Zawose akonga nyoyo za mashabiki – Rainforest Music Festival – Malaysia

July 17, 2009

image

Tamasha la Rainforest ambalo linakusanya wasanii toka kila pembe ya dunia hapa Malaysia limefanyika kwa siku tatu huku Africa ikiwakilishwa na mwanamuziki Hukwe Zawose. Tamasha la mwaka huu lilikuwa na vikundi vingi lakini kwa mujibu wa magazeti ya Malaysia Zawose alifanikiwa kukonga nyoyo za mashabiki na washiriki wenzake hasa kwa mavazi yao pampja na jinsi wanavyoimba na kupiga ala zao za asili.

Tamasha la Rainforest Music World Festival linafanyika kila mwaka katika jimbo wa Sarawak na linafanyika katika misitu ya Santubong na kujuisha vikundi mbalimbali toka duniani kote likiwa na sura ya utamaduni zaidi likiambatana na workshop mbalimbali.

image

kwa habari zaidi gonga hapa na hapa

image


Distance ya Lady Jay Dee kwa waliombali na wapenzi wao!!

July 17, 2009

Ijumaa ya leo naomba nikurudishe nyuma kidogo nikukumbushe kibao cha Lady Jay Dee – Distance na kibao hiki kwa wale wote wanao practice Long  Distance Relationship nikiwemo na mi mwenyewe!! tunawaburudisha na kuwariwaza ki spoti.


MAKING THE VIDEO YA WIMBO MPYA "TEJA" LADY J D

July 17, 2009

Katika harakati za kukamilisha album yake ya Tano, ambayo inaitwa YA 5…hivi karibuni mwanamuziki Lady Jay Dee alikuwa busy na shooting ya baadhi ya nyimbo kwenye albamu hiyo ya Tano, Moja ya wimbo uliomo humo ni huu unaitwa Teja, sina mengi ya kuongea picha zinaongea zaidi na subiri uone Albamu hiyo toka kwa mwanamuziki Jay Dee akiwa ni kati ya wanamuziki wachache walianza kwa moto na kuendeleza vilivyo.


Mambo ya Sweet Easy weekend hii

July 17, 2009

image


Kina Klothing yafungua duka la “PAMBA” mtandaoni!

July 17, 2009

image

Salaam kwa wadau wote wa blogu hii.

Kina Klothing ina furaha kuwafahamisha kuwa tumefungua duka letu mtandaoni na unaweza sasa kununua Tshirt moja kwa moja kupitia www.kinaklothing.com

Kina ni kampuni mpya ya nguo ambayo inawakilisha Bongo na Afrika kwa ujumla. Kwa utambulisho tumetoka na kollektion inayoitwa Uhuru St. kwa sababu neno uhuru linabeba sababu nzima ya sisi kuanzisha Kina.

Vilevile hii ni lebo ya mavazi ya kitaa na Uhuru ni mtaa wa kwanza katika mfululizo wa kollektion zitakazobeba majina ya mitaa mbalimbali ya Bongo na Afrika kwa ujumla.

Kama kauli mbiu yetu inavyosema “Vitu vyetu. Kivyetu” basi ndio tunavyotarajia kuendesha lebo yetu, yaani full uhuru wa kutengeneza kazi zinazotuwakilisha, kwa namna tunayoamua wenyewe.

Tshirt hizi zimesanifiwa mahsusi kwa ajili ya wabongo na marafiki zao ili kuonyesha kuwa wabongo nao tumo katika medani hii ya design; lakini si hivyo tu, ujumbe unaobebwa na nguo kina ni mchango wetu katika harakati za kujenga madaraja kati ya waafrika barani na diaspora kwa kusambaza na kusheherekea yale yanayotuunga pamoja kama waafrika.

Hata hivyo, katika kollektion hii ya kwanza tumeamua “kucheza kwetu” zaidi, tunatumai utatutunza.

Tutembelee www.kinaklothing.com na tuambie mawazo yako.

Pia usisahau kujiunga nasi katika ukurasa wetu ya facebook (http://www.facebook.com/pages/Kina-Klothing/101720604819) na kutufuatia katika http://www.twitter.com/kinaklothing

Kaa mkao wa kula kwa kollektion inayofuatia, Samora avenue. Iko jikoni.

Amani.

Mkuki na Susan (Kina Klothing)

image

 

image

image

image


AY / FA NA BLACK RHYNO WAZIONA TUZO ZA CHANNEL O

July 16, 2009
AY

katika wale waliotajwa kushindania tuzo za muziki za video za chanall o (chanall o video music awards)siku ya tarehe 14 ya mwezi huu kutoka tanzania tumebahatika kuwa na video ya AY NA FA NAONGEA NA WEWE kundi la BEST DUO OR GROUP, na video ya BLACK RHYNO inayoitwa BLACK CHATTA upande wa BEST HIPHOP VIDEO. Habari kwa mujibu wa Dee Jay Fatty mtembelee kwenye Kali na Mpya za Bongo ambapo utapata habari kadha wa kadha juu ya wasanii wa Bongo. Je wajua kuwa Ray C na Lord Eyes uhusiano umekufa? Gonga hapa usome zaidi.


Werason bado amlilia Bibiciya Mfwengi

July 16, 2009

Inasemekana kuwa mwanamuziki Werason bado analalamika na kukerwa mno na kitendo cha Koffi Olomide kumchukua mcheza shoo wake tegemezi Bibiciya Mfwengi. Habari za burudani zinasema kuwa Bibiciya ambaye awali alikuwa kwa Koffi kabla ya kwenda kwa Werason na kurudi kwa Koffi tena mwaka huu zoezi ambalo lilifanikishwa na mashabiki wakereketwa wa Koffi ambao wanataka kuiona bendi hiyo inawika na kung’ara jukwaani kama zamani.

Akiongea na muandishi Guy guy Mpeye hivi karibuni Werason alisema kwamba katika pigo analolikubali kwa mwaka huu basi ni kuondokewa na mcheza shoo huyo kipenzi cha mashabiki na anayejua kulitawala jukwaa. Bibiciya ndiye alikuwa mcheza shoo wa mwaka kwa mwaka jana.

Pata kionjo cha Bibiciya kwa sasa akiwa na Koffi


Mwingine Wenge BCBG atoka kivyake!!

July 16, 2009

image

Kwa wapenzi wa Wenge Musica na JB Mpiana huyu bwana si mgeni ni mcharaza gitaa anayekwenda kwa jina la Accompagnero Alba ambaye kwa miaka mingi amekuwa na wakongwe Wenge Musica BCBG lakini ameamua kutoka kivyake na albamu hii yenye takribani nyimbo nane. Kama ilivyo kwa wanamuziki wengine kutoka na Solo si kazi ndogo hayo ni maneno ambayo hata Mwanamuziki Muumini aliwahi kusema. Alba kwenye CD hii kwa kweli naweza sema kachemsha kwa mtazamo wangu hakuna wimbo ambao unaweza kumfanya mtu akairudia CD kusikiliza naweza sema kati ya wanamuziki ambao waliamua kutoka kivyao kwenye BCBG huyu kachemka sana kuanzia Alain Makaba, Mwamba Ficare, Werason, Dominguez, Blaise Bulla na wengineo. sina mengi ila itafute hii Albamu na we utupe mchango wako.


Anitha na Zecomedy

July 16, 2009

Jamaa wananiachaga hoi sana hawa hebu na we cheka ki spoti kidogo!!


Video ya Natamani kuwa Malaika ya Jay Dee iko jikoni

July 16, 2009

Wimbo wa Natamani Kuwa Malaika wakwake LAdy Jay Dee unatamba na Video yake ndio iko mbioni inapikwa sasa na kikosi cha Ogopa Dee Jays toka kwa Baba Moi, kazi ya shooting ya Video hiyo ilifanyika hivi majuzi na inatazamiwa kukamilika na kuanza kuonekana mwishoni mwa mwezi huu wa July au mwanzoni mwa mwezi ujao. Vazi la Jay Dee limebuniwa na Ali Remtullah

Jay Dee akiwa na baadhi ya watoto kwenye shooting ya wimbo huo pale Gymkhana Club

 

Marcell na Lucas wa Ogopa Dee Jays kwenye moja ya location Kwa habari na Picha zaidi mtembelee Binti Machozi kwenye Blog yake.


Bidhaa za Malkia zazinduliwa Dar!

July 15, 2009

Vijana tuamke tuwe wabunifu kwenye biashara – Mange

image

Kampuni ya Kizalendo imezindua bidhaa za urembo kwa ajili ya kina dada. Kampuni hiyo ambayo inajishughulisha na bidhaa za nywele kwa akina dada ilifanya uzinduzi uliofana kwenye Hotel ya Kempisk tarehe 11 July na kuhudhuriwa wageni wengi waalikwa ambapo bendi ya Machozi ilitumbuiza.

Aidha akiongea na Spoti na Starehe Mmiliki wa Bidhaa hizo Mange Kimambi amesema kuwa kwa sasa bidhaa hizo za Malkia anatengenezea China ila mipango iliyopo ni kuhamishia kiwanda Tanzania si tu kwa soko la ndani bali hata soko la nchi jirani pia, Pia Mange aliwashauri vijana kuzichangamkia nafasi za biashara zilizopo nchini kwani Tanzania ni nchi changa ambayo ina nafasi nyingi za kujikwamua kwa wajasiriamali, “Kwa sasa tanzania kuna opportunities nyingi sana kwa vijana, ni kwasisi wenyewe tu kuamka,kuziona na kuzifanyia kazi” alisema Mange.

Pia nilimuuliza nini kilichompelekea kuamua kujikita kwenye biashara hii “…Mimi binafsi huwa nakuwa disappointed napoona kila dada anaefungua biashara anaamua tu kumuiga mtu na kufungua boutique, lazma tuwe creative ili tuendelee”
”…Kilichoniingiza kwenye biashara hii ni mapenzi yangu kwenye urembo wa mwanamke ha hususan nywele,napenda sana nywele, na niliona nataka kuleta nywele zenye quality bora zaidi kwa bei ya chini zaidi ili kuwapa wanawake wote Tanzania nafasi ya kujihisi kama MALKIA, ndo maana na nywele zinaitwa MALKIA” Alimalizia.

Spoti na Starehe inachukua nafasi hii kumpongeza mjasiriamali na kumtakia kila la heri kwenye maendeleo ya biashara.

Baadhi ya watu waliohudhuria sherehe hiyo ni Miriam Odemba, Lisa Jensen, Basila Mwanukuzi, Lady Jay Dee na Machozi walitumbuiza, Gadna Habash, Chiz Benz, Ali Remtula, Khadija MWanamboka na wengineo wengi kwenye mizania ya urembo na burudani au Spoti na Starehe.

Pata habari kwa Picha juu ya yaliyojiri kwenye uzinduzi huo.

image

Wanadada Mamodel wakiwa kwenye Mstari wakati wakionyesha kwa waalikwa mitindo mbali mbali ya nywele za Malkia

image

Mmiliki wa Malkia akiongea Machache Kwenye Uzinduzi huo

image

Ma model wa Malkia wakiwa tayari kwa ajili ya kupita mbele ya waalikwa wakati wa uzinduzi huo.

image

Chid Benzi alikuwepo pia

image

Akina dada toka Fanaka EVents wakiuza bidhaa za Malkia kwenye Uzinduzi huo kwenye Hotel ya Kempisk

image

Machozi Band waliburudisha uzinduzi huo.

image

wageni mbali mbali walialikwa kwenye usiku wa uzinduzi huo ambao alifana vilivyo.

image

Model akipita Jukwaani wakati wa uzinduzi wa Malkia Kempisk

ONYO: Picha zote kwa hisani ya Malkia, Hairuhusiwi kutumia picha hizi bila idhini ya Malkia.


Werason na Kalonji wakwaruzana kwa kuibiana wanamuziki!!

July 14, 2009

image

Mwanamuziki Bill Clinton Calonji ambaye kwa wakati fulani aliwahi kufanya kazi na Werason amesema anasikitishwa na amechukizwa sana kitendo cha mwanamuziki Werason kumchukua mwanamuziki wake mpiga gitaa la solo Luxembourg ambaye ametangazwa kujitoa kundi linaloongozwa na Kalonji na kujiunga na Maison Merre. Tatizo kubwa sio kwa mwanamuziki huyo kuondoka bali ni kitendo cha mwanamuziki huyo kuondoka na Gitaa mabalo Kalonji amesema kuwa lilimgharimu kiasi cha Euro 25,000 na kusemwa kuwa gitaa la bei mbaya sana.

Bwana Kalonji ametangaza dhamira yake ya kumchukulia hatua  za kisheria Werason ambaye kwa mujibu wa Kalonji anasema kuwa alimrubuni mwanamuziki wake kufanya alichokifanya alisema Kalonji alipoongea na mtandao wa huko Congo wa Digital Congo dot net.

Hata hivyo werason alikanusha habari hizo na kusema kuwa  Luxembourg bado hajasaini mkataba wowote hivyo kumtaka Kalonji aende huko Zamba Playa wakayamalize, aidha akisema kwa nini ameondoka kwenye bendi ya Kalonji Luxenburg alisema kuwa ameamua kuondoka kwa kuwa Kalonji hana shoo za kutosha.


FROM AY to Ya all.

July 14, 2009

image

Here he comes again, with remixes..yeah remixes not a remix. He is dropping two remixes of the song “LEO” at the same time. He promised satisfaction guaranteed and he is here to deliver to both RnB,rappers n Reggae fans.

1st remix is with Kenyan young Songbird Avril, signed with one Kenya’s biggest record label OGOPA DEEJAYS but she is yet to come heavy on your speakers. This Songstress pleads not to be brokenhearted by this guy(A.Y),that he should be serious if he is asking for her hand with her natural “pleading without pleading” vocals. At the end of the song A.Y decides to satisfy those who haven’t heard him “speed rhyming” for almost 4 years and make a statement that he still got it.

2nd remix is also with Kenyan Diva Wahu with couple of awards backing up his talent. This 2nd remix is in Reggae rhythm, something that just happens to be right in Wahu’s alleys. And in this song the boy and girl have found themselves in love now, and they are exchanging sweet promises with commitment involved but using the language only lovers could understand. Also A.Y has tried to change again, breaking down some dancehall vocals. He might sound funny and different but he manages every kind of musical movement, I guess he is wired that way..can’t figure him out either.

NOMINATE A.Y ON THIS YEAR’S MTV AFRICA MUSIC AWARDS (MAMA’s)
THE 2ND ANNUAL MTV AFRICA MUSIC AWARDS with ZAIN WILL TAKE PLACE IN
NAIROBI, KENYA ON 10 OCTOBER 2009.
VISIT: MTVBASE.COM | FACEBOOK FANPAGE: MTV BASE | TWITTER: TWITTER.COM/MTVBASEAFRICA
Click to listen
LEO REMIX ft Arvil
http://babkubwa.ning.com/songs/details?id=2616971:Track:20291
Click to listen Leo Remix ft Wahu
http://babkubwa.ning.com/songs/details?id=2616971:Track:20293

By Michael Mligwa-BabuKubwa


Michu ya nini kunizoom tokea mbali nimekuja karibu nifotoe sasa!!

July 14, 2009

image

wallah kuna watu wakati mwingine wana vituko hii ilifanywa na mchezaji Robinho kwa mpiga picha huyu, hebu pata picha hapo unamfotoaje?


Kwa wapenzi wa Soka Tuu!!

July 13, 2009

TFF yapata mkataba mnono wa Sh5.85bilioni toka Marekani

July 13, 2009

image

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limepata udhamini wa dola zaidi ya 4,5000,000 (Shilingi bilioni 5.85za Tanzania ) kutoka Kampuni ya +One Fashion USA Corporation ya Marekani.

Mkataba huo wa miaka minane, pamoja na mambo mengine utaliwezesha shirikisho hilo kupata fedha taslimu, motisha nyingine nyingi kwa timu zake mbalimbali ambazo ni Taifa Stars , ile ya wanawake, Twiga Stars na vijana, chini ya miaka 23, 20 na 17.

Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema jana kuwa katika mkataba huo, kampuni hiyo itatoa fedha taslimu, dola za Marekani 50,000 kila mwaka kwa kipindi cha miaka minne ya kwanza.

Aliongeza kuwa kampuni hiyo pia itagharamia michezo minne ya kimataifa ya kirafiki ambayo Stars itacheza ndani au nje ya nchi na kwamba wadhamini hao pia watalipia gharama zote za timu hiyo kusafiri nje.

Kulingana na mkataba huo, pia timu ngeni zitaweza kufika nchini ikiwa ni pamoja na wadhamini hao kuandaa mashindano maalum kila mwaka yatakayojumuisha timu za mataifa manne, ikiwemo Tanzania.

Read the rest of this entry »


Albamu za Koffi tangu 1983 hadi 1990 si mchezo maktaba hii!

July 13, 2009

1983
[image]
[image]
[image]
[image]
1985
Side A: Dounia map – Koffi Olomide / Zonga esika owuti – Josky
Side B: Sainte Aimelo – Djenga K / El bongo nero – Dalienst

[image]
[image]
Side A: Bokilo tosuki wapi?
Side B: Kifyoooto

[image]
[image]
[image]
[image]
1986
[image]
[image]
[image]
[image]
1987
[image]
[image]
[image]
[image]
1988
[image]
[image]
1989
[image]
[image]
1990
[image]
[image]


Tanzania kunufaika na Kombe la Dunia

July 12, 2009

Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga ambaye ameelezea kunufaika kwa Tanzania kutangaza utalii wakati wa mashindano ya Kombe la dunia 2010

SERIKALI inakusudia kutumia Kombe la Dunia mwaka 2010 nchini Afrika Kusini kutangaza utalii kwa kuzipa fursa baadhi ya timu zitakazoshiriki nafasi ya kufanya mazoezi katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Pia, timu hizo zitaweza kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii nchini. Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga Bungeni jana alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake.

Alisema pamoja na michezo, wizara yake imeweka mkakati kutumia fursa zingine mbalimbali kutangaza utalii.

"Ili kuongeza idadi ya watalii nchini, wizara inaendelea kuweka mikakati ya kushiriki matukio mbalimbali ikiwamo miaka 50 ya uvumbuzi wa fuvu za Zamadamu (Zinjathrous), mkutano wa African Diaspora, Kilimanjaro Marathon na maadhimisho ya siku ya Utalii Duniani kutangaza vivutio vya utalii nchini.

"Katika Kombe la Dunia la Soka la Fifa mwaka 2010, baadhi ya timu zitahamasishwa kufanya mazoezi katika uwanja wa taifa zitapata fursa ya kutembelea vivutio vya utalii," alisema Waziri Mwangunga.

Na Mwananchi


Didier Masela karudi BCBG?

July 12, 2009

Hivi karibuni mwanamuziki JB Mpiana alifanya Onyesho kubwa la kufa mtu huko CONGO ambapo lilihudhuriwa na mamia kwa maelfu ya mashabiki ambao walikuwa na hamu ya kumuona hasa baada ya kumaliza ziara ndefu ambayo ilimfikisha Ulaya hadi America na hatimaye kurejea nyumbani, Katika onyesho hilo JB Mpiana alitumia kumtambulisha Mpiga gitaa mahiri wa Didier Masela ambaye awali alikuwa na Wenge Musica na hatimaye kuamua kutoka kivyake, hakuna anayejua kama Masela ameamua kurejea Wenge ama la.

Masela ni mmoja wa waanzilishi wa kundi la Wenge ambapo inasemekana JB Mpiana alijiunga na kundi hili miaka ya 80 akimkuta Masela na Werasoni tayari kwenye kundi. Binafsi namheshimu Masela kwa nafasi aliyokuwa nayo akishirikiana vyema wakati ho na akina Allain Makaba na Mwana Ficare, Titina Alcapone kwenye Drums na Ali Mbonda kwenye tumba, kikosi cha zana kilikuwa kimetulia, enzi hizo MAsela alikuwa ndio anapanga vyombo kwamba nani apige wakati gani. Acha bwana ile ilikuwa Dream TEam.

Angalia kipande cha onyesho la majuzi na utamuona Didier Masela humo. mwenye nyepesi atwambie.


Fally Ipupa aja kivingine!!

July 12, 2009

image

Mwanamuziki Fally Ipupa ametoa Albamu mpya inayokwenda kwa jina la Arsenal. Kwa mujibu wa mashabiki wa muziki wa Lingala wanasema kuwa Fally albamu ni nzuri lakini wanamlaumu kwa kuimba style moja kwenye nyimbo karibu zote ambapo sauti zimefanana na kutofautiana maneno tuu, hii inasemwa ni tabia ya Fally kutopenda kuwashirikisha wanamuziki wengine au kuwaachia wanamuziki wake nafasi kutia ladha tofauti.

Ni wanamuziki wachache wa Kongo wenye uwezo wa kuimba nyimbo moja pekee na watua wakawapenda akiwemo JB Mpiana au Koffi Olomide. Hata hivyo Fally amejitahidi kwa kutoa Albamu hii ambayo iko kwenye viwango vya hali ya juu sana, Spoti na Starehe imebahatika kukamata CD Moja na shukrani za pekee zimuendee mdau wangu toka Bruxells Yemimanize Iputa kwa kuniweka katia ya watu 100 waliopata CD zilizosainiwa na Fally heshma ya pekee. (Kama muziki ni uraia basi mi Mzaire!! hehehehee).

Mpaka sasa nyimbo mbili zimekuwa ni chaguo langu nazo ni “Travelling love" na "Nyokalessi".

Nakuinjesha wimbo Arsenal hii si video rasmi ni kwa ajili ya sauti tuu.