Jb mpiana kuja TZ Mwezi ujao
November 17, 2009Kwa mujibu wa Secretary General Mbuta Kisolokele tayari jb mipana ameachia single ya generic kutoka katika albumyake mpya ya Kis, "Be serious" ambayo inamjumuisha huyo kuingia Tanzania kwa show mwezi ujao .
Jean-Bedel Mpiana Tshituka na kuwa ni miongoni mwa wanmuziki wanao subiriwa kwa hamu kubwa sana na mshabiki wake wa wenge bcbg inakadiriwa kuwa mwisho wa mwaka huu 2009 mwanmuziki , JB Mpiana atakuwa ameachia album yake hiyo ya "Let’s be serious." Ambayo ndani ina track 15 na moja tu ambayo ndio ya generic alieifanyia katika studio za CEO na kuwa atazindua album hiyo December kumbuka ,
JB Mpiana kiongozi wa kundi kubwa la wenge BCBG pamoja na group yake wanataraji kutua Tanzania kwa show akiambatana na Thsla muana pamoja na bill Clinton ingawa tahere haijatajwa na kuwa wanletwa na nani hawakusema ni kwa mujibu wa mtandao wa africanhit.com.
Naomba nikuache na kipande cha Live ya Mzee mzima ndio utajua.
JB bwana we acha tuuu!!
Evelyne anahitaji sala zenu
November 17, 2009Umelifanyia nini jiji la Dar Es Salaam? Kauli mbiu ya FIESTA yenye changamoto.
November 16, 2009Katika Fiesta mwaka huu kwa jiji la Dar Es Salaam kauli mbiu yao inauliza je umelifanyia nini jiji la Dar?
Wakizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam moja kwa moja kupitia kipindi cha Power Breakfast leo, Mkuu wa Mkoa alihimiza watu kuwa na moyo wa kujitolea kukemea maovu na yale yote yanayokwenda kinyume na utaratibu ikiwemo utupaji taka hovyo, Udereva usiofuata sheria na taratibu, Kufanya biashara sehemu zisizo rasmi nk.
Mkuu huyo wa Mkoa Bw. Lukuvi ameongeza kuwa si kazi ya serikali na viongozi wake tuu kusimamia hayo bali wananchi wanauwezo wa kufanya hayo kwani wao ndio abiria na wanaishi na wahalifu hao kwenye maisha yao ya kila siku.
Tamasha la Fiesta litafanyika tarehe 21 November kufuatia kuhairishwa baada ya msiba wa Marehemu Mzee Kusaga.
Shime wana Darisalama changamoto ifanyiwe kazi punguzeni kulalamika. mweeeeeeee!!
WAREMBO MISS EAST AFRICA KUANZA KUWASILI DESEMBA 1-2009!
November 16, 2009SELAMAWIT ZERABRUCK GHEBRESLASSIE -18 YEARS (ERITREA)
Warembo wanaoshiriki mashindano ya kimataifa ya MISS EAST AFRICA 2009 wataanza kuwasiri Nchini tarehe moja mwezi ujao kwa ajili ya mashindano hayo yanayosubiliwa kwa hamu kubwa na watu wengi Barani Afrika.
Wakiwa jijini Dar es salaam, warembo hao watafikia katika hoteli ya kimataifa ya Kunduchi Beach Hotel & Resort ambayo ndiyo hoteli rasmi ya mashindano ya Miss East Africa 2009.
Mashindano ya MISS EAST AFRICA 2009 yanatarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi ujao katika ukumbi wa Mlimani City jijini dare s salaam na yatawashirikisha warembo kutoka Nchi 14 za ukanda wa Afrika mashariki ambazo ni pamoja na wenyeji Tanzania,
Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Nchi zingine zinazoshiriki katika mashindano hayo ni Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Somalia, pamoja na visiwa vya Seychelles, Comoros, Madagascar, Reunion na Mauritius.
Mashindano hayo yanayoandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam yanatarajiwa kutizamwa na watu zaidi ya millioni 200 kupitia katika Television barani Afrika.
Mrembo Claudia Niyonzima wa Burundi ndiye anayeshikilia taji la Miss East Africa kwa sasa.
AKAZUBA CYNTHIA-20 YEARS (RWANDA)
QUEEN BELLE MONIQUE-23 YEARS (BURUNDI)
ALIDA GROLIA KANEZA-19 YEARS (BURUNDI)
SEFORA MESSELE GHEBREEZGABIHEIR-18 YEARS (ERITREA)
MARRY KIRABO -18 YEARS (UGANDA)
Swahili Fashion week kwa jicho la Lady Jay Dee
November 16, 2009FNAAZ DESIGNS…….NA FARHA SULTAN
Flower mrembo anaepiga makofi ndio mbunifu wa nguo zote hizo hapo chini Huyo ndie Farha Sultan.
Mwinyi Goha wa Machozi Band
Huyu ni Richa Adhia aliyekuwa Miss Tanzania.
Kwa habari na Picha zaidi mtembelee Lady Jay Dee
Simba bwana! We acha tu,yashinda 3-1, Yanga, Prisons leo
November 16, 2009
SIMBA imetegeneza historia mpya kwa kushinda mechi zote 11 za mzunguko wa kwanza na kufikisha pointi 33 katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku watani zao Yanga leo watakuwa wakijiuliza mbele ya Maafande wa Tanzania Prisons kwenye Uwanja wa Uhuru.
Mabao ya Mussa Hassan Mgosi, Uhuru Selemani na David Naftari yalitosha kuipa Simba ushindi mnono wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mgosi aliunganisha kwa umakini pasi ndefu aliyopewa na kipa Juma Kaseja na kufunga bao la kwanza kwa vijana hao wa Msimbazi katika dakika ya 20. Gonga hapa
Naomi Campbell afanya tamasha la mavazi Dar es Salaam!!
November 13, 2009
Mke wa Rais mama Salma Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) akimweleza jambo Balozi wa kimataifa wa Utepe na msanii na mwanamitindo wakati wa onyesho la mavazi lililoandaliwa na Taassi ya Utepe Mweupe.
Na Anna Nkinda – MAELEZO
Jumla ya dola za kimarekani 10,000/= zimepatikana kutokana na mnada wa nguo ya kike iliyotolewa na msanii na mwanamitindo wa Kimataifa Naomi Campbell katika maonesho ya mavazi ya Relief Tanzania yaliyofanyika jana usiku katika ukumbi wa Movenpick jijjini Dar es Salaam.
Maonesho hayo yaliandaliwa na Naomi Campbell ambaye ni Balozi wa Kimataifa wa Utepe Mweupe kwa kushirikiana na Mustafa Hassanali ambaye ni mwanamitindo wa hapa nchini kwa lengo la kukusanya fedha ili kutunisha mfuko wa Mtandao wa Utepe Mweupe (The White Ribbon Alliance).
Akiongea mara baada ya maonesho hayo Campbell alisema lengo la kufanya maonyesho hayo ni kupata fedha ambazo zitatumika katika kampeni ya kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto.
Kuhusu wabunifu wa mavazi na wanamitindo wa hapa Tanzania alisema anaridhishwa na kazi zao na wanajitahidi kufanya kazi nzuri kwa ufasaha mkubwa na kwa kujituma.
Aliendelea kusema kuwa anaipenda nchi ya Tanzania kwa sasabu inavivutio vingi kama vile mbuga za wanyama, visiwa vya Zanzibar, mito, milima, maziwa na Bahari ya Hindi huku akisisitiza kuwa si mara ya kwanza kuja Tanzania na ana wa kuendelelea kuja hapa nchini.
Katika maonyesho hayo Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) pamoja na Mke wa Rais wa Zambia Mama Thandiwe Banda walihudhuria.
Mtandao wa Utepe Mweupe (White Ribbon Alliance) wenye takribani nchi wanachama 143 duniani ambao jana uliadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake unafanya kazi kubwa yakuhakikisha kuwa nchi wanachama zinaondokana na vifo vya kina mama wajawazito wakati wa kujifungua.
Na Full Shangwe
Duh Soo washkaji! Unga noma si kihivyo!!
November 13, 2009Picha na Abdalla Mrisho
Nafurahishwa sana na uwepo wa Blog mbali mbali ambazo kila moja kwa wakati wake inachambua na kuandika lake.
Wiki hii katika pita pita yangu nilipita kitaa cha bwana Abdallah Mrisho kwani napenda huko ndiye pekee huwa anaandika habari za wasanii bila kuogopa inapobidi.
Moja ya habari zilizonivutia na kunikaa kichwani ni kuhusu suala la bwimbwi kwa wasanii. Ni wazi kwa mujibu wa habari ile wasanii wanapotea kwa kutumbukia kwenye dhahma hii ya kula unga hakuna wa kumfunga paka kengele na kama wakiachiwa kuna hatari kubwa vijana wengi wakatumbukia kwani wengi hupenda kuiga yale ambayo wasanii huyafanya kwa kuamini kuwa wanajua zaidi ya wao.
Kwangu mimi nadhani Recording Lebel zina kazi kubwa ya kufanya pampja na mambo mengine suala la maadili pia ni muhimu sana, kwa kuwa wasanii wengi wako chini ya Lebel fulani basi ingefaa hizo Lebel zisiamamie si tu mapato na muziki bali pia na maisha binafsi kwa kuwaelimisha kwani msanii akitika kwenye chat si tu anajiua kisanii bali hata mapato kwa Lebel husika yanashuka.
Hivyo basi naimani hii itakuwa changamoto kwa wadau wa sekta ya burudani hata vituo vya redio kuwakanya hawa wasanii kwani kwa bahati nzuri vituo vya redio vina mahusiano ya moja kwa moja na wasanii pia.
“
Its dangerous! The only gent on kundi marehemu la Wakilisha, Langa Kileo anaweza kuwa mfano hai, baada ya kukiri kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Ijumaa iliyopita kuwa alikuwa anabwia unga lakini sasa amestop. Langa alisema kuwa alikuwa mbwiaji mzuri wa Cocktail kabla ya hivi karibuni kuugua typhoid, hivyo kukosa access ya kupata unga.
Alisema, alianza kama utani lakini baadaye alizidiwa na akawa hawezi kuacha, ingawa sasa hivi anamshukuru Mungu kwamba yamepita. Katika hilo, Langa alieleza kwamba angalau sasa anajisikia nafuu na afya imeanza kurejea. Hiyo ni kauli ya Langa kupitia session ya Crazy Friday, lakini ukweli ni kuwa madogo kibao wapo kwenye skendo ya kubwia.
Albert Mangwea ‘Ngwair’, Heri Samir ‘Blu’ Mark II B a.k.a Simba ni kati ya majina ambayo yanatajwa kwenye orodha ya wanaodaiwa kubwia unga. Hayo ni majina yanayotajwa lakini nyuma ya pazia ni wengi na hii inasababisha kizazi kipya kisiwe na afya standard. Madogo wanasimama vizuri lakini baadaye wanakuwa dhoofu l’hali. Hii ni hatari na sisi kama wadau tunalaani vikali matumizi ya dawa za kulevya.
”
ni sehemu ya habari hiyo kujua zaidi bofya hapa.
Mzalendo Machupa
November 13, 2009Anaitwa Atumani Machupa, yuko wapi na anafanya nini? tuliwahi kufanya mahojiano naye kama ulipitwa basi bofya hapa.
Ugua pole Hasheem Thabeet
November 13, 2009Hasheem Thabeet ambaye ndio kwanza alikuwa ameanza kung’aa kwenye ligi ya mpira wa kikapu ikiwa ni ligi aghali kuliko zote kwenye mezania ya kikapu ulimwenguni amevunjika taya la chini baada ya kugongana na mchezaji wa timu pinzani.
Hasheem ambaye aligongana na Zach Randolph alisemwa alipata maumivu makali kabla ya kutolewa nje kwa matibabu zaidi. Timu ya Hasheem walikuwa wakikwaana na Portland Trail Blazers katika mtanange wa ligi hiyo ya NBA. Lakini habari zinapasha kuwa Hasheem anaendelea vizuri na matibabu na itamchukua muda kidogo kurudi uwanjani.
Reuters.
Kiddo Kickers Academy, Shule inayokuza na kuwalea watoto kisoka.
November 12, 2009Watoto wakifurahia medali na kikombe baada ya kukabidhiwa mara baada ya msimu wa Ligi yao ya Kiddo Kickers kuisha nchini Malaysia.
Siku ya kwanza nilipowaona wakicheza sikuamini kama ni watoto wa miaka 6 hadi 11. Ni watoto wambao wanaonyesha kiwango cha hali ya juu cha soka, nidhamu ya mchezo, hari ya mchezo, hamasa ya na tamaa ya kufunga hali kadhalika team work.
Kiddo Kickers ni academy ya michezo iliyoko Shah Alam huko Malaysia kwa watoto ikiwa inapata funds toka serikalini kwa ajili ya kuendeleza mchezo wa mpira wa miguu kwa watoto wadogo.
Watoto hawa wa aligi yao ambayo inawadhamini wakubwa na inaonyeshwa kwenye Television mbali mbali nchini Malaysia ikiwemo Astro (DSTV).
Najaribu kushawishika kupata kitu kama hichi hapa Tanzania kwani kwa mujibu wa mkufunzi kwenye chuo hicho kwana Fairuz Jamal Hairudin anasema kuwa nia yao ni kucheza kombe la Dunia miaka 8 – 12 toka sasa ambapo inakadiriwa product ya kwanza ya watoto hawa itakuwa imefikisha wastani wa miaka 17-22 umri ambao ni rahisi kupata hata timu za nje.
Angalia magoli matano bora kwenye wiki ya tano ya ligi yako kwa kubofya player.
Amani Live Titanium Club Malaysia leo.
November 12, 2009Mwanamuziki Amani Toka jijini Nairobi leo anatumbuiza jijini Kuala Lumpur Malaysia katika Club ya Titanium.
Kwa mujibu wa waandaaji wa ujio wa mwanamuziki huyo ambaye alichukua zawadi ya mwanamuziki bora wa kike kwenye mtanange wa MTV mwaka huu wanasema kuwa Amani aliwasili juzi kwa ajili ya onyesho hilo ambalo linatazamiwa kutikisa jiji la Kuala Lumpur, ‘respond ni nzuri kwa kweli kwani Amani ni mwanamuziki wa kwanza wa kike si tuu kutoka East Afrika bali toka Africa kutumbuiza Malaysia, na uzuri anakubalika na sie tumemleta wakati yuko juu, alisema Big Jerry Mshana ambaye ni mmoja wa waandaaji wa ujio huo akiwa anaiwakilisha The Kilimanjaro Entertainment.
Huu ni ujio wa mwanamuziki wa tatu toka East Afrika ambapo wa kwanza alikuwa AY ambaye alifanya vizuri sana na kisha kufuatiwa na Nonini ambaye naye alifanya vizuri.
Kampuni ya Kilimanjaro Entertainment ambayo imeingia kwenye medani hii kwa kasi inampango wa kuandaa show bab kubwa ambayo itajumuisha mwanamuziki mmoja toka TAnzania, Kenya na Uganda.
Robinho haami Man City ng’oo!!
November 12, 2009Habari za kuaminika toka klabu ya Manchester City zinasema kuwa mchezaji Mbrazir Robinho hatikihama kikosi hicho.
Awali habari zilizagaa kuwa Robinho alitarajiwa kuhamia Barcelona mwanzoni mwa mwaka kesho. Habari zinaziri kuhabarisha kuwa Robinho ameingia mkataba ambao mwenyewe amesema hawezi kuuvunja na atachezea timu hiyo hadi mkataba utakapomalizika.
Muonekana wa Flavian na Kivazi vyawakuna wengi
November 12, 2009Muonekano wake na nguo yake ni baadhi ya mambo ambayo wachangiaji wa blog maarufu ya Young Black and Fabolous, YBF walikuwa na mtazamo chanya juu ya nguo ambayo Flaviana alivaa na muonekano wake kwa ujumla. Blog hiyo ambayo inajulikana kwa kuandika habari za mastaa weusi na watu kuchambua watakavyo iliweka picha za Flaviana akiwa huko USA kwenye project ya LIFE Project for Africa iliyoandaliwa na Russell Simmons.
“Go Miss Tanzania..not many women call pull off a bald head..she definitely can!” aliandika mchangiaji aliyejitambulisha kwa jina la BeeJay. naye mchangiaji mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Lanubian alisema “
It’s good to see the former Miss Tanzania after I saw her competing in the Miss Universe a few years back and actually made the top ten in that hair obsessed pageant. She is STUNNING!!!”. (soma zaidi hapa)
Flavian ni kati ya warembo ambao waliandaliwa na kampuni ya Compass Communications chini ya uongozi wake Maria Sarungi na anafanya vizuri sana kwenye medani ya urembo.
Binafsi nafurahishwa na hii kampuni ya Compass Communications kwani si tu kuwashirikisha warembo kwenye matukio mbalimbali bali huhakikisha wanawalea warembo na kuwatafutia maisha kwenye sekta ya Urembo, hongera sana Maria.
Hii inasaidia kupnguza scandal kwa warembo kwani wanakuwa na shughuli ya kufanya ambayo inawahakikishia kipato ambacho ni chanzo kikubwa sana cha vishawishi kwani warembo wengi baada ya kufikia hatua ya juu ya kujulikana kwenye jamii bado wanataka ku maintain status jambo ambalo linakuwa gumu kama hawana chanzo cha uhakika cha mapato.
Nataraji hii inaweza kuwa somo tosha kwa waandaaji wengine wa mashindano ya urembo ambao huishia kuwatosa warembo wao mitaani na kudakwa na mafataki na hivyo kuishia kutengeneza vichwa vya habari kila kukicha.
Tyson matatani tena, Amzabua mtu na kumtoa damu!
November 12, 2009Bingwa wa zamani wa uzito wa juu masumbwi Mike “Iron” Tyson ameingia matatani tena na vyombo vya dola baada ya kutiwa hatiana hapo jana baada ya kuzabua ngumi ya uso paparazzo ambaye alimsogelea ili kupata picha.
Habari zinasema kuwa Tyson alikuwa kwenye dirisha la kukatia tiketi la Shirika la Ndege la United Airline akiwa pamoja na familia yake (Mke na mtoto wake) na mpiga picha huyo alisogea ili apate picha ya karibu lakini aliambulia ngumi iliyomdondosha chini na kuvuja damu, Inasemekana Tyson alikamatwa na Police (pichani) na Paparazzo alikimbizwa hospital na Ambulance.
Tyson akiwa na Mkewe pamoja na Mtoto wake.
Ushabiki bwana we acha tuu…
November 12, 2009Gari aina ya Proton Gen 2 ikiwa katika nakshi za klabu ya Manchester United mitaani jijini Kuala Lumpur. Timu za soka za Uingereza zina ushabiki mkubwa sana kipande hii ya Asia huku zikiwa na Klabu za wanachama ambao inasemekana kuwa wanachama hawa wana nguvu sana na timu hizi zinatambua mchango wao na ndio maana hufanya ziara za mara kwa mara.
Pia timu kama arsenal na Man City zinafadhili mradi wa Football kwa watoto wadogo nchini Malaysia ambapo inasemekana Arsenal tayari wamepata watoto wawili ambao wanawafatilia kwa karibu.
Flaviana ang’ara
November 12, 2009Flaviana Matata former Miss Tanzania Universe and Model.
Russell Simmons hosted the LIFE Project for Africa Benefit at New York’s Ben & Jack’s Restaurant last night.
He brought little Russey, Justine, former Miss Tanzania Flaviana Matata, and his girlfriend Julie along with him.
Flaviana Matata with Russell Simmons at Tuesday night’s show. Flaviana Matata (born 1987) is a beauty queen who won the very first edition of the Miss Universe Tanzania pageant in 2007, and went on to represent her country in the Miss Universe pageant the same year, where she placed among the Top 15 semifinalists and ended up in 6th place after the evening gown competition. She was the first contestant from Tanzania to compete at Miss Universe, and compete with a shaved head.
Posted by piusmickys 
Posted by piusmickys
Posted by piusmickys 











