Surprise Kapangala wa Wenge Musica BCBG ya wakati huo!!

February 9, 2010

wakati huo wakiwa bado kundini wakijulikana kama Wenge Musica BCBG chini ya JB Mpiana, bado watu kama Adolf Dominguez yupo, Allain Prince Makaba, Werasson Ngiama Makanda, Engineer Blaise Bulla, Titina Alcapone, Ali Mbonda na wengineo, Wimbo huu ulikuwa unaitwa Surprise Kapangala ulitungwa na kuimbwa na Werasson, ni moja ya nyimbo ambazo Werasson aliimba peke yake na kuupatia sana.

Tofauti na JB Mpiana ambaye kuimba wimbo mzima na kunata na beat si issue sana, Werason hupatia sana akimpa Verse kunakshi kwenye wimbo wako, lakini hapa Mzee mzima aligangamala.

Aliyeimba ni  Ngiama Makanda na aliyeghani alikuwa Roberto Wunda Ikokota.  Solo ilipigwa na Allain Makaba, Ficare Mwamba, ali Mbona kwenye tumba, Titina alcapone kwenye Drums na Chants. aaaaaah lE Survereign Mukullu Maghambo, Mukubwa Agape Msumari, Julie Babaa na anethe na Sultan De Kighamboni, wadau wangu Kente Kap Kapita Zadio Kongolo, Heshima kwenu kwa pamoja.


Cooler head prevails

February 9, 2010

image

With its national team caught up in controversy, England has found calm in the rise of ex-hot head Wayne Rooney. Read Review here


Bebe Cool adai Polisi Fidia ya Milioni 800

February 9, 2010

image

Bebe Cool, Mkewe  Zuena (centre) na Masengere (with crutches) wakitoka  Mulago Hospital hivi karibuni baada ya masahibu.

Sakata la mwanamuziki Moses Ssali aka Bebe Cool ambaye alipatwa na dhamhma pale alipopigwa risasi na askari baada ya kutokea kutoelewana linaendelea.

Awali ripoti ya polisi ilisema kuwa Bebe Cool alikumbwa na kisanga hicho baada ya kujaribu kuwazuia Polisi kukamata watuhumiwa wawili waliokuwa wakifanya mapenzi ndani ya gari, Hata hivyo mwanamuziki huyu alikana ripoti hoyo ya polisi.

Hapo jana Mwanamuziki huyo pamoja na Mlinzi wake waliwakilisha madai kwa kuishitaki serikali jumla ya Shilingi Milioni Mian Nane (800M) kama fidia kwa kilichotokea. Bebe Cool, Allan Masengere, Godfrey Kayiiza na Abas Bosco Kabobyo kwa pamoja waliwakilisha mashitaka hayo kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali hapo Feb 2 na anapaswa kuwajibu ndani ya siku 45 tokea tarehe hiyo. Bebe Cool ambaye ni mtoto wa waziri wa zamani Bidandi Ssali anadai kuwa Serikali ambaye ni muajiri wa Polisi wanahusika moja kwa moja na uzembe uliofanywa na Polisi hao.

Katika hati hiyo ya Mashtaka ambayo inasemwa kudraftiwa uzuri na mwanasheria wake Bebe Cool, amedai kuwa yeye anapata mkate wake kwa kutegemea muziki na show za jukwaani kutokana na majeraha hayo atakuwa nje ya jukwaa kwa takribani miezi sita kabla ya kurejea stjini hivyo anadai fidia kwa hilo.


Twanga na Valentine

February 9, 2010

image


Namtambulisha kwenu Gie Manie

February 9, 2010

image 

Kwa jina la Muziki anaitwa Gie MAnie, Ye ni nani yuko wapi anafanya nini, tega sikio ni katika mfululizo wa kukuletea vijana wachache wanaofanya mambo makubwa kwenye sekta nzima ya Burudani, ama waliwahi kuwika na sasa hawajulikani wako wapi au wapya wanafanya makubwa huko nje bila kujulikana nyumbani. fuatilia hapa wiki hii.


Bongo bwana Full Ujasiriamali…! duh

February 9, 2010

PICT0168

jiji hili kuna kila ujasiriamali na vituko vya hapa na pale ilimradi laha tuu, Hii ilikuwa majuzi pale Kijiji Beach Kigamboni. Picha na Tamim Ahmed Mngoya Juma Lukuta wa Kibanda Kicheba kwa Semkope. hahahahahaha.


Kiota kipya cha maraha kufunguliwa karibuni….!

February 9, 2010

Kicheba Logo

Mpya ya aina yake inafunguliwa karibuni tega sikio hapa hapa kwa ajili ya mualiko.


Nigeria wamtimua kocha Amodu

February 8, 2010

image

Nigeria imefukuza kazi kocha wa timu ya taifa, Shaibu Amodu, licha ya timu hiyo kumaliza katika nafasi ya tatu ya mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.

Hiyo ni mara ya pili kwa Amodu mwenye umri wa miaka 51 kutimuliwa kutoka wadhifa huo wakati timu ya taifa ya Nigeria ikijiandaa kucheza fainali za kombe la dunia.

Uamuzi ulifikiwa baada ya mkutano wa shirikisho la soka la Nigeria uliofanyika mpaka usiku mjini Abuja.

Mholanzi Guus Hiddink, ambaye kwa sasa anaifundisha timu ya taifa ya Urusi, ni miongoni mwa makocha wanaotajwa kupewa nafasi ya kumrithi Amodu.

Juma lililopita, kocha wa Misri, Hassan Shehata alidai kuwa ameombwa na Nigeria kuingoza timu hiyo kwenye kombe la dunia, wakati kocha wa Zambia, Herve Renard, naye anasema ameshawishiwa na timu kadhaa za Afrika.

Na BBC


TP Mazembe kutumia dola milioni 10

February 8, 2010

image

TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao ni mabingwa watetezi wa Kombe la klabu bingwa barani Afrika, wametangaza bajeti ya dola milioni 10 kwa msimu wa 2010.

Kwa mujibu wa wavuti ya TP Mazembe, kiasi hicho cha fedha kiliafikiwa kwenye mkutano mkuu uliofanyika mwezi Januari.

Rais wa klabu hiyo, Moise Katumbi, pia alitangaza hivi karibuni kuwa ametoa dola milioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa timu hiyo mjini Lubumbashi.

Bw Katumbi amesema kuwa klabu yake sasa ipo katika hali nzuri ya kifedha.

Tajiri huyo anamiliki asilimia 60 ya hisa za kampuni inayoendesha TP Mazembe. Katumbi pia ni Gavana wa jimbo la Katanga lenye utajiri wa madini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mazembe walishinda ubingwa wa vilabu vya Afrika baada ya kuichapa Heartland FC ya Nigeria mwezi Novemba mwaka jana.


Masikini Arsenal,, yachapwa na Chelse 2-0

February 8, 2010

 

image

Drogba akiwatoka mabeki wa Arsenal ambao walikuwa na kazi ya ziada usiku huu.

Chelsea wamerejea tena kwenye uongozi katika msimamo wa ligi ya Primia ya England baada ya kuishinda Arsenal mabao mawili kwa bila.

Mabao yote mawili yalifungwa na Didier Drogba, moja kwa msaada wake nahodha John Terry.

Ilikuwa ni faraja kubwa kwa Terry ambaye wiki hii alivuliwa unahodha wa timu ya taifa ya England kutokana na shinikizo, kufuatia madai kwamba alikuwa na uhisiano wa kimapenzi na mpezni wa zamani wa mchezaji mwenzake katika timu ya taifa Wayne Bridge.

Ushindi wa leo wa Chelsea umewaweka mbele ya Manchester United kwa pointi mbili na ina maana mpambano wa taji la ligi ya primia sasa ni kati ya miamba hao wawili.

Kwenye mechi nyingine iliyochezwa jumaapili Birmigham City iliwafunga Wolverhampton 2-1 .Wolves wanasalia kwenye hatari ya kushushwa daraja msimu ujao.


Mashabiki bwana….!

February 8, 2010

PICT0086

Basi la Hajees linalofanya safari zake katika Mkoa wa Tanga na Dar Es Salaam likikata mitaa ya Ubungu kuingia stendi kuu ya mabasi la nembo ya washika Bunduku Arsenal “The Gunners”  Ligi ya Uingereza imezidi kujichotea mashabiki wa burudani hasa vijana hapa Tanzania.


Ndondi….!

February 8, 2010

PICT0047

Vijana ambao walikataa majina yao kuandikwa Bloguni wakifanya mazoezi jana katika Pwani ya Maese huko Kigamboni. Vijana hawa walisema kuwa wako katika mazoezi makali kabla ya kuzindua rasmi klabu yao mpya ya mchezo wa ngumi na kusema wanataka kuwa moja ya Klabu hatari na zenye mafanikio katika mchezo huu.


McDonald Mariga asajiliwa na Inter Milan

February 5, 2010

image

Mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya taifa ya soka ya Kenya, Harambee Stars, McDonald Mariga amesajiliwa na mabingwa mara nne wa kombe la ligi kuu ya Serie A, nchini Italia, Inter Milan.

Mariga alitia saini mkataba wa miaka minne na klabu hiyo hapo jana kutoka klabu ya Parma. Klabu hiyo ya Inter Millan ilimsajili Mariga, baada ya matumaini ya Klabu ya Manchester City kumsajili kuambulia patupu. Mariga alinyimwa kibali cha kufanya kazi nchini Uingereza na hivyo kudidimiza matumaini yake ya kuwa Mkenya wa kwanza na raia wa kwanza kutoka eneo la Afrika Mashariki kuchezea katika ligi kuu ya Uingereza.

Kama sehemu ya mkataba huo, mchezaji wa Inter Milan, Luis Jimenez, ambaye alikuwa akiichezea klabu ya West Ham, nchini Uingereza kwa mkopo, atajiunga na Parma.


Blackstars wa Ghana watunukiwa

February 5, 2010

image

Wanakandanda wa Ghana ambao walishindwa na Misri katika fainali ya kombe la mataifa ya Afrika wametunukiwa dola elfu 20 kila mmoja.

Wachezaji hao wametunukiwa kiasi hicho na Rais wa nchi hiyo John Atta Mills kwa kufika fainali.

Rais alimsifu kocha Milovan Rajevac na kumhimiza atie bidii zaidi kwa michuano ya kombe la dunia.

Kocha huyo amesema amesuluhisha tofauti zilizokuwepo kati yake na mchezaji wa klabu ya Intermilan Sulley Muntari.

Rajevac amesema pia yuko tayari kuwazingatia wachezaji wengine ambao hawakuwepo nchini Angola.


Misri wapanda chati

February 5, 2010

image

Mabingwa wa soka barani Afrika, Misri wamepanda ngazi katika orodha ya kumi bora ya shirikisho la kandanda la mataifa FIFA.

Kutokana na orodha iliyotolewa leo, Misri ndio timu inayoongoza kutoka Afrika ikishikilia nafasi ya 10.

Hii ndio nafasi ya juu kabisa kushikiliwa na timu ya Afrika tangu mwaka 1994 ambapo Nigeria ilishikilia nafasi ya tano.

Nigeria pia imepanda na inashiklia nafasi ya 15 duniani na ndio ya pili katika timu bora za Afrika.


Kauthar Toka Dar, Alex toka Mbeya na Neema wa Shinyanga waingia kikaangoni Maisha Plus

February 2, 2010

IMG_0079

Kipindi cha Maisha Plus bado kinaendelea na wiki hii majina matatu yametajwa kuingia kikaangoni ila kwa taarifa yako wiki hii hakuna mtu atakayetoka kwani unachotakiwa kufanya katika ya majina hayo matatu yaani Kauthar Toka Dar, Alex toka Mbeya na Neema wa Shinyanga, wawili kati yao wanatakiwa kwenda kwenye hoteli moja ya kula kuku.

Kauthar yeye anaingia kikaaongoni kwa mara ya tatu huku Neema akiingia kwa mara ya pili na Alex kwa mara ya kwanza. Siji kama ingekuwa kutoka nani ambaye angetoka kwani hatima huwa iko kwa watazamaji ambao humpigia kura mtu ya kubaki ambapo kwa wiki iliyopita Neema wa Shinyanga alipata kura zaidi ya elfu moja ili abaki huku mshiriki Kelvin kutoka Morogoro akiambulia kura mia tatu na ushehe tuu.

Angalia maoni ya wanakijiji juu ya nani atoke na kwa nini, Haya ni baadhi tu ya maoni yao.

Alex Mbeya ataka watu wajiamini na kusema kuwa kutokujiamini kunapelekea watu kuwa na hofu na kujenga makundi ndani ya kijiji.

 Neema Tabora

Neneema yeye kwa upande wake alilalamikia ushirikiano mdogo na kusema unapelekea watu kutengana akiwataka watu waishi kama wanavyoishi kwenye uhalisia wao huko nyumbani.

 

William Iringa

Alimlalamikia Kaushak akisema kuwa Kauthar hafai kuwa kiongozi kwa kuwa ni mdhaifu na hajiamini kwa kutolea mfano kuwa kuwa yeye ndie kiongozi wa makundi ndani kijijini.

 

Jeremiah Dar

Yeye kwa upande wake alimpendekeza Alex wa Mbeya atoke kwa kuwa anasema kuwa wakati wake umefika na yeye ndiye anawakoroga pale kijijini kwani amekuwa akiwachanganya na kuwatenganisha. Anasema pale kijijini kila mt anahaki ya kuamua nani anampigia kura

Taiba Zanzibar

naye alimppigia kura Alex kwa sababu zinazofanana na Jeriamia akisema kuwa Alex amekuwa akipita huku na huku kuwataka watu wampigie fulani atoke jambo ambalo kwake anaona ni kinyume cha maadili ya kijijini.

Mwishehe wa Dodoma

Anasema Kauthar anatakiwa atoke kwa kuwa hawezi maisha ya kijijini kwani hata yeye mwenyewe Kauthar wakati mwingine anasema kuwa maisha yale hayawezi. amekuwa akilalamika sana na kuonyesha kuwa ni mdhaifu kwa maisha yale ya kijijini. Aliongeza kusema kuwa Kauthar amezoea maisha ya uzunguni zaidi.

Jaquiline wa Moro

Yeye alimtaja Luthende, yeye alisema mshkaji ana bore sana na anatabia ya uchoyo na umimi sana. Hapendi ushirikiano na saa nyingine kitu kidogo kinaweza kuwa kikubwa huku akitolea mfano mshkaji anaweza kukunyima kisu tuu. Kwa mujibu wa Jaq yeye anapenda kukuza mambo.

 

Leonard toka Dar

alimpendekeza Neema Tabora kuwa atoke ni mvivu hawezi kuamka asubuhi anapenda sana kujipodoa hawezi hata kuchota maji kwa kuwa make up kibao sio. Anasema mshkaji anaushirikiano mdogo kwa sababu ya uvivu wake.

 

Luthende Tabora

Anamshukuru Mungu kwa kumpa uzima na anasema kuwa matatizo yaliyopo ni madogo madogo tuu, kwa upande wa mtu anampendekeza Kauthar, anasema yeye kama yeye anadhani kuwa mchizi anamchukia, ye anasema kuwa hamchukii kuhitilafiana ni jambo la kawaida tuu.

Kingine anasema kuwa yule dada anakosea lakini hataki kuomba msamaha hivyo inamfanya kuwa mbinafsi sana. Kingine aliwahi kulalamika kuwa anabaguliwa alipoambiwa ataje alishindwa ana kusema kuwa ata afanywe nini hataji. Huo ni udhaifu na ameonyesha kutoaminiana. Ila kwa mtazamo wangu nikiangalia naona hapa kuna issue kati ya wawili hawa. ni mtazamo tuu.

Kauthar Dar

Kama nilivyosema kwa Kauthar sijui kati yao ni nini kinaendelea maana kwa washiriki wengine pamoja na kuwa wanatajana majina lakini inawachukua muda mfupi kuelezea sababu za kum nominate mtu jambo ambalo ni tofauti kati ya Luthende na Kauthar, wao wamechukua muda mwingi kila mmoja kuelezea ubaya wa mwenzake.

Kwa upande wa Kauthar ambaye ni mmoja wa washiriki toka mkoa wa Dar Es Salaam, Yeye anasema Luthende hamfagiliii hata kidogo, na pia alilalamikia kuwa watu wanambeza na kusema kuwa msomali akishinda watanzania wataandamana. anasema Luthende hajawahi kumtreat kibinadamu lakini anamuona yeye hastahili kukaa kijijini pale. Anadai kuwa katika kuhakikisha matkwa yake yanatimia hadi Babu aliitwa ili eti yeye aweze kutoa ufafanuzi wa malalamiko yake na aliye engineer ni Luthende jambo ambalo yeye binafsi hakulifurahia hata kidogo.

Julius Arusha (Mmasai)

Anasema kuwa Alex atoke ana kelele na hawezi kuwapa watu wengine nafasi ya kuonyesha kipawa chake na anatumia mwamvuli wa Uchungaji kujifanya mtakatifu wakati mambo anayoyafanya hayana manufaa kwa jamii.

Julius anadai kuwa mtu anatakiwa atajwe kutokana na tabia yake na kusisitiza kuwa Tabia za Alex si za kiungwana, alisema kuwa kutofautiana ni jambo la kawaida na kutoa mfano kuwa hata unapofungia mbuzi kwenye uzio lazima hata mmoja ataruka.

Kwa mujibu wa uongozi, wiki hii unatakiwa kupiga kura ili washiriki wawili wakale misosi kwenye moja ya hoteli za kitalii kwani anayepigiwa kura hatotoka.

Hii inamaana gani hii itawafanya washiriki wapunguze chuku kwa kutajana majina kwa ajili ya visasi zaidi kwani inawafanya kujiona kuwa hakuna nafasi ya kusameheana au kulippiziana kisasi isipokuwa kum nominate mtu jambo ambalo si msingi hasa wa Maisha Plus.

Tuonane kesho tena kwenye muendelezo wa Maisha Plus….


1st Friday of the Month Party returns on 05/02/2010

February 2, 2010

image

Bohemia presents 3 Bands including Thandiswa Mazwai former Bongo Maffins (RSA) on 12/02/2010

image


Mbwembwe za Fainali Angola

February 1, 2010

Beautiful happy African dancers let their joy permeate the stadium during a wonderful performance at the final match between Egypt and Ghana during the African Cup of Nations football championships CAN2010 at November 11 stadium in Luanda on January 31, 2010.


Man U waitandika Arsenal 3-1

February 1, 2010

image

 

Ligi ya Uingereza inaendelea kupamba moto huku Manchester United wakiimarisha nafasi yao ya kubeba kombe hilo kwa kuitandika Arsenal mabao 3-1 kwenye uwanja wa Emirates.

Hadi kipindi cha mapumziko Man U walikuwa wanaongoza kwa 3-0.

Kipa wa Arsenal Manuel Almunia alijifunga, Wayne Rooney akaongeza la pili na Ji-Sung Park la tatu.

Mnamo kipindi cha pili, Arsenal walijaribu kutimua vishindo kiasi cha kujipatia kifuta jasho kupitia mlinzi Vermaelen.

Katika mechi za awali Manchester City waliitandika Portsmouth 2-0, mabao ambayo yalifungwa na Emmanuel Adebayor pamoja na Vincent Kompany.

Portsmouth wanashikilia mkia kwenye ligi kuu huku matatizo ya fedha pia yakiendelea kuwazonga.

Hapo jana Chelsea waliitandika Burnley 2-1.


Gari inauzwa; Mercedes Benz Elegance 2000 Model

February 1, 2010

Make: Mercedes Benz Elegance E200

Model: Elegance E200

Make: Year 2000 Model

Color: Metallic Gold

Price: 12,000,000/=, Tax Fully Paid

IMG_0314

IMG_0316

IMG_0317

IMG_0318