June

Monday, June 30, 2008

Karibuni nyumbani mwayego….!

A German supporter waits on a traffic light for the arrival of the German football team with thousands of supporters who gathered at Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008 to greet their team upon their return from Vienna, where they lost by 0-1 to Spain in the final of the Euro 2008 Football Championships June 29. AFP PHOTO JOHN MACDOUGALL (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Shabiki wa Timu ya Ujerumani akiwa amesimama juu ya Taa za kuongozea magari wakati wachezaji na makocha wa Timu ya Taifa ya Ujerumani wakiwasili huko Ujerumani jana, Hebu pata picha hawa jaa wangeshinda mtiti ungekuwaje?

Germany's striker Lukas Podolski sings to supporters of the German football team at the "Fanmeile" (fan zone) next to Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, the day after the Euro 2008 final Germany vs Spain in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO DDP/POOL/ GERO BRELOER  (Photo credit should read GERO BRELOER/AFP/Getty Images)
Mchezaji wa Ujerumani Lukas Podolski (Juu na chini pichani) akiimba mbele ya mashabiki waliokusanyika kuwapokea mashujaa wao.
Germany's striker Lukas Podolski appears on a giant screen as thousands of fans cheer the German national football team at the "Fanmeile" (fan zone) in front of Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, one day after the Euro 2008 final Germany vs Spain, held at Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria. Spain ended their 44-year wait for a major international title with a 1-0 victory over Germany at the Euro 2008 final.      AFP PHOTO  DDP/ MICHAEL GOTTSCHALK (Photo credit should read MICHAEL GOTTSCHALK/AFP/Getty Images)


Germany's head coach Joachim Loew (L) signs his name in the city's Golden Book next to Berlin's Mayor Klaus Wowereit as supporters of the German football team gather at the "Fanmeile" (fan zone) next to Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, the day after the Euro 2008 final Germany vs Spain in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO DDP/POOL/ GERO BRELOER  (Photo credit should read GERO BRELOER/AFP/Getty Images)

Kocha wa Ujerumani Joachim Loew (L) akitia mkono kwenye kitabu cha city’s Golden Book kulia kwake anayemkazia jicho ni Meya wa Berlin Klaus Wowereit pale mamia kwa maelfu ya washabiki wa Ujerumani walipokusanyika “Fanmeile” (fan zone) huko Berlin
Hii ni baada ya mchezo wao wa jana na Hispania kwenye fainali za Euro 2008 na Spain kushinda kwa 1-0. Picha zote na AFP

Serena na Venus hatarini kucheza Fainali wao kwa wao

Venus Williams
Venus na Serena, Ndugu wote wawili wameshinda mechi zao leo Jumatatu huko Wimbledon, Kama mambo yakienda hivi basi kuna hati hati ya Wawili hao ambao ni mtu na dada yake kucheza Fainali wao kwa wao. (Picha na AP)

Kili Music Award yafana

Wasanii mbali mbali wamefanikiwa kunyakua Tuzo mbali mbali kwenye tamasha la Kili Music Award usiku wa kuamkia leo, Kwa habari na picha zaidi bofya hapa kwa Haki Ngowi (Picha na Haki Ngowi)

Mchezaji Taifa Stars adaiwa “Jezi” baada ya kubadilishana na Eto’o wa Cameroon

Kipanya wa Leo na habari ndio hiyo hapo chini…

Na Phillip Nkini wa Mwananchi

UMILIKI wa jezi za timu ya Taifa Stars umezua balaa kwa baadhi ya wachezaji wa timu hiyo kujikuta wakikatwa fedha zao za posho kwa madai ya kufidia jezi ambazo ama walibadilishana na wenzao wa Cameroon au kupoteza.

Kwa upande wake, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linasema: ”Jezi si mali ya wachezaji.”

Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries na Benki ya NMB, wadhamini wa Stars wamekuwa wakitoa vifaa kwa wachezaji wa timu hiyo kuanzia vile vya mazoezi hadi vya mechi mbalimbali ambazo timu hiyo imekuwa ikicheza.

Lakini, pamoja na hali hiyo kumezuka tatizo kwa baadhi yao (wachezaji) na uongozi wa timu hiyo kukosana baada ya baadhi yao kubadilishana jezi majuzi na wachezaji wa Cameroon, Indomitable Lions, jambo ambalo limewazulia mambo.

Mchezaji mmoja kinda wa timu hiyo (jina tunalo) alishindwa kumpa Geremi Njitap wa Cameroon jezi yake kwenye mchezo kati ya Stars na Cameroon mjini Yaounde baada ya mchezaji huyo kutaka wabadilishane.

Kinda huyo aliiambia Mwananchi kuwa alihofia kuja kurejea nchini na kudaiwa jezi.

Lakini, beki wa timu hiyo alibadilishana jezi na mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto’o Fils baada ya Mcameroon huyo kumfuata mwenyewe na kumtaka afanye hivyo.

Hata hivyo, pamoja na wachezaji hao kudaiwa jezi hizo Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage aliithibithishia Mwananchi kuwa jezi si mali ya wachezaji, bali ni mali ya shirikisho hilo na mchezaji atakapoipoteza, basi utaratibu wa malipo utafanywa.

”Jezi sio mali ya wachezaji ni mali ya Shirikisho la Soka, kila mchezaji anapewa jezi kwa kufuata utaratibu maalum ukipewa lazima urudishe usiporudisha unaandaliwa utaratibu wa kulipia.”

“Sisi bado tupo nyuma sana hatujafika huko walipo hao akina Senegal au Cameroon kuwa na wadhamini wakubwa, kiasi kwamba mchezaji mmoja kuwa na jezi zaidi ya kumi. Hapa kwetu, tunaweza kutumia jezi moja kwenye mechi mbili wenzetu kila mechi na jezi yake.

”Ukiangalia mchezaji kama Eto’o anandaliwa jezi zaidi ya 50 na Kampuni ya Puma ni tofauti sana na sisi, ingawa kubadilishana moja mbili siyo vibaya, lakini isiwe watu kumi na kuendelea,” alisema Kaijage.

Uchunguzi wa Mwananchi umeonyesha kuwa wachezaji hao wa Stars wamekuwa hata wakati mwingine wakipigiwa simu wakiwa majumbani kwao ili warudishe jezi ambazo wamekuwa wakiondoka nazo kwa bahati mbaya au ambazo zimekuwa zikipotea.

Ukweli ni kuwa kila mchezaji wa Stars anapopoteza jezi moja hukatwa posho yake kuanzia Sh20,000 na kuendelea.

Hali hiyo ndiyo inayosemekana kuwa itamkumba beki na nahodha msaidizi, Nadir Haroub Cannavaro aliyeamua kubadilisha jezi na Eto’o.

Eto’o, ambaye yuko katika ziara ya nchi kadhaa za Afrika, alionekana jijini Kampala, Uganda akiwa na jezi yenye nembo ya NMB huku akitoa mafunzo ya soka kwa watoto.

Werasson awakana wanamuziki wa Congo nchini

[image]

MWANAMUZIKI mkongwe wa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Kongo, Werasson amesema hamjui mwanamuziki hata mmoja kutoka Kongo anafanya muziki hapa Tanzania.

Hivi karibuni wanamuziki wengi kutoka Kongo waliokuja hapa nchini walijitangaza kuwa wengine ni ndugu wa Werrason huku wengine wakisema kuwa wenyewe ni watoto wa mkongwe wa Muziki nchini humo Pepe Kalle, na katika tukio la karibuni ni pale mwanamuziki ally Choki alipoonekana amepiga picha na Werason alipokwenda kutafuta wanamuziki huko na kusema kuwa Werasson alimsaidia kutafuta vijana.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam juzi Werasson alisema ‘simfahamu mwanamuziki hata mmoja wa Tanzania wala mkongo ambaye anaimba muziki hapa huyo anayejiita mtoto wa Pepe Kalle pia hamfahamu.

“Mimi nipo na mtoto mmoja wa Pepe Kalle ambaye namfundisha muziki pale Kongo, lakini huyu wa Tanzania mimi simfahamu kwakuwa watoto wake wote nawajua na hivyo labda awe mwingine zaidi,” alisema Werassons.

Werrason alisema kwa kuwa hawajui wanamuziki wa Kongo walipo hapa nchini lakini yuko tayari kukutanao na kufanya mazungumzo ya kuendelea muziki Tanzania.
(Picha na Mpoki Bukuku)

Wajerumani “Mbendembende” kwa Waspaniola

Germany 0-1 Spain
Spain's Iker Casillas celebrates with the trophy after the Euro 2008 final between Germany and Spain in the Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria, Sunday, June 29, 2008, the last day of the European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Spain defeated Germany 1-0.
Wachezaji wa Spain wakisheherekea baada ya kukabidhiwa “mwali ” wao

In this handout picture distributed by Spain's soccer Federation, Spain's King Juan Carlos, right, holds the Euro 2008 European Soccer Championship trophy with Spain's Prime Minister Jose Luis Rodriguez Zapatero, left, standing beside him.  Spain's soccer team won the trophy by beating Germany 0-1 in the final of Euro 2008 championship played Sunday in Vienna, Austria.
Pichani ni Mfalme wa Spain Juan Carlos, aliyeshika kombe walilokabidhiwa Spain jana na kushoto kwake ni Waziri Mkuu wa Spain Jose Luis Rodriguez Zapatero usiku wa kuamkia leo.
Some German supporters sit on the ground on a huge German flag in the Munich fan zone at the Olympic stadium after the Euro 2008 championships final football match Germany vs. Spain on June 29, 2008 at Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO   DDP / TIMM SCHAMBERGER   (Photo credit should read TIMM SCHAMBERGER/AFP/Getty Images)
Mashabiki wa Ujerumani wakiwa hawaamini kilichotokea wamebaki uwanjani hata baada ya mpira kumalizika.
Germany's Micheal Ballack reacts at the end of the Euro 2008 final between Germany and Spain in the Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria, Sunday, June 29, 2008, the last day of the European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Spain defeated Germany 1-0.
Kepteni wa Ujerumani Micheal Ballack akiwa haamini kama dakika 90 zimekwisha na wameshindwa kuchomoa goli moja la Spain katika mchezo uliofanyika Ernst-Happel stadium huko Vienna, Austria,
(Picha zote na AP)

Fernando Torres ndiye shujaa wa Spain baada ya kupachika bao dakika yaa 33 bao lililodumu hadi kipyenga cha mwisho na kuwafanya Spain kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa Mtanange wa Euro 2008 baada ya kuisaka nafasi hiyo kwa miaka 44.

Torres alipachika bao hilo swafi dakika ya 33 ya mchezo kipindi cha kwanza licha ya juhudi za Kapteni wa Ujerumani Ballack waspaniola walikaza na kulinda goli lao huku wakifanya mashambulizi ya hapa na pale.

Huku akisherehekea miaka 70 ya kuzaliwa , Kocha Luis Aragones alitanabaisha atang’atuka kuifunza timu ya Spain na inasemekana Kocha mwingine Vicente del Bosque ndiye anaweza kuchukua timu hiyo ambayo kwa bahati atarithi vijana wenye vipaji wadogo na wenye hari na mtazamo kwenye kombe la Dunia.
Mpaka dakika 90 bao likabaki 1-0, ama kwa hakika kanauma, kamonga tuu!!

Sunday, June 29, 2008

Vijimambo ndani ya Zoo Negara – Malaysia

Naambiwa hawa Rhino na Twigo walichukuliwa wadogo kutoka mbuga yetu ya Serengeti.!!
Nia yangu ilikupa nami nipate picha kama ya mdau wangu Mwinda hapo chini kwa ajili ya kumbukumbu tuu ila mhh jamaa akakohoa tuu huo mcheche wake usipime, Huyu jamaa anatisha kinoma. Ni vijimambo ndani ya Zoo Negara.

Sio mbaya

Saturday, June 28, 2008

Werason awasha moto Dar








Mwanamuziki Werasson Ngiama Makanda usiku wa leo amefanya balaa katika ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwapagawisha vilivyo mamia kwa maelfu ya mashabiki walifika katika onyesho hilo.
Werasson ambaye ameingia nchini majuzi aliingia jukwaani kama kawaida lilitangulia sebene na kisha yeye kuingia huku akiimba wimbo maarufu wa Kala Yi Boing Remix huku mashabiki lukuki nao wakimfatiisha kwa kuimba naye, kisha alifululizwa kwa vibao kama Sourire ambacho kinapatikana kwenye Albamu ya Zamani ya Volume I, Solo la bien,Kibuisa Mpipa, Kuna nyimbo inaitwa Simeone inapatikana kwenye single Album Soul Soul.
Mashabiki walipagawishwa na mauno ya mwandada mrembo aliyeumbika si kitoto Bibiciya Mfwengi kila mara alikuwa akijivuta mbele na kijana wa atalaku kama kawa anampa mapande mashaki wote wana lipuka kwa mayowe.

Kwa ujumla shoo ilikuwa nzuri na kila mtu aliyeingia aliridhika na burudani ya haja aliyoipa.
Awali akizungumza na waandishi wa habari Werasson alisema kuwa amekaidi wito wa Rais wa Kongo Brazaville Denis Sasou Nguesso aliyemtaka kwenda kufanya shoo kadhaa kwa wiki nzima lakini alisema kuwa hawezi kuwaangusha mashabiki wake wa Dar Es Salaam ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakimngojea hasa baada ya onyesho la awali kutofanyika huku watu wakiwa wameshakata tiketi.
Werasson na kundi lake la wanamuziki 24 watapiga Arusha kesho.
Kama nakuona Big Producer Maghambo Philipo – Baba Martha, Collins na Fikire wazee wa USA, Mukubwa Ling’ande, Mwanangu Dulla nakati ya IFM, Abuu na Boss Chizenga!! Tuko pamoja.
Picha na Big Producer Magambo/Mpoki Bukuku

Sylvia Mashuda atwaa taji la Miss Ilala 2008

Kanda ya Ilala imekuwa ya kwanza kufungua pazia la mashindano ya Miss Tanzania ngazi ya Kanda kwa Mkoa wa Dar Esalaam hapo jana na mrembo Sylvia Mashuda katikati kunyakua taji hilo katika shindano lililofanyika usiku wa kuamkia leo pale Raiway Gerezani sasa ni City Garden Club. Kushoto ni mshindi wa pili, Nelly Kamwelu(kushoto) na mwingine ni Aneth John. Sylvia anamiaka 19 amemaliza, Form VI anangojea kujiunga na chuo kikuu.

mpira Maalum wa Fainali EURO 2008

Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas kwa kushirikiana na EURO2008 wametangaza aina ya mpira maalum utakao tumika kwa ajili ya Mtanange wa fainali kesho kati ya mabingwa mara tatu Ujerumani na mabingwa wa 1964 Hispania. Mpira huo umepewa jina la Euro Pass.
Mipira 30 yenye rangi ya Silver ambayo itakuwa na majina ya wababe hao wa timu mbili zinazokutana fainali.

Pia imefahamika kuwa Kombe ambalo litanyakuliwa ama na Michael Balack wa Ujerumani au Casillas wa Hispania hapo kesho litakuwa na kilo mbili za uzito zaidi wa kombe la awali ambalo Theodoros Zagoraskis wa Ugiriki alilinyakua mwaka 2004.

Kombe jipya lina uzito wa kilo 8 na urefu wa sentimita 60 limepewa jina la Henri Delaunay, aliyekuwa Katibu wa zamani wa shirikisho la mchezo huu Mfaransa ambaye alitoa mchango mkubwa kwenye historia ya mashindano haya.

JB Mpiana alipofanya kweli Ufaransa

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

Kama kawaida Ziara ya JB Mpiana ilihitimishwa Ndani ya Bataclan Paris, Ufaransa tarehe 22 mwezi huu na mambo yalikuwa moto, JB Mpiana anayetamba na Albamu yake Mpya Ya Quel Est Ton Probleme? Aliwaburudisha mashabiki walijaza ukumbi kwa nyimbo za zamani na zikichanganyika na mpya, Kama Zadio Congolo, Mtindo wa Lopele pia mashabiki walilipuka nao kinoma, Kali ni pale kibao matata cha Liberez kilipoanza kuimbwa, Wimbo huu umo kwenye Albamm yake mpya na umetokea kupendwa sana. Liberez ni utunzi wa mwanamuziki mpiga Bass gitaa wa Wenge BCBG Sunda Bass. Onyesho limesifiwa kwa kuwa na Sound System nzuri na Jb alitumia muda vizuri na muda wote mashabiki walifurahi.
Pata Kitu Liberez

Jiachie Kisela

Lebo zinazidi kutoka kila kukicha, ubunifu ndio unaotakiwa, Jiachie Kisela Kitu ndani ya Ulimwengu wa Lebo za nyumbani.

Friday, June 27, 2008

Werasson: Niko tayari kupiga na JB Mpiana Tanzania

Pichani ni Rais wa Kongo RDC Joseph Kabila akiwa na timu ya Wanamuziki akiwemo Marehemu Madilu System alipokutana nao na kuwapatanisha baadhi yao akiwemo JB Mpiana na Werasson mwaka juzi.

MWANAMUZIKI hodari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ngiama Makanda ‘Werrason’ amewasili Dar es Salaam na kusema yupo tayari kupiga pamoja na Jean Bedel Mpiana ‘JB Mpiana’ endapo atapatikana promota wa kuwaleta Tanzania kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania.

Msanii huyo aliwasili juzi jioni akitokea Jamhuri ya Kongo ambapo na kundi la wanamuziki 24, anatarajiwa kutoa burudani kesho kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza kabla ya kupiga Arusha Jumapili kwenye Hoteli ya Naura Springs.

Endapo ‘Werrason’ atapiga pamoja na ‘JB’ Mpiana itakuwa ni historia baada ya nyota hao kuingia katika mzozo mkubwa ulioibua vita kati yao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Makanda alisema atafurahi kupiga pamoja na Mpiana ambaye inadaiwa ni wapinzani na chanzo cha kuvunjika kwa kundi maarufu la Wenge BCBG lililowahi kutamba Afrika.

“Sina matatizo na Mpiana ni rafiki yangu napenda siku moja nije naye hapa tufanye onesho la pamoja nipo tayari hata sasa cha msingi apatikane promota mwenye uwezo nitamwambia lakini naomba nipate uhakika kama mnatuhitaji kabla ya mwaka huu kumalizika,” alisema Makanda.

Makanda alisema anapenda kuona muziki wa Tanzania unapiga hatua kama ilivyo Jamhuri ya Kongo na kuongeza kuwa endapo atapata fursa ya kuzungumza nao atawashawishi watengeneze albamu ya pamoja.

Msanii huyo alisema alishindwa kutoa burudani mwaka jana kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake na alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi Watanzania kutokana na tukio hilo.

Alisema amejiandaa kuacha historia kwa kupiga nyimbo zake mfululizo ili kukata kiu ya mashabiki wa burudani ambao walikuwa na shauku kubwa ya kumuona nyota huyo akiwa jukwaani katika ardhi ya Tanzania.

Ziara ya mwanamuziki huyo imedhaminiwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya Embassy kwa kushirikiana na Club E.

Kipanya adhamini Miss Temeke

MSANII maarufu katika uchoraji wa katuni za siasa na sasa akiwa mbunifu maarufu wa mitindo nchini, Ali Masoud ‘Kipanya’ amejitosa kudhamini wa mashindano ya kumsaka Miss Temeke 2008.

Mratibu wa Miss Temeke, Benny Kisaka alisema Masoud, ambaye hutumia lebo ya KP, ambayo ni kifupi cha Kipanya, atawazawadia washindi watatu wa kwanza wa Miss Temeke nguo za watakazotumia katika fainali za Vodacom Miss Tanzania 2008, zitakazofanyika baadaye mwaka huu.

Alisema Temeke, ambayo inafunga dimba katika mashindano ya urembo ya kanda kwa mwaka huu, pia atatoa nguo maalum za shoo ya ufunguzi kwa warembo wote.

Alisema kwa sasa vimwana 12 wanaendelea kujifua chini ya Miss Temeke 2006, Jokate Mwegelo, ambaye anawafundisha mbinu za kutumia vyema jukwaa, unadhifu, kujengwa kisaikolojia na kuwapa uwezo wa kujiamini na hata kujibu maswali. Wasichana hao wanatoka katika vitongoji vya Kigamboni, Kurasini, Temeke Kusini na Chang’ombe.

Warembo hao ni Sheila Ally, Radhia Omary, Lilian Shayo, Zainabu Ally, Rona Swai, Nuru Hassan, Mwash Ramadhan, Angela Lubala, Caroline Sechuma, Glory Charles, Florence Josephat na Evelin Issack.

Werasson kuanzia Ubungo Plaza Leo

Mkurugenzi wa Clouds fm/Prime Time Promotions Joseph Kusaga akiteta jambo na Werrason mara baada ya kuwasili Dar. Werrason anatafanya onesho lake la kwanza leo Ijumaa usiku Ubungo Plaza ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni sh 20,000/= pamoja na msosi wa nguvu, Pia leo atafanya mahojiano ya moja kwa moja na kituo cha Radio cha Clouds FM kupitia kipindi cha African Bambataa kinachoongozwa na Bibi Sophia KEssy, Big Producer Maghambo, Boss Chizenga, Mukubwa Collins, Dulla Boy na kati ya IFM, Mama Irene Maggi, Fikiri Le Boss, Abuu na wapenzi wote wa Werasson kila la heri najua hamtakosa. Picha na Issa Michuzi.

Brazil yasherehekea miaka 50 tangu ichukue Kombe la Dunia

Brazilian President Luiz Inacio Lula da Silva (L) embraces Brazilian football legend Edson Arantes do Nacimento, known as Pele, as he decorates the winners of the 1958 World Cup, during the opening ceremony of an exposition celebrating the 50th anniversary of Brazil's first victory in this tournament, at Planalto palace in Brasilia on June 26, 2008.  AFP PHOTO/Joedson ALVES (Photo credit should read JOEDSON ALVES/AFP/Getty Images)
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva shoto, akiwa amemkumbatia Mfalme wa soka la Brazil Edson Arantes do Nacimento, au Pele, Brasil inasherehekea miaka 50 tangu walipochukua Kombe la Dunia mwaka 1958 kwa shamra shamra za ina mbali mbali, sherehe hizi zilifanyika Planalto palace huko Brasilia jana tarehe June 26, 2008.

Spain yaigalagaza Russia 3-0….!

Russia 0 – 3 Spain

Spain's Xabi Alonso, Joan Capdevila, Xavi Hernandez and Fernando Navarro

Wachezaji wa Hispania, wakisherehekea ushindi wao mara baada ya kipyenga cha mwisho

Ama kweli ukitaka kumuua nyani usimuangalie usoni, ndivyo walivyofanya Waspaniola usiku huu walipomchapa Russia bila huruma mabao matatu bila kufurukuta.
Ikiwa ni fainali yao ya kwanza baada ya miaka 24 wamewafungisha virago Russia na sasa watautana na Ujerumani na Russia watacheza na Uturuki kutafuta mshindi wa tatu.

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa vijana wa Luis Aragones kwani walikuwa wakishambulia muda wote bila kupumzika na kufanikiwa kupata goli la kuongoza kipindi cha pili kupitia kwa Xavi, ambaye baadaye alibadilishana na Xabi Aronso dakika ya 69. Pia aliingia Daniel Guiza dakika hiyo ya 69 na dakika 4 baada ya kuingia alipachika bao la pili kwa Hispaniola na goli la tatu lilifungwa na David Silva dakika ya 82 na kuwapa tiketi ya kukutana na Ujerumani siku ya Jumapili.

Russian football fans celebrate the success of the Russian national soccer team in Euro 2008 after watching the semi-final match between Russia Spain in Moscow early June 27, 2008. Despite Spain's 3-0 win, it has been more than 20 years since Russia has had such a serious presence on the international footabll stage and many citizens are proud of their team's performance. AFP PHOTO / NATALIA KOLESNIKOVA (Photo credit should read NATALIA KOLESNIKOVA/AFP/Getty Images)
Pamoja na kufungwa Mashabiki wa Russia walikuwa wakisherehekea kwa kile walichosema mafanikio ya timu yao kufika nusu fainali, si haba.

Matokeo haya yameinyima Russia nafasi ya kucheza Fainali kwa mara ya kwanza tangu kuunjika kwa muungano wa kisobvieti. Russia alichapwa 4-1 na Spain wakati wa mchezo wa ufunguzi.

Spain waliutawala mchezo kuanzia kipindi chwa kwanza lakini hawakuweza kupata goli lolote kwani Russia walikaza namna fulani, lakini marekebisho na mawaidha ya kocha kipindi cha mapumziko yalizaa matunda.

Thursday, June 26, 2008

Ngoma Africa Band na Nyimbo za masimulizi!

*Ras Makunja kamrushia madongo Baba wa Kambo!?

Bendi maarufu ya mziki wa dansi the Ngoma Africa Band,inayoongozwa na mwanamziki

maarufu Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Ebby Makunja “Bw.Kichwa Ngumu”

Imeibua zogo la gumzo lingine kwa kufyatua wimbo wao uliobeba jina la “Baba wa kambo”

wimbo huo umefyatuliwa wakati CD yao “Apache wacha Pombe” inawasha moto mkali wa kimataifa !

wimbo wao huo wa “Baba wa Kambo” ulifyatuliwa katika kuadhimisha sikuu ya watoto dunian! wimbo huo unawakilisha kilio cha mamilion ya watoto wanao teseka katika utwala wa kidikteta wa kina “Baba wa Kambo” ni utunzi wake tena kiongozi na mwimbaji wa bendi

Ebrahim Makunja.

Katika wimbo huo Ras Makunja amemrushia lawama(madongo) “Baba wa kambo” na kikosi

cha Ngoma Africa kikimsindikiza kwa kumzomea !baba wa kambo tunakushikia bango!

Kindumbwe Ndumbwe Charia ! na Nguo! kaitia moto!

Bendi hiyo maarufu inayopeperusha bendera ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa,

imefanikiwa kuliachia song hilo ambalo linamshitaki “Baba wa kambo” Kwa Jamii!

na jamii pamoja na tahasisi zake zifanye kila njia kutupia jicho swala la maelezi ya watoto

ambao ulelewa na kina baba wa kufikia maarufu kwa jina la “Baba wa Kambo”

madongo hayo ya Ras Makunja na kikosi chake The Ngoma Africa hayakuishia hapo tu

bali lawama nazo zimerushiwa kwa kwa MAMA ALIYELEWA MAPENZI na kumshau mwanae akiteswa na “Baba wa Kambo”

Mzozo huo katika ya Baba wa kambo na The Ngoma Africa band utapelekwa kwa jamii hili

upatikane uhamuzi nani ?mwenye makosa Baba wa Kambo! au Mama Aliyelewa Mapenzi!

au Ngoma Africa Band waliomzomea baba wa kambo na kuweka mateso yake yote uwanjani yajadaliwe na jamii?

Baadhi ya Malalamiko ya ngoma africa kuwa “Baba wa Kambo” anamfanyishwa YATIMA kazi ya kutafuta kuni !wakati watoto wengine wapo shuleni! anamnyima ELimu yatima!

wakati Elimu ni ufunguo wa maisha,anampa KISAGO CHA MOTO yatima,anamlaza chumba cha Uwani karibu na chooni !kula na kulala kwa shida!

Baba wa Kambo naye labda atalalamika kuwa kiongozi wa bendi hiyo ni mwanamziki mwenye GUBU! kawashawishi wenziwe kumzomea wakati mila zinasema usimzomehe mkubwa!

hatujui Jamii itamuhua nini? au nani mwenye makosa

Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri aja kivingine July

Solo thang akiwa na Mtoto wake Yassir nyumbani kwake, huko UK

Muziki ni safari, Kwa wanaokumbuka enzi hizo ukilitaja jina Solo Thang kila mtu mpenda Muziki anasisimuka, kwani ni mmoja wa wanamuziki wa Kizazi kipya ambao kwa kiasi kikubwa “walipigana vita ya msituni” kufanya muziki huu ukubalike kwa jamii. Kwa sasa Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri anaishi Uingereza akiwa ameoa na mtoto mmoja anayeitwa YASSIR na Mama yake anaitwa YASMIN.
Kwa muda sasa mwanamuziki Solo Thang amekuwa kimya kutaka kujua yuko wapi Spoti Starehe tumefanya mahojiano naye kutaka kujua machache toka kwake na maisha yake hasa ya kisanii kwenye sanaa nzima ya Muziki.

Spoti na Starehe (S na S): Mara ya mwisho nilisoma Interview yako Bongo5 ile Albamu uliyofanyia huku ughaibuni ilitoka kaka nataka mawili matatu kaka.

Solo: okee,bado ndo naiweka sawa kakakuna mambo mengi na shule ilinibana mkuu.

S na S: Jina ni bado lile lile la Albamu?

Solo: Yaa inaitwa TRAVELLER, ndio jina waliokuwa wananita enzi nasoma jitegemee….99

S na S: oooh poa sana, sasa unategemea kuimaliza lini, i mean itakuwa sokoni?

Solo: Kama nilivyo Kwambia kuna mambo namalizia ila Inshallah Hivi karibuni nitaanza na Single

Akiwa pamoja na Dj lee flex, na mdau baraka, DJ Lee ni mmoja wa Madj ambao wanaitangaza Bongo Flava Nje.

S na S: Vipi Maisha kwa ujumla nasikia ulikuwa unasoma, Je zaidi kumaliza Chuo cha Diplomasia pale Kurasini kuna chochote tena?

Solo : Shule kama kawa kaka haina mwisho,we learn new things daily ..nilishamaliza baadhi ya courses na nitaendelea na buku.kwa sasa napiga mzigo nakuiweka sawa family!


S na S: oooh safi sana mkuu kila la heri, Je unaionaje game kaka na ujio wa vijana wapya ukilinganisha na enzi zenu? nani mpya unamfeel sana?

Solo: Mmh well vijana wanatisha wanajitahidi ila FID Q yuko poa, CHIDI mwanangu yuko bomba

S na S: Je hufikirii kufanya kolabo na wanamuziki tofauti na wa nyumbani ili uende kimataifa zadi unalizungumziaje hili mkuu?

Solo: hicho ndio kilichonifanya niwe kimya kidogo,kunavitu vingi nilikuwa nafikiria jinsi kuviboresha ikiwa na kuliingilia soko la kimataifa babu, natarajia kutoa single mwezi july tarehe nitaitangaza baadae kaka

S na S: Single hiyo umemshirikisha nani babu? ni ya kiswahili au?

Solo: Nyimbo nitakazo toa kuanzia sasa zitakuwa na version mbili moja ya kiswahili na remix ambayo itakuwa ya kiingereza

S na S: Je mkubwa unazungumziaje wanamuziki wa Kenya ukilinganisha na wenzao wa Tanzania ambapo wengi wa Kenya wanapata shoo nyigi za nje, je hii ni kusema Genge inakubalika zaidi ya Bongo Flava kaka?

Solo hakuna babu,show ni connections na jinsi gani wasanii wanajiuza,inabidi wabongo tutumie sana mitandao katika kunadi kazi zetu…..kwa hiyo matumizi ya computer ni muhimu sana katika kujitangaza babu na nijukumu la wabongo walio nje ya nch kusupport vipaji vya home,kama Uk wapo baadhi ya maDj wakibongo wanajitahidi sana katika kuutangaza mziki wetu kuna jamaa wanajiita bongo flavour familly,Dj Jimmy blanks,kina Dj habib,Dj lee flex…..etc, ni jukumu la wabongo walio na michongo kumegeana babu

S na S: Kuna upande mwingine hata wewe uliupigia kelele sana kuhusu Wasambazaji kule nyumbani Bongo ambao bado ni hao hao kuna jinsi kweli ya kuepukana nao “wadosi” kama ipo kwa jinsi gani?

Solo: ipo dawa ni kuwa na umoja na kuwatosa,pia tunaweza kuuza kazi zetu kwa njia ya mtandao….kama itunes, beta record na store nyingine nyngi tu za muziki

S na S: Hapo utakuwa unalizungumzia soko la nje je kwa mikoani ambapo kazi zenu zinanunuliwa zaidi na jijini ambapo ndio kuna soko kubwa lakini ni rahisi kupata nyimbo za mwanamuziki kwa mtu ku burn CD tena toka kwa wanamuziki unasemaje kwa haya mawili?

Solo:ndo maana nikasema umoja muhimu!naamini wanamuziki sisi ndio waathirika wa hili,kama tutakuwa na msimamo kwa pamoja si kazi kupata suluhisho la hil, kama wadosi watakataa kubadilika ni kususia kuuza kazi zetu kwao naaamini watajitokeza tuwatu wa kununua kazi zetu,au tunaweza kuweka utaratibu wa kuuza wenyewe vyote inawezekana muhimu ni kujipanga….nakumbuka Mr Two alishawahi kukomaa na kusambaza mwenyewe na Kilimanjaro band kama sikusei

its all possible..pia wabongo waelimishwe umuhimu wa kununua nakala halisi na si zakukopy,ili kusupport vipaji vya nyumbani,la sivyo itabaki majina tu yanavuma mifuko imetoboka

“Traveller” Mitaani ughaibuni.

S na S: Je umewahi kuwaza kuwa na Chama chenu ili muwe na sauti moja? unafikiri hili linawezekana?

Solo: unajua tatizo njaa babu kwenye njaa hakuna msimamo…..vyama huwa vinaanzisha ila havidumu na huwa havina nguvu…..sababu mnaweza kupanga hili,baadhi wakazunguka! sauti moja ndo inatakiwa ya wasanii nchi nzima. Tukae chini na wadosi watueleze tatizo nini?kazi zinavuka mpaka mipaka hakuna mjadala wa hilo!, pia nimeanzisha blog yangu ili kuwapa latest mashabiki zangu pamoja na habari zingine za burudani ndani na nje ya bongo http://www.solothang.blogspot.com.

S na S: Elimu na usanii haviingiliani ila vinategemeana pia je kuna mabadiliko yeyote unayahisi kwa kipindi kile na sasa baada ya vidato kadhaa kimuziki?

Solo: makubwa kaka,am grown up now ha ha with wife and son,kuishi ngambo pia kunakupa experience kubwa kila ninachokiwaza na kwa faida yangu na family, which means siwazi kunyonywa tena.
S na S: Hongera sana kwa hilo!! Kila mtu anafikiria kuwekeza kwenye Studio na kwa sasa kila kona kuna Studio Dar hadi limekaa njema hili mkuu?
Solo: Studio kila kona poa muhimu kama zitakuwa na viwango tu babu,pia inaleta ushindani na ni mzuri kibiashara.

“when it comes to Mic,Rhyme!! man am baaad..”

S na S: Je una lolote la kuwaeleza MAshabiki, Wanamuziki wenzio, au hata wadau wa Muziki hata “wadosi”?

Solo; Mashabiki kwanza nawaomba msamaha kwa ukimya,pili wakae mkao wa kula soon tunaanzia July kwa washkaji ni muhimu kuwa na plan B,wasitegemee tu mziki kama kitega uchumi,wa Invest pesa wanayoipata ili kuwa na nyenzo nyingine ya kuingiza kipato,maisha mchakamchaka, fani yetu haina pension,so we need to work hard for the future,na nawatakia kila la kheri

S na S: Asante kaka kwa muda wako kila la heri kwenye shughuli zako

Solo: Asante sana kaka nawe pia.

Pata burudani ya Solo thang na Q Chilla kwa kubofya hapa


Esther Nabaasa: Mshindi wa Tusker Project Fame mwaka huu

Esther Nabaasa Mugizi
Esther ana miaka 21 ni mwanafunzi wa Makerere University ambako anachukua Degree ya Telecommunication Engineering.

ESTHER Nabaasa kutoka Uganda, ametwaa kitita cha Sh85milioni baada ya kushinda shindano la Tusker Project Fame lililomalizika mwishoni mwa wiki jijini Nairobi.

Kwa ushindi huo, Esther alijipatia zawadi ya S milioni tano za Kenya na mkataba wa kutengenezewa albamu na kampuni kubwa ya kurekodi ya Galo iliyopo Afrika Kusini.

Nafasi ya pili ilitwaliwa na Wendy Kimani wa Kenya ambaye alijipatia shilingi milioni 2.5 za Kenya.

Katika hatua hiyo ya mwisho iliyokusanya maelfu ya mashabiki ukumbini, washiriki wanne waliobaki walipanda jukwaani na kuimba nyimbo tatu kila mmoja.

Washiriki wengine wawili wa kiume, David Ogola na Victor Asava walishindwa kuimba katika hatua hiyo.

Baada ya kila mshiriki kuimba wimbo mmoja, msanii kutoka Tanzania, Ambwene Yesaya ‘AY’ alipanda jukwaani na kutoa burudani kwa kuimba wimbo wake wa Usijaribu, ambao ulipokelewa kwa shangwe na mashabiki.

Kumalizika kwa zamu ya AY, washiriki walipanda tena jukwaani kuimba nyimbo zao za pili, David akiwa wa kwanza akifuatiwa na Esther, Victor na Wendy, kabla ya msanii nyota kutoka Uganda, Bobby Wine naye kupanda jukwaani.

Mbali na wasanii hao, msanii kutoka Kenya, Red Sun, naye alipanda jukwaani na kutoa burudani ambayo pia ilishangiliwa na mashabiki lukuki waliohudhuria.

Baadaye, MC wa shughuli hiyo, Gaitano Kagwa kutoka Uganda, aliwaonyesha mashabiki gari maalum lililoingia ukumbini likiwa na kitita hicho cha fedha za zawadi, ambao wanaume wanne waliokuwa wamevalia suti na miwani nyeusi, walipopanda jukwaani wakiwa na begi lenye fedha.

Esther amekuwa msichana wa pili kushinda mchuano huo baada ya Mkenya, Varerie Kimani kufanya hivyo mwaka jana

Tony Nyadundo, Mfalme wa Nyimbo za Ohangla

The Benga Maestro, Tony Nyadundo katika moja ya maonyesho yake

Tony Nyadundo ni mzaliwa wa Kanda ya Ziwa huko Kenya. Anatokea katika kabila la Wajaluo (Luo), Tony Nyadundo amejipatia umaarufu kwa aina ya mziki wake na ni jambo la kawaida kupita mitaani na kusikia nyimbo zake zikichezwa. Aina ya muziki wake inajulikana kama Ohangla (Muziki toka kanda ya Ziwa) na sasa yeye anajulikana kama Mfalme wa Ohangla. Tony ni mmoja wa wanamuziki walifaidika na muziki wake na kuufanya muziki huo kukubalika na rika lote. Tony pamoja na kaka yake anayejulikana kwa jina la Jack Nyadundo naye anapiga aina ya muziki kama wa Tony kama mdogo wake naye anakubalika sana kwenye Muziki na umaarufu wao ni mkubwa hasa Sehemu ambazo Wajaluo wanatoka.

Tony ambaye anatamba na nyimbo kama Dawa ya Mapenzi,Isanda Gi hera, Obama na nyinginezo nyingi ameshafanya matamasha ya muziki nchi mbali mbali ikiwemo Ujerumany na USA pia achilia mbali hizi za Afrika. Umaarufu huu unafuatia aina ya muziki wake ambao unajumuisha ala za asili, uchezaji pamoja na uimbaji ambao huvutia kwa taratiibu na kuupandisha toka Mziki wa Vilabu vya Pombe, Bar mpaka sasa zimbo zake zinapigwa hata kwenye Kumbi za Burudani zikichanganywa na Genge, muziki maarufu wa Kenya.

Mwaka 2006 alitoa albamu yake iliyoitwa Obama. Ikiwa ni kumuenzi Seneta Barak Obama wakati huo ambaye Baba yake ni Mzaliwa wa Kenya kama Nyadundo.

Wakati wa tamasha la Kisima Music Award mwaka 2007 alishinda kwenye kundi la Muziki wa kiasili. Tony ambaye binafsi anaweza kutumia ala zote za kiasili, muziki wake anatumia ala za kiasili tupu isipokuwa kinanda cha kupuliza tuu amefanikiwa kuweka utamaduni na muziki huo katika chati ya Muziki kitaifa na kimataifa.

Bonyeza Player upate Uhondo wa mwanamuziki Tony Nyadundo, Ukiangalia kwenye hii Video Utamuona Waziri Mkuu Raila Odinga, Prof Anyang Nyong, na wajaluo wengine ambao wapo kwenye nafsi za juu kichama(ODM) au kiserikali.

Serengeti Boys kufunzwa na Carlos Alberto Perreira Brazil


Pichani anaonekana Kocha Pereirra akiongea na Ronaldo

TIMU ya soka ya vijana walio chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, itaondoka nchini Juni 5 kuelekea Brazil , ambako itakuwa chini ya kocha aliyeiongoza Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1994, Carlos Alberto Perreira.

Mratibu wa mashindano ya Copa Coca-Cola, George Rwehimbiza alisema timu hiyo itafikia kwenye kituo cha michezo cha Brazil Football Academy, na itaondoka na viongozi wanne akiwemo kocha mkuu wa timu ya vijana, Marcus Tinocco.

“Timu itaondoka Juni 5 kuelekea Brazil itakaa huko kwa muda wa wiki moja,” alisema Rwehimbiza. “Timu itafikia kwenye kituo hicho kilicho chini ya Carlos Alberto Perreira.”

Perreira aliiongoza Afrika Kusini kwenye fainali za Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu, lakini akajiondoa kwenye kazi hiyo hivi karibuni, akieleza kuwa mkewe alikuwa ni mgonjwa.

Vijana watakaokuwa kwenye safari hiyo watapatikana kutoka katika mashindano ya Copa Coca-Cola yanayoeelekea ukingoni jijini Dar es salaam baada ya kuendeshwa kwa takriban wiki mbili.

Mashindano hayo yanashirikisha timu za kombaini za mikoa yote ya Tanzania Bara na visiwani, zikiwemo wilaya za Ilaya, Kinondoni na Temeke zilizopewa hadhi ya mkoa.

Vijana wengi walioteuliwa kwa ubora katika mashindano ya kwanza yaliyofanyika jijini Dar es salaam kwa sasa wanasomeshwa na Shirikisho la Soka (TFF) kwenye shule ya sekondari ya Jitegemee, ambako huhudhuria vipindi vya masomo ya kawaida na yale ya soka.

Wakati huohuo, kocha Tinoco amesema kuwa hatapata kazi kubwa ya kuwanoa vijana 17 watakaopatikana katika michuano ya Copa Coca-Cola, anaripoti Sosthenes Nyoni.

Akizungumza baada ya mechi baina ya timu ya mkoa wa Kigoma na Kusini Pemba, Tinocco alisema kuwa hilo linatokana na wachezaji wengi kuonekana kuwa wamefundishika.

Alisema kuwa tofauti na mwaka jana mashindano ya mwaka huu yameonyesha baadhi walimu wa timu shiriki kuwa wana uwezo mkubwa wa kufundisha soka na ndio maana baadhi ya timu zinacheza soka lenye mpangilio.

Ally Kiba nakati ya Ujeruman

Ally Kiba akiwa na mashabiki wakisherehekea ushindi wa timu ya Ujerumani jana usiku

Ali Kiba akiwa na Wadau wa Ujeruman, wapili kushoto ni Bibie Nashe Mvungi mmoja wa waandazi wa Miss Tanzania EU.
Mwanamziki wa kizazi kipya Ali Kiba Amewasili Ujerumani 25.06.08 Tayari kabisa kwa show Miss Tanzania EU. Inayotegemewa kufanyika Jumamosi 28.06.08 mjini Essen Germany.
Ally ambaye aliwasili pamoja na promota wake Kassim wakitokea Oslo – Norway ambako waliwarusha mashabiki vilivyo.

Pia imefahamika kwamba warembo washiriki wa Miss Tanzania EU wako kambini na tayari kabisa kwa mchujo wa round ya kwanza pre-selection utakaofanyika kesho ijumaa 27.06.08.

Ali kiba alipata nafasi ya kushangilia Mjini Essen na baadhi ya washabiki wa Ujerumani wa mpira wa miguu kwenye mtanange wa Ulaya kati ya Uturuki na Ujerumani ambapo Ujerumani Ilishinda 3-2.

Nani wa Kumfunga “Paka” Kengele Jumapili?

Germany 3 – 2 Turkey

Germany's Bastian Schweinsteiger and Miroslav Klose
Goli lililofungwa na Philip Lahm katika dakika ya 90 limewawezesha Ujerumani kufuzu kucheza Fainali za mtanange wa EURO 2008, na kuwafungisha virago waturuki katika mchezo uliochezwa usiku wa kuamkia leo huko St Jakob-Park in Basel.
Mpaka mapumziko timu zote mbili zilikuwa 1-1, huku Turkey wakiwa wakwanza kupata goli lililofungwa na Ugur Boral dakika ya 22 na dakika tano baadaye Ujerumani walisawazisha kupitia kwa Bastian Schweinsteiger.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kushambuliana mashambulizi ya hapa na pale huku Ujerumani wakilisakama lango la Uturuki kama nyuki kwa mashambulizi ya kustukiza na dakika ya 79 wakapata goli Ujerumani lililofungwa na Miroslav Klose.
Huku mashabiki wa Ujerumani wakishangilia timu yao kuongoza kwa goli mbili walistukizwa na goli la kusawazisha toka kwa Semih Senturk dakika saba tuu baada ya goli lao, kiukweli mpira ulikuwa mtamu.
Timu zote zikawa zinahaha kupata walao cha “kuraria”, huku makocha viti vikiwa havikaliki na mashabiki wakiwahamasisha wachezaji wao kwa ushangiliaji non-stop, bahati haikuwa ua Waturuki na bahati hiyo ya Mtende iliwaangukia Wajerumani na kupachika bao dakika ya 90 ya mchezo kupitia kwa Philip Lahm . Mchezo wa jana ulikuwa na kufa mtu kwani kila timu ilikuwa inataka nafasi walao ya kucheza fainali kama sio kuchukua ubingwa.
Timu zote zilifanya mabadiliko ya hapa na pale walao kufufa hali ya mchezo kwa Wajerumani Torsten Frings aliingia badala ya Simon Rolfes dakika ya 46 na Marcell Jansen badala ya Miroslav Klose dakika ya 90.
Kwa upande wa waturuki walifanya mabadiliko mara tatu Mevlut Erding aliingia badala ya Ayhan Akman (81) na Gokdeniz Karadeniz alichukua nafasi ya Ugur Boral (84) na dakika ya 90 walimuingiza Tumer Metin na kutoka Colin Kazim-Richards.
Tanzania Dream naona kautabiri kako kanafikia kaka!!

Wednesday, June 25, 2008

Huyu ndiye Bush!!

Bush Plays Basketball in BelfastRaw Video: Bush Plays Basketball in BelfastThe Associated PressPresident Bush travelled to Belfast on Monday and watched basketball practice at a local school. The President even took a few shots of his own. (June 16)

Mashabiki bwana!!

A supporter of the Turkish team has his national flag painted on his head ahead of the Euro 2008 championships semi-final football match Germany vs. Turkey on June 25, 2008 at Saint Jakob-Park stadium in Basel, Switzerland.  AFP PHOTO  DDP / PHILLIPP GUELLAND  -- MOBILE SERVICES OUT -- (Photo credit should read PHILLIPP GUELLAND/AFP/Getty Images)
Shabiki wa Turkey akiwa na Bendera ya nchi yake kichwani.
Germany supporters cheer before the start of the Euro 2008 championships semi-final football match Germany vs. Turkey on June 25, 2008 at St Jakob-Park stadium in Basel, Switzerland. AFP PHOTO / VALERY HACHE -- MOBILE SERVICES OUT -- (Photo credit should read VALERY HACHE/AFP/Getty Images)
Mashabiki wa Ujerumani chiboko!!
Supporters of the German team cheer ahead of the Euro 2008 championships semi-final football match Germany vs. Turkey on June 25, 2008 at St Jakob-Park stadium in Basel, Switzerland. AFP PHOTO  DDP / TORSTEN SILZ    -- MOBILE SERVICES OUT -- (Photo credit should read TORSTEN SILZ/AFP/Getty Images)

Nusu Fainali EURO 2008 Nani ni nani?

Germany:

German supporters play instruments outside the Germany national  soccer team Hotel in Basel, Wednesday, June 25, 2008. Germany reached the semifinal stage of the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland and will face Turkey. From AP Photo by LUCA BRUNO.
Mashabiki wa Timu ya Taifa ya Ujerumani wakiwa nje ya Hotel wanapokaa wachezaji wao huko Basel leo, Timu ya Ujerumani inaingia dimbani kumenyana na Turkey, chochote chweza tokea.

Hii ni timu nzuri inayocheza kwa kujituma ila inashindwa kuwa na motivation at times.Ila katika siku yao hakuna timu inayoweza ishinda.Kwa jicho la karibu naona bado wana hali ngumu dhidi ya Uturuki kutokana na ukweli kwamba Waturuki wameonekana kuwa vichwa ngumu karibu katika kila kazi waliyokutana nayo

…………………………………………………………………………….

Waturuki:

Supporters of the German and Turkish teams wave their national flags in the "Fanmeile" (Fan zone) in Berlin, ahead of the Euro 2008 championships half-final football match Germany vs Turkey held on June 25, 2008 at the St. Jakobs-Park stadium in Basel, Switzerland.  AFP PHOTO   DDP / MICHAEL KAPPELER (Photo credit should read MICHAEL KAPPELER/AFP/Getty Images)
Mashabiki wa Ujerumani na Turkey wakiwa pamoja wakichemshana hii ikiwa ni muda kabla kuanza kwa mchezo kati ya timu zao.

Hawa jamaa mpira wao sio mbaya ila kutokana na kutokuwa na majina makubwa inafanya kazi kwao iwe rahisi.Nafasi waliyofikia ni mafanikio tayari kwao.Hawana presha yeyote ya kujidhihirisha zaidi ya waliyofikia tayari.Hii inafanya game kwao iwe rahisi zaidi ya Ujerumani.

…………………………………………………………………………….

Waspeini:

Spain's Cesc Fabregas signs autographs after a training session of the national soccer team of Spain in Neustift im Stubaital, Austria, on Tuesday, June 24, 2008. Spain will play Russia in the semifinal at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. From AP Photo by Bernat Armangue.

Cesc Fabregas wa Spain akisaini Autograph mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu yao hapo jana.

Hawa kwa rekodi wana tabia ya kupata matokeo mabovu lkn kwa matokeo yao dhidi ya Italia yanarudisha imani ya kuweza kufanya mengi japo bado wana presha kutokana na kupewa nafasi kubwa na mashabiki na wataalamu wengi wa soka.Kwa upande wangu nawapa nafsi kubwa ya kucheza final.

…………………………………………………………………………….

Warusi:

Russian supporters cheer and wave Russian flags prior to the Euro 2008 Championships Group D football match Spain vs. Russia on June 10, 2008 at  Stade Tivoli Neu, in Innsbruck, Austria. From Getty Images by AFP/Getty Images.
Mashabiki wa Russia wakishangilia timu yao, usilogwe kuingia kwenye anga zao hawa jamaa ni noma.

Hawa jamaa kama ilivyo ada hawakupewa kabisa nafasi lkn waliyofanya tayari yamelipa matarajio na hivyo wanaingia kwenye hii game wakiwa na imani kuwa timu walidhodhani ni ngumu kwamba nazo zinafungika.Hii inakuwa rahisi kwa wao kukumbana na waspeini ila tatizo kwao ni kwamba wana wachezaji wengi wa kikosi chak wanza ambao hawatacheza kwenye hii game hivyo kupunguza matunda ya kikosi imara chao.

Wachezaji wa kuangaliwa kwa hii hatua ni bastian schweinsteiger,Fernando Torres,Arda Turna na Andrei Arshavin

Review By Tanzania Dream, Pamoja Kaka.

Bibisiya Mfwengi, Dansa wa Werrason anayedatisha jukwaani

Anaitwa Bibisiya Mfwengi, huyu ndiye kiongozi wa kikosi cha wachezaji cha Werason, mdada anatisha na kudatisha awapo jukwaani kwanza kwa umbile lake pia anavyokizungusha. Mara nyingi kwenye Sebene la Werrson huyu mdada huwa akipewa nafasi mashabiki hawataki aongoke na inakuwaga kazi kweli kweli, Werrason anaingia Dar Leo hii, habari kamili muda si mrefu. Pata kionjo.

Muangalie na HApa Pia

Tuesday, June 24, 2008

Master J, CEO MJ Records

Master J
PROFESSION: Producer
COMPANY: MJ Records
NATIONALITY: Tanzanian

Joachim Kimaryo a.k.a. Master J as he is fondly known in Tanzania’s growing music industry founded in 1996 what is today one of Tanzania’s foremost digital recording studios – MJ Records.

This man is undisputedly one of the pioneers of ‘Bongo Flava’ a distinctive predominantly hip-hop Tanzanian sound that has taken the continent by storm. He has played an integral role in the development of Bongo Flava and the growth of the broader music industry in Tanzania.

Master J holds a degree in electronics engineering from City University of London, and has always had a keen interest in music. Recording almost all genres of Tanzanian music from gospel, Bolingo to the famous Bongo Flava, Master J has worked with the best in the Tanzanian music industry.

Khangalicious. na Changamoto ya Vazi la Kitaifa

Mustafa Hasanali na Ma modela wake mara baada ya shoo ya Khanga licious

Mwanamitindo mkongwe kuliko wote duniani, Bibi Kidude akipita jukwaani kuonyesha vazi la khanga lililobuniwa na mbunifu Mustafa Hassanali.

Nakumbuka miaka hii ya 2000 na ushehe(naomba kusahihishwa) Serikali kupitia wizara ya Elimu ilikuwa na shindano la vazi la Taifa ambalo fainali ilifanyika Dodoma, Watu wengi walionyesha kutoridhishwa na mchakato mzima na hata Vazi lenyewe kwani tangu hapo sikuwahi kuona wala kusikia vazi lililoshinda likienziwa, inawezekana nipo mbali kihabari lakini sidhani kama hata we msomaji umesikia, Najaribu kuangalia hili onyesho la Khangalicious lililoletwa na Mustafa Hasanali na umuhimu wa changamoto ya vazi la kitaifa, Je lipi hapo linaweza kuwa Vazi la kitaifa angalau ukivaa unasema nimevaa vazi la Kitanzania? Picha na Father Kidevu

Flaviana Matata

Kwa wengi,nchini Tanzania na duniani,anabakia kuwa mrembo kutoka nchini Tanzania aliyeiwakilisha nchi yake katika shindano la dunia la Miss Universe mwaka 2007 na kuwa mshiriki wa kwanza aliyeamua kulipanda jukwaa akiwa kipara.Kwa wengine,wakiwemo ndugu,jamaa na marafiki zake,anabakia kuwa Flaviana Matata.

Hivi karibuni alilivua rasmi taji lake la Miss Universe Tanzania 2007 baada ya kulitumikia kwa muda wa mwaka mzima.Tulipata nafasi ya kuongea machache na Flaviana baada ya kumkabidhi rasmi mrembo mwingine,Amanda Sululu, taji la Miss Universe Tanzania. Hivi tunavyoongea tayari Amanda yupo nchini Vietnam tayari kabisa kwa shindano la Miss Universe litakalofikia kilele nchini humo tarehe 13 Julai mwaka huu.

Flaviani amefanya Mahojiano na Bongo Celebrity gonga hapa upate Kujua anasemaje?

Da Chemi amaliza uigizaji The Surrogates

DADA Chem ambaye ameshiriki katika filamu ya The Surrogates itakayotoka majira ya kiangazi mwakani amemaliza kucheza nafasi yake katika filamu hiyo na kurejea kijiweni kwake.
Dada Chemi ambaye pia ni mwanachama wa Screen Actors Guild (SAG) amesema kazi ya kuigiza ilikuwa bomba.
Amesema katika blogu yake kwamba katika filamu hiyo ambayo kinara wake ni Bruce Willis amecheza kama Dred.
Nafasi ya kucheza aliipata mwezi wa tatu wakati alipoitwa kwenye audition ya sinema hiyo.
Ingawa hakupata sehemu aliyofanyiwa audition alipewa nafasi ya kucheza Dred na alicheza vyema nafdasi hiyo akiwa mchafu na kuvaa nguo zilizochakaa akionekana kama kama ombaomba.
Isome Zaidi kwa Lukwangile Entertainment

Ngoma Africa na Muziki wa Dance ughaibuni

Habari hii imeletwa na Msemakweli

Mwanamziki nyota Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Ebby Makunja na ´bendi yake The Ngoma Africa banad wenye makao yao huko Ujerumani wamefanya kweli na wamedhihirishia ulimwengu kuwa bongo dansi la Tanzania ni sawa na moto wa mstuni! habari za kuaminika kutoka katika mashirika mbali mbali ya habari ya kimataifa kama vile jarida hili la South Africa BIZ, gazeti la kenya http://www.coastweek.com/3124-19.htm ,shirika la habari la scandinavia http://www.nanews.net huko spain nako jarida la http://www.fundicuionsur.com/spip.php?article1308 na kama hilivyo mila na desturi za waswahili kuwa ndio wenye watoto wao wazee wa http://www.bongocelebrity.com wamefanya kweli kwa kuweka wimbo huo! wastarabu wa Engaland http://www.tzuk.net nao hawakuwa nyuma katika kuwa nafasi vijana wao The Ngoma Africa,Nchini Holland majarida mengi nayo yamewafagilia Ngoma africa. Ukiachia mbali mitandao na majarida hayo kuna majarida ma kubwa ya inside world ya New Zerland,africa News la Italy. Pia habari za kuaminika zinaeleza kuwa song hilo jipya limeshapokelewa katika nchi zaidi ya 50, zikiwemo visiwa vya Caribean Dominica Rep.Antigua,Baadhi ya Radio za Brazili nazo zimepokea mdundo huo na kuukubali japo hawajui kiswahili. Raha ya mdundo huo hata kama ujui kiswahili hule mrindimo wa beat zake ni Raha juu ya raha! na ukikijua kiswahili basi utakubali kuwa mtunzi huyo Ebrahim Makunja ni mtunzi anaye yafahamu matatizo ya jamii yake ya Uswahilini,kuwa Pombe ni mojawapo ya Tatizo kubwa!linalo isumbuwa jamii.

Ras Makunja au Ebrahim Makunja ni mtunzi aliyebobea katika shughuli yake hiyo ya kutunga nyimbo na kuimba katika kuishauri jamii au hata kutoa onyo lakini mara nyingi huwa ni mwanamziki mwenye kuzua hoja kama utamsikiliza sana katika tungo zake za RUSHWA NI ADUI WA HAKI,hiliyopo katika CD ya “Anti-Corruption Squard” na ule mjadala wa mchezo mchafu wa “Mama Kimwaga”(Sugar mum)katika album hiliyobeba jina la “Mama Kimwaga”! kwa watu waliyo karibu na Ras Makunja na bendi ya The Ngoma Africa wanatonya kuwa jamaa hao ni watu utani sana na Ras Makunja mwenyewe ni mtu mwenye kupenda mizaa sana !lakini hawapo jukwaani na ukimsikiliza sana nyimbo zake zina maneno ya ukweli napenginepo yanachoma moyoni,na hakiona kuwa unamwangalia sana huwa anaimba na kufunika uso kwa kutumia kiganja cha mkono wake moja au kuvaa miwani ya jua mkubwa hata kama usiku !akimaliza kuimba uwazawadia washabiki kwa tabasamu ya kicheko ambalo uwariwadha !

Ujumbe uliomo katika nyimbo za Ngoma africa band kila wakati unasindikizwa na mlindimo au mdundo wa nyuzi kali zinatoka vidoleni mwa wanamziki mahili wa bendi hiyo wakiwamo mcharaza solo Gitaa machachari Mr.Christian Bakotessa aka Chris-B,ambaye mara nyingi uhimba pamoja na Ras Makunja,pia kuna yule mpiga gitaa la Bass Said Vuai aka Prince Jazbo Vuai,wapo kakribani wanamziki 7 hivi.

Tamazi ya habari tumalizie kwa kutoa wito kuwa wanamziki wa nyumbani hizi ndizo habari njema msiogope wala kusita kuzitoa nje kazi zenu,kuwa mziki wa dansi wa Tanzania sasa unakubalika. Hongera Ras Makunja Na wenzako The nGoma Africa Band au kama wanavyojilikana “the Golden Voice of East africa”.
Gonga hapa usikilize

Monday, June 23, 2008

basketball wapata mdhamini

Kampuni ya Uniliver imedhamini Sh milioni 10 kwa michuano ya kikapu ya Miji Mikuu ya Afrika Mashariki kati na kusini

inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho katika Uwanja wa Ndani wa Taifa na Uwanja wa Sigara.

Akichonga na wanahabari Rais wa Kamati ya Mpira wa Kikapu Miji Mikuu ya Afrika Mashariki Kati na Kusini, Simon Msoffe alisema Kampuni hiyo imetoa kiasi hicho kwa ajili ya shughuli mbalimbali za michuano hiyo.

“Tunatarajia Kampuni zingine zitajitokeza kufanikisha michuano hiyo ili ikonge nyoyo za mashabiki wa mpira wa kikapu waliopo hapa Tanzania, ” alisema

Msofe. Majiji yanayoshiriki michuano hiyo kutoka Tanzania ni Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Mbeya na Tanga, Kenya ni Nairobi na Mombasa, Uganda ni Kampala, na jiji jingine ni Mogadishu.

Mashindano hayo yaliyoanza toka mwaka 1999 na kufanyika kila mwaka, mwaka jana bingwa wa michuano hiyo ilikuwa ni Nairobi walioifunga Dar es Salaam katika fainali iliyofanyika Nairobi, Kenya.

KIli Music Award yaiva

Wasanii wa muziki wakae mkao wa kula kwani zile tuzo za ‘Dandu’ zitatolewa Juni 28 mwaka huu ndani ya Hoteli ya Kempisky. Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi hayo Oscar Shelukindo alisema mwaka huu wahudhuriaji hawataingia kwa tiketi bali kadi maalum.
Pichani kushoto ni Afisa Uhusiano wa Kampuni iliyoandaa tuzo hizo Oscar Shelukindo na Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya inshu hiyo, John Mhina wakionesha aina ya tuzo zitakazotolewa siku hiyo wakati wakiongea na waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dar es Salaam leo mchana. Tuzo hizi zilianzishwa na mwanamuziki James Dandu ambaye hivi sasa ni marehemu. Picha/Habari na GPL

Kolabo ya Juliana na Bushoke

Wimbo ni wake Juliana Kanyomozi toka nchini Uganda akimshirikisha Bushoke wa Tanzania, Wimbo huu ambao uko kwenye Albamu ya sasa ya Juliana bado unawika kwenye chat za Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla, Kwa mengi yamhusuyo Juliana gonga hapa, na kwa kusikiliza wimbo huu gonga player.

Hispania wafuzu Nusu Fainali kwa mbinde!

Spain 4 – 2 Italy

Spain celebrates

Wachezaji wa Spain wakisherehekea mara baada ya kumalizika kwa hatua ya kupigiana penati na Italy hapo jana.

Hispania wamekwenda hatua ya Nusu fainali za michezo ya Euro 2008 baada ya kufikia hatua ya kupigiana penati kwenye mechi kali kati yake na Italy hapo Ernst-Happel Stadium jana.

Golikipa wa Hispania Iker Casillas aliokoa mishuti ya penati toka kwa Daniele De Rossi na Antonio Di Natale hii likuwa ni baada ya dakika 120 za bila kufungana kabla ya mchezaji matata Cesc Fabregas kufunga penati yake ya mwisho na kuwainua mamia kwa maelfu ya mashabiki waliokuwa uwanjani na mitaani.

Kwa upand wake Cassillas, aliokoa mkwaju kwa mguu uliopigwa na Mauro Camoranesi, ulisaidia kuiweka Spain kwenye matokeo mazuri ambayo hata kwa penati ilobaki Italy wasingeweza kufikia magoli ya Hispania.

Italy walishinda kombe la Dunia mwaka 2006 kwa Penati dhidi ya Ufaransa lakini Buffon ambaye alikuwa shujaa kwenye fainali zile jana alishindwa kuonyesha makali yake na badala yake golikipa wa Spain Casillas akawa ndio shujaa.

Lakini ikumbukwe pia kipa huyu wa Italy ndiye aliyewafikisha kwenye hatua hiyo baada ya kuokoa mkwaju wa Adrian Mutu walipocheza na Romania, na hata hivyo aliicheza penati ya nne ya Daniel Guiza hapo jana.

Kwa matokeo haya Hispania watakutana na Russia hapo tarehe 26 Juni huko Vienna Austria ambapo bingwa atacheza na mshindi kati ya Ujerumani na Turkey ambao watacheza tarehe 25 Basel.

Mechi za Awali Kombe la Mataifa na Kombe la Dunia kwa Afrika

Matokeo kadha ya mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia 2010 ya mechi za Jumapili tarehe 22 Juni 2008

Kundi la 2
Zimbabwe 0 Kenya 0

Kundi la 3
Angola Uganda (mechi iliahirishwa Jumapili hadi Jumatatu)
Benin 2 Niger 0

Kundi la 7
Msumbiji 3 Bukini 0

Kundi la 8
Ethiopia 6 Mauritania 1

Kundi la 10
Congo 2 Chad 0

Kundi la 12
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 5 Djibouti 1

Mechi za Jumamosi tarehe 21 Juni 2008

Kundi la 1
Cameroon 2 Tanzania 1

Kundi la 4
Nigeria 2 Equatorial Guinea 0
Afrika Kusini 0 Sierra Leone 0

Kundi la 5
Morocco 2 Rwanda 0

Kundi la 6
Senegal 3 Liberia 1

Kundi la 9
Tunisia 2 Burundi 1
Burkhina Faso 4 Ushelisheli 1

Kundi la 11
Zambia 1 Swaziland 0

Mechi zilizochezwa Ijumaa tarehe 20 Juni 2008

Kundi la 5
Libya 4 Lesotho 0

Kundi la 6
Algeria 1 Gambia 0

Mashindano ya Pool kuanza Juni 27

Pichani mmoja wa wachezaji Pool maarufu Dar, Robert William Mwafrika akiwafundisha vijana zaidi ya 20 sheria za mchezo wa Pool huko Kijijini Mlimba, Morogoro hivi karibuni.

Mashindano ya taifa ya mchezo ya pool 2008 yanayotarajiwa kushirikisha timu kutoka baadhi ya mikoa ya Tanzania bara yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Kwa kuzingatia umuhimu wa mashindano hayo, chama cha waamuzi wa mchezo huo wa Pool mkoa wa Dar es Salaam -DAPORA-kimeandaa semina kwa waandishi wa habari iliyohusu mchezo huo na sheria zake.

Mashindano hayo yameandaliwa na chama cha mchezo wa Pool mkoa wa Dar es Salaam-DARPA- na kudhaminiwa na kampuni ya bia Tanzania- kwa kupitia bia aina ya safari.

Miss Arusha ajinyakulia gari

Miss Arusha 2008, Glory Emson akiwa ndani ya gari yake Toyota Sprinter mpyaa aliyokabidhiwa mara baada ya kushinda hivi karibuni, gari hii imetolewa na wadhamini wa Miss Arusha TanzaniteOne
(Photo by Nicky Mchau)

Sunday, June 22, 2008

Huu ndio unazi!!

Dutch supporters look dejected at the end of the Euro 2008 Championships quarter-final football match the Netherlands vs. Russia on June 21, 2008 at St. Jakob-Park in Basel. Russia won 3-1.AFP PHOTO / JOHN MACDOUGALL -- MOBILE SERVICES OUT --             (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Mashabiki wa Holland juu na chini wakiwa wamebaki wawili tu jukwaani mara baada ya mpira kumalizika kati ya Holland na Russia na Holland kubugizwa 3-1.
Dutch supporters look dejected after Russia won the Euro 2008 Championships quarter-final football match the Netherlands vs. Russia on June 21, 2008 at St. Jakob-Park in Basel. Russia won 3-1.    AFP PHOTO / PATRICK HERTZOG   -- MOBILE SERVICES OUT --                                                                                                                                                     (Photo credit should read PATRICK HERTZOG/AFP/Getty Images)

Russia yawafungisha Virago wakali Holland

Netherlands 1-3 Russia

Netherlands' Edwin van der Sar grabs the ball out of the net after failing to save a shot by Russia's Dmitri Torbinski, unseen, during the quarterfinal match between the Netherlands and Russia in Basel, Switzerland, Saturday, June 21, 2008, at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Russia defeated Netherlands 3-1.
Golikipa wa Holland au Dutch au Uholanzi au Netherland Netherlands’ Edwin van der Sar akiokota mpira kimiani baada ya kufungwa goli la pili na Dmitri Torbinski,
Russian forward Andrei Arshavin
Wandamba wanasema MATU!! Ndivyo anavyoelekea kuwaambia Andrei Arshavin mashabiki wa Holland ambao walikuwa wakiishangilia timu yao kwa nguvu baada ya kupachika goli la tatu dakika ya 116.

Netherlands' Wesley Sneijder, bottom, is comforted by a teammate as goalkeeper Edwin van der Sar, right, walks past, while Russian players celebrate in background after the quarterfinal match between the Netherlands and Russia in Basel, Switzerland, Saturday, June 21, 2008, at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Russia defeated Netherlands 3-1.
Mchezaji wa Holland Wesley Sneijder, chini akipoozwa na mwenzake huku golikipa wao Edwin van der Sar akipita mara baada ya mechi kuisha, kwa mbaali Russia wakijipongeza,

Russian soccer fans celebrate their team's victory after the quarterfinal match between the Netherlands and Russia at the Euro 2008 European Soccer Championships in Red Square in Moscow, early Sunday, June 22, 2008. Russia defeated the Netherlands 3-1.
Russian soccer fans celebrate their team's victory after the quarterfinal match between the Netherlands and Russia at the Euro 2008 European Soccer Championships, in the center of Moscow with the Kremlin and historical museum in the background, early Sunday, June 22, 2008. Russia beat the tournament favorite 3-1 in extra time to secure its first ever European Championship semifinal appearance.
Kama kawa mashabiki mitaani wakisherehekea.

Magoli yaliyofungwa na Dmitri Torbinski na Andrei Arshavin dakika za majeruhi yameiwezesha Russia kucheza nusu fainali na kuwafungisha virago Holland ambao walianza kwa mkwara.

Mpaka dakika 5 kabla ya mpira kumalizika Holland walikuwa wameshalala kwa goli moja bila ndipo Ruud van Nistelrooy aliposawazisha kwenye dakika ya 86 na kufanya dakika za nyongeza ziongezwe.

Russia ambao walizidi kuongeza spidi ya mpira na dakika kadhaa walifanikiwa baada ya Torbinski kupachika bao la pili baada ya kazi ngumu ikiwa ni dakika ya 112 ya mchezo, Goli hili liliwachanganya kidogo Holland ambao walipewa nafasi kubwa ya kucheza hata fainali hasa baada ya kuwabwaga vigogo kama Italy na Ufaransa ambao kwa pamoja walikuwa hili “kundi la kifo” na dakika nne baadaye Arshavin akaongeza goli jingine na kufanya uwanja ulipuke kwa mashabiki waRussia na kuleta majonzi kwa mashabiki wa Holland ambao waliupamba uwanja kwa rangi yao ya chungwa kama kawa.

Kocha wa Russia mholanzi Guus Hiddink kwa ajana ameonekana kama msaliti lakini alikuwa kibaruani kwani ameitoa timu ya nchi yake na uzalendo kuonyesha kumshinda, binasi simlaumu!

Kwa sasa Russia watakutana na Spain au Italy jijini Vienna siku ya Alhamisi na kufanya kuwa timu ya tatu kufikia hatua ya nusu fainali. Rafiki yangu Tanzania Dream hongera kwa kubashiri, natumai ubashiri wako utakwenda sawia.

Taifa Stars Yafa Kiume!! yatoka 2-1 na Kameroon

TIMU ya Taifa ya Tanzania, ‘Taifa Stars’ imekufa kiume ikiwa ugenini mjini Yaounde, baada ya kufungwa mabao 2-1 na Kameruni katika mchezo wa marudiano kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika 2010.

Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Uwanja Mkuu wa Taifa, Dar es Salaam Jumamosi iliyopita, Stars iligangamala na kutoka suluhu na Kameruni. ‘Indomitable Lions’ inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 10.

Stars imebakiwa na pointi mbili baada ya kutoka sare 1-1 na Mauritius, ilichapwa bao 1-0 na Cape Verde, ilitoka suluhu na Kameruni kabla ya jana kufungwa mabao 2-1 na wapinzani wao. Timu hiyo imebakiwa na michezo miwili dhidi ya Mauritius na Cape Verde.

Katika mchezo huo, Stars ilicheza vizuri na kuwabana Kameruni iliyosheheni nyota wengi wanaocheza mpira wa kulipwa katika klabu za Ulaya licha ya kupoteza mchezo huo.

Kameruni ilianza kupata bao lake dakika 66 lililofungwa na mshambuliaji wa Barcelona, Samuel Eto’o baada ya kipa Ivo Mapunda kuutema mpira wa krosi uliopigwa kutoka pembeni kulia mwa uwanja. Eto’o alifunga bao la ushindi dakika 88.

Stars ilitulia na kucheza pasi fupi fupi ambazo zilichangia kuwapa wakati mgumu mabeki wa Kameruni ambao walianza kupoteana na kutoa mwanya kwa Danny Mrwanda na Nizar Khalfan kumsogelea kipa wa Kameruni, Idriss Kameni.

Kasi ya Stars ilimchanganya nahodha wa Kameruni, Rogobert Song ambaye alifanya makosa yalimpa nafasi, Mrwanda kupachika bao la kusawazisha dakika 77 akifunga kwa shuti lililompita kipa Kameni kabla ya kujaa wavuni.

Kiungo wa pembeni wa Stars, Mrisho Ngassa alifanikiwa kuitoka ngome ya Kameruni dakika 11 lakini mpira wake wa krosi aliopiga kutoka upande wa kuliwa mwa uwanja uliokolewa na beki wa kati, Rogobert Song.

Kameruni ilijibu shambulizi hilo dakika 24 baada ya kiungo, Alexander Song kupenyeza mpira katika ngome ya Stars lakini beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ aliokoa hatari hiyo.

Dakika mbili baadae Stars ilitulia na kuanza kupanga mashambulizi ambapo Nizar Khalfan na Shaaban Nditi waligongeana vizuri kabla ya mabeki wa Kameruni kuokoa.

Stars ilibisha hodi langoni mwa Kameruni dakika 32 kabla ya mabeki wa Kameruni kuokoa hatari hiyo na kuwa kona ya kwanza kwa kikosi hicho iliyopigwa na beki wa kushoto, Amir Maftah ambayo haikuzaa matunda.

Eto’o alifanikiwa kuitoka ngome ya Stars dakika 37 na kufumua shuti lililotoka nje ya lango kabla ya dakika mbili baadae beki wa kulia, Geremi Njitap kupiga shuti lililowababatiza mabeki wa Stars kabla ya kuokolewa.

Kameruni iliendelea kutawala sehemu ya kiungo iliyokuwa ikichezwa na Godfrey Boniface na Nditi ambao walimpa nafasi Song kuwalisha mipira washambuliaji wa Kameruni walioongozwa na Eto’o.

Kameruni iliwatumia zaidi mabeki wa pembeni, Njitap aliyecheza upande wa kulia na Thimotheo Atouba ambao walikutana na vikwazo kutoka kwa Maftah na Nsajigwa Shadrack ambao walicheza kazi kupunguza kasi ya mashambulizi.

Baada ya kumalika mchezo huo, Eto’o alivua jezi yake nambari 9 na kumpa ‘Cannavaro’ ambaye naye alimpa ya kwake.

Stars: Ivo Mapunda, Nsajigwa Shadrack, Amir Maftah, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Salum Sued, Godfrey Boniface, Henry Joseph, Shaaban Nditi, Danny Mrwanda, Nizar Khalfan na Mrisho Ngassa/ Emmanuel Gabriel.

Saturday, June 21, 2008

KAMBI YA MISS TANZANIA EU KUANZA JUMATATU,

  • TIKETI ZAUZWA KAMA NJUGU

Kambi ya washiriki wa kumtafuta mrembo wa kitanzania katika nchi za Schengen yaani miss Manzania Schengen,inatarajiwa kuanza jumatatu hii ambapo vimwana 10 kutoka nchi mbalimbali za jumuiyayaUlaya watashiriki.Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika jumamosi ijayo katikaukumbi wa EFES mjini Essen Ujerumani ambapo mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Mh Ahmada Ngemera.

Mratibu wa shindano ambalo kwa mara ya kwanza linafanyika katika nchi za Schengen, Nashe Mvungi amesema kuwa maandalizi yote yamekamilika ikiwa pamoja na kuongezeka kwa wadhamini.

Amesema kuwa wadhamini hao ni Gazeti la African Positive lililoko Dortmund nchini Ujerumani ambalo pia linamiliki magazeti mengine maarufu kwa jamii yawaafrika barani Ulaya, African Heritage na African Courier.Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo Bi Veve Tata amesema magazeti hayo yataingia mkataba na mrembo atakayeshinda ili kumtafutia mikataba yaurembo katika nchi nyingine hapa barani Ulaya.

Wadhamini wengine wa shindano hilo ni shirikala ndege la Ethiopea airline pamoja na kampuni ya utalii ya Western Tours ya Bonn Ujerumani.

Katika shindano hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wadau kutoka nchi mbalimbali za ulaya msanii wa kizazi kipya kutoka Tanzania anayetamba na kibao chake Cinderela Ali Kiba atatumbuiza,pamoja na msanii kutoka Cameroon wa miondoko ya Makossa Eyum Anneh.

Tiketi za onesho hilo zimekuwa zikiuzwa kwa kasi katika vituo mbalimbali.Bei ya tiketi hizo ni euro 10,lakini kwa wale watakaonunua mlangoni ni euro 15 pamoja na kinywaji kimoja bure.

Innomizizi na Kiuno Viuno

Weekend ya leo nakuacheni na kibao toka kwake Innomizizi cha Kiuno Viuno. Mambo ya Mombasa haya na wale watu wa Pwani wanafurahia sana wakisikia midundo hii, pata starehe… na Weekend njema. Hemed safari njema ya kurejea Dar, Rashid kaka Maandalizi mema ya harusi, Abdul Kareem mwako humu Raithiiii, Mamaa Fardhana na Minah vya Pwani hivi!!! lol

TAIFA STARS TUPENI RAHA LEO

“…Furaha ya Watanzania milioni 37 ipo miguuni kwenu, Tupeni raha.
Dawati la Spoti na Starehe linaungana na watazania kukutakieni kila la heri kwenye mchezo wa leo na Kameroon, msiogope majina, kama walishangaa uwanja wetu hakuna cha kushangaa kule hata kamoja tuu kanatutosha kufurajia.”

Werrason Kutua Dar July

MWANAMUZIKI wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Werrason Ngiyama Makanda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika onesho maalum la utambulisho wa mashindano ya marepa utakaofanyika Juni 26, mwaka huu, Dar es Salaam. Mashindano yenyewe ni July 4, Akizunguza jana mmoja wa waandaaji wa mashindano hayo Kim (Kim and The Boys) alisema Werason ndiye atakuwa mgeni rasmi, hii inawapa matumaini mashabiki ambao kwa nyakati tofauti walikuwa wakiulizia kuhusu ujio wa Werrason, Bila kulizungumzia kwa Kina Kim alisema kuwa Werason anakuja jijini, Pichani chini ni Werasoni na kikosi chake wakiwa kwenye moja na matamasha. Werrasoni ambaye anatamba na nyimbo zake mpya bado haijajulikana kama atafanya matamasha mangapi ila habari za ujio wake tu ni furaha tosha kwa mashabiki wake wa Dar Es Salaam akina Big Producer Maghambo, Mukubwa Mwemtsi, Collins na Fikiri wazee wa USA, Boss Chizenga na wapenzi wote wa Werrason inawahusu hii. Weekend njema
Gonga player hapo chini Kupata Sebene la Werason na vijana wake, Muangalie kwa makini stage show wa Wera anaitwa Bibiceya Mufwengi. Selamat Datang…

Libya yaichapa Lesotho 4-0

Libyan fans watch a World Cup qualifier football match between Libya and Lesotho in Tripoli on June 20, 2008.  Libya won 4-0.  AFP PHOTO / MAHMUD TURKIA (Photo credit should read MAHMUD TURKIA/AFP/Getty Images)
MAshabiki wa Libya wakiangalia mechi ya awali ya kombe la Dunia kati ya timu yao ya Libya na Losotho, mchezo uliochezwa Tripoli Libya juni 20. Libya iliibugiza Lesotho mabao 4-0.

Turkey yasonga mbele

Croatia 1 – 3 Turkey

Croatia's Ivan Klasnic, left, scores the opening goal during the quarterfinal match between Croatia and Turkey in Vienna, Austria, Friday, June 20, 2008, at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Turkey beat Croatia 3-1 on penalties after a 1-1 draw in extra time.

Mchezaji wa Croatia Ivan Klasnic, shoto akifunga goli wakati wa mchezo wa robo fainali dhidi ya Turkey huko Vienna Austria jana left, Turkey walishinda kwa 3-1 kwa mikwaju ya Penati baada ya timu hizo kutoka suluhu ya goli moja kwa moja. Hivyo Turkey itakutana na Ujerumani kwenye mchezo wa Nusu fainali.

A Croatian fan react after the quarterfinal match between Croatia and Turkey in Vienna, Austria, Friday, June 20, 2008, at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Turkey beat Croatia 3-1 on penalties after a 1-1 draw in extra time.
Sabaiki wa Croatia akiwa anahuzunika mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa jana kati ya Croatia na Turkey.

A police cordons off Croatian fans after the quarterfinal match Croatia against Turkey in Vienna, Austria, Friday, June 20, 2008, during the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Turkey defeated Croatia 3-1 in the penalty shoot-out.
Polisi wakijenga ukuta kuwazuia mashabiki wa Croatia ambao walikuwa wakipita mitaani wakifanya fujo baada ya timu yao kuondolewa hapo jana.

Turkish soccer fans sit on top of a car as they celebrate the victory of the national soccer team of Turkey over Croatia in the quarterfinal match in Vienna, Austria,  early Sunday, June 21, 2008, at the Euro 2008 European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Turkey defeated Croatia 3 - 1 in the final penalty shoot-out.
Mashabiki wa Turkey wakipita mitaani Austria wakishangilia timu yao baada ya kuichapa Croatia 3-1 hapo jana, Mji wa Viena ulikuwa ni nyekundu tupu!

Friday, June 20, 2008

Mshindi wa Talaku kuzawadiwa Gari

Mwandaaji wa pambano ya marapa, Abdulhakim Magomelo ‘Kim’ akizungumza na waandishi wa habari, kuhusu shindano la kumsaka ‘rapa’ mkali linalotarajiwa kufanyika Julai 4 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Mshindi wa shindano la nani mkali katika marapa anatarajia kuondoka na zawadi ya gari.

Abdurahakimu Magomelo alisema shindano hilo limeandaliwa na taasisi ya kukuza vipaji (THT) na kuwa zawadi kamili zitatangazwa Alhamisi kwenye mkutano wa kutambulisha washiriki hao.
“ THT imeamua kuandaa shindano la kumpata nani zaidi katika marapa, lengo likiwa ni kuonyesha uwezo wa wasanii na kuthamini mchango wao katika muziki,” alisema. Gonga hapa uzisome zaidi

Salama naye aachia…

TUPHOTOE YA UKWELI Adam Mchomvu akiwa katika picha ya pozi na mtangazaji wa kituo cha Luninga na Redio cha East Afican Salama Jabir mara baada ya mkutano wa Kelly na waandishi wa habari kumalizika ndani ya Hotel ya Kilimanjaro.
hapo jana, Habari zinapasha kuwa Salama ambaye alipata umaarufu kwa kipindi chake cha Planet Bongo kilichokuwa kikirushwa hewani na East African Television ameacha kuendesha kipindi hico bila kuelezea kiundani zaidi. PICHA NA CHRISTOPHER LISSA / GPL.

Wachezaji Taifa Stars walamba mapesa!!

  • Kila Mchezaji ajinyakulia 1.2 milioni.
  • Timu imendoka kwenda Cameroon na matumaini

Kikosi cha Taifa Stars pichani ambacho kilicheza na Cameroon hivi majuzi

SIKU moja kabla ya timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ kuivaa Kameruni katika mchezo wa marudino wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika, wachezaji wa kikosi hicho wamejazwa mapesa ambapo kila mmoja amevuna kitita cha sh. milioni 1.2.

Taifa Stars na Kameruni ‘Indomitable Lions’ zinatarajiwa kukwaana kesho mjini Younde, ukiwa ni mchezo wa marudiano baada ya kutoka suluhu kwenye Uwanja Mkuu Mpya wa Taifa, Dar es Salaam wiki moja iliyopita.
Katika mchanganua huo, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa sh. 34,000,000 ikiwa ni motisha kwa wachezaji hao wakati benki ya NMB ambao ni wadhamini wa timu hiuo ilitoa sh. 6,200,000.

Kutokana na fedha hizo kila mchezaji atapata sh. milioni 1.2 katika kikosi cha wachezaji 27 na benchi la ufundi litapata sehemu ya fedha hizo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Frederick Mwakalebela, alisema TFF imeamua kutoa fedha hizo ili kuwapa changamoto wachezaji wanaojiwinda na mchezo huo mgumu dhidi ya Kameruni.

Mwakalebela alisema TFF imeamua kutoa fedha hizo kwa kutambua mchango mkubwa wa wachezaji wa Stars na benchi la ufundi.
Alisema kutokana na motosha hiyo ana uhakika wachezaji hao wataweza kufarijika na kujituma zaidi na hatimaye kupeperusha vizuri bendera ya Tanzania katika michezo yake ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia.

“Vijana wamefanya kazi kubwa sana katika mchezo wao wa awali dhidi ya Kameruni na pia bado wana kazi ya kuhakikisha wanafanya vema katika mchezo wa marudiano hivyo fedha tulizotoa zitawapa changamoto kubwa,” alisema Mwakalebela.

Akizungumzia mchezo wa marudiano dhidi ya Kameruni unaotarajia kufanyika leo mjini Younde, Kocha Mkuu wa Stars Marcio Maximo, alisema mchezo huo ni mgumu kwa timu yake ambayo inahitaji ushindi.
Maximo alisema hata hivyo anatarajia kupata matokeo mazuri kwa timu yake baada ya kufanya maandalizi ya kutosha na kuhakikisha inakabiliana na Kameruni ikiwa ugenini.

Maximo alisema timu yake ipo katika hali nzuri na wachezaji wake wamejengwa kisaikolojia licha ya kuwa na majeruhi wachache ambao anatarajia kuwatumia katika mchezo huo akiwa na matumaini ya kurejea katika hali nzuri.

Stars inatarajiwa kuondoka leo alfajili ikiwa na wachezaji 21, viongozi saba wakiongozwa na Mbunge wa Singida Magharibi Mohamed Misanga ambaye atakuwa mkuu wa msafara kwa upande wa Serikali.
Taifa Stars ina pointi mbili baada ya kutoka sare 1-1 na Mauritius, imefungwa bao 1-0 na Cape Verde kabla ya kutoka suluhu na Kameruni.
Habari na Majira, Picha na Mpoki Bukuku

Wazee wa Ngwasuma kupamba Miss Morocco Leo

mambo yameshaiva na tayari warembo takriban 10 wako tayari kugombea taji la miss morocco, kitongoji kinachosifika kwa walimbwende wilaya ya kinondoni. mambo yatakuwa pale new msasani club nyuma ya ubalozi wa marekani kuanzia saa mbili usiku ambapo fm academia wana wa ngwasuma wanaotamba na kibao cha ‘si kila mwanamke aendaye baa ni malaya’ watakuwepo kusindikiza usiku huo unaosimamiwa na mama wa mitindo aisa idarous, Habari hii na Muhidini Issa Michuzi ambaye ni mmoja wa wadhamini wa shindano hilo. Hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania wameamka na kuanza kuzipa nafasi Blog kama sehemu ya Media na mchango wake kuthaminiwa katika jamii.

Bado anatakiwa….

Both Real Madrid and Manchester United want his services for next season, but Portugal's Cristiano Ronaldo must now reveal his future plans after his Euro 2008 heart-break on Thursday.
Zote Real Madrid na Manchester United zinamtaka kuwachezea kwenye msimu ujao wa ligi zao, Yampasa Ronaldo kutulia na kufikiria zaidi hatma yake kisoka kutokana na utashi wake binafsi. hasa baada ya timu yake ya taifa ya Portugal kusimamishwa na Ujerumani hapo jana.

Ronaldinho kwenda Galaxy?

FC Barcelona's Brazilian Ronaldinho plays with the ball during a training session, at Camp Nou stadium in Barcelona in April 2008. Manchester City owner Thaksin Shinawatra is determined to bring Ronaldinho to Eastlands.

Na Yahoo Sports News:
Mchezaji wa FC Barcelona Mbrazili Ronaldinho akicheza na mpira wakati wa mazoezi ya timu yake huko Camp Nou stadium, Barcelona April mwaka huu, Habari zinapasha kuwa timu ya Galaxy ya Marekani ambayo imemchukua David Beckham imetoa Ofa ya kumchuua Ronaldinho kwa mkataba wa dola milioni 16 na dola milioni 16 nyingine kwa haki miliki ya Picha yake. Habari zinasema mazungumzo yapo pazuri.

Masikini Portugal!!, Ujerumani yapaa Nusu Fainali

Portugal 2 – 3 Germany

Portugal goalkeeper Ricardo (left) and Germany's Michael Ballack

Mchezaji wa Ujerumani Michael Ballack (kulia) akipachika bao la tatu kwa timu yake.

German players celebrate after the Euro 2008 Championships quarter-final match Portugal vs. Germany on June 19, 2008 at St. Jakob-Park in Basel.  Germany won 3-2. AFP PHOTO/JOHN MACDOUGALL  -- MOBILE SERVICES OUT -- (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Wachezaji wa Ujerumani wakisherehekea ushindi mara baada ya mchezo wao na Portugal kumalizika

Portuguese soccer fans react as they watch the live TV broadcast of the Euro 2008 European Soccer Championship quarterfinal soccer match between Portugal and Germany, at a public viewing zone in the city center of Porto, Portugal, Thursday, June 19, 2008. Germany defeated Portugal 3-2.
Mashabiki wa Portugal wakiwa hawaamini macho yao mara baada ya kipyenga cha Mwisho
Supporters of the German team use their national flag to protect themselves against the rain and celebrate as they watch the Euro 2008 quarter final match of Germany against Portugal held in Basel, Switzerland, during a public viewing session on June 19, 2008 in Berlin. Germany won 2-3 and qualified for the semi-final.    AFP PHOTO    BARBARA SAX (Photo credit should read BARBARA SAX/AFP/Getty Images)

Macho yote yalikuwa kwa Cristiano Ronaldo jana lakini mambo hayakuwa hivyo kwani ilikuwa ni kinyume chake na mchezaji wa Ujerumani mwenye namba yaka yake Bastian Schweinsteiger ndiye aliyeng’ara jana na kuihakikishia Ujerumani nafasi ya kusonga mbele kwenye hatua ya Nusu Fainali na kuwatupa Portugal nje.

Nyota ya Bayern Munich Schweinsteiger alifunga goli moja na kutengeneza mengine mawili kwa Miroslav Klose na Michael Ballack, mpaka mapumziko mabao yalikuwa ni 2-1 huku ujerumani wakiongoza na bao la Portugal lilifungwa na Nuno Gomes kwenye dakika ya 42 ya kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili kulianza kwa mshike mshike kweli kweli huku mashabiki wakishangilia goli toka kwa Michael Ballacks mnamo dakika ya 62, mashabiki wa Portugal walionyesha kukata tamaa kidogo. Ujerumani ambao kwa kiasi kikubwa walianza michuano hii kwa kusuasua na watu waliitaja zaidi Portugal kucheza Fainali jana walionyesha uhai na ile ladha ya Mpira ambao wapenzi wameizoea kwa Ujerumani.

Kwa matokeo hayo Ujerumani itakutana na ama Croatia au Turkey, timu ambazo zote hazitabiriki.

Huu ni mhitimisho wa mkataba wa miaka mitano wa kocha Luiz Felipe Scolari ambaye atajiunga na Club ya Chelsea mapema baada ya michuano hii kwani alitazamiwa kumaliza ‘s five-year reign as Portugal coach to an inglorious end before he heads off to become Chelsea mamkataba wake kwa mafanikio ya kikombe hiki.

Kocha wa Ujerumani Joachim Low, hakuweza kukaa kwenye benchi la akiba la Ujerumani kwa kuwa alifungiwa mechi moja mapema wiki hii alipokwaruzana na Kocha mwenzie wa Austria Josef Hickersberger na kutolewa nje ya uwanja. Mpaka mwisho wa mchezo matokeo ni 3-2.

German fans celebrate at the end of the Euro 2008 Championships quarter-final match Portugal vs. Germany on June 19, 2008 at St. Jakob-Park in Basel.  Germany won 3-2. AFP PHOTO/JOHN MACDOUGALL  -- MOBILE SERVICES OUT --       (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Shangwe nderemo hoi na vifijo ghafla vilitawala kwenye jukwaa la Ujerumani ambayo ilikuwa kwenye hati hati kwani Portugal walionyesha mchezo mzuri tangu mwanzo mwa mashindano haya.

Thursday, June 19, 2008

Manchester kucheza na Portsmouth nchini Nigeria mwezi ujao.

Timu za Manchester United (Pichani) na Portsmouth zote za Uingereza zinatarajiwa kucheza mechi ya Kirafiki nchini Nigeria mwishoni mwa mwezi ujao wa July. Mpaka Sasa Timu ya Manchester United imekwisha thibitisha habari hizo na kusema itacheza mchezo mmoja tuu, ilihali timu ya Portsmouth wao watacheza na timu ya Taifa Super Eagle. Tayari Uingereza imekwisha tuma maofisa wake nchini Nigeria kufanya maandalizi ya timu zake ikiwa ni pamoja na kuukagua Uwanja kwa ajili ya mechi hiyo.

Mabondia wa Tanzania walikuwa na jumla ya kilo 6 za madawa!!

Polisi jijini Dar Es Salaam wamethibitisha habari zinazohusu Kukamatwa kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya Ndondi ambayo ilikuwa nchini Mauritius.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Peter Kivuyo alisema kuchelewa kwa jeshi la polisi kutoa tamko kuhusiana na sakata hilo ni kwa kuwa ilibidi Jeshi la Polisi kupitia kitengo cha Interpool kuwasiliana na wenzao wa Mauritius ili kupata habari na undani wa mkasa huo. Kamanda Kivuy alisema kuwa katika kamata kamata hiyo kuna mwanamke Mkenya pia yuko kwenye mkasa huo ambao unajumuisha Watanzania sita na Mkenya mmoja. Habari zaidi zinasema Mwanamama huyo ambaye aliingia nchini humo Juni 10 mwaka huu alikuwa akifuatiliwa kwa karibu na maofisa wa upelelezi wa Mautius baada ya nyenendo zake kutiliwa shaka. tarehe 11 vijana mambondia wawili wa Tanzania walikamatwa Indre Street nchini Mauritius wakiwa na jumla ya pipi 373 zenye jumla ya kilo 6 ni dawa aina ya Heroin. Baada ya kukamatwa hao wawili ilibidi Polisi waende kuwachukua na wenzao wanne ambao walikuwa hotelini kwa kipindi hicho.

Watuhumiwa hao walifikishwa kwenye mahakama jumatatu wiki hii mjini Port Luis.
Kamanda Kivuyo amesema watanzania hao wanashitakiwa kwa makosa ya aina mbili.
i) Kujihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya
ii) Kuingiza nchini Mauritius Madawa hayo.
na Mama wa Kikenya atashtakiwa kwa kushirikiana na watu hao.
Jeshi la polisi bado linafanya uchunguzi kujua kama madawa hayo waliondoka nayo hapa au la.

Muungano wa Africa Mashariki na Magharibi Kimuziki

NI RAY C NA RF CHORD

Original ya wimbo huu uliimbwa na Ray C Peke yake ikiwa ni Remix ya wimbo wa Sikuhitaji wenye mahadhi ya Taarabu enzi hizo alipopachikwa jina la Kiuno bola mfupa, Wanamuziki wa Bongo Flava wameamua kwenda kimataifa kwani Ray C aliamua kuukarabati huu wimbo na kuuimba tena akishirikiana na mwanamuziki RF Chord toka Siera Leone ambaye makazi yao ni nchini, RF Chord ni wanachama wa UMPA [Union Movement of Performing Artists of Sierra Leone] ,Wakiwa ni moja ya vikundi vya muziki vyenye chart ya juu kabisa nchini mwake Siera Leone.

RF Chord ambaye anatumia zaidi mtindo wa “Dance Hall” huku akichanganya na midundo ya asili kwa nyimbo zake nyingi amejipatia umaarufu sana na Wimbo huu aliopiga na Ray C.Hii inasaidia kuufanya muziki wa Kizazi kipya kutambulika zaidi ingawaje kwenye wimbo huu Ray C aliuimba kwenye mahadhi ya Kipwani zaidi, ukiwa ni Remix ya wimbo wake wa Sikuhitaji ambayo ilipigwa kitambo kidogo, Hivi karibuni tumesikia Mwanamuziki toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anayeishi Uingereza Blanchard Deplaizir akitangaza kutaka kufanya Kolabo na Ali Kiba na majuzi tena Ali Kiba huyo huyo amesikiaka akiingia Studio na Vijana wengine, Shime kumekucha muziki huu umekubalika nchini ni wakati wa kuuza kimataifa na kwa jinsi hii mtatoka.
Pata burudani kwa kubofya Player…

Banana na Hafsa kuwapa “Pressure” mashabiki Club Afrique

Siku: Ijumaa

Ukumbi: Club Afrique

Wakisaidiwa na

DJ Dubwise – Voice of Africa Radio

Jessie – Afrique

Talent – Afrique Tallent

Biggz – Afrique/Nytce

wasiliana na

Lawrence -07931819416, Jesse-07944545555, jimmy-07877418535

Starehe Mita 1800 juu ya usawa wa Bahari

Sehemu ya Genting kama inavyoonekana jioni, taa zinazoonekana kwa mbali ni mji wa Kuala Lumpur unavyoonekana toka Milima ya Genting.

Panaitwa Genting Highland, Ni umbali wa Kilomita 50 toka Kuala Lumpur mjini kuelekea Genting Highland, sehemu ya milima nchini Malaysia, kwa kawaida Malaysia ni nchi ya joto kama ilivyo Dar Es Salaam lakini tofauti ni kuwa joto la malaysia ni 30c to 36c na Fukuto ila kuna mvua mwaka mzima, wastani wa mvua kunyesha ni kila baada ya siku 2 hadi tatu. Hii hufanya mji huu kuwa wa kijani mwaka mzima lakini huwezi amini kuna sehemu ya Malaysia jotoridi lake ni 12c to 20c na wakati wa baridi hasa kunadondoka barafu, Huku ndio kunaitwa Gentini umbali wa Mita 1800 toka usawa wa bahari.
Huku hasa ni mji wa mapumziko, naita mji kwani panajitosheleza kwa kila kitu kuanzia mahoteli hadi Hospitali ambapo watu hupendelea kwenda kupumzika na kupata starehe mbali mbali kama Cable Car ambazo zina urefu wa Kilomita tatu na nusu, na inapita katikati ya misitu minene ya Tropiki na ubaridi mwanana pia utaona ndege na wanyama kama nyani wakiruka kwenye miti huku ukipita kwenye kijikombe kilichobebwa na mkanda (cable) ambacho kina tembea mwendo wa wastani wa kilomita 10 kwa saa, ni burudani tosha ambayo inahitaji ujasiri kwani kama hujazoea utatamani kushuka.

Genting Highlands Malaysia
'xxxx'
Safari ndio imeanza ndani ya “Cable Car”


Ndani ya Cable Car kule kwenye ukungu ndio tunakoelekea na ndio raha zote zilipo, kuzifikia sasa kasheshe.

wadau washafika kwenye safari ya mashaka
Siku yapili “vakesheni” inaendelea

Baadaye unafika Theme Park huku kuna michezo zaidi ya 60 ya kila aina ikiwa ni pamoja na Roller Coaster yenye urefu wa Kilometa moja, Train, Speed Car, Speed Boat, Mashua, Michezo ya Jukwaani, Maonyesho ya Wanyama mbali mbali, Muziki, Vyakula vya kila aina, utamaduni, Bustani ya Ndege, Bustani ya Mamba, Bustani ya Nyoka, kwa ujumla panakufanya ujione uko mahali tofauti.


Live Performances usiku ni sehemu ya starehe za Genting

Pia kuna ukumbi wa Concert mkubwa ambao una uwezo wa kuchukua watu zaidi ya 10,000 na ukumbi huu ni full kipupwe, ambapo wanamuziki maarufu wakija pia hutumbuiza huko.Usiku kuna burudani za aina mbali mbali ikianziwa na sarakasi toka kwa akina dada ambao nadhani hawana mifupa, ije ngoma na utamaduni wa Wamalay (kama taarab) hadi Vikundi vya Kizazi kipya na nyimbo za kimagharibi pia, Kwa ujumla ni raha yaani mpaka unaona unapewa zaidi kuliko gharama halisi.

Image Hosted by ImageShack.us
Mambo ya mwambao hata huku yapo atii

Pia kuna uwanja wa Golf kwa wenye mchezo wao, ambao wengi ni wageni mahoteli zaidi ya 30 yaliyopo kwenye kijiji hiki cha maraha. Mbali na hiyo kuna Casino kubwa, hii ndio Licensed Casino kwa Malaysia na inakusanya wacheza kamali toka Singapore, Malaysia, Indonesia na Brunei ambao wote hufika kucheza kamali hapa.

Wednesday, June 18, 2008

SERIKALI YAONGEZA MKATABA KWA MAXIMO

Baada ya majadiliano ya watanzania kuhusu kama kuongezwa au kusitishwa mkataba wa Kocha wa Taifa Stars Marcio Maximo, hatimaye kocha wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ Marcio Maximo ameongezwa mkataba na Shirikisho la soka Tanzania (TFF) baada ya kuridhika na kaiz aliyoanza kuifanya ambayo imeipandisha chati Tanzania katika medani ya soka.

Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema hayo Juni 18 jijini Dar es Salaam mwezi mmoja kabla ya kumalizika kwa mkataba wa kocha huyo wa miaka miwili. Mkataba wa miaka miwili aliosaini kocha huyo kutoka Brazil utamalizika mapema mwezi ujao.
“ Maximo aliingia mkataba nasi wa miaka miwili kuanzia Julai 28,2006 hivyo mkataba wake huo utakamilika Julai 2, mwaka huu hivyo tumeona ni vema tulizungumzie jambo hili mapema na tumeamua kumwongezea mkataba huo kwa miaka miwili mingine” alisema Tenga
Hatahivyo Tenga alisema pamoja na TFF kuamua kumwongeza mkataba wa kwa miaka miwili mingine na Kocha Maximo katika mazungumzo yao juu ya kuongezwa mkataba huo ameomba uongezewe mwaka mmoja tu kutokana na sababu zake binafsi ambazo hakuzitaja.
Akizungumza mara baada ya Tenga kutangaza uamuzi wa TFF kumwongezea mkataba wa kuinoa Stars, Maximo alisema sababu kubwa ya kufurahia jambo hilo na kushukuru kwa ushirikiano aliopewa kutekeleza majukumu yake na kueleza kuwa sababu yake ya kuomba apewe mwaka mmoja tu katika mkataba mpya ni kutoa nafasi kwa makocha wengine kuendeleza pale alipofikia katika programu ya kuinua na kuendeleza soka la Tanzania.
“ Unajua mtu huwezi kutekeleza programu ya miaka 10 ya kuinua na kuendeleza soka la nchi pekee yako kwani kila programu ya kocha ina muda wake wa kukamilika hivyo katika mikaka hiyo 10 kuna ulazima wa kocha mwingine kuja kuendeleza pale nilipofikia” alisema Maximo
Aidha Tenga alisema uamuzi huo kuongeza mkataba wa Maximo umefikiwa baada ya Shirikisho hilo kutathmini kazi ya kocha huyo na kuonekana ametekeleza majukumu yake ipasavyo kutokana na hadidu rejea alizopewa na kuifanya TFF kuridhishwa na utendaji wake.
Akizungumzia suala la kocha huyo kuomba kuongezewa mkataba wa mwaka mmoja tu katika mkataba huo mpya Tenga alisema wamekubaliana kuwa endapo Taifa Stars itafuzu kushiriki fainali ya michuano ya kombe la dunia na zile za Mataifa ya Afrika za mwaka 2010 nchi Afrika Kusini na Angola ataendelea na kazi ya kuinoa timu hiyo.

Maximo ambaye kutokana na kuinyanyua soka ya Tanzania kwa kiwango kikubwa kwa kipindi hiki cha miaka miwili kuna taarifa kuwa kuna mataifa matano yanamnyemelea ili aende kuzinoa timu za mataifa hayo.

Holland yaendeleza kichapo

Holland 2-0 Romania
Dutch players celebrate at the end of the Euro 2008 Championships Group C football match Netherlands vs. Romania on June 17, 2008 at  the Stade de Suisse Wankdorf in Bern. Holland beat Romania 2-0 on Tuesday in Berne with goals from Klaas-Jan Huntelaar and Robin van Persie in their Group C match, a result which sent the Romanians crashing out of Euro 2008.  AFP PHOTO / PATRICK HERTZOG  -- MOBILE SERVICES OUT --        (Photo credit should read PATRICK HERTZOG/AFP/Getty Images)
Wachezaji wa Holland wakijipongeza na mashabiki mara baada ya kuwachapa Romania 2-0.

Magoli ya Klaas-Jan Huntelaar na Robin van Persie katika kipindi cha pili yailiipa Holland ushindi wa 2-0 dhidi ya Romani, Huu ni muendelezo wa ushindi kwa timu ya Holland ambayo imeshinda mechi zake zote.

Wa dutch wamemaliza ratiba ya awali kwa ushindi mzuri na sasa kwenye hatua ya Robo Fainali watakutaka na Sweden au Russia.
Romania ambao walihitajika kushinda mechi yao ya jana ili waweze kusonga mbele waliishia kusononeshwa tuu na waholanzi ambao hawakuwa na mchezo huku wakishangiliwa na wapenzi wao waliufanya uwanja mzima kuwa rangi ya machungwa.

Masikini Ufaransa, Italy yapaa

France 0 – 2 Italy

Celebrating a second-half goal.
Ushindi wa Italy wa mabao 2-0 dhidi Vibonde Ufaransa umeiwezesha Italy kufuzu kuingia hatua ya Robo Fainali, hii ni kutokana na mkali wa Kundi hili Holland kuichapa Romania na hivyo kufanya wanaokwenda mbele kundi hili kuwa ni Holland na Italy.

Andrea Pirlo ndiye alikuwa wa kwanza kupata bao kwa mabingwa hao wa dunia katika dakika ya 25 kwa penati baada ya Eric Abidal kumchezea madhambi Luca Toni ndani ya kumi na nane.

Abidal alipewa kadi nyekundu kwa tukio hilo na kuwaacha Ufaransa wakihangaika kuupanda mlima kufuatia mchezaji mwingine Frank Ribery kuwa majeruhi.

Italy walicheza kufa na kupona huku Ufaransa wakijitahidi kutaka kusawazisha bao mcheza ukawa wa vuta ni kuvute lakini mnamo dakika ya 62 Italy wakapata tena mpira wa adhabu ukaenda kupigwa na Daniele De Rossi na moja kwa moja ukaingia nyavu ndogo na kufanya Italy kuongoza kwa mabao mawili.

Ufaransa wamekuwa na wakati mbaya kwani angalao waliambulia sare kwenye mechi yao ya ufunguzi kabla hawajaja kubugizwa na Holland 4-1 na sasa Italy, Ikumbukwe kuwa Fainali za Kombe la Dunia ziliwakutanisha Iyaly na Ufaransa, ndio huku mchezaji wa Ufaransa Zinedine Zidane alimchapa kichwa cha kufa mtu Materazi.

Italy, ambao wamemaliza wakishika nafasi ya pili nyuma ya Dutch itakutana na mshindi wa Kundi D Spain siku ya jumapili katika hatua ya Robo Fainali huko Vienna lakini Waitaliano watawakosa wachezaji wao mahiri Pirlo na Gennaro Gattuso, ambao kwa pamoja walipata kadi kwenye mchezo wa jana.

Tuesday, June 17, 2008

Mzee Mwinyi akatiza safari ya Mlima Kilimanjaro

Pichani ni Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa kwenye moja ya njia za Mlima Kilimanjaro, Mzee Mwinyi alikatisha safari yake hiyo.Hakuna maelezo kutoka kwa wadhamini wa safari yake lakini imeelezwa kuwa amekatisha kwa sababu binafsi.Rais mstaafu alikuwa anakwea mlima huo mrefu katika kipindi kigumu kabisa cha mvua na baridi kuchangia wale wanaoishi na VVU katika mustakabali ambao unaendeshwa na mgodi wa dhababu wa Geita.

Pichani rais mstaafu (katikati)akiwa na wafanyakazi wa Celtel Tanzania,Prisca Tembo (kulia) na Cuthbert Raphael (kushoto),muda mfupi kabla ya kupanda Mlima Kilimanjaro.Picha hii ni kwa hisani ya Celtel.

Kelly atembelea uwanja wa Fisi!!


Msanii maarufu wa Marekani Kelly Rowland (mwenye mtandio juu na chini), ametinga uwanja wa fisi Manzese Dar es salaam jioni ya leo baada ya kusikia sifa za maeneo hayo ya uswahilini tangu akiwa USA. Msanii huyo ametua nchini kwa tiketi ya MTV kupitia taasisi yake inayojishughulisha na kampeni za kupambana na Ukwimwi (Staying Alive Foundation) ya nchini Marekani, Kelly akiwa balozi wake. Akiwa Uwanja wa Fisi, ambako kunasifika kwa ufuska wa kupindukia na rate kubwa ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wasichana wadogo, Kelly alitembelea NGO ya EYG (Elizabeth Youth Group) inayojishughulisha na kutoa misaada ya elimu ya HIV/AIDS, uchangudoa, ulevi pamoja na uvutaji bangi kwa vijana nchini. Pichani juu akiongea na waandishi wa habari katika hoteli ya Kempinsk jioni ya leo mara baada ya ziara ya Manzese na Tandale. PICHA: CHRISTOPHER LISSA wa GPL

Salamu za Cynthia Masasi

“…Welcome everybody on my New Website http://www.cynthiamasasi.com its been a while since i updated my website but its ON now..i will be chatting with my Fans,friends on my msg board everyday..So feel free to ask any question u have and i will try to answer all the questions as soon as possible..

Why im writing this msg is b’cause im shutting my HI5 profile down by June 20th 2008,so i wont have HI5 anymore friends..Welcome to my world i will have all the cool staff from video’s,new pictures,shows and many more cool things..And if u have any questions about modeling or tryna get into it holla at ya girl cause i gotchu..

Woooo i forgot one thing LOL i will be in columbus ohio for the old school party on July 4th weekend so everybody is welcome its gonna be bananas trust me The number one DJ Bon Luv from Tanzania will be in the building..People u dont wanna miss that come on so we can PAAAARTYYYY..

Love Cynthia masasi..

Gonga Player hapo upate kuona moja ya Video ambamo ameshiriki Cynthia

ZIKO: Scolari atawafungulia Brazili Uingereza

Mchezaji matata wa zamani wa Brazili Ziko amesema Luiz Felipe Scolari atakuwa na mafanikio makubwa na klabu ya Chelsea na atamfurahisha mmiliki wa klabu hiyo.

Scolari amechanguliwa kuifundisha klabu ya Chelsea kwa mkataba wa Paundi million £6 kwa mwaka akiwa na jukumu gumu la kukichukua kikombe cha Premier Ligi kutoka kwa Manchester na lililo muhimu ni kuchukua kikombe cha UEFA Champions Ligi kwa mara ya kwanza.

Kocha huyo wa Brazili ambaye kwa sasa anaifunza timu ya Taifa ya Portugal katika michezo ya fainali ya EURO 2008 ameshatajwa kutaka kuwachukua wachezaji mahiri kama Kaka, Ronaldinho, Franck Ribery, Rafael van der Vaart, Samuel Eto’o, Deco, Fernando Torres na David Villa ambaye anaongoza kwa ufungaji kwenye michezo ya EURO 2008.

Kujiunga kwa Scolari kwenye ligi ya Uingereza kutaifanya Brazil na wachezaji wengi wa Brasili kuiangalia ligi hiyo kwa jicho jingine ambapo wengi wa wa Brasili walipendelea kucheza sehemu nyingine za Ulaya sio Uingereza kikubwa ilikuwa ni Lugha na pia jinsi utamadubni wa waingereza ulivyo tofauti.

Zico anaamini kuwa hii itawanufaisha sio tu Premier League ila pia Brazil, na akasema: “Kufika kwa Scolari huko Chelsea ni mafanikio makubwa kwa Brazili na majaliwa ya soka la Brazili pia, tuna tatizo, hatupendi waingereza wanavyofanya mambo yao, na tunapingana hapo tuu inabidi kubadilika hiyo ndio maana yangu aliongeza Ziko.

“Hii ni nafasi kwa wachezaji wa Brazili kutoka Brazili na kwenda kucheza Uingereza itaifungua BRazili na soko la wa Brazili Uingereza pia. na sisi tutajifunza mengi si tu mpira hata maisha na utamaduni pia, soka inalipa kwa Uingereza, watu kule wanapenda soka na wanmefanikiwa kuianya ligi yao kupendwa ulimwenguni huko ndio kwa kwenda kucheza, aliongeza Zico.sement

Hatimaye Ujerumani wavuka

Austria 0-1 Germany
(From L) German defender Christoph Metzelder, German midfielder Michael Ballack and German midfielder Thomas Hitzlsperger wave to the crowd after winning 1-0 during the Euro 2008 Championships Group B football match Austria vs. Germany on June 16, 2008 at Ernst Happel stadium in Vienna.        AFP PHOTO / JOE KLAMAR       -- MOBILE SERVICES OUT --    (Photo credit should read JOE KLAMAR/AFP/Getty Images)
Wachezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani toka shoto Christoph Metzelder, Michael Ballack na Thomas Hitzlsperger wakiwapungia mashabiki baada ya mchezo wao kumalizika jana dhidi ya Austria na kushinda goli 1-0.

Michael Ballack ndiye aliyefanya booking ya Ujerumani kwenye nafasi ya Robo fainali kwa shuti safi kipimo iliyopatikana kwa mpira wa adhabu ikiwa ni dakika ya 49 ya mchezo mara tu baada ya kipindi cha pili kuanza na kuwanyamazisha kabisa wenyeji Austria katika mchezo wa mwisho wa kundi B.

Mchezaji huyu wa Klabu ya Chelsea ambaye mapema jana alilalamika kuwa hafurahii kiwango alichoonyesha kwenye michuano hii aligeuka ghafla na kuwa mwiba wa sumu kwa Austria.

Austria ambao nao walipoteza mchezo mmoja a kutoka droo mmoja walikuwa wanategemea ushindi wa jana na kuombea mabaya mchezo wa Poland na Croatia ili wajihakikishie nafasi ya Robo fainali lakini bahati haikuwa yao jana.

Ballack anakwenda kukutana na Kocha wake mpya kwa klabu ya Chelsea Philipe Scolari kwenye mchezo wa Robo Fainali kati yao na Portugal mchezo ambao mashabiki wanaungoja kwa hamu. Luiz Felipe Scolari, ndiye ataifundisha Chelsea kuanzia msimu huu na atajiunga na Klabu hiyo mara baada ya michuano hii kumalizika.

Ujerumani wanabahati mbaya kwani hawatakuwa pamoja na Kocha wao kwenye chumba cha kubadilishia nguo na wala benchi huko Basel’s St Jakob-Park siku ya alhamisi ambapo watamenyana na Portugal, baada ya kutolewa nje mechi ya jana baada ya kutupiana maneno na mwenzie na maofisa wa UEFA. Mpaka mwisho wa mchezo Austria 0-1 Germany.

Sheria ni msumemo…

German coach Joachim Loew (L) speaks with Austrian coach Josef Hickersberger (R) after being ordered out of the field during the Euro 2008 Championships Group B football match Austria vs. Germany on June 16, 2008 at Ernst Happel stadium in Vienna.      AFP PHOTO / OLIVER LANG      -- MOBILE SERVICES OUT --       (Photo credit should read OLIVER LANG/AFP/Getty Images)
Kocha wa Ujerumani Joachim Loew (L) akiongea na Kocha wa Austria Josef Hickersberger (R) baada ya kutakiwa kutoka nje ya uwanja katika mchezo baina ya Timu zao jana.

Do or Die ya Ufaransa Leo

French forward Thierry Henry reacts after missing a goal opportunity during their Euro 2008 Championships Group C football match vs the Netherlands in Bern, Switzerland, last week which Holland won 4-1. France go into their do or die clash with Italy beset by doubt, reports of internal strife and player fatigue.

Mshambuliaji wa Ufaransa Thierry Henry akihudhunika baada ya kukosa bao katika mchezo wao na Netherland wiki ilopita ambapo waliloweshwa 4-1, Ufaransa wanakutana na Italy katika mchezo wa Kundi C ambapo kama wakifungwa basi watakuwa wmeaga mashindano haya. kwani kundi hilo linaongozwa na Netherland ambao wana Pointi 6 mpaka sasa kwa kushinda michezo yao miwili kwa jumla ya mabao 7, na kufuatiwa na Romania ambao wana pointi 2 kwa kutoka sare mara mbili na Itally ana pointi moja kwa sare yake na Romania na Ufaransa ambaye ameoteza mchezo mmoja na kutoka sare mmoja katika mchezo wa Kundi C.

Croatia haoooo Robo fainali

Poland 0-1 Croatia
Croatian midfielder Nikola Pokrivac (R) walks on the pitch with a ball under his jersey next to Polish defender Adam Kokoszka after the Euro 2008 Group B football match Poland vs. Croatia on June 16, 2008 at the Woerthersee Stadium in Klagenfurt, Austria. Croatia beat Poland 1-0 here on Monday in their final Euro 2008 Group B match here on Monday.     AFP PHOTO / DDP - RONNY HARTMANN   -- MOBILE SERVICES OUT --        (Photo credit should read RONNY HARTMANN/AFP/Getty Images)
Mchezaji wa Croatian Nikola Pokrivac (R) akitembea huku ameweka mpira tumboni baada ya kuifunga Poland kwenye mchezo wa jana wa Kundi B. anayemuangalia ni Mchezaji wa Poland Adam Kokoszka.

Goli lililofungwa na Ivan Klasnic katika dakika ya 52 ya kipindi cha pili liliwafanya Croatia kumaliza mechi zake zote tatu toka kundi B kwa ushindi. Croatia ambao awali waliifunga Australia 1-0, wakaifunga Germany 2-1, na jana wameifunga Poland 1-0, matokeo yaliyowapeleka moja kwa moja Robo Fainali ambapo watakutana na Mshindi wa pili wa Kundi A ambaye ni Turkey.

Ndoto ya Poland kufika mbali haikuweza kufanikiwa kwani waliihitaji kushinda mchezo huu na pia hata kushinda kwao kulitegemeana na matokeo kati ya mchezo wa Australia na Germany ambapo Australia alikuwa ame droo mara moja na na kuwa na point 1 na Germany alishinda mara moja dhidi ya Poland na kuwa na Point tatu. na Poland ame droo mara moja na kuwa na point 1 ambapo kama angeshinda jana basi angefikisha point 4 na kama Australia na Germany wangetoka Droo pia Germany angekuwa na Point 4 ambapo labda wangezidiana magoli.

Fans of the national soccer team of Croatia celebrate Croatia's 1-0 win over Poland in the EURO 2008 soccer match in the city center of Frankfurt, central Germany, on Monday, June 16, 2008.

Mashabiki wa Croatia mitaani

Hata hivyo mchezo wa jana ambao kila timu ilihitaji kushinda ulikuwa mzuri kwa kila timu kuonyesha mashambulizi ya hapa na pale na huku Poland wakionyesha dhahiri kukamia ushindi ila bahati haikuwa yao.

Turkey ambaye alipoteza mchezo wake na Portugal katika kundi A anakibarua kigumu akija kukutana na Croatia ambao wao kwao ushindi ndio nguzo yao na wanacheza kwa kujiamini dakika zote. Tungoje tuone.

KELLY ROWLAND NDANI YA BONGO

Bila shaka utakuwa bado unalikumbuka kundi maarufu la muziki lililokuwa linajulikana kama Destiny’s Child kutoka nchini Marekani. Miongoni mwa mabinti waliokuwa wanaunda kundi hilo ni Kelly Rowland(pichani).Wenzake walikuwa ni Beyonce Knowles(mke wa Jay Z hivi sasa) na Michelle Williams. Kundi hilo lilivunjika rasmi mwaka 2005 ingawa mara moja moja bado huwa inatokea wakafanya maonyesho pamoja. Bonngo Celebrity wameiweka kwa mapana zaidi

Miss Tanzania UK kapatikana


MISS TANZANIA 2008 UK!

Kimwana Tusekile Mwakibinga alitawazwa rasmi juzi kuwa Miss Tanzania Uk 2008 kwenye sherehe zilizofanyika ndani ya Silver Spoon New Light Complex karibu na wembley Stadium.Pichani Miss Tanzania Uk 2008 Tusekile Mwakibinga akiwa katika picha ya pamoja na First Runner Up Miss. Jacqui Majebele(kushoto) na Second Runner up Miss. Alice Kapya.

Washiriki na washindi wa shindano la Miss Tanzania Uk 2008 wakiongozwa na Miss Tanzania Uk 200 Tusekile Mwakimbinga wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Hon Mwainda Maajar.

Washiriki wakijinadi mbele ya majaji

Mshiriki wa Big Brother Africa 2008 kutoka Tanzania Richard Bezuidenhout (kulia)nae alikuwepo Miss Tanzania Uk 2008

Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania Hashim Lundenga (Kulia)nae alikuwepo kwenye shindano la Miss Tanzania Uk 2008. Picha na Habari zote kwa hisani kubwa kabisa ya Blog ya Haki Ngowi, Bonyeza Hapa kupata Picha Zaidi

Monday, June 16, 2008

Akudo Impact kupekecha na Miss Sinza

BENDI maarufu ya muziki wa dansi nchini ya Akudo Impact ‘Wazee wa Masauti’ wataongoza burudani katika mashindano ya kumsaka mrembo wa kitongoji cha Sinza Ijumaa kwenye Ukumbi wa Vatican City, Sinza.

Akudo kwa sasa ambayo inakubalika na mashabiki wengi wa muziki wa dansi inatamba na wimbo wa Binadamu� huku nyota ya rapa na muimbaji wake, Christian Bella ikiendelea kung’ara zaidi.

Mratibu wa mashindano hayo, Somoe Ng’itu alisema jana kwamba tayari kwa takribani wiki mbili sasa wanamuziki wa bendi hiyo walikuwa wakifanya mazoezi kwa ajili ya mashindano hayo.

Somoe alimtaja msanii wa kizazi kipya, Kassim Mponda Cassim anayetamba na Siamini na Awena na kwa upande wa muziki wa asili ni Mrisho Mpoto anayefanya vizuri katika nyimbo mbalimbali ukiwamo Mjomba alioshirikishwa pamoja na Wanne Star ambaye ni maarufu kwa kucheza na nyoka katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Tumeamua kuchanganya burudani ili kila mtu apate anachotaka japo kikubwa watu wataona pia burudani ya kutosha kutoka kwa warembo bomba, alisema.

Wadhamini kadhaa wamejitokeza kudhamini shindano hilo ni pamoja na Mama Tike Hair Fashions, Redds, Multchoice Tanzania, Vannedrick (T) Ltd, 2080 Fashions, Break Point, Coca Cola, Vodacom, gazeti la Tanzania Daima na Clouds FM 88.4.

Msondo usipime!!

Bendi ya Msondo Music usiku wa kuamkia leo ilifanya makamuzi ya kufa mtu katika Ukumbi wa Africentre uliopo Ilala jijini Dar es Salaam, kama kawaida yake, naye mnenguaji mwenye mbwembwe wa bendi hiyo Nacho Said, eikeiei Mama Nzawisa, alianza mbwembwe hizo kama ifuatavyo. Pichani Mama Nzawisa akimpelekesha puta jukwaani mwamuziki wa bendi hiyo Roman Mng’ande ‘Romario. Picha na Richard Bukos wa GPL

Etoo kazuliwa kijambo!!

Pichani Samuel Etoo katika picha ianyosemekana alitoroka kambia na kulia ni dada aliyekuwa naye.

Kama kawaida kwenye wengi kuna mengi, Timu ya Taifa ya Kameroon ilikuwa Tanzania kucheza na Taifa Stars katika mchezo wa awali wa kuwania tiketi ya Kombe la Dunia, Ikiwa imekwenda na Wachezaji wake mahiri kama Samuel Etoo na Song iliambulia Sare na Taifa Stars, Je wajua kilichotokea nyuma ya pazia kwa Striker wa Kameroon Samuel Etoo? Gonga hapa uisome!!

Karibu Malaysia!!

Selamat Datang Ke Malaysia, Hikli tangazo limo ndani ya Train ya Umeme sasa OLE wako!! Hii ndio Malaysia!. Hahaha Denda maana yake ni Adhabu!!, (USd 1=3.2 RM-Malaysian Ringit)

Turkey yawafungisha virago Czech

Turkey 3 – 2 Czech
Young Enes, a supporter of the Turkish national soccer team, is reflected in the roof a car as  he celebrates the victory of his team after the Euro 2008 soccer match between Turkey and Czech Republic on the streets of the district Kreuzberg in Berlin, on Sunday, June 15, 2008.
Mashabiki wa Turkey wakiwa mitaani

Nihat Kahveci ndiye aliyekuwa nyota wa mchezo wa jana kwa kufunga magoli mawili dhidi ya matatu ambayo Turkey walishinda na kuwafungisha Virago Jamhuri ya Czech kwenye mchezo wa fainali wa undi A jijini Geneva.

Kwa ushindi huo Turkey wamejihakikishia nafasi ya pili ya kundi A kwa kufikisha Point 6 kama Portugal baada ya kushinda mchezo wake wa mwanzo dhidi ya Switzerland kwenye mchezo wa ufunguzi.

Mpaka dakika wa 62 Czech walikuwa wakiongoza kwa 2-0 mabao yaliyofungwa na Jan Koller dakika ya 34 na Jaroslav Plasil dakika ya 62.

Turkey ambao walibadilika kabisa hasa dakika 25 za mwisho za mchezo iliwachukua hizo hizo dakika 25 kupachika mabao matatu yaliyowapa ushindi.

Mabao ya Czech yalifungwa dakika ya 75 na Arda Turan (75), dakika ya 87 na Nihat Kahveci (87) na la tatu dakika ya 89 na Nihat Kahveci (89). na kuwanyong’onyeza kabisa mashabiki wa Czech ambao walikuwa wakiishangilia kwa nguvu timu yao na kujua wameshinda mchezo huo.

Kwa ushindi huo Turkey wanaungana na wenzao Portugal kwenye hatua ya Robo Fainali ambapo Turkey watapambana na mshindi wa kundi B.

Switzerland yazizima Mbwembwe za Portugal

Switzerland 2 – 0 Portugal
Swiss forward Eren Derdiyok 9top0 vies with Portuguese defender Pepe during the Euro 2008 Championships Group A football match Switzerland vs. Portugal on June 15, 2008 at Jakob-Park stadium in Basel.   AFP PHOTO / DANIEL MIHAILESCU    -- MOBILE SERVICES OUT --  (Photo credit should read DANIEL MIHAILESCU/AFP/Getty Images)
Forward wa Swiss Eren Derdiyok akiwa kwenye heka heka na na na beki wa Portugal Pepe wakati wa mchezo wa Kundi A ambapo Swiss waliibuka washindi kwa 2-0.

Magoli mawili yaliyofungwa na Hakan Yakin dakika ya 71 na 83 ndio yaliyowakosesha raha mashabiki wa Portugal (nikiwemo mimi), na kuipa ushindi Switzerland wa 2-0 dhidi ya Portugal.
Ushindi huo umewasaidia waandaaji hao angalao kuambulia ushindi na kwao ni ushindi mwanana kwani wameifunga na kuishinda timu ambayo haijapoteza mchezo hata mmoja tangu mashindano haya yaanze.

Pamoja na kichapo hicho Portugal wanakwenda Robo fainali kama washindi wa kundi A na Swiss wamejikongoja baada ya kupoteza michezo yao yote miwili ya awali hivyo ushindi wa jana umefanya wafikishe pointi 3 pekee.
Yakin alifunga bao la kwanza baada ya pasi toka kwa Eren Derdiyok ikiwa ni dakika ya 71 ya mchezo na kuachia shuti toka umbali kama wa yadi 15, shuti lililopita tobo golikipa wa Portugal na kuandika goli la kwanza.

Dakika 12 baadaye Yakin aliifungia timu yake goli la pili kwa njia ya Penati.
Portugal wanacheza Jumamosi hii na mshindi wa pili wa kundi B.

Sunday, June 15, 2008

Klynn

Anaitwa Klynn, Miss, Mwanamitindo na Mwanamuziki, mtembelee kwenye wavuti wake kwa kubofya hapa au waweza Tembelee 8020 uone Wadrobe yake na Mamaa Zeze.
Nawaacha na Video yake ya Crazy Over You…… Jumapili Njema,
Papaa Pius

Mke wa Snoop Dogg Mbaroni kwa kuendesha akiwa amelewa

Habari zinapasha kuwa mke wa Mwanamuziki Snoop Dogg alikamatwa na Police huko Calfornia kwa kosa la kuendesha gari huku amelewa.
Luteni Craig Brower alisema maofisa wake walimsimamisha Shante au Shahn-taye (32) pichani kulia (Picha iliyotolewa na Police baada ya kukamatwa) majira ya saa sita na robo usiku wa jana jumamosi huko Sherman Oaks na wakamchukua na kumtupa lupango lakini baadaye jana hiyo hiyo aliachiwa kwa dhamana lakini atafikishwa kortini.
Maofisa wa polisi walisema kuwa MNkwe wa mwanamuziki huyo alikuwa peke yake kwenye gari,.Snoop na mkewe wana miaka 11 ndani ya ndoa yao na wana watoto watatu.

Jioni ya “KHANGALICIOUS” June 20

Mustafa Hassanali Juni 20,2008 atafanya onyesho kubwa la mavazi yanayotokana na Khanga. Maonyesho hayo yatafanyika katika hoteli ya kitalii ya Moevenpick Royal Palm na yamepewa jina la “KHANGALICIOUS”,Kwa maneno yake mwenyewe onyesho hilo limelenga kutunza umaarufu wa vazi la khanga ambao umetamba katika mwambao wa Afrika Mashariki kwa miaka mingi.

Miss Ubungo 2008 huyu hapa

Miss Ubungo Amatha Chrispin (katikati) akipunga mkono kufurahia taji hilo (kulia) kwake ni mshindi wa pili wa taji hilo, Ansia Kweka, na Rahma Gege. Picha na Issa Mnally.

Jk Boys waliowatoa Kamasi Cameroon

Picha hii iliyopigwa na Global Publishers Inaonyesha wachezaji wa Taifa Stars wakiomba Dua kabla ya mechi yao na Cameroon jana, Sala ambayo kwa kwa kiasi kikubwa ilisaidia na Mungu akajalia kukinga kifua.

Kikosi cha Taifa Stara – JK Boys kilichoumana na Cameroon hapo jana, waliosimama nyuma toka kulia ni Dan Mruanda, Nadir Haroub ‘Canavaro’ (kipenzi cha Maximo), Athumani Iddi ‘Chuji’, Shaaban Nditi na Salum Swedi. kati toka kushoto ni Nizar Khalfani, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Bonny, Mrisho Ngassa na Amiri Maftaha. mbele ni Ivo Mapunda –Tanzania One, Picha na Mpoki Bukuku

Keeping Up With the Kardashians mitaani Monaco

Wakiwasili sehemu ya mapumziko ya Hotel

Wakila boti ku zunguka baharini kidogo!

Mtu na nduguye Kim na Kourtney Kardashian ndani ya Ferrari mitaani Monaco

Mitaani
Kwa waangaliaji wa E! Channel mdada huyu si mgeni kwenye Reality show ya Keeping Up With the Kardashians, Kila mwanaume aulizwapo mdada gani humvutia basi atamtaja Kim Kardashian na kweli huwatoa udenda wakware si kitoto, kwani ana vituko vya makusudi hasa, Hivi karibuni kamera za mapaparazi zilimnasa akila maraha huko Monaco(pichani) akiwa na dada yake Kourtney Kardashian. Pata picha na habari zaidi za mwanadada huyu kwa kubofya Website yake ambapo yeye mwenyewe huandika kila kitu anachokifanya kila siku!.

Saturday, June 14, 2008

Villa aibeba tena Spain dhidi ya Sweden

Spain 2 – 1 Sweden
Wachezaji wa Spain wakimpongeza Villa mara baada ya kupachika bao la pili huku mashabiki wa Sweden wakiangalia kwa uchungu.
Goli lililofungwa na David Villa dakika ya 90 limewapa Spain ushindi wa 2-1 dhidi ya Sweden katika mechi ya mashindano ya EURO kundi la D. Spain waliongoza kwa kupata goli katika dakika 15 ya mchezo toka wa Fernando Tores lakini Sweden walijitahidi na kufanikiwa kurudisha goli hilo katika dakika ya 34 ya mchezo kipindi cha kwanza kupitia kwa Zlatan Ibrahimovic ambaye alipachika mpira huo kimiani. Dakika ya 90 mwishoni mchezaji mahiri na matata Villa aliipatia Spain goli la ushindi na hili kuwa ni goli lake la nne tokea mashindano haya yaanze.
Mpaka sasa Spain wamefanikiwa kufikisha pointi 6 na Sweden 3. Greece ambao ni mabingwa watetezi wanacheza na Rushia usiku huu huko Salzburg.

Zali, Jezi ya Etoo

Kijana mdogo wa Kikosi cha kuokota mpira uwanja wa Taifa akiwa amevaa Fulana ya mchezaji wa Cameroon Samuel Etoo, Kijana huyu aliamua kuivaa Fulana hiyo baada ya kuona dalili za kunyang’wanywa na wababe. Hii ni baada ya mechi kati ya Taifa Stars na Cameroon ambapo Stars waliilazimisha sare ya 0-0.
Picha na Mpoki Bukuku.

Malawi yaichapa Egypty 1-0

MABINGWA wa Afrika, Misri wamepata mshtuko baada ya kupata kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Malawi mjini Blantyre.

Katika mchezo huo wa jana wa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika mwaka 2010, Misri iliamini mchezo huo ungeisha suluhu.

Misri, ambayo inafundishwa na Hassan Shehata ilifungwa bao hilo pekee ndani ya dakika tatu za majeruhi, ambalo lilifungwa na Chiukepo Msowoya wa Malawi.

Katika mchezo mwingine, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo iliifunga Djibout mabao 6-0 katika mchezo uliofanyika juzi.

Kwenye mchezo mwingine jana, Tembo wa Ivory Coast walilazimishwa sare nyingine walipocheza na Botswana.

Dipsy Selolwane aliipa Botswana bao la kuongoza dakika ya 25 mjini Gaborone na kuwafanya Ivory Coast wasubiri mpaka dakika ya 64 kusawazisha bao kupitia kwa Kanga Akale.

Ni mara ya pili kwa Ivory Coast ambao walicheza bila Didier Drogba kutoka sare ndani ya mwezi huu kwani wiki iliyopita walibanwa na kutoka suluhu na Madagascar.

Taifa Stars yailazimisha Sare Cameroon

Taifa Stars 0 – 0 Cameroon
Picha na Mpoki Bukuku habari na Mwananchi


Haya huyu jamaa rigobert Song aliamua kuwafanyizia vijana kwa kuwachezea faulo za nguvu imagine hapa anamfanyizia Amir maftah!

Hakutosheka akaamua kumweka kipepsi Athumani Idd, jamani vijana wanatisha tuache kuwakatisha tamaa!

Msajigwa leo katisha katika mechi kafanya mambo kichizi kawachanganya wacameroon!

Jamaa hapa alipita mpira ukabaki yaani ilikuw amsalie Mtume kama tungekuwa na wafungaji wazuri jamaa wangekoma.


Mchezo kati ya Taifa Stars na Cameroon umemalizika jioni hii katika uwanja wa Taifa kwa Timu hizo kutoka droo ya bila kufungana.

Katika mchezo huo ambao Taifa Stars walionyesha kuumudu vilivyo kutokana na Timu hiyo kuipa Upinzani wa hali ya juu timu ya Cameroon ambayo kila mmoja aliipa nafasi ya ushindi.

Viungo wa Stars; Athuman Idd, Geofrey Bonny, Shaabani Nditi na Nizar Khalfan walifanya kazi kubwa kutibua mipango ya Cameroon.

Ingawa Stars walipiga mashuti matatu tu langoni mwa Cameroon, lakini yalikuwa ya hatari na hasa kama Danny Mrwanda ambaye aliwasumbua sana angetulia.

Dakika ya 13, Mrwanda alikosa bao baada ya kutengenezewa pasi nzuri na Athuman Idd lakini mpira huo uliondoshwa na Rigobert Song ambaye baadaye alionekana kuhamaki kutokana na kasi ya Danny Mrwanda na Mrisho Ngassa.

Kama Ulaya!!!! Golikipa wa Taifa Stars Ivo Mapunda akiondoa hatari golini mwa Taifa Stars, Katika mchezo wa Leo ambapo naye aliwakatisha tamaa Wa Cameroon mara kadhaa

Cameroon, ambao walionekana kucharuka kuanzia dakika ya 20, walipata kona tatu mfululizo ambazo hazikuwa na madhara kwani Mapunda alipangua kichwa cha Eto’o na mabeki wakafanya kazi kubwa kuondoa kona nyingine zilizokuwa zinapigwa na

Njitap.

Matumaini ya mashabiki wa soka yalikuwa makubwa baada ya kuona Cameroon ikikubali kwenda suluhu mpaka wakati wa mapumziko huku Ngassa na Mrwanda wakionekana tishio.

Kipindi cha pili kilikuwa kizuri zaidi kwa Stars kwani walionana kwa muda mwingi na kukaba vizuri huku sehemu ya kiungo ikimiliki vizuri.

Mabeki wa Stars, Shadrack Nsajigwa, Salum Sued, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Amir Maftah walifanya kazi nzuri ya kuwadhibiti Eto’o, Achille Webo na Jean Makoun ambao hawakuleta madhara licha ya kuonekana hatari kila walipogusa mipira.

Mwamuzi bora Afrika, Bonaventure Kofi Kodjia wa Benin alilalamikiwa na mashabiki kwa kushindwa kutoa penalti wakati Mrwanda alipoangushwa eneo la hatari na Andrey Bikey dakika ya 75 wakati akienda kumuona kipa Idrissa Kameni dakika ya 75.

Dakika kumi za mwisho, Mrwanda alionekana kuwa tishio lakini alishindwa kuzitumia nafasi, huku Cameroon wakionekana kuhamaki kutokana na kushindwa kwenda sawia na kasi ya Stars.

Maximo aliwatoa Nizar na Athuman Idd na kuwaingiza Abdi Kassim pengine kwa kutaka mashuti ya mbali na Kigi Makasi kwa lengo la kutaka kuimarisha upande wa kushoto kama ambavyo Maximo amewahi kusema siku za nyuma.

Stars: Ivo Mapunda, Shadrack Nsajigwa, Amir Maftah, Salum Sued, Nadir Haroub, Geofrey Bonny, Shaaban Nditi, Athuman Idd/Kigi Makasi, Danny Mrwanda, Nizar Khalifan/Abdi Kassim na Mrisho Ngassa. Leo ni Mauritius na Cape Verde.

Watoto wa Mitaani na Bendi yao

Wiki iliyopita niliandika habari ya Vijana wa Ifakara wanaoburudisha watu na kuelimisha kuhusu janga la Ukimwi (Bofya hapa usome tena) , kutokana na vifaa duni wanavyo tumia nashukuru Mdau mmoja msomaji wa Blog hii toka Japan anafanya mipango ya kuwapatia vyombo vya muziki vijana hao na mambo yakikamilika tutawaletea habari kamili, Wiki hii tunakutana na vijana wa Mitaani ambao waliamua kuanzisha Bendi yao katika kujitafutia lizki na kutumbuiza mitaani jijini Dar es SalaamVijana hawa walinaswa na Kamera ya Global Publishers hivi karibuni maeneo ya Soko kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakiburudisha watu kwa kuwapigia muziki ili kujipatia chochote. Vijana kama hawa wanatakiwa wapewe msaada na kuendelezwa.

Sanaa na wasanii

kivazi.jpg
Picha hii ya Bob Sankofe inaonyesha Vijana wa Zawose ni matata sana. Cheki hawa jamaa vivazi vyao. Hivi vivazi ni zaidi ya vivazi, ni vyombo vya muziki pia. Jamaa wakiruka juu na kurudi chini vivazi hivi vinatoa mlio fulani murua sana, lakini inabidi uwe na sikio la kimuziki kuweza kutumia ala hii la sivyo ukipewa kama huna hicho kipaji utaishia kuharibu muziki mzima kwa kukosa kitu wataalamu wanaita ‘tempo’ au mwendokasi wa muziki. Mzee wangu Edwin Mikongoti anampenda sana Zawose, Heshima kwako.

Mabondia wa Tanzania Mbaroni Mauritius kwa Madawa ya Kulevya

Breaking News!!!! wabongo sita, wakiwemo mabondia wanne, inasemekana wametiwa mbaroni huko mauritius leo asubuhi kwa kile kilichoelezwa kukutwa na madawa ya kulevya.

Isome zaidi kwa Issa Michuzi

Patchou Lumiere, Nyota mpya ya kizazi kipya cha Kongo

kila siku kuna sauti mpya, wimbo mpya, mwanamuziki mpya, Hivi karibuni kundi la Rhumba la Muziki lilifanya rekodi ya albamu yake chini ya Kiongozi Pitshou Lumiere na mwanamuziki huyu anasemekana kutumia pesa nyimngi katika kutengeneza Video za Nyimbo za Albamu yake, kwa sasa Koffi Olomide anatajwa kuwa ndiye Mwanamuziki wa Zaire ambaye hutumia pesa nyingi katika kutengeneza Video za nyimbo zake ikiwa ni kuanzia Kampuni ya Utengenezaji, Mavazi na sehemu anazotengenezea Video hizo, lakini Video za Muziki za Pitshou zilipigwa kwa mbwembwe kama picha zinavyoonyesha.
Kava la juu la CD ya Bendi ya Rhumba la Muzika
Kiongozi Pitchou Lurmiere akiwa kwenye shooting ya wimbo wa Chez Ntemba

Mbwembwe za Pitshou wakati wa shooting ya wimbo wa Moise Katumbi unaopatikana kwenye Albamu hiyo.

Vimwana wakiwa wamekula pozi wakati wa shooting ya wimbo wa Chez Ntemba kwenye albamu ya kundi la Rhumba la Muzika.
Lumiere akiwa na Vimwana katika moja ya vibwagizo vya nyimbo zake.

Wanamuziki wa Kongo katika suala la burudani ya muziki wa dansi wamepiga hatua, hivi karibuni mjadala wa kuhusu kitendo cha kundi la TOT Respect chini ya uongozi wa Kamarade Ali Choki kwenda Kongo kutafuta wanamuziki kwa ajili ya kuipa nguvu kikosi chake lilipigiwa kelele na wengi wakaonyesha kuwa ni kuua na kutothamini muziki wetu, lakini katika dunia ya leo ya utandawazi ambapo kimsingi hakuna mipaka kila mmoja anajaribu kuangalii kama si unafuu basi kiwango katika kukamilisha liziko la nafsi (satisfaction). Je ni kweli kuna haja ya kufanyiwa mabadiliko muziki wetu? Kwani tumeona jinsi bendi zilnazopiga muziki wetu kuchanganya na Rhumba ya Congo kama Twanga Pepeta zinavyofanikiwa.

JB Mpiana: Fally, Celeo, Ferre i kizazi cha nne si cha tano.

JB Mpiana Bin Adam Tshituka Papa Cherry

Jumatatu ya Wiki hii mtangazaji wa kituo cha Clouds FM Sophia Kessy kupitia kipindi chake mwanana cha Afrika Bambataa alifanya mahojiano na Mwanamuziki toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo toka kundi la Wenge BCBG, JB Mpiana Bin Adam Tshituka Papa Cherry.

1. vipi amefikia wapi kuhusu kutoa albam na werasoin

kuhusu kutoa nyimbo na werasoine ni kweli lakini kwa sasa tumeanza na sigle ya publicity na tutakapo maliza tutafanya kazi nzuri kwa sababu ni gharama sana kufanya kazi hii.

2. unaongeleaje kuhusu kumeguka kwa bendi yako hasa kwa watu kama akina alen mpela ambae inasemekana hata kwenye onyesho lako la hivi karibuni hakuwapo?

kuhusu kutoka kwa vijana ni kawaida ni sawa na baba mwenye watoto wanapo kuwa wakubwa huamua kutoka kujitafutia maisha yao , mimi binafsi nimefurahi kwa hilo kuona kuwa wanaweza kujitegemea sasa sina tatizo juu ya hilo nawaombea kwakuwa wakinufaika, pia ni sifa kwangu kwakuwa wametoka kwangu na hata kama hawata fanikiwa wakiona mambo yanaenda vibaya wakiomba kurudi nitawapokea ni wangu sitawatupa.

Sofia Kessy wa Clouds Fm, Afrikan Bambataa

3. muziki nu burudani kwanini mnakuwa na uaduni na mtu kama werason mpaka wapenzi wenu wanakuwa wanaumizana na hii imekuwa ikitokea mara kwa mara

ni ngumu kumtuma mashabiki kuwafanya wagombane akili tunayo itumia katika kazi ndio inayo wapelekea wao kutoelewana kila mtu anamuona mwenzie ni bora zaidi na kila msahabikianaamua kuvutia upande wake. ndio maana unaona kwa sasa kongo kuna chama kinaitwa MAISHA PARK, ambapo ukigundulika umegombana na mwezio basi wanakuiteni na kuwapatanisha lakini pia wanashauri kutogombana, ni baya kutukanana, na hii ndio inaleta umoja sasa katika muziki maisha park, ugomvi sikuzote unarudisha muziki nyuma.

4.unazungumziaje ujio wa wanamuziki chipukizi kama Fally Ipupa, Celeo scam, Ferre Gola ambao kwa kiasi kikubwawanaubadili muziki wa kongona kusemwa kuwa ndio kizazi kipya cha tano baada ya kizazi chanu cha nne.

kwanza ni vijana na wananfanya kazi vizuri, ninacho washauri mimi ni kuwa wawe na adabu, mungu atawasaidia lakini kuna jambo moja nataka kusema kuweka wazi kuwa zamani watu walituita wenge kizazi cha nne kwasababu hatukutoka katika bendi yoyote kongo tuliibuka tu tulikutana tukaunda kikundi chetu wenyewe tukiamini kila mmoja anaweza tulitoka nyumbani kwa kifupi, sio jibe katoka kwa zaiko, au wera katoka kwa tabu lay, sio blaiz bula katoka kwa papa wemba hapana sisis wote tulitoka nyumbani tukaunda kundi letu la wenge na ndio maana tulikubalika na wakatuita kizazi cha nne lakini kuhusu fally na ferre na tutu kaluji, na celeo scam,hawa ni kizazi cha nne kwasababu kuitwa kizazi cha tano sio kweli kwasababu wanamuziki hao wametoka kwangu na kwa kofi na kwa wera, na bendi walizotoka ni kizazi cha nne hivyo watu waelewe si kizazi cha tano bali ni cha nne na kizazi cha tano ni kizazi ambacho hakijajulikana kwenye bendi yoyote.

Pamoja na mambo mengine aliulizwa kuhusu chakula anachopendeleani mchicha, samaki, na wali maharage, pia aliulizwa timu anayoipendelea na kusema ni Brazil

JB Mpiana aliweka bayana kuwa anawatoto 7 wasichana wawili wavulana wa tano wa kwanza miaka 19 wa pili miaka 17 wa tatu miaka 15 wa nne miaka 14 wa tato miaka 12 wa sita miaka 10 na wasaba miaka 9

kuhusu kuja tanzania ni muda wowowte yupo tayari mara baada ya manager wake kumpa ushauri wa kufanya hivo.

Mji wa Bern ni rangi ya chungwa tupu!!

Mashabiki wa Holland wakiwa mitaani wakisherehekea ushindi dhidi ya Ufaransa, Mashabiki wa Holland ambao wanaongoza kwa staili yao ya ushangiliaji na mavazi ya rangi ya chungwa wamejaa na wanazidi kumiminika mjini Bern ambapo ndio kituo cha Timu yao, mji mzima umekuwa rangi ya Chungwa.

Ufaransa Mbendembende kwa Holland


Uholanzi 4 – 1 Ufaransa

MDutch Andre Ooijer (L) akiubeba mpira langoni mwa Ufaransa baada ya Dirk Kuyt kupachika bao la kwanza dakika ya nane ya mchezo katika mchezo wa kundi C.
Uholanzi jana walifanya maajabu kwa mara ya pili tena baada ya kuitandika bila huruma Ufaransa kwa 4-1 na kujihakikishia nafasi ya kucheza robo fainali huku wakiwafungisha Wafaransa virago katika michuano hiyo.

Dirk Kuyt ndiye aliyefungua karamu ya magoli kwa Waholanzi na baadaye kufuatiwa na Robin van Persie, Arjen Robben na Wesley Sneijder. huku goli pekee la Ufaransa lilifungwa na Thiery Henry. Kipondo hiki ni muendelezo wa kipondo kama hicho walichompa Italy jumatatu.

Mshabiki wa Ufaransa akiwa amelowa majonzi kwa kutoamini macho yake baada ya timu yake kula kichapo cha 4-1.

Ufaransa wanakutana na Italy jumanne ijayo ambapo wote wanawania kijinafasi lakini nafsi yao inategemeana na matokeo ya mchezo kati ya Romania na Uholanzi ambap Romania inashika nafasi ya pili katika kundi hilo, kwani Romania ikiishinda Holand itakuwa na nafasi hiyo hiyo ya pili. Wadatch wameweka historia kwa kuzichapa timu mbili ambazo zilicheza Fainali ya kombe la dunia 2006 kwa jumla ya mabao 7.

Italy yajitutumua kwa Sare

Italy 1 – 1 RomaniaMchezaji wa Romania Muttu shoto akipiga penati ambayo golikipa wa Itali aliicheza kwenye mchezo wao wa Jana.

Italy imeponea chupu chupu kupata kichapo jana baada ya kudumisha sare ya 1-1 na Romania, Sala za waitaliano zilisikika pale Romania walipopata penati na Golikipa wa Italy Gianluigi Buffon akaicheza.

Straika wa Fiorentina Adrian Mutu ndiye aliyefungua mlango kwa kuipachikia Romania goli la kwanza dakika ya 55. Lakini goli hilo lilidumu kwa dakika moja tu waitaliano wakasawazisha kupitia kwa Christian Panucci.
Matokeo ya Droo angalao yamewapunguzia machungu Italy ambao bado wanakidonda cha kichapo cha 3-0 walichochapwa na Holland ambao wanaonyesha makali kwenye kundi hilo la C.

Romania walipata penati dakika 5 kabla ya mchezo kumalizika baada ya Panucci kumchezea madhambi Daniel Niculae ambayo kwa kiwango kikubwa iliwanyong’onyeza Italy na washabiki wao na Romania walimchagua Mutu kupiga penati hiyo ambayo aliipiga kiufundi iende kwenye post lakini kipa Buffon wa Italy aliicheza na kusababisha mayowe toka kwa mashabiki wao ambao walikuwa wameshakata tamaa.

Kwa matokeo haya Italy inatakiwa ishinde mechi yake ijayo na Ufaransa ili waweze kujihakikishia kusonga mbele.

Waitaliano jana walilalamikia maamuzi ya refa wakidai aliwabana sana wao, Refa huyo Mnorwee hasa pale alipokataa goli la Italy kwa kudai mfungaji Luka Toni alikuwa ameotea.. Mpaka mwisho wa mchezo Italy 1 – 1 Romania.

Friday, June 13, 2008

Maneno ya mwisho ya “KUNGWI”

Kocha wa Stars Maxio Maximo akipiga saikolojia kwa vijana wake homa inayowapata watzania ni kama homa ya wakati ule tulipocheza na Senegal na kuibuka kidedea, naimani mchezo wa kesho tutashinda kama tutacheza kama timu, kwa kujiamini na kujali mafunzo yaliyochanganyika na vipaji binafsi vya wachezaji wetu. Kila la heri Stars

KUMRADHI: Haha habari ndio hiyo!!

Naomba radhi kwa kushinda kuweka habari toka jana usiku hii ni kutokana a sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wetu. lakini naomba mburudike na Video ya kwake AY inayoitwa Habari ndio hiyo!!

!

Vimwana wa Miss Dar City Centre

Pichani ni Washiriki wa shindano la Miss Dar City Center, ambo leo wamefanya kitu cha maana cha kuzuru gari lao ambalo wanashindania.Katika picha hii warembo hao wakiwa wamezunguka gari hilo. Shughuli ya kumsaka mrembo wa kitongoji hicho muhimu itafanyika Jumamosi Juni 14,2008 kwenye ukumbi wa Cine Club, jijini Dar es Salaam.

Thursday, June 12, 2008

haki miliki yawabana Ze Comedy

Kundi la ucheshi la Ze Comedy leo mchana limekilalamikia kituo cha Televisheni cha East Africa kwa kuwawekea pingamizi la kutumia staili za ucheshi walizokuwa wakitumia walipokuwa kituo hicho kama wataamua kuendelea kufanya shughuli hiyo iliyolipatia kundi hilo umaarufu mkubwa.

Kundi hilo limesema limekatazwa kutumia staili za kijotijoti, Masanja Mkandamizaji amekatazwa kutumia jina hilo na mtindo aliokuwa akiutumia, Wakuvanga amekatazwa kutumia staili ya kujiremba kama mwanamke na kutumia jina hilo wala kuigiza kama Lowassa, na waigizaji wengine wote wa kundi hilo wamepigwa top na COSOTA. Kwa kiasi kikubwa kilicholalamikiwa ni haki miliki ambapo East Africa Television wanadai kumiliki walivyovitaja.
Haya wadau mwalionaje hili?
Pata kipande cha Shoo yao hapa:-

video

Maelfu wajitokeza Kununua Tiketi za Stars na Kameruni

Na Mwananchi

MAELFU ya wapenzi wa soka jijini la Dar es Salaam wamejitokeza kununua tiketi za mechi baina ya Tanzania na Cameroon itakayofanyika kesho, huku polisi wakizuia maandamano yaliyopangwa kufanywa na chama cha siasa cha DP kupinga viingilio.

……………………..

Tiketi hizo zitauzwa kwa viingilio vya Sh 50,000 kwa V.I.P, Sh 40,000 kwa V.I.P B na Sh 20,000, Sh 10,000 na 7,000 kwa mzunguko

……………………………

na vituo vilivyopangwa kwa mauzo ya tiketi hizo ni mgahawa wa Steers, Uwanja wa Zamani wa Taifa, Zizou Fashion, hoteli ya Royal Prince na kituo cha mafuta cha Big Bon cha Kariakoo.

Pia kuna vituo vya Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa, vituo vya mafuta cha Kobil na Oil Com, hoteli ya Mbezi Beach Park na Wizara ya Miundo Mbinu.

Mwananchi ilishuhudia mistari mirefu ya wapenzi wa soka wakisubiri kununua tiketi hizo zilizokuwa zikitolewa kupitia kwenye magari kuanzia saa 4.00 asubuhi huku kukiwa na ulinzi wa askari polisi wenye silaha.

“Mimi nimeridhika na utaratibu wa uuzwaji wa tiketi kwani umezingatia muda, lakini pia pongezi zangu ni kwa TFF kwa kuongeza idadi ya vituo vya kuuzia tiketi kwani umepunguza adha ya kulundikana sehemu moja kwani mimi nimekuja muda huu na nimeshapata,” alisema shabiki aliyejitambulisha kwa jina la Yassin Adballah.

Mechi hiyo itakuwa ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika Afrika Kusini na pia itatumika kama michuano ya awali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, ambayo fainali zake zitafanyika Angola mwaka 2010.

Wakati mashabiki wakijazana vituoni kutaka tiketi hizo, kamishina msaidizi wa Polisi wa kanda maalumu ya Dar es salaam, Selemani Kova alisema kama DP, inayoongozwa na Mchungaji, Christopher Mtikila kama imekosa kiingilio, iangalie mpira kupitia kwenye luninga na si kufanya maandamano yasiyo rasmi.

Kova aliongeza kuwa endapo mwanachama au mtu yeyote atakaidi amri hiyo ya jeshi la polisi, hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Sebene la Koffi usipime!!

Koffi Olomide anasemwa kuwa anawajali sana mastage show wake na kuna kipindi aliwahi kukorofishana an JB Mpiana kwa kuwa alimchukulia mcheza shoo wake. na ukitaka kukosana naye basi gusa stage shoo wake huwa anasafiri nao mwenyewe kwa kawaida akiwa na shoo anatangulia yeye kwenda nchi husika na akitangulia basi huenda ndege moja na vimada wake.
Gonga chini hapa uone ni kwa nini huwapenda sana hawa wacheza shoo wake, Mopao Mokonzo Sakozy!! Kuna mtu anaitwa Abuu MWenda mpenzi mkubwa wa Koffi na Big Producer Maghambo salute kwenu!!

Felipe Scolari akabidhiwa Mikoba CHELSEA

Klabu ya Chelsea imethibitisha kumchukua kocha wa timu ya Taifa ya Portugal Mbrazir Luiz Felipe Scolari kama Manager na Kocha mkuu wa timu hiyo. Mbrazir huyu ndiye aliyeonekana kuweza kurithi mikoba ya Grant darajani Stamford.

Kwa sasa kocha Scolari yuko na timu ya Taifa ya Portugal kwenye michezo ya Euro 2008, na hakutarajiwa kuweka bayana mustakabali wake mpaka mwisho wa mashindano.
Chelsea walisema kwenye taarifa yao “Chelsea Football Club inayofuraha kuwajulisha kuwa Luiz Felipe Scolari ndiye atakuwa kocha mpya wa Klabu ya Chelsea mkatabu atakaoanza kuutumikia tangu July 1, 2008. ‘Felipe ana viwango vya hali ya juu. Ni mmoja wa makocha wa renki ya juu kabisa Duniani, akiwa na rekodi nzuri ya Vilabu na Timu mbali mbali za Taifa alizofundisha. atakuja kuungana na kikosi cha wachezaji bora na wenye moyo wa kucheza mpira wenye viwango nafikiri tutakuwa na Combination nzuri.
Ni muda mzuri wa kumtangaza kocha Scolari kwani kwa sasa timu yake ya Portugal inafanya vizuri tuombe Mungu huko mbeleni na hata wachukue Kikombe, Inshallah.

Vilabu vyapigana vikumbo kwa Villa

Baada ya kuonyesha maajabu kwenye mchezo wa juzi mchezaji wa Spain David Villa ameanza kusakamwa na madalali wa wachezaji wakimtamanisha kwa donge nono ili afikirie kusajili na timu zinazowakilishwa na Maajenti hao. Habari zinapasha kuwa maajenti wa Vilabu vikubwa vywa Uingereza ndio wanaongoza kwa kutaka kufanya mazungumzo na Villa.

“Kitakuwa ni kipindi kigumu katika maisha yake kuamua anakazi kubwa lakini ni wakati mzuri kwake kwani thamani yake kwenye soko imeonekana na kila mtu yuko tayari kutoa kitika awe naye” alisema Vah Geuella ambaye ni agent wa wachezaji toka Spain.

Nyota huyo anayechezea Valencia aling’aa kwenye mchezo wa Spain na Russia jumanne ya juzi kwa kuipachikia timu yake magoli 3 kati ya manne ambayo Spain ilishinda.

Vilabu ambavyo vinamnyemelea ni pamoja na Chelsea na Arsenal, pamoja na bingwa wa La Liga Real Madrid na klabu kubwa ya Catalan Barcelona, ni miongoni mwa vilabu vikubwa ambavyo vinaongoza kuisumbua kambi ya Spain na inatazamaiwa huenda Villa akajiunga na mmoja ya vilabu hivi.

Turkey yawafungisha Vilago wenyeji Switzerland

Switzerland 1 – 2 TurkeyWachezaji wa Turkey wakishangilia ushindi baada ya kuibwaga Switzerland 2-1

Mchezaji wa Turkey Arda Turan aliwaliza Switzerland katika dakika za majeruhi na kuipatia timu yake ushindi wa mabao 2-1 na kuwafanya wenyeji hao Switzerland kuyaaga mashindano hayo.

Hakan Yakin ndiye aliyefungulia mashambulizi na kupachika bao la kwanza kwa timu yake ya Switzerland kwa bao dakika ya 32 ya mchezo. Switzerland ambao kwa mchezo wa jana walijitahidi washinde lakini bahati haikuwa yao, Mchezaji wa akiba Semih Senturk alisawazisha bao kwa timu ya Turkey na kufanya droo ya moja moja.

Mchezo uliendelea hivyo hadi dakika za mwishoni ambapo umati ulishatarajia mchezo utamalizika hivyo kufumba na kufumbua Arda mchezaji wa Turkey akapachika kimiani goli lapili katika dakika za majeruhi kabisa.

Shuti lake la kulia lilipita ngome ya Swiss na kwenda moja kwa moja kimiani na kuzima nderemo za waswiss ambao walikuwa wakiishangilia timu yao kwa nguvu zote.

Swiss walikuwa na nafasi ya kufunga goli lakini kipa wa Turkey Volkan Demirel kwa kiasi kikubwa aliwakatisha tamaa kwa kuokoa mpira uliopigwa na Yakin hapa na hapa ambao mashabiki walishainuka wakidhani ni goli.

Turkey watakutana na Czech Republic kwenye game ya mwisho ya Kundi A hapo jumapili ilihali n Swiss watakutana na timu isiyofungika Portugal.

Portugal haooo Robo Fainali

Czech Republic 1 – 3 Portugal

Baada ya usshindi wa magoli 3-1 dhidi ya Jamhuri ya Czech hapo jana, na baadaye Switzerland kupoteza mchezo Portugal wamefanikiwa kuingia hatua ya Robo Fainali ya EURO 2008. kimsingi wan kila sababu ya kusherehea hatua hii.

“Sisi ni kati ya Nchi nane bora kisoka katika Ulaya” alisema kocha wa Portogal Luiz Felipe Scolari said. “hatujaridhika tunahitaji zaidi ya hapo, na ninamatumaini makubwa ya kufika huko juu zaidi.”

Kiwango cha Portugal kwenye michuano hii kiko juu na kama wataendelea kucheza kwa kiwango hiki basi lolote laweza kutokea.

Portugal walipata goli la kwanza dakika ya nane ya Mchezo lililofungwa na mchezaji Deco lakini goli hilo lilidumu kwa takriban dakika tisa tu kwani Czech walisawazisha dakika ya 17 kupitia kwa Libor Sionko (17). Mpaka mapumziko magoli yalikuwa droo ya 1-1.

Kipindui cha pili kilianza kwa speed kali huku Portugal wakiongeza mashambulizi langoni mwa Czech huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale na dakika ya 63 huku akicheza kwa kuonana vizuri na Deco Cristiano Ronaldo akafanya alichotarajiwa kufanya kupachika bao la pili kwa timu ya Portugal baada ya kupata pasi toka kwa Deco. Czech ambao walikuwa na kibarua kigumu cha kumlinda Ronaldo jana iliwabidi wafanye kazi ya ziada kwani kijana hakabiki!. Dakika za majeruhi dakika ya 90 mchezaji kipenzi changu Ricardo Quaresma akaipatia timu yake goli la tatu.

Mpaka kipyenga cha mwisho, Portugal 3- 1 Czech.

Wednesday, June 11, 2008

Jalamba

Wachezaji wa Italy toka shoto Daniele De Rossi, walinzi Andrea Barzagli, Marco Materazzi na Fabio Grosso, striker Luca Toni na forward Marco Borriello wakipiga jalamba wakati wa mazoezi ya timu yao kwa ajili ya michuano ya Euro 2008 huko Maria Enzersdorf karibu na jiji la Vienna leo June 11, 2008. Italy watacheza na Romania katika mchezo wao wa kundi C tarehe 13 keshokutwa.

Utambulisho ndoa ya Dotnata

Aliyekuwa muigizaji maarufu Husna Shabani ‘Dotnata’ na mumewe Mohamedi Poshi wakivishana pete mara baada ya kutambulishana katika sherehe iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Msasani Beach ambako kulikuwa na hafla ya ya kuitambulisha ndoa yao kwa ndugu, jamaa na marafiki iliyofanyika usiku wa kuamkia leo.
Mmoja wa Ma-Mc kati ya Ma-Mc 10 waliokuwepo ukumbini humo msanii wa fani ya maigizo Muhsin Awadh ‘Dk Cheni’ akimwaga sera zake kwa maharusi Dotnata na mumewe Mohamedi Poshi.
Habari na Picha na Global Publishers

Czech na Portugal Usipime!!

Mashabiki wa Czech na Portugal wakishangilia kabla ya mechi kati ya timu zao leo, Mpambano huu unatazamiwa kuwa mkali kwani kila timu ina kiwango kizuri cha mchezo.

Teddy wa Total Knockout!!

Anaitwa Teddy Kalonga, Ni Model na ametumika sana kwenye matangazo ya TV hasa ta TBL na mengineyo, kwa sasa Teddy yuko Ughaibuni katika kujiendeleza. Teddy ni Blogger chini ya Total Knockout amejikita kwenye Burudani na Mitindo, kama una habari inayohusu burudani, vipaji, fashion au urembo, kama wataka kuwa featured na story yako binafsi basi wasiliana naye. kwa Kugonga hapa!

Under Water Wedding

Siku ya Kuoa au kuolewa ni siku pekee ambayo mtu anatakiwa asiisahau kwani kwa wengi wanaoamini siku hii huja mara moja ila kama tuu kutakuwa na ndoa ya mitala. Inaitwa Under water Wedding, ni maarufu kwa kipande hii ya Asia (Malaysia na Thailand) kwa Malaysia Chama cha Waogeleaji ndio mtaji wao mkubwa wakishirikiani na Hotel kubwa ambapo utapenda Harusi yako ifanyike. Package ya harusi hii ni Malaysian Ringit 160 (55,000 Tsh) kwa kila kichwa na idadi ya chini ni watu 60. Hii inakuwa ni pamoja na Vinywaji na Vilaji kwa waalikwa wako, Keki kwa ajili ya maharusi, Champagne 5, Mitungi ya Gas kwa ajili ya maharusi na yeyote atakaye hitaji kuzamia, Albamu ya Picha pamoja na DVD moja ya kumbukumbu ya tukio zima, Fataki 10Kg, pamoja na gharama za kuiandikisha ndoa na Cheti cha Ndoa kwa anayetaka anakaribishwa kuja Malaysia hakuhitaji VISA kwa Mtanzania.

Kelly Rowland naye kutua Bongo

IJUMAA SHOWBIZ!

Kwa mara nyingine tena Wabongo wengi watakuwa wakisubiri kwa hamu kubwa kumwona supastaa mwingine kutoka Marekani. Sasa ni zamu ya Kelly Rowland, ambaye atatia maguu nchini mapema mwezi huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kituo cha Televisheni cha MTV, Kelly yupo katika ziara ndefu akizunguka sehemu mbalimbali duniani kwa ajili ya kutimiza majukumu yake kama Balozi wa mfuko wa MTV Staying Alive Foundation.

Mwanamuziki huyo ambaye ni mtunzi na mkali wa kuimba staili ya R&B ni miongoni mwa warembo watatu waliokuwa wakiunda kundi maarufu la Destiny’S Child, kabla hawajaamua kila mmoja kutoka kivyake.

Khadija Kopa kupamba Kimasomaso keshokutwa

Pichani Kushoto (Khadija Mwanamboka na Mama Asia Idarous wa FABAK Fashions) ambao ni moja ya viongozi wa shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Mitindo house wakizunguza na waandishi wa habari hivi karibuni jijini Dar kuhusu onesho lao la mavazi watakaloliita KIMASO MASO litakalofanyika ukumbi wa Waterfront juni 13/08,Kuanzia saa Moja Usiku,Kwa Kiingilio cha 12000/= Tu.
Khadija alisema kuwa katika onyesho hilo litajumuisha Wabunifu 10 nao ni ROSE VALENTINE, ASIA IDAROUS, ANGELO MLAKI, MUSTAFA HASSANALI, JAMILA SWAI, FANCISCA SHIRIMA, MONICA LIHAWA , HILDA BANDIO, KHADIJA MWANAMBOKA na Wataonyesha Mavazi ya
KITCHEN PARTY/ BAG PARTY ,

SENDOFF

HARUSI

Aidha kwa upande wa burudani Khadija alisema kuwa burudani itatolewa na Malkia wa Mipasho KHADIJA KOPA, SABAHA MUCHACHO na Kikundi cha Ngoma ya BAIKOKO kutoka Tanga.

Alisema onyesho la KIMASOMASO limedhaminiwa na Sabuni ya OMO, Kampuni ya simu za mkononi TIGO, Kinywaji cha REDD’S, SHEAR ILLUSIONS, GOLDEN TOUCH SALOON, BIG TV, VISUAL LAB: NEXT LEVEL, LEOPARD MODELLING AGENCY, VAYLE SPRINGS NA RAQEY.COM
Khadija alimaliza kusema kwa kuvitaja vituo vya tiketi kuwa ni: MANYWELE BEAUTY COSMETICS- KINONDONI, CHOCOLATE PRINCESS – MASAKI, SUMMER MIX FASHION – NAMANGA SHEAR ILLUSIONS – MILLENNIUM TOWERS.

Temptation kwa Jicho la ZEZE

Mnaweza kuwa pamoja lakini kila mtu ana jicho lake kila mtu anataka kuona chake, Camera ya Zeze kwenye Usiku TEMPTATION NA ALLY REMTULLA ilipata ya kupata kwani waliohudhuria pia walikuwa burudani kwa kupeneza kwa mavazi, ungana na Zeze kwenye 8020.














MAMBO YA TEMPTATION YA ALLY REMTULLA

Eto’o, Song, Njitap watua Dar

*Eto’o agoma kuzungumza na waandishi wa habari

*MO ahamasisha ushangiliaji

Na Majira
Timu ya Kameruni jana iliwasili nchini ikiwa na nyota wake wote tayari kuikabili timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ katika mchezo wa michuano ya kutafuta tiketi ya kufuzu fainali za Kombe Dunia zitakazofanyika Afrika Kusini mwaka 2010 na Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Angola uliopangwa kufanyika Jumamosi kwenye Uwanja Mpya wa Taifa, Dar es Salaam.

Kameruni iliwasili jana alasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimul Nyerere, Dar es Salaam ikiwa na kikosi cha wachezaji 20 wakiwemo Samuel Eto’o anayecheza Bacelona ya Hispania, Geremi Njitap na nahodha Rigobert Song.

Timu hiyo baada ya kutoka nje ya Uwanja wa Ndege ilikwenda moja kwa moja kwenye gari waliloandaliawa huku Eto’o na Kocha Mkuu wa kikosi hicho, Pfister Otto wakigoma kuzungumza na waandishi wa habari.
Song beki wa kati mwenye nguvu, alisema wamejiandaa vizuri kuikabili Stars ingawa hawana taarifa kuhusu uwezo wa kikosi hicho na kuongeza kuwa anatarajiwa pambano hilo litakuwa gumu.

Naye Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Marcio Maximo amekifananisha kikosi hicho na gari ya kubeba abiria (daladala) ambayo haiogopi kugongana na gari ya kifahari.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Maximo alisema timu yake itakuwa daladala itakapovaana na Kameruni katika mchezo wa kimataifa wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini mwaka 2010 na Mataifa ya Afrika yaliyopangwa kufanyika Angola.

Maximo alisema Stars inateremka uwanjani huku ikijua kuwa inavaana na kigogo cha mchezo huo Afrika ambacho kinaundwa na nyota wanaotamba na klabu kubwa duniani hatua ambayo anafananisha wachezaji wake (daladala) na gari la kifahari.
Alisema hata hivyo amewaandaa kikamilifu wachezaji wake kucheza kufa au kupona katika mchezo huo na amewaambia wasiogope ukubwa wa majina ya nyota wa Kameruni na wacheze mpira.

Maximo alisema katika mchezo huo anatarajia kuwatumia wachezaji wake wawili wa kiungo waliokuwa majeruhi, Mrisho Ngassa na Abdi Kassim ambao wamepona. Wachezaji hao walikosa michezo miwili ya Stars ilipomenyana na Mauritius na Cape Verde.

Maximo alisema ana imani wachezaji hao watakuwa msaada mkubwa katika mchezo huo na kuongeza kutokana na uwezo wao uwanjani ambapo Kassim anasifika kwa mashuti makali wakati Ngassa ni mahiri kwa chenga za maudhi dhidi ya mabeki wa wapinzani wao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mohamed Enterprises, Mohamed Dewji amesema Kameruni inafungika licha ya kuundwa na wachezaji nyota ambapo amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani kuishangilia Stars katika mchezo huo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Dewji alisema Watanzania wanatakiwa kuipa nguvu Stars katika mchezo huo bila kujali majina ya wachezaji wa Kameruni ambao wengi wao ni maarufu.
Alisema hakuna sababu ya mashabiki wa soka kwenda uwanjani vichwa chini wakiihofia timu hiyo licha ya Stars kufanya vibaya katika michezo miwili ya awali kwa kutoka sare 1-1 na Mauritius kabla ya kufungwa bao 1-0 Cape Verde.

Alisema Stars ilipocheza na Senegal na Burkinafaso ikiwa ugenini wachezaji wa kikosi hicho walicheza kwa nguvu dakika zote za mchezo bila kuangalia ukubwa wa majina ya nyota wao wanaocheza Ulaya.
Mwaka jana Dewji alitumia zaidi ya sh. milioni 100 katika mkataba wake na Stars ambazo zilitumika kwa ajili ya shughuli za uendeshaji wa timu hiyo ikiwemo kambi na mambo mengine.

Kameruni inaongoza kundi A ikiwa na pointi 6 baada ya kushinda michezo miwili dhidi ya Cape Verde mabao 2-0 kabla ya kuibanjua Mauritius 3-0. Inafuatiwa na Cape Verde yenye pointi 3,Tanzania inashika nafasi ya tatu na Mauritius inakamata mkia.

“Ukiwa Makka basi ishi kama watu wa Makka…”

Mchezaji wa Los Angeles Galaxy David Beckham akiwa na mwanaye Brooklyn akipozi kabla ya mchezo wa Ligi ya kikapu kati ya Boston Celtics na Los Angeles Lakers jana jumanne, Bekham amekuwa gumzo tangia aingie USA na kila anapokwenda watu hujitokeza ku chill naye.

Faida ya Magoli kwa KAKA

Pichani ni mchezaji wa Brazili Ricardo Izecson dos Santos Leite, au Kaka, anaonekana akiwa na mkewe Caroline na mtoto wao wa kiume Luca, huko Sao Paulo, jana jumanne, June 10, 2008. Caroline Celico Leite alijifungua mtoto huyo jana saa 1:05 a.m, Taarifa zinasema mtoto ana kilo 3.6 na anaendelea uzuri.

Spain yaisambaratisha Russia 4 – 1

Spain 4 – 1 Russia
David Villa ndiye aliyekuwa Stearing wa mchezo wa jana baada ya kufanya mauaji kwenye mashindano ya mwaka huu ya Euro 2008 kwa kupachika magoli 3 kati ya manne wakati wa mchezo kati ya Spain dhidi ya Rusia ambao ulimalizika kwa 4-1.

“Magoli matatu kwenye mechi moja tena ya ufunguzi ni mwanzo mzuri kwa kweli aliesema Vila mara baada ya mchezo wa jana. Hii ni mara ya kwanza kwenye mashindano haya kufungwa mabao matatu na mtu mmoja mara moja tangu mwaka 2000ambapo mchezaji Patric Kluivert wa Netherland alipoifungia timu yake.Tumeanza vizuri ingawaje kuna mechi zinakuja lakini mwanzo utawaogopesha hata wapinzania wetu aliongeza Villa. Spain itakuja kukutana na Greece na Sweden kwenye mechi za kundi hilo la D. ambapo inategemea kukutana na kaupingamizi toka kwa Sweden ambao walionyesha mchezo mzuri jana.

Ni katika kundi hili rafiki yangu Tanzania Dreams anasema mshindi atatoka, sijui naona mechi zinatabiri kwa bingwa Greece kuonja kichapo. Goli moja la Spain lilifungwa na Mchezaji wa ArsenalFrancesc Fàbregas Soler au Cesc Fabregas ambao kwa pamoja walitengeneza karamu ya magoli.
Bao pekee la Russia lilifungwa na Roman Pavlyuchenko.

Sweden yaikomalia Greece 2-0

Strika wa Sweden Zlatan Ibrahimovic ndiye aliyeakuwa wa kwanza kufungua safu ya ufungaji kwa timu yake ya Sweden ilipowalaza mabingwa Greece 2-0 kwenye mchezo wa kundi D wa michuano ya EORO 2008 hapo jana jijini Salzburg.

<>Ibrahimovic pichani, ambaye hajafunga goli kwa timu yake ya Taifa tangu October 2005 aliifungia timu yake bao maridadi mnamo dakika ya 67 ya mchezo.
<>

Timu ya Greece ilikuwa kama imechanganyikiwa ngome yao kutokana na mchakamchaka wa jana ambapo Sweden walionyesha mchezo mzuri na kwa kiasi fulani kuumudu mchezo.
Dakika tano baada ya goli la kwanza Sweden walipata goli la Pili kutoka kwake Petter Hansson baada ya mabeki wa Greece kujichanganya. Mchezo huo wa kwanza ulikuwa muhimu kwa timu zote kwani unajiweka kwenye nafasi nzuri kipindi chwa mwanzo, Kwa mchezo walioonyesha Greece jana wanatakiwa kufanya kazi ya ziada ili kuendelea kuwepo kwani kazi bado Pevu mbeleni.

Tuesday, June 10, 2008

Kilichowaponza Taifa Stars

-Exclusive toka kwa Haki Ngowi-

Picha juu ni vimwana ambao ni washangiliaji wa timu ya Cape Verde wakifanya vitu vyao juzi kwenye mpambano wao na Taifa Stars nakuwalamba 1-0.kufungwa kwa Taifa Stars kumesababisha Baadhi ya Mashabiki kukata tamaa na hata kupoteza matumaini ya mchezo ujao dhidi ya Cameroon.
Stars itapambana na Cameroon katika mchezo wa tatu wa michuano hiyo utakaofanyika Jumamosi kwenye Uwanja Mkuu waTanzania jijini Dar es Salaam.Picha hizi kutoka Cape Verde kwa msaada mkubwa wa Mdau Saleh Ally. (Kaka Robert Mwafrika wa Azam ananiambia Taifa Stars walikuwa wakikodolea macho vimwana hahahahaa)

Wanyange wa Miss Tanzania UK 2008

Picha mwanana za washiriki mbalimbali wa shindano la Miss Tanzania Uk 2008 linalotarajiwa kufanyika jmosi ya Tarehe 14-06-2008 ndani ya Silver Spoon New Light Banqueting Suize ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini Uingereza Bi Mwanaidi Maajar.

KAseja: Nimesign Yanga lakini nina Mkataba na Simba!!

Kaseja akianguka saini mbele ya Madega.
SIKU moja baada ya kipa wa Simba, Juma Kaseja kukiri amesaini mkataba wa kuichezea Yanga kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya kimataifa msimu ujao, amesema bado ana mkataba na klabu yake.

Kauli hiyo ni mara ya kwanza kwa kipa huyo nambari moja kuitoa hadharani baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja kuwatumikia mabingwa hao wa mpira wa miguu Tanzania Bara.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kaseja alisema amesaini mkataba na uongozi wa klabu ya Yanga huku akijua mkataba wake na Simba unamalizika mwakani.

Kaseja alisema kabla ya kusaini mkataba mpya na uongozi wa Yanga aliwaonesha kopi ya mkataba wake wa Simba lakini uongozi wa klabu hiyo ya Jangwani ulimtaka asaini na wao wangefikia muafaka na wenzao wa Simba.


Ufaransa yashindwa kutamba

Timu ya Taifa ya Ufaransa imeshindwa kufurukuta mbele ya Romania kwa kulazimishwa sare ya 0-0 kwenye mchezo wa Euro 2008 kundi la C, Kundi hili ambalo ni moja kati ya makundi magumu kwani Ufaransa ina kibarua kigumu itakutana na Italy na Netherlands (waliomchapa Muitaliano 3-0) Mchezo ulikuwa mzuri kila timu ikionyesha mchezo mzuri lakini nafasi za umaliziaji za Ufaransa zimeonyesha kupwaya huku wakicheza bila Thiery Henry na Captain wao Patric Viera. Kipindi cha kwanza Romania walisimamamia kulinda lango lao zaidi huku France wakitoa mashambulizi ya hapa na pale ila umaliziaji butu. Nicolas Anelka ambaye jana alicheza nafasi ya Henry alikosa magoli mawili ya wazi dakika ya 9 na dakika ya 17 kwa kupaisha nje ya goli mipira yote.
Hadi mwisho wa mchezo Ufaransa 0 – 0 Romania.

Italy Mbendembende kwa Netherlands

Netherlands 3-0 ItalyUshindi wa magoli 3-0 walioupata wa Dtch dhidi ya waitaliano umeinua nderemo si tu kwa kushinda mechi hiyo bali kusherehekea ushindi wa kwanza dhidi ya Italy tangu mwaka 1978, Pichani mchezaji wa Netherlands Ruud van Nistelrooy (R) akifunga goli la kwanza wakati wa Mchezo wa kundi C wa Euro 2008 didi ya Italy. Netherlands waliwabugiza mabingwa wa Kombe la Dunia mabao 3-0. Katika mchezo ulikuwa mkali na wa kusisimua, goli la pili la Netherlands lilifungwa na Wesley Sneijder dakika ya 31 na kufanya Netherlands waende mapumziko kwa kuongoza 2-0. Kipindi cha pili kilianza kwa piga nikupige huku Italy wakuionyesha matumaini kidogo lakini ushambuliaji na Ngome ya Netherlands vilikatisha tamaa waitaliano na dakika kumi kabla ya mchezo kumalizika Giovanni Van Bronckhorst akaipatia timu yake bao la tatu na kuhitimisha karamu hiyo ya magoli, Rafiki yangu Tanzania Dreams wa India alitabiria kuwa hawa jamaa wamo katika watu wanaweza kuondoka na kikombe mwaka huu na dalili zinaonekana.

Mzee anacheza leo!!


Sylvie van der Sar, Mke wa golikipa wa Dutch Edwin van der Sar, akisubiri kuanza kwa mchezo wa Kundi C wa mashindano ya Euro 2008 kati ya Netherlands vs. Italy jana June 9, 2008 katika uwanja wa stade de Suisse huko Bern.

Monday, June 9, 2008

YANGA yamsajili Kaseka kwa USD 30,000

*Asajiliwa kwa makeke kumbadili Ivo, atamba kazi itafanyika
*Friend’s of Simba wachanga ‘vijisenti’ kumkomboa,waning’inia
*Asaini mkataba unaoeleza atakuwa kipa wa kwanza Yanga

Na Majira

KIPA mahiri nchini Juma Kaseja wa Simba ya jijini Dar es Salaam, jana alisaini fomu za mkataba kwa ajili ya kuichezea Yanga pia ya jijini katika michuano ya kimataifa mwakani, pamoja na Ligi Kuu Tanzania Bara.

Habari zilizopatikana mapema jana zilieleza kuwa kipa huyo alisaini fomu hizo mchana, baada ya mazungumzo yaliyochukua karibu saa tatu, ambayo ni mwendelezo wa mazungumzo ya kusaini fomu hizo yaliyoanza Ijumaa jioni.

“Tumemalizana naye ni fedha ambayo kila mwenye akili timamu hawezi kuiacha, hata kama ungekuwa wewe, huwezi kuacha kusajili, sasa ni Kaseja wa Yanga si Simba tena.

“Tunasajili kwa akili, hatukurupuki, tunajua tunachokifanya, Yanga itatisha, kijana amefika mahali alipokuwa akipataka,” kilieleza chanzo chetu ndani ya Yanga na kudokeza kuwa kwa jana tu kipa huyo alikabidhiwa dola 30,000.

Chanzo hicho kilieleza kuwa awali Kaseja ilikuwa asajiliwe leo, lakini kutokana na habari hizo kuvuja kwenye gazeti hili jana, pamoja na gazeti dada la Spoti Starehe, suala hili lilifanyika jana katika moja ya ofisi za mdau nyeti ndani ya Yanga.

Alisema licha ya juzi kutokuwepo fomu za usajili za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), lakini pia suala la mkataba wa kipa huyo na Simba lilikuwa likisumbua, ambapo mkataba huo unaonesha unamalizika mwakani.

Hata hivyo mkataba huo wa Kaseja unaeleza kuwa kila mwaka kutakuwa na mazungumzo kuhusiana na usajili na kama wakishindwa kuafikiana, yupo huru kutafuta timu nyingine, hivyo kama Simba watahitaji watalazimika kuilipa Yanga kiasi alichopewa kipa huyo pamoja na ahadi nyingine nyingi, ambazo utekelezaji wake tayari umeanza.

Gazeti la majira lilimpata kipa huyo ambaye alikiri kusaini fomu za Yanga na kusema ana imani kazi kubwa itafanyika kwenye ligi na michuano ya kimataifa.
“Elimu yangu ni mpira, maisha yangu ni mpira, nimeamua kusaini Yanga na nina imani Mungu ataniongoza nifanye vizuri, wamenipa kiasi kizuri sana, nami nitawapa raha uwanjani.

“Mimi si wa kwanza kucheza Simba kisha nikaenda Yanga, au kucheza Yanga nikahamia Simba, naomba mashabiki wa soka waelewe hilo,” alisema Kaseja.
Alikiri kusaini mkataba wa dola 30,000 na kwamba ni wa mwaka mmoja, ambapo moja ya vipengele vilivyopo ni kuwa yeye ndiye atakuwa kipa wa kwanza wa timu hiyo, hali itakayomfanya kipa wa sasa Ivo Mapunda kukaa benchi, au kutafuta timu nyingine.

Kaseja alisema kabla ya kufikia uamuzi huo aliwasiliana na baadhi ya viongozi wa Simba na kuwajulisha kuhusiana na dau la Yanga, ambao walimjulisha hawana uwezo kulifikia na kwamba yupo huru kuondoka.
“Niliwaeleza kiasi Yanga walichoniahidi wakanambia hawawezi kunipa, pia wakanipa baraka kuwa hela haikataliwi, nikasaini Yanga mkataba wa mwaka mmoja, ambao utahusu ligi ya 2008/2009,” alitamba kipa huyo.

Awali jana asubuhi, mmoja kati ya wanazi wa Simba wanaounda kundi la vibopa wa timu hiyo lijulikanalo kama Friend’s of Simba alipiga simu kwenye ofisi za gazeti hili akielezea kuhusiana na habari zilizoandikwa kwamba Yanga imemficha Kaseja.
“Si kweli Yanga haijamficha, ila mnataka kumsaidia Kaseja apewe dau kubwa Simba, hilo tunalijua,” alilalamika mdau huyo ambaye jina tunamhifadhi.

Hata hivyo alipoelezwa kwa undani kuhusiana na habari hizo, alionekana kushangaa na kuahidi angepiga mchana jana, ili asaidiwe kuelezwa alipo kipa huyo, kwani kulingana na maelezo aliyopewa na gazeti hili aliamini kweli Kaseja anaenda Yanga.

Kigogo huyo alipiga simu baadaye jioni jana na kusema tayari Friend’s of Simba walipata uhakika wa taarifa hizo na walichanga kiasi cha sh. milioni 20 ili wampe Kaseja, lakini alipoelezwa fedha aliyopewa ni nyingi zaidi aling’aka: “Ha. Huyu mtoto sisi tunamsaidia sana, lakini anatusaliti ngoja aende (anasonya), sisi hela hiyo hatuwezi kumpa.

“Lakini nasi tutalipa kisasi, hatuwezi kukubali kufa kikondoo, mwambie kila la kheri, kwanza hata Taifa Stars haitwi,” alilalama mdau huyo kwa kauli ya mfa maji, ambaye haishi kutapatapa.
Katibu Mwenezi wa Simba, Said Rubeya alipoulizwa jana kuhusiana na taarifa hizo alisema anachojua Kaseja ni kipa halali wa Simba.

“Habari hizi zimeandikwa katika gazeti lenu, hivyo mwandishi aliyeandika anajua zaidi, si mimi, lakini ninachojua fomu za usajili bado hazijatoka, Kaseja ni wa Simba,” alisema Rubeya.
Naye Katibu Mwenezi wa Yanga, Francis Lucas alipoulizwa alidai habari zilizoandikwa hazina ukweli na zina nia ya kumpigia debe Kaseja.

“Hatujazungumza naye, wala hakuna nia ya kumsaini Kaseja, haya mambo wala hatuyatambui,” alidai Lucas.

Angeline Jolie na Jack Black

Angeline Jolie akiwa na Jack Black walipokutana kwenye tamasha la filamu la Canes, Inasemwa Angeline amejifungua mapacha na Mashuirika makubwa ya Habari yametangaza dau kubwa kwa ajili ya picha ya kwanza ya Watoto/Mtoto wa Jolie. Kazi kwenye mapapa na mamamarazi.

Kwa akina Dada tu

Anaitwa Kim Kardashian, Mwanadada huyu huwaacha “Wakware” mate yakiwatoka kila apitapo kwa shepu yake hutoa Tips za urembo kwa akina dada kwenye Blog yake, picha hii ilipigwa wakati yeye pamoja na wifi yake wakifanya Shoping ya Furniture. Gonga hapa utapata vitu vyake

Chelsea yairuhusu AC Milan kufanya mazungumzo na Drogba

Klabu ya Chelsea imeipa ruksa klabu ya AC Milan kuongea na Drogba kuhusu nafasi ya mchezaji huyo kujiunga na AC Milan ila wamesema hawako tayari kumuachia alisema Makamu wa Rais wa timu ya AC Milan.
Chelsea wameturuhusu kufanya mazunguzmo na Drogba na tunatarajia mazungumzo yatafikia mafanikio mazuri alisema Adriano Galliani alipokuwa akiongea na gazeti la michezo la La Gazzetta dello Sport. Kwa sasa wasiwasi wetu uko kwa Shevchenko. Chelsea wanasema huyu hauzwi hii itakuwa imetunyima combination nzuri ambayo tunataka kuifanya aliongeza.

Galliani alisema kuwa Timu yake ambayo ni mabingwa wa Ulaya mara 7 wameanza kufanya mazungumzo na nyota mwingine toka klabu ya Barcelona Samuel Eto’o. Alisema Mcameruni huyo alikuwa anawaniwa na klabu nyingine ila wamempatia ofa yao kupitia kwa ajenti wake wanatumai majibu yatakuwa mazuri, vile vile imefahamika kubwa klabu hiyo pia ilifanya mazungumzo ya agenti wa Adebayo ingawa habari zinasema Arsenal hawako tayari kumuuza mchezaji huyo. Gillian alisema hawa wawili ni mapema kusema chochote ila maongezi yakifanyika tutatoa taarifa.

Croatia 1 – 0 Austria,

Mchezaji wa Croatia Luka Modric, kulia akikimbia kushangilia baada ya kufunga kwa mkwaju wa penati huku golikipa wa Austria Juergen Macho, akibaki hana la kufanya katika mchezo wao wa kundi B jana.

Mchezo mwingine wa kundi B ulikuwa kati ya Croatia na Austria, Mchezo ulianza kwa kasi kwa Croatia kumiliki kipindi cha kwanza na hatimaye kujipatia goli ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo.
Kipindi cha pili kilikuwa ni azamu ya Austria walifanikiwa kwa kiasi fulani kuumiliki mchezo lakini jitihada za milki yao hazikuzaa matunda.

Luka Modric aliifungia Croatia kwa njia ya Penati katika dakika ya nne tu ya mchezo.
“Goli la mwanzoni mwa mchezo limetusaidia sana alisema kocha wa Croatia, lilitufanya kuwa na uhakika ama wa kuongeza goli au kulinda hayo matokeo ya moja bila, Tulimiliki kipindi cha kwanza lakini kipindi cha pili kiligeuka, tuliwapa nafasi nyingi za free kick ila Mungu yuko pamoja na jitihada zetu, alimalizia kusema kocha huyo. Mpaka kipyenga cha mwisho magoli ni moja kwa Bila.

Germany 2-0 Poland

Magoli mawili yaliyofungwa na Lukas Podolski ameipa Ujerumani nafuu na ahueni kubwa kwa kujiweka kanafasi kazuri kwenye mhcezo wao wa kwanza wa kundi B hapo jana. Mshambuliaji huyo ambaye ni mzaliwa wa Poland alipata wakati mgumu kwani ilibidi atetee Taifa lake kwa kuimiza nchi alikozaliwa lakini alifanya kama Kumkoma nyanyi vile. Poland walionyesha uhai kipindi cha pili kwa mashambulizi mazuri lakini ilikuwa kama mbwa aliyekosa meno!! na kuachia matokeo kubaki mbili bola.
Pichani Lukas Podolski (L) akipachika mpira kimiani wakati wa mashindano ya Euro 2008 kundi B dhidi ya Poland jana June 8, 2008 huko Woerthersee stadium, Klagenfurt, Austria. German walishinda 2-0.

Sunday, June 8, 2008

Matokeo ya Michezo mbali mbali ya awali ya kuwania Kombe la Dunia inayoendelea Ulimwenguni, Gonga sehemu ya Magoli kupata Data zaidi ikiwa ni pamoja na wafungaji

WC 2010 qual. – Asia (Group 1)
02:06 June 8
FT Iraq 1 – 0 Australia
WC 2010 qual. – Asia (Group 2)
03:06 June 8
FT Oman 1 – 1 Japan
FT Bahrain 1 – 1 Thailand
WC 2010 qual. – Asia (Group 3)
03:06 June 8
FT Jordan 0 – 1 Korea Republic
WC 2010 qual. – Asia (Group 4)
02:06 June 8
FT Uzbekistan 1 – 0 Singapore
FT Lebanon 1 – 2 Saudi Arabia

DSTV na EURO

Jana, pale MovenPick Hotel, MultiChoice Tanzania ilitangaza rasmi kuonesha michuano ya UEFA kwenye mtandao wake wa DSTV iliyoanza rasmi jana. Pichani ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Lucy Kiwhele, akinadi mpira katika bahati nasibu iliyochezeshwa hotelini hapo kwa wageni waalikwa!

Misri, Aljeria zatisha Afrika

Misri 4-0 Jibuti.Amr Zaki wa Misri ndiye alifungua karamu ya Magoli

Wakati Taifa Stars ikishindwa kutamba mbele ya Cape Verde , Timu ya Taifa ya Misri imepanda kileleni mwa Kundi la 12 katika michuano ya kutafuta nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Duniab 2010 na fainali za Matifa ya Afrika pia mwaka hu, baada ya juzi kuiadhibu bila huruma Jibuti mabao 4-0 .

Katika mechi hiyo mabingwa hao wa Afrika walianza mechi hiyo kwa kasi lakini iliwabidi kusubiri hadi dakika 40 ilipopata bao mfungaji akiwa Amr Zaki.

Misri ambao walikuwa wageni waliongeza bao la pili dakika 47 , mfungaji akiwa Hosni Abd Rabo, kabla ya nahodha wa timu hiyo, Ahmed Hassan kupachika la tatu dakika 54 na Ahmed Abdelmalik kufunga la nne muda mfupi baadaye.

Mechi nyingine za kundi hilo la 12 zinatarajiwa kuendelea leo, wakati timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo DRC itakapoikaribisha Malawi mjini Kinshasa.

Mbali na mechi hiyo pia juzi kulikuwepo na mechi nyingine ya Kundi la 6 kati ya Algeria na Liberia ambapo katika mechi hiyo iliyofanyika mjini Blida , Algeria waliibuka na ushindi wa bao 3-0

Yanga wamemficha Kaseja

Na Majira

KIPA galacha (maarufu) nchini, Juma Kaseja amefichwa na klabu ya Yanga ya Dar es Salaam kwa nia ya kumsajili kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao na michuano ya kimataifa.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Yanga zilieleza kuwa tangu juzi kipa huyo amekuwa katika mazungumzo na baadhi ya viongozi wa Yanga (majina tunayo) kuhusiana na kusaini fomu hizo.

Jana mchana kipa huyo alionekana katika ofisi ya mmoja wa wadau wakubwa wa Yanga, ambapo haikuwa rahisi kwa watu wa kawaida kumtambua.

“Ni kweli tupo na Juma, amezungumza na watu muhimu ndani ya Yanga, ni jukumu letu kuhakikisha tunamalizana naye,” kilieleza chanzo cha uhakika ndani ya Yanga.

Chanzo hicho kilieleza kuwa kwa asilimia 80 Kaseja wamemalizana naye Yanga, lakini kuna fomu za mkataba kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), ambazo hazikuwepo, hivyo atazisaini wakati wowote.

“Kilichopo sasa tumemuweka chini ya himaya yetu hadi hapo atakaposaini hizo fomu, hata namba ya simu tumembadilishia,” kilisema chanzo hicho cha uhakika.

Hatua ya kumchukua kipa huyo aliyefungwa mara moja na Yanga, tangu ajiunge Simba karibu miaka saba iliyopita, inaonekana ni Yanga kutaka kukomoa baada ya kushindwa kuwasaini wachezaji wa Simba Henry Joseph na Kelvin Yondani. Wachezaji hao walisaini mkataba wa kuchezea tena timu hiyo wiki hii.

Katibu Mwenezi wa Yanga, Francis Lucas alipoulizwa jana kuhusiana na suala hilo alisema hakuwa na taarifa hizo kwa wakati huo. “Sina taarifa hizo, sidhani kama tunaweza kumsaini, si katika wachezaji wanaotajwa kusajiliwa Yanga. Lakini pia wachezaji wapo Simba tu?

“Hili la kumficha pia silijui, lakini hiki ni kipindi cha usajili mengi utayasikia, ila sisi Yanga usajili anafanya kocha, si viongozi,” alisema Lucas.

Gazeti hili (majira) lilijaribu kuwasiliana na kipa huyo kwa namba yake ya kawaida ambayo haikuwa hewani, hadi baadaye kipa huyo alipatikana kwa namba yake mpya na alipoulizwa alishtuka kwa kiasi kikubwa.

“Hapana mimi nipo na mambo yangu, nimebadili namba kwa masuala yangu binafsi, ambayo sidhani kama ni habari, suala la mimi kutakiwa si jambo la ajabu, mimi ni mchezaji, hivyo aliyekupa taarifa hiyo ndio akueleze kwa kirefu, maana hata timu za mikoani pia zinanitaka,” alisema Kaseja.

Alipobanwa zaidi ikiwemo kutajiwa namba ya gari iliyomchukua pamoja na muda alionekana na viongozi wa Yanga pamoja na mahali alipowekwa kwa sasa alijibu: “Naomba tuyaache.”

Makamuzi ya Ali Kiba Milton

Mwanamuziki kutoka Bongo Ali Kiba ameendelea kufanya makamuzi ya nguvu ndani ya tour lake nchini Uingereza na kudatisha karibu kila mji anaotia maguu.,Pichani ni show yake ya kukata na shoka iliyofanyika Milton Keynes.Kwa wadau wa Reading kaeni Mkao wa kula kwa Show bab’kubwa kutoka kwa Ali Kiba Tarehe 14 june 2008 ndani ya The FACE nite Club.Kazi Kwenu..
Kwa picha zaidi tembelea Haki Ngowi

Tanzania Vipaji vingi basi tuu

Rafiki yangu Hans Von Dykie ameniletea hii kutoka Ifakara ananiambia hawa jamaa huwa wanaburudisha baada ya kazi zao za Shamba wanajiita Big Tone Band hapa wanaimba kuwaelimisha vijana kuhusu gonjwa la Ukimwi. Hans Von Dykie ni mmoja wa wasamaria waliokwenda huko kwa ajili ya shughuli za kujitolea hasa kwa mradi wa Malaria na Ukimwi.

Wamkumbuka huyu?

Anaitwa Khamisa, alikuwa ndiye Miss Temeke 1998, kwa sasa yuko nchini Marekani alikojikita na kuendeleza maisha huko.

Njaa kipimo cha Akili

Kuna msemo unasema “Njaa Kipimo cha Akili”, Kama una njaa akili hufanya kazi mara dufu kufikiria ni jinsi gani utajitahivi kupata mkate wa kila siku, katika kutafakari mkate huo ndio hapo unapata Negative na Positeve ideas kwani hapo ndipo mawazo ya Ujambazi, U Richmonduli, na vipaji hujitokeza, Ninachotaka kumaanisha ni kuwa kuna njia nyingi za kujitafutia riziki moja wapo ikiwa huyu bwana akitoa burudani kupitia sanaa yake na hapo hapo kujipatia riziki yake.

Cape Verde yaisononesha Taifa Stars

Cape Verde 1-0 TanzaniaTaifa Stars ya Tanzania
Mechi ya pili ya Kundi 1 baina ya Cape Verde na Tanzania iliisha kwa kuwanyong’onyesha vijana wa nyumbani Taifa Stars katika mchuano mkali kuwania nafasi ya kufuzu katika kombe la dunia 2010.Mchezaji aliyeingia katika kipindi cha pili wa cape verde Babanco aliifungia timu yake mnamo dakika 73 na kuiwezesha Cape verde kunyakua pointi 3 zote.Taifa Stars sasa wanakabiliana na kazi kubwa mbele hasa baada ya kutoka sare ya nunge kwa nunge nyumbani na Mauritius wiki iliopita.Mechi yao ya tatu watamenyana na mabingwa mara nne wa kombe la bara Africa Cameroon nyumbani hapo June 14.

Pepe aipeperusha Portugal

Portugal 2-0 Turkey


Pepe na Cristiano wakishangilia baada ya goli la kwanza

Portugal wako kifua mbele katika Kundi A baada ya kuicharaza Turkey 2-0 kupitia mlinzi pepe na mshambulizi mdogo Raul Meireles.Portugal walicheza mechi ya kufana sana wakisaidiwa na mchezaji bora duniani mtarajiwa Cristiano Ronaldo.wangeongeza bao la tatu ambapo mchezaji matata Ronaldo kutoa kombora kali na kugonga chuma na kubanduka nje.Turkey vilevile walijikakamua na kukosa nafasi kadha wa kadha kupitia mchezaji Tuncay Sanli na hata kunyimwa penalti wanavyodai.Portugal sasa wanaongoza Kundi A juu ya Czech kwa sababu ya magoli mengi lakini pointi sawa.Mechi yao ya Pili ni dhidi ya wapinzani wao Czech.

Switzerland yashangazwa nyumbani na Czech.

Switzerland 0-1 Czech


Switzerland ilipigwa na mshangao baada ya kushindwa mbele ya mashabik wao mjini Basle Switzerland katika mechi ya kwanza la kombe la Bara Ulaya Euro 2008.Mchezaji Vaclav Sverkos’ aliengia katika kipindi cha pili na kuifungia Czech.Switzerland walicheza mechi nzuri na kuhatarisha lango la Czech lakini hatimaye kushindwa,timu hiyo inaongozwa na Senderos wa Arsenal,mchezaji mrefu kwa wote duniani Jan Koller wa Borussia Dortmund na wengineo ilhali Czech inaongozwa na Petr Cech wa Chelsea,Rosicky wa Arsenal vilevile wakiwemo wengine.

Saturday, June 7, 2008

Kenya yaiburuza Guinea 2-0.

Mshambulizi mkenya Mc Donald Mariga wa Parma FC Serie A Italy.


Kenya iliicharaza Guinea 2-0 hapo jana katika mechi ya kukata na shoka katika mashindano ya kufuzu kwa kombe la dunia na bara Africa.Mshambulizi matata anayoichezea Auxerre FC ya Ligi kuu ya ufaransa Denis Oliech aliiongoza Harambee stars ya kenya na kuitingisha nyavu mara mbili baada ya dakika tatu tu ya kipindi cha kwanza na ya pili baada ya dakika tano ya kipindi cha pili.Harambee stars ya kenya ilijipatia ari kubwa baada ya kushindwa mechi ya kwanza 2-1 na Namibia mjini Windhoek Namibia wiki iliopita.Guinea vilevile walishindwa kunyakua pointi tatu didhi ya Zimbabwe baada ya kutoka sare ya 0-0 nyumbani Conakry.Kufikia sasa kenya yaongoza kundi B baada ya Namibia,Guinea kisha Zimbabwe.Guinea walileta kikosi yote iliocheza kombe la Bara Africa mwaka huu ikiongozwa na mshambulizi na nahodha matata Pascal Feindouno wa Ufaransa St Etienne na beki hatari wa Celtic Bobo Balde na wengine walipigwa na butwaa na kubaki na kibarua kigumu ya kushinda mechi zilizobaki ilikujikomboa.

Mbwembwe za Mashabiki mitaani

Kijibwa kikiwa kimevalishwa jezi mitaani

Shabiki wa Croatia akiwa ameweka Tatoo ya bendera ya timu yake
Shabiki wa Germany

Mrithi wa Richa Adhia Dar Indian Ocean keshapatina

Mshindi wa Taji la Miss Dar Indian Ocean Joan Fast (katikati) akionesha tabasamu mara baada ya kutwaa Taji hilo katika ukumbi wa Cine Club Mikocheni Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.Kushoto kwake ni mshindi wa pili wa Taji hilo Grace na kulia ni mshindi watatu Groly. Picha na Global Publishers

Chris Tucker adata na Maajabu

Mwigizaji maarufu na mcheza sinema kutoka Marekani,Chris Tucker akiwaimbia wimbo wa mwanamuziki Michael Jackson,Wamasai aliowakuta katika Hifadhi ya Ngorongoro juzi.

——–
MCHEKESHAJI maarufu wa Marekani Chris Tucker amesema kuwa atakuwa “balozi wa hisani” wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ili kuitangaza hifadhi hiyo duniani .Amesema kuwa baada ya kuvutiwa na maisha mseto kati ya wanyama na binadamu katika hifadhi hiyo.
Tucker ambaye alikuwa mjini Arusha kuhudhuria mkutano wa nane wa taasisi ya Leon Sullivan akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea kreta ya Ngorongoro na kujionea vivutio mbalimbali vya utalii vilivyoko ndani yake. Ifate kwa undani zaidi kwa Haki Ngowi

Logo, Wallpaper, Ring Tones na Video Ipod za EURO 08

Je unapenda Logo, Wallpaper, Ring Tones na Video Ipod za Euro 2008?
Basi Gonga hapa ujinafasi

Tutashinda bila Viera: Makelele

Mchezaji wa timu ya Taifa tya Ufaransa Claude Makelele amesema Ufaransa inawezakushinda bila Kepteni wao Patrick Vieira ambaye ataukosa mpambano wa ufunguzi kutokana na maumivu ya kwenye mguu sehemu ya paja.

‘Pat ni mchezaji muhimu lakini tunaweza kuishi bila yeye kwenye timu kama tunataka, Makelele aliwaambia waandishi wa Habari juzi walipotaka kujua anasemaje kuhusu kutokucheza kwa Pat.

Viera ambaye aliumia mazoezini wiki iliyopita hatocheza kwenye mechi ya ufunguzi wa Group C dhidi ya Romania hapo Jumatatu mchezo utakaochezwa Zurich. “Tunategemea Viera atakuwa fit kwa ajili ya mechi zilizobaki kwani tunamuhitaji kwenye timu yetu, na nadhani Mungu atabariki apone haraka”, alimalizia Makelele.

Nionavyo mimi

Maximo apewe Muda zaidi
Zimebaki siku chache kabla mkataba wa kocha Mbrazili Marcio Maximo (pichani) umalizike, Mengi yamesemwa kuhusu kocha huyu mgeni ambaye jukumu lake ilikuwa ni kutupeleka CAN, tunaiangalia leo Stars kwa macho mawili , Tujaribu kujiuliza je dhumuni lilifikiwa na tuangalie tulikotoka na tulipo sasa na nini kifanyike.
Kimsingi ni kweli Maximo ameinua kiwango cha Timu yetu ya Taifa kwa kiwango chake. Najaribu kuiangalia Taifa Stars ya wakati huo chini ya Kocha wazalendo na ndani ya ukwasi mkubwa wa pesa ambapo wachezaji walikuwaa hawana hata vifaa vya mazoezi, ni mara ngapi tulisikia wasamaria wema tu kama Mohammed Enterprises akijitolea viloba vya nafaka na carton za maji kwa Timu yetu?.

Ninachoona mimi ni kuwa tofauti pekee ambayo timu yetu ya Taifa inayo ni support. Kwa sasa angalao timu ina support licha tu ya serikali bali pia toka kwa makampuni makubwa kama Serengeti Breweries na NMB na mengineyo. Huu ni wakati mzuri kwa Timu yetu kufanya vizuri kama tuna Kocha Mzuri na support ipo ya kutosha kwa nini tusishinde basi?

Fikiria jinsi watu walivyohamasika kwa timu yao ya Taifa kipindi tunagombea kucheza CAN Ghana!! Nafikiri kwa kiasi kikubwa tumeona mabadiliko ingawa ni kweli mabadiliko hayawezi kuja mara moja. kwa mfumo wetu wa Soka wa kukusanya wachezaji dakika za mwisho hatuwezi kuona mabadiliko kwa muda mfupi kamwe. Ni lazima tuwe na Program ya muda mrefu na muda mfupi, muda mrefu ni kwa Serikali kuimarisha michezo kuanzia ngazi ya shule za msingi, na kuimarisha mashindano kama ya Taifa Cup.

Tujaribu kuangalia mechi za kirafiki za kimataifa, Taifa Stars imecheza michezo tisa ya kimataifa ya kirafiki chini ya Kocha Mkuu Mbrazili Marcio Maximo tangu aanze kibarua hicho karibu miezi 19 iliyopita.

Katika michezo hiyo Taifa Stars imeshinda mitatu dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Uganda na Zambia na kutoka sare mara nne dhidi ya Kenya, Angola, Zambia, Uganda na juzi sare ya Malawi ya 1-1. na kufungwa na Yemen. Tukiangalia na tulikotoka haya tunayaita mafanikio.

Kimsingi ninachotaka kusema ni kuwa Kwangu mimi Maximo akipewa muda anaweza kuleta mabadiliko kwani ni mapema mno ikumbukwe kuwa anachokifanya Maximo ni kukutanishwa na wachezaji wanaotoka kwenye Vilabu vyao na kazi yake ni kuwafanya hawa wacheze kama Timu, sio kumfundisha mtu jinsi ya kutoa pasi hiy anafundishwa kwenye club yake huko. Ni lazima Club ziwe na mbinu mpya za ufundishaji, huko ndio soka linapoanzia. kwani vilabu ndio vinalisha Timu ya Taifa wachezaji, Pia kurudishwa kwa michezo ya Taifa Cup itakuwa Chachu ya mabadiliko kisoko kwani huko ndiko vipaji vinaanzia.

Friday, June 6, 2008

Salamu Toka kwa Kaka Chibiriti Italy

Habari yako Mkuu,

Nimekuwa nikifuatilia sana blog yako, kwakweli ni nzuri sana kwa sisi wapenda michezo, hasa soka mimi umenifikisha penyewe kabisa. Kila siku nilikuwa nikifikiri kukushukuru kwa kazi nzuri unayo ifanya ila mda ulikua ni mdogo, leo nimepata huu mda ninasema asante sana kwa habari zako, safi sana.

Ninakutakia kazi njema na mafanikio mema kila siku.

Ni mimi Baraka Franco Chibiriti

kutoka hapa Cesena-Italy.

Bila Hiyana nami nazipokea, nashukuru Kaka, Tuko Pamoja.

Pius

Collie Budz Show Ndani Ya Cine Club! Katika Picha

Picha na dar411 kupitia Sheria Mavazi Blog

Je wajua?

Wakati Mtanange ukikaribia kuanza si vibaya ukajikumbusha historia za timu husika.
Gonga Kwenye Timu Husika upate Data kuanzia Mechi za Kwanza za Matanange huu mpaka Hapo ilipo.

GROUP A
TURKEY TURKEY
CZECH REP CZECH REP.
PORTUGAL PORTUGAL
SWITZERLAND SWITZERLAND
GROUP B
AUSTRIA AUSTRIA
POLAND POLAND
GERMANY GERMANY
CROATIA CROATIA
GROUP C
FRANCE FRANCE
HOLLAND HOLLAND
ITALY ITALY
ROMANIA ROMANIA
GROUP D
SWEDEN SWEDEN
GREECE GREECE
SPAIN SPAIN
RUSSIA RUSSIA

Kila La heri

Dj Bonny Luv wa Mawingu Studio

Historia ya disco nchini Tanzania haiwezi kukamilika bila kumtaja DJ Bonny Luv (pichani). Ukifanya hivyo,wanaoielewa historia, ladha na utamu wa disco, enzi hizo lilipokuwa disco haswa, watakuona una lako jambo. Soma zaidi; http://bongocelebrity.com

Sebene la Werrason Usipime!!

Big Producer Maghambo, Mukubwa Mwemtsi, Collins na Fikiri wazee wa USA, Boss Chizenga na wapenzi wote wa Werrason inawahusu hii. Weekend njema

Simba yaipiga bao Yanga

Henry Joseph asajili Simba.

Uongozi wa Klabu ya Yanga umeanza kuchanganyikiwa baada ya wapinzani wao Simba juzi kufanya kufuru ya usajili kwa kuwasajili nyota wake wote waliokuwa wakitakiwa na timu hiyo.

Kuhaha huko kwa Yanga kumekuja baada ya Simba kuwasajili Musa Hassan Mgosi, Henry Joseph na Kelvin Yondani ambao wote walikuwa wakitupiwa macho na klabu hiyo kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao kitakachoshiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Afrika.

Baada ya Simba kufanya hivyo na jana kutangazwa kuwa wanawania kumsajili mchezaji wao Mrisho Ngasa kufuatia baba yake mzazi kuamuru mwanae aichezee Simba, viongozi wa klabu hiyo wamekuwa wakikutana mara kwa mara kujadiliana juu ya suala la usajili.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya uongozi wa klabu hiyo zimeeleza kuwa imekuwa ni suala la kawaida kwa viongozi wa Yanga kukutana zaidi ya mara sita kwa siku.
IPP Media

Miss Tanga hiyoooo Kupekecha na Akudo mpaka Lyamba!!

Kati yao mmoja atamnrithi Victoria MArtin Kesho
Miss Tanga ndio hiyo si ya kukosa kama kawaida Akudo Sound watatumbuiza na Kijana toka Jumba la Vipaji – THT Andrew G pia atafanya mambo, ni Kupekechapekecha tuu.

Miss Tanga2007, Miss Tanzania Kanda ya Kaskazini, Redds fashion Ambassador Victoria MartinAmbaye amepata mikataba na kampuni za Modelling za South Afika. Hivi karibuni alikwenda South Afica kuangalia soko la uanamitindo na tayari kampuni mbili zimevutiwa naye na kumpa mapendekezo yao. Kampuni hizo ni O Model na EXTRA. Soma hapa zaidi

Simba yawatema Athuman Machupa, Joseph Kaniki na Yahya Akilimali.

KLABU ya Simba ya Dar es Salaam imewatema wachezaji saba waliochezea timu hiyo msimu uliopita akiwemo chipukizi Julius Mrope aliyesajiliwa mwaka jana akitokea Moro United.

Habari za uhakika kutoka ndani ya uongozi wa klabu hiyo, ziliwataja wachezaji wengine walioachwa katika kikosi hicho kuwa ni Athuman Machupa, Joseph Kaniki na Yahya Akilimali.

Chanzo hicho kiliwataja wachezaji wengine kuwa ni Said Sued, Soud Abdallah na Moses Odhiambo, ambaye amehamika APR ya Rwanda.

Hata hivyo chanzo hicho kilidai kuwa Machupa, Kaniki na Sued wameomba kuachwa kutokana na kutaka kwenda kucheza mpira wa kulipwa nchi za nje.

Kutokana na hatua hiyo ya kuacha wachezaji hao, chanzo chetu kilieleza kuwa hivi sasa Kamati ya Usajili ya Simba inahaha kukamilisha usajili kwa wachezaji 10 wapya kwa ajili ya msimu ujao.

“Simba imepanga kusajili wachezaji kumi wapya, kwa kuwa ilikuwa na jumla ya wachezaji 28 waliosajiliwa msimu uliopita, hivyo Kamati ya Usajili imepewa jukumu la kuhakikisha inasajili wachezaji imara,” kilieleza chanzo.

Tayari kamati hiyo imeshaanza kazi hiyo kwa kuwarudisha kundini wachezaji Henry Joseph na Kelvin Yondan ambao walikuwa wananyemelewa na Yanga, huku ikiwasajili chipukizi, Juma Jabu na Jabir Aziz.

Miss Dar City Centre atatoka hapa

Warembo wa Katikati ya jiji hawa hapa!

Vimwana wanaowania taji la Miss Dar City Centre 2008 wakiwa katika pozi la picha ya pamoja jana katika ukimbi wa Cine Club jijini Dar es Salaam ambako Juni 14 mwaka huu watachuana vikali kuwania taji hilo. Kampuni ya TSN kupitia magazeti yake ya HabariLeo/Daily News ni miongoni mwa wadhamini wa shindano hili.

Mitindo House na Kimasomaso

MAMBO YA TANZANIA MITINDO HOUSE AMBAYO INAKUJA NA FASHION SHOW AMBAYO WATAONYESHA NGUO ZA MAHARUSIIII KATIKA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO KITCHEN PARTY, SEND OFF, AQDI NA RECEPTION
HAYA KAZI ZENU WADAU POSTER CHINI HAPO INAJIELEZA!!!

Taifa Stars yaenda Cape Verde

TIMU ya taifa ya soka, Taifa Stars inaondoka leo alfajiri bila ya mchezaji wake nyota, Mrisho Ngassa na kiungo Abdi Kassim, huku kocha, Marcio Maximo akiahidi kwenda Cape Verde kupambana, na Naibu Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Joel Bendera akigeuka mbogo kwa wachezaji.

Stars, iliyopoteza pointi mbili katika mechi yake ya kwanza ya michuano ya awali ya Kombe la Dunia ilipolazimishwa kwenda sare ya bao 1-1 na Mauritius nyumbani, itavaana na Cape Verde Jumamosi.

Maximo alisema Ngassa bado hajapona vizuri na kwamba Abdi Kassim bado anahitaji muda zaidi wa kujiweka ‘fiti’ kabla ya kurudi uwanjani kikamilifu baada ya kutatizwa na nyama za misuli.

“Wataendelea na mazoezi hapa hapa kujiandaa kwa mechi ya Cameroon,” alisema Maximo.

Hata hivyo, kocha huyo Mbrazili alionekana kuwaamini wachezaji wengine waliosalia, aliposema kuwa wanaenda Cape Verde kupambana.

“Tulicheza na Mauritius, watu wakatupa nafasi kubwa ya kushinda lakini matokeo yakawa sare. Hii ndio itakavyotokea kwa Cape Verde. Watu wanasema Cape Verde ina timu nzuri, lakini na sisi tunakwenda kuwashangaza kama tulivyoshangazwa,” alisema Maximo.

Mziki wa EURO 2008

Sanamu kubwa zilizotengenezwa kwa sura na maumbo ya wachezaji kutoka Timu za Nchi tofauti duniani zanazoshiriki Kombe la EURO 2008 wakiwa ni pamoja na Michael Ballack na Philipp Lahm toka Germany, Karim Benzema na Patrick Vieira toka France, Angelos Charisteas toka Greece, Petr Cech wa the Czech Republic, Cristain Chivu wa Romania, David Villa toka Spain, Tanquillo Barnetta toka Switzerland, Andreas Ivanschitz wa Austria and Robin van Persie wa Netherlands.

U-Modo una karaha zake

Kusimama, Kutembea na hata Kuongea mbele za watu ni kazi kubwa inayohitaji ujasiri, fikiria uko mahala halafu watu zaidi ya 100 wote wanakuangalia wewe halafu ghafla kinatokea cha kutokea.
Ili uwe “Modo” inabidi uwe na vigezo fulani kama Figure, Urefu, na kikubwa kulitawala jukwaa ikiwa ni pamoja na mwendo, Angalia jinsi “Modo” huyu alipopata aibu ya mwaka jukwaani na kuwaacha hoi mpaka watangazaji wakifa kwa kicheko.
Bonyeza Player

Thursday, June 5, 2008

Ronaldo aweka wazi, Siku zake zahesabika Manchester

LONDON, Uingereza
HATIMAYE kiungo nyota na machachari wa klabu ya Manchester United, Christiano Ronaldo amesema ataihama klabu hiyo mwakani.

Kauli ya nyota huyo huenda ikatonesha donda la Kocha Mkuu wa United, Sir Alex Ferguson ambaye amekuwa hapati usingizi baada ya fununu kuvuja kuwa Ronaldo alikuwa na mpango wa kujiunga Real Madrid ya Hispania msimu ujao kabla ya kuvunja jaribio hilo.

Mwanzo mwa wiki hii, Ronaldo alimhakikishia Fergie atabaki Old Trafford kutokana na mafanikio aliyopata chini yake tngu alipojiunga na klabu hiyo mwaka 2003 akitokea Sporting Lisbon.

Kiungo huyo wa pembeni aliyeongoza kwa ufungaji mabao msimu huu katika Ligi Kuu England akipachika wavuni mabao 30 na 11 ya kimataifa, alisema kama ameshindwa kuhama msimu ujao basi itakuwa mwakani.

Ronaldo na wakala wake, Jorge Mendes wamefikia muafaka wa kuangalia ofa za klabu nyingine kutoka nje ya England. Real Madrid, Barcelona, AC Milan na Inter Milan zinammezea mate nyota huyo.

Ronaldo aliweka bayana kuwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la Ligi Kuu England ni mafanikio makubwa na sasa wakati umefika wa kuondoka kwenda Real Madrid.

TEARS OF A CLOWN

Cristiano Ronaldo wa Ureno akipozwa baada ya kulia sana wakati wa mchezo wa Fainali ya EURO 2004 kati ya Ureno na Ugiriki (Portugal na Greece), Baada ya Ureno kupoteza mchezo huo kwa goli 1-0. hii ilikuwa Euro 2004, Je mwaka huu atalia au atacheka?

Kujifungua kwa Angeline Julie bado ni siri kubwa

NEW YORK – “Entertainment Tonight” walitangaza jana habari za kujifungua mcheza Sinema maaruf Angelina Julie ila kila wakati walikuwa wakisisitiza kuwa habari hizi ni kwa mujibu wa chanzo chao. Hata Shirika kubwa la habari la Associated Press katika taarifa yake limesema kuwa wao walipokea e-mail iliyotoka kwa mtu aliyejitambulisha kama mtu wa karibu na mcheza Sinema huyo. Kumekuwa usiri mkubwa kuhusu kujifungua kwa Angelina Julie tangu ijumaa ya wiki iliyopita, habari hizo zinasema mwanadada huyo amejifungua Mapacha.

Brazil yajipigia “debe” Olympic 2016

Tambara kuuubwa likipitishwa kwenye jukwaa la mashabiki katika Kupigia debe jiji la Rio De Janeiro kuwa muandaaji wa michezo ya Olympic 2016, Hii ilikuwa ni kwenye mchezo wa Mzunguko wa pili wa mchezo wa nusu fainali ya kombe la Libertadores Cup kati ya Fluminense ya Brazil na Boca Junior ya Argentina, Mchezo ulichezwa Rio de Janeiro, June 4, 2008. Fluminense alishinda 3-1

Amanda

Miss universe tz 2008 Amanda katika Pose, Mdau wangu Jimmy Mlay anasema wanakuwaga wapi hawa mbona mitaani hatuwaoni?
Picha na Issa Michuzi – Criss Tucker

Safari ya Ndoa ya Salma Msangi

Salma Msangi
Salma Msangi

Bi Khadija Kopa

Salma Msangi mtangazaji mahiri wa vipindi vya burudani Channel Ten hivi karibuni alifanyiwa sherehe ya Kitchen Party (sijui kiswahili chake tusaidiane) katika maandalizi ya awali ya Kufunga ndoa, Serehe hii ilifanyika katika ukumbi wa Water Front na ilinogeshwa na Malkia wa Mipasho Khadija Kopa na “Pembe” ilikuwa Live. Vazi lake limebuniwa na Asia Idarusi, Safari ya kuolewa inaanza na Kitchen Party, Send Off, Ndoa na baadaye Harus i duh!! si mchezo, Kila la heri dadaa, Kwa picha zaidi za sherehe hii na mengineyo Muone Mamaa Zeze hapa

Wednesday, June 4, 2008

Ali Kiba ndani ya Milton

INFINITY ENT’ ALONGSIDE BONGO FAMILY UK PRESENTS……SPRING BREAK TOUR ’08FEATURING ALI KIBAPERFORMING HIS HIT SINGLE CINDERELLA, NAKSHI NAKSHI MREMBO AND MANY MOREMILTON KEYNES ON SATURDAY 07TH JUNE@ SILK ROAD REST (MAHARAJA) 151 GRAFTON GATEMORE INFO
WWW.BONGOUK.COM

Cannavaro kuikosa UEFA – EURO 2008

Nahodha wa Italy Fabio Cannavaro akiwa ameshikilia Kombe la Dunia wakati timu yake iliponyakua kombe hilo mwaka 2006. Nahodha huyo na mchezaji wa timu ya Real Madrid hatokuwemo kwenye kikosi cha Italy cha sasa kitakachoshiriki mtanange wa kombe la UEFA – EURO 2008 baada ya kuumia mguu wakati wa mazoezi na daktari wake kuthibitisha kuwa hatoweza kucheza michuano hiyo.

Msiba wa Mama Mere Malou na Zadio Kongolo

Titina ambaye ambaye alimuwakilisha Koffi na Quartier Latin na Mpiga Gitaa la Rhythm wa Wenge BCBG Alba ambaye alimuwakilisha JB Mpiana na Wenge BCBG wakiwasili msibani.

Papa Wemba (wa pili) akiongoza waombolezaji kubeba jeneza la mama Mere Malou, Inasemwa kuwa Marehemu Mere Malou alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mzee Papa Wemba.

Fallu Ipupa Di Cap akiwa na Producer maarufu Manuru vaka kwenye msiba wa Mere Malou. Fally alitoa rambi rambi ya Euro € 1,500 kwenye msiba huo.

Kuna Post inayosema Zadio Kongolo shabiki namba mojawa Wenge BCBG,

Kwenye maoniya post hiyo Kuna mdau analalamika kuwa huyu bwana si maarufu kama tunavyomkuza na kusema hakwenda Bruxelles kwa ajili ya Onyesho la BCBG, ila alikwenda kwa ajili ya msiba wa Mama Mere Malou “madame ya poto“, ukweli ni kwamba kuna tofauti kubwa tangu mama Mere Malou afariki alizikwa siku ya Jumamosi tarehe 29 ya Mwezi March kwenye Makaburi ya jumping Jack na Onyesho la JB Mpiana lilikuwa tarehe 3 May 2008 huko huko Bruxelles. Si nia ya safu hii kubishana bali ni katika hali ya kuwekana sawa. Kwa faida ya wasomaji wangu, Mama Mere Malou alikuwa Mkongo anayeishi Paris Ufaransa, alishiriki kwa kiasi kikubwa kuukuza na kuutangaza muziki wa Kongo bara Ulaya, alikuwa ndio mdhamini na mpokezi wa wanamuziki wa Kongo kila wakifanya ziara Ufaransa.
Hii ndio “starehe” ya burudani, Big Producer Maghambo umesomeka.

Nastaafu 2010: Fergie

Kocha wa timu ya Manchester United Mkongwe Sir Alex Ferguson amesema kuwa atastaafu kazi ya ukocha rasmi akifikisha miaka 70, kwa sasa umri wa Ferguson ni miaka 66 hivyo basi ni wa “misimu” mitatu toka sasa.

Feruson aliweka wazi uamuzi wake huo jana alipokuwa akihojiwa kwenye mahojiano na Sir David Frost. Ferguson ataondoka huku akiwa na mafanikio makubwa na timu yake hiyo ya Manchester United kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili alichokaa na timu hiyo.
Aliongelea mambo mengi ikiwa ni pamoja na urafiki wake na Tony Blair na Gordon Brown pia aliongelea umuhimu kwa makocha na wachezaji kuwa na aliyoiita”njaa” ya ushindi.
“mchezaji mwenye kujituma ambaye timu ikishindwa anaumia huyo ndio napenda zaidi, pia nampenda mchezaji mwenye njaa ya magoli, njaa ya ushindi, hapo atafanya kila linalowezekana kimchezo timu ishinde, ndio kitu nawaambia kila siku wachezaji wangu. Hii ni changamoto kwa uongozi wa timu ya Manchester kwani ni kibarua kingine kutafuta mtu mwenye uwezo sawa na Ferguson.

UEFA – EURO 2008 Maandalizi ya timu moto!

Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ufaransa Thierry Henry (R), akielekeza jambo kwa Mwanamuziki maarufu wa Ufaransa Grand Corps Malade, wakati wa kipindi cha mazoezi kwa klabu hiyo June 4 mwaka huu, kwenye kambi ya timu hiyo Clairefontaine, kusini Magharibi mwa Paris, mwanamuziki huyo aliitembelea timu hiyo kuipa moyo kwani Ufaransa wanacheza na Romania June 9, 2008 kwenye mechi yao ya kwanza ya mashindano ya UEFA – EURO 2008.

Tuesday, June 3, 2008

WANAITWA ‘ASHIERS’

HUYO WA KATI NI MADAM RITA AKIWA NA WASICHANA WAREMBO KWENYE MOJA YA EVENT HAO WASICHANA KITAALUM NAAMBIWA WANAITWA ‘ASHIERS’ SINA UHAKIKA NA SPELLING WAJUZI WATATUJUZA…ANAKUWA WANAWAPOKEA WAGENI N.K NAONA NI KAMRADI BONGO SIKU HIZI KWA WADADA HUSUSAN WENYE SHEPU ZA KIMISS,
Kwa Habari za Nyumbani za Burudani na mitindo tembelea 8020 Yuko Juu!!

Bingwa wa “Atalaku” kusakwa, Wadhamini ni Afrika Bambataa

Kuta kuwa na mpambanao wa marapa wa muziki wa dance Tanzania kutoka bendi mbali mbali ingawa hii haita husisha bendi bali mtu mmoja mmoja

Zawadi kubwa kutolewa waandaaji wakiwa ni kipindi cha African Bambataa ya clouds fm radio ya watu.

Mpaka sasa tayari marapa wamesha jaza fomu na kuanza kujitapa katika kipindi hiki kila mmoja akijiona yeye ni bora kuliko mwezie lakini ukweli utajulikana tu nani atatwaa taji la ufamle wa kurap katika muziki wa dance hapa nchini.

Akithibitisha hilo malkia wa bambataa ambae pia ni brand manager wa Nite X-Press amesema kuwa maandalizi yanaenda vyema na kuwa tayari baadi ya marapa wamesha jaza fomu za kukubali kushiriki katika kinyanganyiro hicho.

Mashindanpo haya yanataraji kuwa ya awamu 3 ambapo awamu ya kwanza ni ya utambulisho , awamu ya pili itakuwa ni ya kupiga live na mashabiki ndio watakao kuwa majaji na hatimae fainali.

Hii ni changamoto kwa vijana ambao tunasema ni kizazi kipya cha dance hapa Tanzania nia na lengo letu ni kuhakikisha marapa na wao kama sehemu ya ladha na burudani wanatambulika wanaheshimika na kudhaminiwa popote pale kwakuwa bila wao pia muziki unakuwa hauja kamilika. alisema Bi Sofia Kessy mmoja wa Waandaaji wa mpambano huo.
Na tutajitahidi kardi ya uwezo wetu kuhakikisha kuwa wanakubalika kudhaminiwa na kuheshimika pia kujulikana kote nchini.

Zadio Kongolo Shabiki nambari wani wa JB Mpiana na Wenge BCBG

Anaitwa Zadio Kongolo ukipenda muite ZK wengine humuita Sir Joe Kongolo, ni mfanyabiashara wa Kongo anayeishi Uingereza, Huyu ni mpenzi mkubwa wa JB Mpiana na Wenge BCBG kwa ujumla, ni maarufu kwa kutunza pesa, kwenye onyesho moja la JB alimtunza mwanzo hadi mwisho wa nyimbo (kwa nini asiimbwe!!!) kwenye kila onyesho la JB Mpiana Ulaya humkosi huyu bwana, kama anavyoonekana pichani alisafiri kwenda Belgium hii ilikuwa kwenye onyesho la JB Mpiana mwezi uliopita tarehe 3 May Bruxelles. JB Mpiana humuimba karibia katika kila wimbo lazima atamtaja ni kama vile unavyosikia PDG Ndama, Abdul Tall Omary Tall, Andrew Traders wanavyotajwa kwenye nyimbo za nyumbani, lakini Zadio amekwenda mbali zaidi kwani kwenye Albamu ya JB Mpiana ambayo inatamba sasa ya “Quel est ton probleme” akimaanisha Nini Tatizo lako?. Jb amemtungia wimbo kabisa Zadio unaoitwa Zadio Kongolo – ZK. Angalia na usikilize hapo chini, pia wimbo huu uwaburudishe wadau wangu PDG Mukubwa Ling’ande, Big Producer Magambo, Papaa Masabo, Mukulu Biloko Zadio wa Darisalama, Papaa Kasapila, Mukubwa Shabani, Ally Tandika – Tajiri mtoto, Batty William Mwafrica na wengine wengi, Mna nini bwanaaa. Pata burudani.
Leo Jioni JB Mpiana atahojiwa LIVE katika kipindi cha Afrika Bambataa, Clouds FM na Sophia Kessy tega sikio

Baba Januari akicheza Sebene la T Respect

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba (Babake Januari) akisakata sebene la T- Respect akiwa na Mbunge wa Kuteuliwa Mh. Al-Shymaa Kwegyir, kwenye ukumbi wa Travertine Magomeni Jumamosi.
Picha/GP

Ronaldo awatunisha vifua matajiri

Rais wa Real Madrid Ramon Calderon jana amesisitiza kuwa Timyake inayopesa ya kutosha kumnunua mchezaji machachari wa Manchester United Christian Ronaldo (pichani).
Katika taarifa ya hivi karibuni akinukuliwa na vyombo vya habari Kocha wa Man Sir Alex Furguson alisema mmiliki wa Manchester “the Glazer family” hawako tayari kumuuza Ronaldo kwa gharama yeyote ile na hawako tayari kumuona Ronaldo akiondoka Man kwa vyovyote, Kama ni kumnunua Ronaldo gharama itakuwa zaidi ya Pound Milioni 40 ambazo Real MAdrid alimnunua Mchezaji Zinedine Zidane miaka 6 iliyopita. Presidaa Calderon amesema “hakuna bei kubwa kwa mchezaji ambaye anachukuliwa kama ni the best duniani, kiwango chake ni cha juu hilo halina ubishi, bado nia yetu ipo pale pale kumsajili na nitafurahi kumuona Real Madrid msimu ujao” alisema kwa majigambo.
Kwa habari za sasa za uhamisho kujua nani kaenda wapi Kong’oli hapa.

Wengi wazimia baada ya uwanja “kufurika” watu Liberia

Wafanyakazi wa huduma ya kwanza wakimbeba mmoja wa mashabiki walipoteza fahamu kwa kukosa hewa kutokana na mrundikano wa mashabiki kwenye mchezo wa kuwania tiketi ya kombe la Dunia kati ya Liberia na Gambia, uliochezwa kwenye uwanja wa Samuel K. Doe . Uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 33,000 ulijaa kupita uwezo wake kwani inakisiwa zaidi ya watu 40,000 waliingia kuona mchezo huo uliochezwa jumapili ya juzi.

Ukisema chanini, wenzio wanasema watakipataje

Jose Mourinho (pichani) jana alilamba dume baada ya kuapishwa rasmi kuwa kocha wa timu ya Inter Milan, ambayo imemfukuza kocha wake Roberto Mancini.

Mourinho, aliondolewa kuifunza Chelsea September mwaka jana, amesaini mkataba wa miaka mitatu na klabu ya Inter Millan, ambao walighadhabishwa na matokeo ya timu yao kwenye michuano ya Champions ligi iliyomalizika hivi karibuni..

Mourinho aliiwezesha timu ya Porto kushinda kombe la Champions Ligi mwaka 2004 na akaiwezesha Chelsea kuchukua ubingwa wa England kwa mwana 2005 na 2006. Kila la heri kaka.

Mbwembe za Euro’08

Gari likipita mbele ya bango kuuuubwa likiwa na mchezaji mpira likiwakaribisha wageni kwa ajili ya Michuano ya Euro inayotarajiwa kuanza hivi karibuni. Bango hili limewekwa Airport Schwechat, kilomita 25 mashariki mwa jiji la Vienna, Mamia kwa maelfu ya wageni wanamiminika kwa ajili ya ichuano hii inayotarajia kuanza wiki ijayo.

Monday, June 2, 2008

Hasheem ndani ya Sullivan

supa staa hasheem thabeet na wadau wa boston pia wapo a-taun kwa ajili ya sullivan
Picha na Michuzi

Miaka 90 ya Mandela kwa Mbwembwe

Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini, Mzee Nelson Mandela akiwa ameshikilia Kombe la Dunia, Afrika Kusini ndio waandazi wa Mtanange ujao wa Kombe la Dunia. Mandela atasherehekea miaka 90 ya kuzaliwa kwake mnamo tarehe 27 Mwezi huu katika Concert iliyoandaliwa Hyde Park mjini London ikiwa ni kuchangisha fedha kwa ajili ya Charity.
Miongoni mwa wanaotarajiwa kutumbuiza tamasha hilo ni pamoja na Amy Winehouse, Lady Jay Dee, Queen, Simple Minds, Leona Lewis na kikundi cha kwaya cha Soweto. Pia watu maarufu wamealikwa akiwemo Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton na Oprah Winfrey .

England yainyuka Trinidad and Tobago 3-0

Mchezaji wa England Dean Ashton (L) na Jerman Defoe wakipongezana baada ya timu ya kupata goli la pili dhidi ya Trinidad and Tobago wakati wa mechi yao ya kirafiki huko Hasley Crawford stadium nchini Spain. England alishinda 3-0.

D-Day Jumatano

Mchezaji wa Manchester United na Portugal Christiano Ronaldo akiwapungia mashabiki wakati wa mazoezi ya timu yake ya Taifa inayojiandaa kwa michezo ya EURO 2008, Ronaldo anatazamiwa kuwa na mkutana na waandishi wa habari siku ya jumatano kuzungumzia hatma yake kisoka ikiwa ni pamoja na tetesi za uhamisho wake kwenda Real Madrid.

Santos mabingwa wa Mexico

Wachezaji wa timu ya Santos wakiwa wameshikilia Kombe la Ubingwa Juu mwisho mwa mchezo wa fainali wa Ligi ya Mexico dhidi ya Cruz Azul Torreon, Mexico, Sunday, June 1, 2008. Santos walishinda kwa agregate ya 3-2.

Kutoka wazo hadi kitu kinachoonekana

Kufanya shooting ya Video za wanamuziki ni kazi ambayo inahitaji vipaji mchanganyiko kuanzia, mwanamuziki, Mpiga Picha, Muongoza Picha na mtu wa editing wote wawe wanazungumza lugha moja, wakati mwingine inagharimu sana kuzalisha wazo na kufanya “Imagination to became reality”. kutoka wazo mpaka kitu kinachoonekana na mi na wewe tukakubali ni kizuri patamu hapo!!. Naongelea kutoa wazo kichwani mwako na kumfanya mtu aelewe unataka nini. Angalia Jose Chameleon na Video yake ya Kipepeo wakati akijiandaa kuishoot na ilipomalizika, Huu nidio ulimwengu wa sanaa.

Na hii ndio baada ya Shooting

Naike Binti mtanzania mwenye ndoto kubwa

Binti wa kitanzania mwenye ndoto ya kuwa super model, bado yuko gado na anaonekana kufanya vizuri ndani mji wa Knoxville, Tennessee hapa Marekani. Kwa habari na picha zaidi mtembelee Teddy Kalonga kwenye Total Knock Out

Teddy Kalonga awashauri waandaaji wa maonyesho ughaibuni

Hii ni kwa wadau wote waishio pande hizi za dunia, USA, UK, Canada, na sehemu zote ughaibuni.

Nikiwa kama mtangazaji mzoefu, ambaye nilipokuwa kazini bongo niliipenda na kuifanya kazi yangu vyema, EATV(channel 5).

Wadau, najua kumekuwa na kawaida ya kualika wasaniii kuja nje na kufanya show. Lakini tatizo siku zote ni wasanii wale wale hivyo basi kupelekea baadhi ya wadau waishio nje kutowafahamu wasanii wengine wa bongo flava ambao nao wanasifa ya kuwapa washabiki wao burudani nzuri kabisa( bila maringo). Gonga hapa uisome zaidi

Mbunifu Yves Saint Laurent afariki dunia

Yves Saint Laurent (pichani), mmoja kati ya magwiji wa mitindo katika ufaransa kwa miaka 50 sasa amefariki dunia jana jioni huko PAris Ufaransa akiwa na umri wa miaka 71.

Habari zinasema kwamba Designer huyo alianza kuumwa tangu wiki iliyopita ambapo alilazwa hospitalini Paris, habari zinazidi kupasha kwamba hali ya Laurent ilizidi kuwa mbaya kuanzia jumatano ambapo alipoteza fahamu kabisa mpaka mauti yalipomkuta jana jioni.

Laurent alikuwa na mlolongo wa bidhaa za fasheni chini ya lebo yake (pichani) kuanzia viatu, nguo, manukato, mikoba ya akina baba na akina mama, kwa ujumla amejijenga kwa ulimwengu wa fasheni, Mwenyezi Mungu Amrehemu.
kwa habari zadi gonga hapa

Kanda Bongoman (KBM) awasha moto Dublin

Kijana wa Atalaku wa KBM akighani huku KBM akionyesha mambo na vijana


Hivi karibuni mwanamuzikii wa Congo Kanda Bongo Man alifanya onyesho huko Dublin Ireland ndani ya ukumbi wa Ambassador, onyesho ambalo lilivuta sio tuu wa Congoman bali waafrica wengi wanaoishi huko na viunga vya jirani, waliohudhuria onyesho hilo wanasema lilikuwa la aina yake kuanzia mangilio, sounding, ukumbi na hata Bongoman mwenyewe alianza kwa muda na kumaliza kwa muda ulitakiwa, alianza kwa kibao chake laini cha Yesu Kristu na kumaliza na kibao matata cha Inde Monii.
Wapenzi wa Muziki najua wanamkumbuka Kanda Bongoman, kwani ni kati ya wanamuziki wa kwanza kwanza kutoka Zaire wakati huo (Congo) kufanya shoo Tanzania, Shoo ya Kanda Bongo Man kwa East Africa ilikuwa ya kufa mtu kwani ilibidi atolewe mkuku na Mzee Moi kwa watani wetu wa jadi baada ya kuambiwa kwenye maofisi nusu ya wafanyakazi kama sio robo tatu hawapo wamekwenda kumuona Kanda Bongoman. Huyo ndiye KAnda Bongoman baada ya hapo walianza kumiminika wanamuziki toka Congo kwa shoo kadhaa jijini Dar Es Salaam na wenginewalilowea (usifanye mchezo na Dar Bwana) Muulize Mayaula Mayoni hahahaha alifikia hoteli ya laki na nusu kwa siku akaja ishia guest ya 5000 kwa siku, hii ndio Bongo yenye kisima cha burudani.

Mmoja wa wacheza shoo wa KBM akiwajibika

KBM na wacheza shoo wake

Wapenzi wakipata Burudani ndani ya ukumbi wa Ambassador

Sunday, June 1, 2008

Miss Chang’ombe ndio huyooooo!!

Mshindi wa taji la Miss Chang’ombe 2008 Angela Deo Lubala (katikati) mshindi wa pili Lilian Shayo (kulia) na mshindi watatu Shadia Ally (kushoto) katika picha ya pamoja mara baada ya kutangazwa washindi kwenye shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa TCC Club Chang’ombe Temeke Jijini Dar es Salaam likishirikisha vimwana 10.
Waliokuwa washiriki wa shindano la Bongo Star Search (BSS) 2008, Maangaza Nyange (kushoto) na Rogers Lucas wakikonga nyoyo za mashabiki wakati wa fainali za kumsaka mrembo wa kitongoji cha Chang’ombe usiku wa kuamkia leo.
Picha/Habari na Global Publishers

Kitine na Majuto Jr

Jaji wa shindano la Bongo Star Search (BSS) John Kitine shoto akiwa na mpiga gita la Bass Majuto Jr wa Bendi ya Kalunde inayoongozwa na Deo Mwanambilimbi, Majuto ni mtoto wa muigizaji na mchekeshaji maarufu wa kwenye TV Majuto. Kalunde Band kila ijumaa na Jumamosi wanapiga Giraffe Ocean View Hotel

Brasil yainyuka Canada 3-2

SEATTLE – MAY 31: Robinho #11 wa Brazil akimrukia Diego #10 baada ya Diego kufunga goli katika kipindi cha kwanza cha mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Canada jana may 31 kwenye uwanja wa Qwest huko Seattle, Washington. Brazil walishinda Canada 3-2.

Brasili utawataka kwa kushangilia, Samba uwanjani mpaka kieleweke. Hii ilikuwa jana kwenye mchezo dhidi ya CANADA ilibidi wacanada wenyewe kuwakodolea macho hawa jamaa.

Gianluca Zambrotta atua AC Milan

Fullback muitaliano Gianluca Zambrotta (pichani), aliyeichezea Barcelona kwa takribani misimu miwili amejiunga na klabu ya AC Milan, imesema taarifa ya klabu hiyo bila kueleza habari za undani wa pesa za uhamisho. Kabla ya hapo timu ya Manchester ilionyesha kumtaka na walikuwa wanangoja kumalizika kwa michuano ya EURO mipango ikamilishwe.

Bekham kuongoza England leo

Kwa mara ya kwanza tangu fainali za kombe la dunia 2006 mchezaji David Bekham amepewa jukumu la kuiongoza timu yake leo watakapo kuwa wakipambana na Trinidad and Tobago.

Responsible Father



Sean “P. Diddy” Combs akiwa na watoto wake pacha D’Lila Star na Jessie James kwenye bustani ya michezo huko Beverly Hills, California.

Wakati wa Shida na Twanga Pepeta

Pata Burudani toka kwa Twanga Pepeta
video

Albam mpya ya mwanamuziki Koffi Olomide inatarajiwa kuzinduliwa June 6 huko Paris Ufaransa, Uzinduzi huo utatanguliwa na Utambulisho rasmi kwa wanahabari utakao fanyika June 5 World Press Presentation katika mgahawa wa Posh Fouquet’s restaurant, Paris. Kama kawaida Spoti na Starehe tutaleta habari na picha za uzinduzi huo.
Wakati huo huo mwanamuziki mwingine Werason Ngiama anatarajia kuzindua Albamu yake tarehe kama hiyo huko Beuxells Ubelgiji.

JB mpiana aendeleza mashambulizi Rotterdam

JB Mpiana na kundi zima la Wenge BCBG wikiend hii liliendelea na ziara yao ya Ulaya na usiku huu walipiga Rotterdam katika Concert iliyofana lakini kutonogeshwa na baadhi ya vijambo.

Ukiachilia mbali ufinyu wa stage ambao JB Mpiana aliulalamikia sana pia “hujma” na “fitna” ya kukatiwa umeme ilipunguza utamu wa onyesho hilo. Lakini wapenzi wa muziki waliofika mapema walifurahishwa na jinsi Mpangilio mzima wa onyesho ulivyokuwa kwani JB na kundi lake walipiga Non Stop nyimbo zaidi ya kumi na mbili jambo lililonogesha na kuwachengua zaidi mashabiki waliohudhuria onyesho hilo. Ukilinganisha na onyesho la Sweden au Bruxells kwa idadi ya mashabiki onyesha la jana halikuwa na mashabiki wengi ki viiile!! kwani palikuwepo na hati hati ya kutofanyika na wengi walisafiri kumuona JB Sweden na Bruxells kabla. Mdau Twaha Makau na kati ya IFM nafikiri tuko pamoja.
Papa Cherry JB Mpiana Sultan Bin adam akiwajibika jukwaani jana.

Baadhi ya wanamuziki wa Wenge BCBG wakishambulia Jukwaa ipasavyo
Mmoja wa wakongwe wa BCBG Chai Ngenge.

Mashabiki wakijinafasi

JB Mpiana Papa Cherry akimtambulisha mmoja wa mashabiki mpiga solo wa zamani wa bendi ya Chock Stars SOS Matondo.

Wapenzi wa muziki wakiwa karibu kabisa na Stage ili kuweza kuwaona Wenge BCBG

Taifa Stars yatoka Saew na Mauritius

Ilikuwa patashika Uwanja wa Taifa jana jioni lakini mashambulizi yetu yote hayakuzaa matunda. Tumepata nafasi zaidi ya 15 na kona kama 26 lakini tumetoka patupu!
Pamoja ana udhanmini wa nguvu lakini bado Stars haijakaa sawa, mpira ulikuwa bomba lakini magoli haba.
Mchezaji wa Taifa Stars Danny Mruanda akishangilia mara baada ya kupachika bao la kusawazisha,
(Picha na Mpoki Bukuku)

PAMOJA na kupata nafasi nyingi za kufunga, Stars jana ilijikuta ikishindwa kuzitumia nafasi hizo na kuambulia sare ya bao 1-1 dhidi ya Mauritius katika kampeni zake za kwanza za kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika mwaka 2010.

Mauritius ndio ilianza kuziona nyavu za Stars dakika ya 39 ya mchezo kupitia mchezaji wake Wesley Marguette kutokana na uzembe wa Salum Sued, huku kipa Ivo Mapunda akiwa nje ya goli.

Stars ilisawazisha bao hilo dakika ya 64 kupitia kwa Danny Mrwanda akiwa amepokea pasi kutoka kwa Sued.

Mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja Mkuu wa Taifa, Stars ilianza kwa kasi mchezo huo huku ikishambulia lango la Mauritus lakini ubutu wa safu ya umaliziaji ndio uliyoingusha Tanzania.

Kwa hesabu za haraka haraka Stars imepoteza kona zaidi ya 18 na penati moja kutokana na umaliziaji butu.

Sekunde ya 10 Stars ilipeleka shambuzi kali langoni mwa Mauritus, lakini ilijikuta ikipata kikwazo kutokana na ngome imara ya wapinzani hao.

Dakika moja Mrwanda alishindwa kutumia vema pasi ya Ulimboka Mwakingwe na kujikuta akikosa bao, dakika ya nne Henry Joseph alipeleka mashambulizi hayakuzaa matunda na kuambulia kona butu, huku Emmanuel Gabriel akipoteza mipira mingi ya wazi dakika ya nne alipata nafasi lakini alipaisha mpira juu.

Stars itajutia nafasi ilizopata hasa kipindi cha kwanza dakika ya 16 Henry Joseph aliachia shuti kali mita 20 lakini kipa wa Mauritius, Francois Ammomoothoo alipangua, na dakika ya 30 alikosa bao la wazi.

Dakika ya 35 mwamuzi Marange Kenias kutoka Zimbabwe alitoa penati kwa Stars baada ya Henry Joseph kufanyiwa madhambi eneo la hatari, lakini Emanuel Gabriel alikosa penati hiyo baada ya kipa wa Mauritus kuiona.

Awali Gabriel alipata penati hiyo lakini mwamuzi Kenias aliikataa na kuamuru ipingwe upya baada ya wachezaji wa Stars kuingia ndani ya penalti kabla ya filimbi kupulizwa.

Akizungumza mara baada ya mchezo huo kocha wa Taifa Stars, Marcio Maximo alisema “Kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wangu ni kizuri lakini hatujashinda, wametengeneza nafasi nyingi nzuri lakini mpira si hesabu, Mauritius nawapongeza kwa jinsi walivyofanya kazi nzuri ya kuzuia inagawa tumeonyesha kiwango kizuri na mashindanio ndio yaanaza sasa,”alisema Maximo.

24 Responses to June

  1. sellah says:

    i lyk the P.dd pic wit his babies its so luvly and he is a real responsible father.

  2. upendo mathew says:

    nyc photos and inf. i have enjoyed

  3. Awesome post, will be a daily visitor from now on!

  4. Kiyoya says:

    beautfully…!!!

  5. Considering that the medical doctor doesn’t reside daily or nightly with all the kid it is as much as the parents to become vigilant on their child’s day-to-day
    activities and behavior’s, but even more critical, what occurs to their child while sleep at evening. If your youngster has been diagnosed of ADHD, before letting them go on any sort of medication, make your self aware for the fact of their being any snoring troubles on a nightly basis or not.

  6. Hi, this weekend is pleasant in favor of me, because this point in time
    i am reading this enormous informative article here at
    my residence.

  7. Monty says:

    I hardly leave a response, but I browsed a few of the
    remarks on this page June | Spoti na Starehe.
    I do have a couple of questions for you if it’s allright. Could it be only me or do a few of these remarks come across like they are written by brain dead people? 😛 And, if you are posting at other social sites, I would like to follow everything new you have to post. Could you list of the complete urls of all your social networking sites like your twitter feed, Facebook page or linkedin profile?

  8. Cesar says:

    Infact many such casinos offer no deposit casino bonus to the players.
    Once you have released instant welcome bonus, you collect bonus money on your following deposits.
    It offers a wide selection of European rules games and a second-to-none
    array of over 50 flavors of video slots.

  9. Pam says:

    The money that these people save from not traveling can be utilized to
    increase the budget for the gambling. Players can
    always choose exactly which method they want to use and which is most convenient for them.

    The upper limit of cash, that is the cap on gambling in high stake games
    like blackjack, roulette and other games.

  10. Etsuko says:

    Everything wrote made a lot of sense. However, what about this?
    suppose you typed a catchier post title? I ain’t saying your content isn’t good.
    , however suppose you added something to possibly get people’s attention? I mean June | Spoti na Starehe is kinda boring. You should peek at Yahoo’s
    front page and note how they create post headlines to grab
    viewers to open the links. You might add a video or a pic or
    two to get readers interested about what you’ve written. In my opinion, it might bring your website a little livelier.

  11. It’s remarkable designed for me to have a website, which is useful in support of my know-how. thanks admin

  12. If you wish for to improve your knowledge only keep visiting this site and be updated with the most recent news posted here.

  13. August says:

    I don’t even know how I ended up here, but I thought this post was good. I don’t know who you are but definitely you’re going to a famous blogger if you aren’t
    already 😉 Cheers!

  14. Maria says:

    My family every time say that I am wasting my time here at web, except I know I am getting familiarity daily by reading such fastidious articles or reviews.

  15. The net vendors believed during that time the great part connected with
    personal Manhattan slots. Ultimately the ball player having a tracker however has to plan to bet, gamble, improve,
    call up, as well as crease, though the software presents them a lot of facts
    to help starting their decission in.

  16. WOW just what I was looking for. Came here by searching
    for sex cams live

  17. You will have to get into the Casino Online not any put in bonus value and
    find out exactly what it can be by yourself!
    Casino Online, one example is, has been online for many years and overall appeal is actually easy to
    understand.

  18. Wow! This could be one particular of the most useful blogs We’ve ever arrive across on this subject. Actually Wonderful. I’m also a specialist in this topic so I can understand your hard work.

  19. Thank you for your superior writeup. From the way, how could we communicate?

  20. Wonderful data, great and valuable layout, as share superior things with good tips and concepts.

  21. With everything that seems to be developing throughout this area, all your points of view are actually very exciting. Nonetheless, I appologize, because I can not subscribe to your entire theory, all be it exciting none the less. It seems to everyone that your opinions are actually not completely justified and in actuality you are generally your self not completely convinced of your argument. In any event I did appreciate reading through it.

  22. Anonymous says:

    Very well written post. It will be helpful to anybody who usess it, including yours truly :). Keep doing what you are doing – for sure i will check out more posts.

  23. Exec Leads says:

    Currently it sounds like BlogEngine is the preferred blogging platform out there right now. (from what I’ve read) Is that what you are using on your blog?

  24. Andrewflign1 says:

    Hello there 🙂
    Anybody home?

Leave a comment