Kipindi cha Maisha Plus bado kinaendelea na wiki hii majina matatu yametajwa kuingia kikaangoni ila kwa taarifa yako wiki hii hakuna mtu atakayetoka kwani unachotakiwa kufanya katika ya majina hayo matatu yaani Kauthar Toka Dar, Alex toka Mbeya na Neema wa Shinyanga, wawili kati yao wanatakiwa kwenda kwenye hoteli moja ya kula kuku.
Kauthar yeye anaingia kikaaongoni kwa mara ya tatu huku Neema akiingia kwa mara ya pili na Alex kwa mara ya kwanza. Siji kama ingekuwa kutoka nani ambaye angetoka kwani hatima huwa iko kwa watazamaji ambao humpigia kura mtu ya kubaki ambapo kwa wiki iliyopita Neema wa Shinyanga alipata kura zaidi ya elfu moja ili abaki huku mshiriki Kelvin kutoka Morogoro akiambulia kura mia tatu na ushehe tuu.
Angalia maoni ya wanakijiji juu ya nani atoke na kwa nini, Haya ni baadhi tu ya maoni yao.
Alex Mbeya ataka watu wajiamini na kusema kuwa kutokujiamini kunapelekea watu kuwa na hofu na kujenga makundi ndani ya kijiji.
Neema Tabora
Neneema yeye kwa upande wake alilalamikia ushirikiano mdogo na kusema unapelekea watu kutengana akiwataka watu waishi kama wanavyoishi kwenye uhalisia wao huko nyumbani.
William Iringa
Alimlalamikia Kaushak akisema kuwa Kauthar hafai kuwa kiongozi kwa kuwa ni mdhaifu na hajiamini kwa kutolea mfano kuwa kuwa yeye ndie kiongozi wa makundi ndani kijijini.
Jeremiah Dar
Yeye kwa upande wake alimpendekeza Alex wa Mbeya atoke kwa kuwa anasema kuwa wakati wake umefika na yeye ndiye anawakoroga pale kijijini kwani amekuwa akiwachanganya na kuwatenganisha. Anasema pale kijijini kila mt anahaki ya kuamua nani anampigia kura
Taiba Zanzibar
naye alimppigia kura Alex kwa sababu zinazofanana na Jeriamia akisema kuwa Alex amekuwa akipita huku na huku kuwataka watu wampigie fulani atoke jambo ambalo kwake anaona ni kinyume cha maadili ya kijijini.
Mwishehe wa Dodoma
Anasema Kauthar anatakiwa atoke kwa kuwa hawezi maisha ya kijijini kwani hata yeye mwenyewe Kauthar wakati mwingine anasema kuwa maisha yale hayawezi. amekuwa akilalamika sana na kuonyesha kuwa ni mdhaifu kwa maisha yale ya kijijini. Aliongeza kusema kuwa Kauthar amezoea maisha ya uzunguni zaidi.
Jaquiline wa Moro
Yeye alimtaja Luthende, yeye alisema mshkaji ana bore sana na anatabia ya uchoyo na umimi sana. Hapendi ushirikiano na saa nyingine kitu kidogo kinaweza kuwa kikubwa huku akitolea mfano mshkaji anaweza kukunyima kisu tuu. Kwa mujibu wa Jaq yeye anapenda kukuza mambo.
Leonard toka Dar
alimpendekeza Neema Tabora kuwa atoke ni mvivu hawezi kuamka asubuhi anapenda sana kujipodoa hawezi hata kuchota maji kwa kuwa make up kibao sio. Anasema mshkaji anaushirikiano mdogo kwa sababu ya uvivu wake.
Luthende Tabora
Anamshukuru Mungu kwa kumpa uzima na anasema kuwa matatizo yaliyopo ni madogo madogo tuu, kwa upande wa mtu anampendekeza Kauthar, anasema yeye kama yeye anadhani kuwa mchizi anamchukia, ye anasema kuwa hamchukii kuhitilafiana ni jambo la kawaida tuu.
Kingine anasema kuwa yule dada anakosea lakini hataki kuomba msamaha hivyo inamfanya kuwa mbinafsi sana. Kingine aliwahi kulalamika kuwa anabaguliwa alipoambiwa ataje alishindwa ana kusema kuwa ata afanywe nini hataji. Huo ni udhaifu na ameonyesha kutoaminiana. Ila kwa mtazamo wangu nikiangalia naona hapa kuna issue kati ya wawili hawa. ni mtazamo tuu.
Kauthar Dar
Kama nilivyosema kwa Kauthar sijui kati yao ni nini kinaendelea maana kwa washiriki wengine pamoja na kuwa wanatajana majina lakini inawachukua muda mfupi kuelezea sababu za kum nominate mtu jambo ambalo ni tofauti kati ya Luthende na Kauthar, wao wamechukua muda mwingi kila mmoja kuelezea ubaya wa mwenzake.
Kwa upande wa Kauthar ambaye ni mmoja wa washiriki toka mkoa wa Dar Es Salaam, Yeye anasema Luthende hamfagiliii hata kidogo, na pia alilalamikia kuwa watu wanambeza na kusema kuwa msomali akishinda watanzania wataandamana. anasema Luthende hajawahi kumtreat kibinadamu lakini anamuona yeye hastahili kukaa kijijini pale. Anadai kuwa katika kuhakikisha matkwa yake yanatimia hadi Babu aliitwa ili eti yeye aweze kutoa ufafanuzi wa malalamiko yake na aliye engineer ni Luthende jambo ambalo yeye binafsi hakulifurahia hata kidogo.
Julius Arusha (Mmasai)
Anasema kuwa Alex atoke ana kelele na hawezi kuwapa watu wengine nafasi ya kuonyesha kipawa chake na anatumia mwamvuli wa Uchungaji kujifanya mtakatifu wakati mambo anayoyafanya hayana manufaa kwa jamii.
Julius anadai kuwa mtu anatakiwa atajwe kutokana na tabia yake na kusisitiza kuwa Tabia za Alex si za kiungwana, alisema kuwa kutofautiana ni jambo la kawaida na kutoa mfano kuwa hata unapofungia mbuzi kwenye uzio lazima hata mmoja ataruka.
Kwa mujibu wa uongozi, wiki hii unatakiwa kupiga kura ili washiriki wawili wakale misosi kwenye moja ya hoteli za kitalii kwani anayepigiwa kura hatotoka.
Hii inamaana gani hii itawafanya washiriki wapunguze chuku kwa kutajana majina kwa ajili ya visasi zaidi kwani inawafanya kujiona kuwa hakuna nafasi ya kusameheana au kulippiziana kisasi isipokuwa kum nominate mtu jambo ambalo si msingi hasa wa Maisha Plus.
Tuonane kesho tena kwenye muendelezo wa Maisha Plus….