheshimu kazi yako basi unayonafasi ya kufika mbali.

Big up kaka unaonyesha ubunifu na ukomavu kwenye fani na kuwa mfano wa kuigwa.


Kipanya wa Leo

December 14, 2009

image


Fulham yawakera Waghana kumng’ang’ania Pantsil

December 14, 2009

image

Chama cha soka cha Ghana(GFA) kimekasirishwa na matamshi ya meneja wa klabu ya soka ya Fulham ya England.

Roy Hodgson amesema anatumai mlinzi wa timu yake John Pantsil ataichezea Fulham tarehe 28 mwezi wa Desemba.

Hodgson amesema ni utovu wa nidhamu unaooneshwa na mataifa ya Afrika yanayovitaka vilabu ya Uingereza kutaka wachezaji waruhusiwe tarehe 27 wakati wakijua fika vilabu vyote vina michezo tarehe 28.

Lakini GFA kimesema Pantsil ni lazima aruhusiwe kuijiunga na timu ya taifa ya Ghana.

Fulham katika moja ya michezo ya Ligi Kuu ya England itapambana na vinara wa ligi hiyo Chelsea katika tarehe hiyo na Hodgson amesema Pantsil atacheza mechi hiyo.

Katika taarifa yake mwalimu huyo wa Fulham amesema iwapo FIFA hawataingilia, watamtumia Pantsil tarehe 28.

Sheria za Fifa zinasema vilabu havina budi kuwaachilia wachezaji wao siku 14 kabla ya kuanza mashindano ya kimataifa yanayotambuliwa.

Fifa inaweza kuipokonya poiti ambazo Fulham watazipata katika mchezo huo na Chelsea iwapo Pantsil atacheza pambano hilo.

Mchezaji mwengine ambaye yupo katika mzozo baina ya klabu na nchi ni Madjid Bougherra kutoka Algeria.

Klabu yake ya Rangers inajaribu kuiomba Algeria imruhusu kucheza mechi dhidi ya Celtic tarehe 3 mwezi wa Januari.

Na BBC


Arsenal waambia Liverpool “Maatu”, Waichapa 2-1

December 14, 2009

Andrey Arshavin

Arshavin ameiwezesha Arsenal kuingia nafasi ya tatu katika ligi kuu ya Premier

Kwetu sisi wandamba mtoto akilia unamyamazisha kwa ukali na neno Maatu!!

Andrey Arshavin alifunga bao la kusisimua, na kuiwezesha klabu ya Arsenal kuingia katika nafasi ya tatu katika ligi kuu ya Premier, kwa kuishinda Liverpool magoli 2-1.

Arsenal ilikuwa imeachwa nyuma baada ya Liverpool kufunga kwanza, kupitia Dirk Kuyt, katika dakika ya 41.

Lakini kweli kutangulia sio kufika, na wenyeji katika uwanja wao wa Liverpool walilegeza kamba baadaye.

Manuel Almunia aliiokoa Arsenal baada ya kombora la Fernando Torres, na huku Liverpool wakidai penalti ambayo mwamuzi alikataa katukatu.

Kimakosa, Glen Johnson aliuelekeza mpira kutoka kwake Samir Nasri katika lango lake mwenyewe.

Mkwaju wa Arshavin kutoka yadi 14 hatimaye uligonga mwamba, huku ukielekea wavuni na kuiangamiza Liverpool. Kwa matokeo yangu Uncle Dee, Robert Mwafirika aka Batty, Papaa Six na wengineo nadhani mmekuwa na jumapili njema kabisa ila pole zake kaka Dulla, Michuzi, Mbango, Kimati poleni sana mpira si dini badilisheni jamani khaaa!!!


Mazembe hoi mashindano ya dunia

December 14, 2009

image

Mshambuliaji Denilson aliifungia mabao mawili Pohang Steelers ya Korea Kusini iliyokuwa nyuma kwa bao moja na kufanikiwa kuwalaza mabingwa wa Afrika TP Mazembe mabao 2-1 katika mashindano ya ubingwa wa dunia kwa vilabu.

Mabingwa hao wa Afrika walitangulia kufunga katika mashindano ya Abu Dhabi kwa bao lililofungwa na Mbeza Bedi kwa shuti kali la mbali.

Denilson aliwaswazishia mabingwa hao wa Asia kwa kichwa dakika ya 50 ya mchezo.

Mbrazil huyo aliwamaliza kabisa Mazembe zikiwa zimesalia dakika 12 kabla ya kumalizika mchezo kwa kupachika bao la pili.

Pohang Steelers sasa watapambana na mabingwa wa Amerika Kusini Estudiantes ya Argentina katika hatua ya nusu fainali siku ya Jumanne.

Mazembe nao watacheza siku ya Jumatano kutafuta nafasi ya mshindi wa tano.

Watacheza na timu itakayopoteza siku ya Jumamosi katika robo fainali baina ya mabingwa soka wa nchi za Ocenia timu ya Aukland City ya New Zealand na Atlante ya Mexico wanaowakilisha Kaskazini na Amerika ya Kati


Siku zahesabika VETO kuzinduliwa!

December 14, 2009

image

Albamu ya 10 ya mwanamuziki Joseph Mbilinyi aka II Proud amesema kuwa maandalizi yote yote yamekamilika na wasanii wote wanaotazamiwa wamesha confirm kushiriki.

akiongea na Spoti Starehe Mr II amesema kuwa washiriki wote wako poa na watu wasubiri tarehe 24 kuamkia 25 mkesha wa Christmass pale Diamond Jubilee.

Spoti starehe iko pamoja na ni mshirika wako katika habari za mdau Mr II.


Matokeo:Ligi kuu England 12/12/09

December 13, 2009

image

Matokeo ya Ligi Kuu ya England kwa michezo iliyochezwa siku ya Jumamosi tarehe 12/12/09.

Birmingham 1-0 West Ham

Bolton 3-3 Man City

Burnley 1-1 Fulham

Chelsea 3-3 Everton

Hull 0-0 Blackburn

Stoke 2-2 Wigan

Sunderland 1-1 Portsmouth

Tottenham 0-1 Wolves


JB Mpiana na Tshala Muana kuwasha moto Ubungo Plaza Desemba 18

December 11, 2009

Below are ticket Selling Point

we will start selling them on Monday 14th December 2009 at 9:00am

Dar es Salaam:

Jackie’s Bar

Steers – mjini

Steers-Millennium towers

Steers– Milimani City

Zizzou Fashion – Sinza Africa Sana

Engen Petrol station – Mbezi

Kampuni ya Sigara – Pugu road

Arusha:

-Nikki’s Pub-Njiro

Digital Entertainment– Shoprite

Tawi la Kampuni ya Sigara – Arusha

For more information please contact Club E Team at telephone number 078 7333315

m45

Pichani JB Mpiana akiwa na kundi zima la Wenge BCBG akitumbuiza kwenye Onyesho huko Belgium mapema mwaka huu.


Lyrics ya BED AND BREAKFAST ya AY

December 11, 2009

Intro:
Bed and Breakfast X 4

1st Verse:
Mambo yamejipa yaani BANG!
Muda wa kupumzika umefika umecome again,
Ndio maana watu wanashine,
Ndio maana kila kona nayopita watu ni wengi,
Ukidelay utapotea,
Mtoto anajiachia kama ameshapata mmea,
Kwenye bo body yake mi ndo sarveyer,mzeiya
Nazidisha miguso anadai (endelea)
Sa naona club haifai,
Hata washkaji wangu nishawaambia bye
Mtoto ashalalia bega mi naride
Namuuliza anataka nini kwangu
BED AND BREAKFAST……..

CHORUS:
Ebwana mi nampa (BED AND BREAKFAST)
Hataki vingine anataka (BED AND BREAKFAST)
Aaah aaaah (BED AND BREAKFAST)
Satisfaction guaranteed (BED AND BREAKFAST) X2

2nd VERSE:
Tushafika mtoto nae yupo front,
Bila kuchelewa mi nalock door,
Kama tumeambiana simu ziko off,
Chumba ndo cha baridi twapeana joto,
Mlaini kama bamia,mtamu ka lasagna,
Slow but sure si kumvamia,
Room sound proof so hutomsikia,
Tukipeana huku nikimsmack,
(You and I) Bed moja mtu mbili tu,
(You and I) Sink moja povu mpaka juu
(You and I) YOU x7 you and I aaaaah
BRIDGE
I don’t care hata simu ikiwa ON sipokei,
I don’t care hata waseme nini kwako siongei
I don’t care,kwako sitapretend,
I don’t care,we ni duu mi ni rudebwoy
I don’t care hata kama nikikupa overdose,
I don’t care,I don’t care…haaa haaaa..
CHORUS: X 2
BRIDGE:
You took me to Paradise
You’re the one unayenijazz,
Hook me with one more dose,
Pleaseee ONE MORE DOSE …. X 2

3rd VERSE:
Karibu himaya ya Rudebwoy AY,
Sura ya upole ila namba haifai,
Anadai…
Nimpe zaidi huku anacry,
Nikirefuse basi she gonna die…
CHORUS: X 2

Mwanamuziki Ambwene YEssaya aka AY hivi karibuni aliachia kibao songi jipya na tayari imeanza kushika vilivyo kwenye baadhi ya vituo vya redio, Wimbo huo unaokwenda kwa jina la Bed and Breakfast umeimbwa na AY akimshirikisha mwanadada mmoja ambaye mwenyewe alisema kuwa mwanadada huyu hapendi kujitangaza ila AY anamkubali kuwa yuko Juu.

Producer wa wimbo huo ni Hermy B na umetengenezwa kwenye Studio za B. Hitz Music Group na Mastering imefanywa na Lucas wa Ogopa Dee Jays wa Nairobi huko nchini Kenya. Kuisikiliza basi bofya HAPA


JB na Wenge BCBG walivyoichengua Zambia

December 10, 2009

image

Mwanamuziki JB Mpiana na wanenguaji wake wa Wenge BCBG akiongoza mashambulizi ya kikosi kizima cha Wenge BCBG huko Zambia hivi karibuni.

image

image

Dada huyu anaitwa Dina alijitambulisha kama Shabiki nambari One wa JB Mpiana na alionyesha kupagawa na show nzima ya mzee mzima.


Michael Essien kukosa mchezo na Everton

December 10, 2009

image

Na BBC

Kiungo wa Chelsea Michael Essien atakosa mchezo wa siku ya Jumamosi na Everton baada ya kuumia goti walipocheza na Apoel Nicosia.

Essien alitoka nje ya uwanja akichechemea kipindi cha kwanza katika mchezo ambao timu hizo zilitoka sare ya mabao 2-2 kukamilisha hatua ya awali ya ligi ya mabingwa wa Ulaya katika uwanja wa Stamford Bridge.

Mwalimu wa Chelsea Carlo Ancelotti amesema Michael anakabiliwa na matatizo ya mguu na watamuangalia zaidi wiki ijayo.

Hata hivyo ameonesha matumaini yake kwamba tatizo si kubwa sana. Lakini akasema anadhani hatacheza siku ya Jumamosi.

Essien alifunga bao zuri la kusawazisha kwa Chelsea baada ya timu hiyo ya Apoel Nicosia kuongoza mapema katika dakika ya sita ya mchezo.


Owen amkosha Ferguson kwa mabao matatu

December 10, 2009

image

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amemsifu Michael Owen baada ya kupachika mabao 3 wakati timu hiyo ilipowalaza Wolfsburg 3-1.

Manchester United imefanikiwa kuongoza katika kundi lake la B baada ya Owen kupachika mabao saafi huku akiwa na matumaini ya kuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ya England kwa ajili ya kombe la dunia mwaka 2010.

Ferguson amesema Owen ameonesha kiwango kizuri sana, umaliziaji wake na namna alivyokuwa akitafuta nafasi za kufunga ulikuwa ni wa kuvutia.

Manchester United ikicheza na walinzi wasio wa timu ya kwanza nchini Ujerumani, tayari ilikuwa imefuzu katika timu 16 za hatua ya mtoano, ilikuwa inahitaji sare tu imalize kinara katika kundi hilo na kwa muda mrefu walikuwa wakitawala mchezo.


Sandra Lina mcheza show wa Wenge BCBG aliyeponzwa na Didi Kinuani.

December 10, 2009

image

Anaitwa Sandra Lina, huyu aliwahi kuwa Mcheza Show wa JB Mpiana na alifukuzwa kwenye bendi baada ya kubainika kuwa alipokea pesa (alisaidiwa) na Didi Kinuani jambo ambalo lilimkasirisha sana JB Mpiana.

Baada ya kufukuzwa Sandra ambaye alikuwa na urafiki mkubwa sana na Bibiciya Mfwengi ambaye kwa wakati huo alikuwa ni kiongozi wa madancer wa Wenge Musica Maison Mere baada ya kubwaga manyanga akitokea kwa Koffi Olomide, (lakini kwa sasa Koffi amefanikiwa kumrejesha tena kwake). Bibiciya alimuombea Sandra ili ajiunge na WMMM lakini mwanamuziki mwingine na muandamizi wa Wenge BCBG Seguin Mignon alimpigia simu Werason na kumtahadharisha kuhusu sakata hilo na mpango mzima ukafa.

Sandra ambaye ni yatima alihangaika na wakati fulani alikimbilia Ivory Coast na kujiunga na bendi moja ya huko hatimaye ameibukia kwenye uimbaji na kutoka na kibao hiki ambacho aliki dedicate kwa Didi Kinuani.

Inasemekana kuwa Sandra amesaidiwa kwa kiasi kikubwa na Didi Kinuani ambaye pia ilisemekana kuwa aliwahi kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi.

Mkorogano wa JB Mpiana na Didi Kinuani ulijitokeza pale tajiri huyo ambaye ni mshirika mkubwa wa Presidaa Kabila kuamua kumchukua mke wa JB Mpiana na kufunga naye ndoa, jambo ambalo hata wanamuziki wenzie na wapenda burudani pia hawakulifurahia.  Werason kiongozi wa WMMM binafsi alikataa kwenda kutumbuiza kwenye harusi hiyo licha ya donge kubwa alilotengewa kwa madai kuwa yeye alikuwa mshenga wakati JB Mpiana akienda kumchumbia mwanamke huyo, na kuongeza kuwa tofauti zao ni katika burudani tuu na si kimaisha.

Pata kibao chake Sandra.