Marehemu Abdulhakim Magomelo aka Kim Pichani wakati wa uhai wake.
Picha hii ilipigwa mwaka 1991 wakati wa harusi yake.
DJ maarufu nchini aliyewahi kutamba katika medani ya muziki jijini Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla, Abdulhalim Magomelo ‘Kim & The Boys,’ hatimaye amezikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar Es Salaam jioni hii.
Kim ambaye alifariki majuzi kwa maradhi ya moyo. alijizolea umaarufu jijini na nchini kwa ujumla.
Wapenzi na mashabiki wa burudani, wataukumbuka mchango wake katika muziki na ucheshi wake, Kim ni Dj aliyewika vilivyo kwa umahiri wa kazi yake katika madisko mbalimbali jijini Dar es Salaam kama Mbowe Disco, na Silver Sands Disco. Vile vile Kim ni muasisi wa shindano la Yo-rap Bonanza.
Kwenye mazishi na shughuli nzima ya msiba watoto wote wa mjini walikuwepo, vijana wazamani, kuanzia wanamuziki wa kizazi kipya, ma Dj wa zamani na wapenda burudani wote.
Kim ndiye aliyeyatoa majina kama Black Moses (RIP), Ommy Sidney , Othman DigaDiga, Saleh Jabir, II Proud (Sugu / Mr II) pamoja na wengine wengi.
Kim ameacha mke na watoto watatu.
Ma DJ wa zamani wakiwa katika picha ya pamoja mara mbaada ya mazishi ya DJ mwenzao Abdulhakhim Magomelo DJ Kim and the Boy katika makaburi ya kisutu jijini Dare es salaam mazishi hayo yamefanyika saa kumi jioni na yamehudhuriwa na watu maarufu mbalimbali.
Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi. Amina.
Picha zote na Full Shangwe
Posted by piusmickys
Posted by piusmickys
Posted by piusmickys 












