Baada ya takribani nusu muongo toka watumbuize Zenith JB Mpiana na kundi lake la Wenge BCBG na Werason na kundi lake la WMMM inawezekana kwa mara ya kwanza wakapanda jukwaa moja.
kwa mujibu wa habari ambazo Spoti na Starehe imezipata kutoka kwa watu wa karibu zinasema kuwa waandalizi wapo kwenye mazungumzo ya awali kutaka kuzikutanisha bendi hizi mbili mahasimu kwenye onyesho la Zenith. Werasson na WMMM tayari wamepata VISA za Tshengen huku JB Mpiana na Vijana wake onyesho lao likiwa tayari limekubalika kufanyika na tarehe ya onyesho la BCBG ni tarehe 21 December.
“wanakubaliana kuhusu kupanda jukwaa moja kwani WMMM nao wamekubali onyesho lao liwe la kuchangia waathirika wa vita mashariki mwa Congo kama JB Mpiana” kilisema chanzo hicho. Kama hili litafanikiwa itakuwa ni ndoto ambayo mashabiki wengi walikuwa wakiisubiria. Zaidi ya mara mbili mipango ya onyesho hili linashindikana. JB Mpiana na Werasson wote kwa pamoja wana Single ziko sokoni kwa sasa na zote zinafanya uzuri, hivyo tunategemea watatupatia burudani ya kipekee.