Taarabu yazidi kuchengua
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE6Eub4yWI/AAAAAAAAAts/Ru2M86fhc3I/s400/1212145619_1web.jpg)
VINARA AWARDS 2008: COPY YAIBUKA KIDEDEA, YANYAKUA JUMLA YA TUZO SABA!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE4PlPdo9I/AAAAAAAAAtk/6ADf6YSC_v0/s400/1212210438_img_0453.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE3_LZKYJI/AAAAAAAAAtc/i5QjsQ57-W4/s400/1212210332_img_0305.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE3nDcYN7I/AAAAAAAAAtU/QLixL7be20M/s400/1212210332_img_0351.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE3T6lo0WI/AAAAAAAAAtM/xp6TxtGWFhQ/s400/1212210438_img_0403.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE21FwDu7I/AAAAAAAAAtE/oNleVORLHo8/s400/1212210438_img_0427.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE2hNpMOCI/AAAAAAAAAs8/JDfyXtFroJo/s400/1212210438_img_0471.jpg)
PICHA ZOTE: CHRISTOPHER LISA/RICHARD BUKOS/GPL)
Nyumba ya 50 Cent yaungua MOTO!!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEEh-YauEmI/AAAAAAAAAss/N-U6RAP8vsE/s400/50cent_burn.jpg)
Nyumba hiyo yenye vyumba sita vya kulala, mabafu matano, pamoja na vikorombwezo kadha wa kadha imejengwa kwenye eneo lenye ukubwa wa hekari moja, imeungua na kuteketea kabisa.
Habari zinasema moto huo wanahisi unahusiana na njama fulani lakini Mwanamuziki huyo bado hajasema kama anamhisi mtu yeyoye.
Gonga hapa kwa picha zaidi
Timu 40 za Africa zashuka dimbani leo, Taifa Stars yaikaribisha Mauritius
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEE9wPLMAQI/AAAAAAAAAt0/Uqiqs3kdQWs/s400/4.jpg)
TIMU ya soka ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars‘ leo inatarajia kushuka dimbani kuvaana na Mauritius katika mchezo kuwania tiketi ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2010 unaotarajia kufanyika Uwanja Mkuu wa Taifa, Dar es Salaam.
Taifa Stars itashuka dimbani ikiwa kamili kuikabili timu hiyo, ikiwa ni wiki moja baada ya kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na Malawi na kufungana bao 1-1.
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Mbrazili Marcio Maximo amesema timu yake ipo vizuri na ana imani watashinda leo na kujiweka vizuri katika msimamo kwa ajili ya kufuzu fainali hizo zitakazofanyika nchini Afrika Kusini.
Kwa wikiend hii tu zaidi ya timu za soka 40 toka Africa zinashuka dimbani kwa ajili ya kuwania kucheza nafasi ya fainali ya Kombe la Dunia na Kombe la Mataifa ya Africa.
Misri Vs Congo DRC
Pharaohs ya Misri (pichani juu) itawakaribiosha Simba wa Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Kongo ,Kocha wa Kongo Mbelgiji Patrice Neveu amewaita wachezaji muhimu wa kikosi chake kama Shabani Nonda na Tresor Lualua kujiunga pamoja kwa ajili ya ichuano hii. Mchezaji wa Misri na mfungaji bora wa Kombe la Mataifa ya Africa mwaka jana Mohamed Abu Traika atakosa mchezo huo wa ufunguzi kwa kuwa ni majeruhi.
Cameroon Vs Cape Verde
Timu ya Taifa ya Cameroon Indomitable Lions itawakaribisha Cape Verde, kikosi cha Cameroon kinaundwa na wachezaji chipukizi ambapo wameongeza vijana sita watakao ongozwa na kijana mwenzao Samuel Eto’o, Rigobert Song na Geremi Njitap.
Ivory Coast wakiwa ndio kwanza wamerejea toka Japan walipokwenda kucheza Kirin Cup wakiwa ni wawakilishi wa Africa kwenye michuano hiyo watakutana na Msumbiji. Mkongwe Didier Drogba anakazi kubwa ya kukiongoza kikosi hicho ambapo mchezo huu ndio mtihani mwingine kwa kocha mpya Vahid Halilhodzic wa Bosnia.
………………………………………………………………………………
Nigeria Vs Bafana Bafana
Nayo Nigeria Super Eagles ambao wameonyesha kutojali tena makocha wageni baada ya kocha Mjerumani Berti Vogts wa Germany kushindwa kuwaridhisha wapenzi wa soka kwa michuano iliyopita ya Ghana. Kwa sasa timu hiyo inafundishwa na makocha wazalendo Shaibu Amodu na mkongwe Daniel Amokachi, watakuwa na kibarua kigumu kukabiliana na waandaaji wa fainali hizo kwa mwaka 2010 timu ya Bafana bafana ya Africa Kusini.
Morocco Vs Ethiopia
Baada ya mafanikio mabovu Atlas Lions ya Morocco itawakaribisha Ethiopia kwa kile ambacho kocha wao anasema ni mchezo wa kuanza kurudisha heshima ya Morocco kwa mchezo wa soka kimataifa.
……………………………………………………………………..
Senegal Vs Algeria
Simba wa Teranga wa Senegal nao walimtosa kocha wao wa kigenibaada ya kutofanya vizuri Ghana kocha mpya Lamine Ndiaye ana kibarua kwa kukutana na timu ya Algeria.
………………………………………………………………………………
Ghana Vs Libya
Ghana wanakutana na Libya huko Kumasi Ghana. nao pia ni mtihani hasa baada ya kuaachana na kocha wao Claude Leroy.
………………………………………………………………………………
Togo Vs Zambia
Timu ya taifa ya Togo inakutana na Zambia katika tukio ambalo si la kawaida kwani watachezea Ghana katika jiji la Accra. Hii ni baada ya FIFA kuwafungia Togo kwa kufanya fujo kwa timu ya Malian.
Kolabo ya Celeo Scam na Fally Ipupa Dicap
BCBG Ndani ya Rotterdam
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEC-4InA3UI/AAAAAAAAAr0/yblEonEkE0A/s400/f_gentam_6dbcc5a.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEC-5ZYEC4I/AAAAAAAAAr8/g0LHrzkGMdI/s400/f_chaim_f11b665.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEC-9B0lIQI/AAAAAAAAAsE/lqGOW2pRObk/s400/f_450nfm_65be147.jpg)
MISS UNIVERSE TZ 2008 NI AMANDA
Mrembo Amanda Sululu(pichani) jana aliibuka mshindi katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Miss Universe Tanzania 2008. Shindano hilo lilifanyikia jana usiku katika ukumbi wa Hoteli ya Movenpick jijini Dar-es-salaam.Kwa maana hiyo Amanda ndiye anarithi taji kutoka kwa Flaviana Matata mrembo ambaye mwaka jana alifanikiwa kuiletea sifa Tanzania baada ya kufanikiwa kuwemo katika tano bora ya mashindano hayo katika ngazi ya dunia yaliyofanyikia nchini Mexico.
Tatu bora-Katikati ni Amanda Sululu,kushoto ni Jamila Nyanga(mshindi wa pili) na kulia ni Eva Babuely(mshindi wa tatu)
Mashindano ya Miss Universe mwaka huu yanatarajiwa kufanyika tarehe 14 Julai katika ukumbi uitwao Crown Convention Center(Diamond Bay Resort) mjini Nha Trang nchini Vietnam.Zaidi ya washiriki 80 kutoka nchi mbalimbali wanatarajiwa kushiriki.
Habari na picha Bongo Celebrity
Ze Comedy waibukia TBC1
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SEC4e__X5fI/AAAAAAAAArs/796mDox0WFw/s400/ze-comedybc1.jpg)
Alisema kwa sasa wameamua kuweka wazi mkataba huo, ili wapenzi wao wajue kuwa kundi lipo na sasa linaanza kazi rasmi kituo hicho walichokitangaza.
Pia alisema kundi hilo limepata mlezi mpya ambaye ni Yusuph Manji, hivyo wanaamini watafanya kazi vizuri.
Wasanii wanaounda kundi hilo ni Emanuel Mgaya ‘Masanja’, Vengu Shamba, Lucas Mhuvile ‘Joti’, Alex Chalamila ‘Mark Leagan’, Issaya Mwakilasa ‘Wakuvwanga’, Mjuni Sylvery ‘Mpoki’ na Sekion David.
Friday, May 30, 2008
Wazee wa Masauti kupamba Miss Tanga
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD-3CdQpRSI/AAAAAAAAArc/ZfKE6fXxgBg/s400/vimwana%2Bfresh.jpg)
BENDI ya Muziki wa Dansi ya Akudo Impact ya Jijini Dar es Salaam, inatarajia kutumbuiza katika mashindano ya Urembo ya Miss Tanga yanayotarajia kufanyika Juni 7 mwaka huu Mkoani humo.
Akizungumza na Mwananchi Mkurugenzi wa Kampuni ya Five Brothers Intertainment Nassor Makau alisema kuwa shindano hilo litafanyika katika Uwanja wa Mkwakwani.
Akizungumzia mashindano hayo Makau aliwataja warembo watakaoshiriki kinyang’anyiro hicho kuwa ni Doris Steven, Judith Assey, Mariam Mhando, Amina Sadick, Halima Khalfani, Aisha Abdalah, Nuru Salim na Beatrice Lwimba.
Aliwataja wengine kuwa ni Oliver Mango Mwajuma Msangi, Agnes Mwakipesile, Hadija Ramadhani, Hawa Njama, Mariamu Hajibu, Marie Frederick, Mwanamina Bausi, Silvia Urio, Samia Mohamed, Shamim Said, na Evelyine Thomas.
Makau alisema kuwa warembo hao wamepatikana kutokana katika vitongoji vya Miss Usagara, Miss Korogwe, Miss Vyuo na Miss Lushoto.
Warembo watatui watakaopatikana katika shindano ya Miss Tanga, watapata tiketi ya kushiriki Miss Tanzania mwaka huu. Mrembo anayeshikilia taji hilo ni Victoria Martin ambaye alifanya vyema katika mashindano ya Taifa mwaka jana na kuingia tano Bora.
Blanchard Deplaizir anataka “Kolabo” na Alikiba
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD-1mtQpRRI/AAAAAAAAArU/7y45b4-HqCA/s400/de_plaizir2.jpg)
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 29 anayeendeleza makamuzi huko nchini Uingereza katika jiji la Manchester ameweka wazi sana kuwa anavutiwa saaaaaana na msanii Alikiba na yuko mbioni kuangalia uwezekano wa kurekodi nae wimbo wa pamoja “nadhani nitafurahi sana iwapo nitapata nafasi ya kupiga nae mkono” alisema msanii huyo alipokuwa akifanya mahojiano na Bongo5.
Alitaja sababu zilizopelekea yeye kuvutiwa na msanii Alikiba, ni wimbo wake wa ‘cinderela’ kuanzia sauti na melody hata mpangili wa Beat vinamfanya jamaa azidi kupagawa na msanii huyu.
Wimbo wa Cinderela inasemekana uko juu sana nchini Uingereza kuliko ngoma kibao za watanzania ambazo husikika.
Msanii Alikiba ambaye yupo nchini Uingereza kwa sasa, kwa ziara maalum ya kimuziki ambapo ameshafanya maonesho kadhaa na hivi karibuni anatarajia kurejea nchini.
De Plaizir nusra achanganyikiwe baada ya kusikia msanii Alikiba amekuja nchini Uingereza kwa ajili ya maoenesho “nilipata taarifa ya ujio wa Alikiba Uk kutoka kwa meneja wangu wa Tanzania Sophia Kessy ambaye alikutana na Alikiba kabla ya kuja huku na kumtaka akutane na mimi na kupanga lolote kuhusiana na kazi za kisanii na yeye hakuwa na pingamizi, sasa nachokifanya nadhani nitahakikisha namtafuta kabla hajaondoka”
Unaweza kuona ni jinsi gani msanii De Plaizir anavyoweza kujitanga za pande hizi za bongo na afrika kwa ujumla, jitihada za kumtafuta alikiba bado zinaendelea na akipitakana tutasikia nae upande wake una lipi kuhusiana na show yake na kolabo yake na mtu mzima De Plaizir.
Bongo5
Thursday, May 29, 2008
Ali Kiba ndani ya Club Afrique – London
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD54O9QpRQI/AAAAAAAAArM/yPoYG4UPNN4/s400/k1.jpg)
Mtanange wa Taifa Stars na Mauritius
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD51FtQpRPI/AAAAAAAAArE/Tqoem42jWRc/s400/4.jpg)
Na Haki Ngowi
WENGE BCBG yawakati huo
CHELSEA yatenga Paund M80 kwa ajili ya usajili
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4whdQpROI/AAAAAAAAAq8/-HQUVmQWmDE/s400/drogba_abramovich.jpg)
“Kocha mpya lazima aelewe tunataka nini, pesa imetengwa kwa ajili ya usjili, tutasajili kutokana na mapendekezo ake pia, ila mwisho wa siku ni vikombe ndio tunataka” alisema Abramovinch
Chelsea imewataja Straika wa Valencia David Villa, Mchezaji kijana wa Barcelona Giovan Dos Santos pia wamemtaja mpachika mabao wa Inter Millan Zlatan Ibrahimovic
Celtel imejitosa kudhamini Gofu
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4t0tQpRNI/AAAAAAAAAq0/Agg7bmSYWok/s400/Close-up-of-a-Golf-Club-Hitting-a-Golf-Ball-on-a-Tee-Photographic-Print-C12478830.jpeg)
Alisema Celtel ilisaini mkataba huo na klabu ya gofu ya Lugalo ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Februari mwaka huu, ambapo jana Celtel ilikabidhi sh. milioni 7 ikiwa ni sehemu ya mkataba huo, ambao ni sh.milioni 40 kwa mwaka.
Naye nahodha wa klabu ya gofu ya Lugalo, Brigrdia Jenerali, Julius Mbilinyi, aliishukuru Celtel kwa kuokoa mashindano hayo na kuyapa nguvu ya uhakika wa kufanyika kwa miaka mitatu mfululizo.
Alisema mashindano hayo ya siku tatu yatakayokuwa wazi kwa washiriki wa ndani na nje ya nchi yanatarajiwa kuanza kesho na yanatambuliwa na Shirikisho la Gofu Tanzania (TGU) na yanatarajia kushirikisha wachezaji 150 kutoka nchi mbalimbali duniani.
Alisema kwa udhamini huo wa Celtel, klabu hiyo ya Lugalo imeweza kumwagilia maji kwenye uwanja utakaotumika na kuupa hadhi ya kimataifa na kutoa zawadi bora kwa washindi, ambazo zitahusisha vikombe na fedha taslimu na pia kuboresha miundombinu mingine uwanjani hapo.
Serikali ya China yasimamisha burudani kwa siku 3 kuomboleza
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4c4NQpRKI/AAAAAAAAAqc/UkGyKfTkUuM/s400/166px-YaoMingonoffense2.jpg)
AFP/Shanghai
Television nchini China zilisimamisha kwa muda kutangaza aina yeyote ya michezo na burudani kwa siku tatu mfululizo ikiwa ni ishara ya kuomboleza walikufa kwa tetemeko ambalo limegharimu maisha ya maelfu ya watu nchini humu siku za karibuni.
Pamoja na machungu ya kupotelewa na ndugu jamaa na marafiki bado wachina walilalamika kwa idara husika na kuomba walao mechi za NBA pekee ziruhusiwe. Kwa kuonyesha mchezo huu ni maarufu kwa sasa NBA wamefungua ofisi China ambayo pamoja na mambo mengine inaratibu shughuli zote za kibiashara ikiwa ni mauzo ya Jezi, usimamizi wa Matangazo ya biashara na mikataba kwani kwa sasa kampuni za huko zinatangaza zaidi kwenye ligi hiyo.
Wimbo wa Taifa
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4Y0dQpRJI/AAAAAAAAAqU/yIETtG45ZlQ/s400/capt.e0f0c1cfd87b4843b07cc09013ed642c.britain_us_soccer_lmd138.jpg)
BASATA wachimba mkwara kuzifungia FM Academia, TOT Respect na Akudo Impact
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4WsNQpRGI/AAAAAAAAAp8/-lj8RJluwYw/s400/pp.jpg)
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) limetishia kuzifungia bendi za FM Academia, TOT Respect na Akudo Impact kwa maelezo kuwa wanenguaji wake kuvaa vichupi wawapo jukwaani.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na BASATA kwenda kwa Wakurugenzi wa bendi hizo yenye tarehe ya juzi na kusainiwa na F.Magoti kwa niaba ya Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, ilieleza kuwa katika siku za karibuni bendi hizo zimekuwa zikifanya maonesho ya muziki yanayoambatana na wanenguaji wa kike waliovaa ‘vichupi’.
Barua hiyo ilieleza kuwa kitendo hichoo ni ukiukwaji wa maadili ya Watanzania na ni kuwdhalilisha wanenguaji na watazamaji wanaohudhuria maonesho ya bendi hizo.
“Kwa barua hii Baraza la Sanaa la Taifa linawapa onyo kali kuacha kabisa vitendo hivyo na kuhakikisha kuwa wanenguaji wenu wanavaa nguo za heshima zisizoonesha kwa namna yeyote ‘vichupi’ hadharani.
” Baraza halitasita kuchukua hatua ikiwemo ya kufungia bendi zenu, ikithibitika kuwa mnaendelea na ukiukwaji huo,” ilisema sehemu ya barua hiyo.
Alizitaka bendi hizo kukumbuka kuwa maonesho yao hayaishii katika kumbi za burudani pekee, bali yamekuwa yakiharibu kwa kuwaonesha watoto wadogo kupitia vyombo vya habari kama vile magazeti na televisheni.
“Tukiamini kuwa lengo letu ni kuonesha umahiri na ustadi wa muziki wa bendi zetu, basi suala la kuonesha ‘vichupi’ halitajitokeza katika bendi zenu, “ilisema barua hiyo.
Nakala ya barua hiyo imepelekwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni na Maofisa Utamaduni wa Wilaya za Temeke, Kinondoni na Ilala.
Bekham na kofia ya dhahabu
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4T1NQpRFI/AAAAAAAAAp0/O1-N0AzMTz4/s400/c771c342d650e1fd6abf97b9b8f1d6c0-getty-80943892mt013_england_v_usa.jpg)
ENGLAND yaichapa USA 2-0
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4Qi9QpRAI/AAAAAAAAApM/fvnipKvbfiI/s400/1212006757.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4QjNQpRBI/AAAAAAAAApU/_JPilyKuCQs/s400/26b84c7458a5d9c11d1e57ece9dd6901-getty-fbl-eng-usa-friendly.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4QjdQpRCI/AAAAAAAAApc/z3tfZOOwD3c/s400/capt.cps.moh16.280508235902.photo03.photo.default-512x329.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SD4QjdQpRDI/AAAAAAAAApk/TFiiL0GzDN0/s400/capt.cps.moh06.280508234436.photo00.photo.default-435x512.jpg)
LONDON (AFP) –
John Terry aliweka pembeni machungu ya Champions League na kuisaidia timu yake ya taifa ya England kushinda dhidi ya timu ya taifa ya USA katika mchezo wa kirafiki uliochezwa jana.
Krosi ya David Bekham ndio iliyozaa goli la Terry mwishonbi mwa kipindi cha kwanza ambapo England hawakuonyesha machchari ki viiile.
Gareth Barry Stephen aliingizwa na kocha Cappelo ili kuongeza nguvu na kusaidiana na Steven Gerrard aliyepachika bao la pili.
Nafasi pekee ambayo USA waliipata ya wazi ni pale Eddie Johnson mpira wake ulipogonga besela kwani walikuwa na wakati mgumu wakishambuliwa sana hasa kipindi cha pili.
Mechi ya jana ilikuwa muhimu kwa Terry kupachika bao kwanza kama Kepteni kwa wakati mwingine chini ya kocha Capello na pili ni kufuta machungu ya kukosa penati siku saba zilizopita kwenye mechi ya Champions Ligi dhidi ya Manchester United.
Kocha Fabio Capello alisema ni “nafasi pekee ya kumsaidia kisaikolojia vinginevyo angeona hatuna imani naye, penati ni 50 kwa 50, lakini tabia ya waingereza hawaoni ni kwa nini ukose penati, kipa anasamehewa kwa kufungwa penati lakini sio mpigaji” alisema Capello.
Kwangu mimi kama kocha naelewa ni nusu nusu lakini wapenzi wa huku hata kwa maoni yao hawaoni ni kwa nini ukose penati aliongeza Capello huku akicheka.
Hapakuwa na idadi kubw ya watu kama ilivyotarajiwa kwani baadhi ya viti vilikuwa wazi hasa upande mwekundu kwa kile kilichooelezwa ni “Low profile match” na mashabiki.
Wednesday, May 28, 2008
John Terry kuongoza kikosi cha England dhidi ya USA
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDzMH9QpQ_I/AAAAAAAAApE/4ulCazd6F9E/s400/JohnTerry_1280x1024.jpg)
Terry amepewa heshma hiyo ikiwa ni utaratibu wa sasa wa kubadilishana kabla ya kuteuliwa mchezaji mmoja kuongoza hilo jahazi kwa kipindi chote.
Capello amesema kuwa anatumai kumpa Terry ukepten ni kuonyesha imani yake kwake na kumfanya aone kuwa bado tunaimani naye hasa baada ya kukosa penalti dhidi ya manchester jambo ambalo Terry linamuuma sana na hataki kamwe kukumbushwa hilo, “nafikiri ataichukulia ile kama changamoto aweze kuonyesha umma kuwa kosa ni kurudia kosa” alisema Capello. Mchezo wa leo n wa kirafiki baina ya England na USA lakini kila mtu katika mataifa hayo mawili amekuwa akiuzungumzia.
Barcelona yamchukua Gerald Pique wa Manchester
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDzIedQpQ-I/AAAAAAAAAo8/sDlXiZJVOFA/s400/_44672119_pique_get_203body.jpg)
Mchezaji huyo mwenye miaka 21 alijiunga na klabu ya Manchester mwaka 2004 lakini alikuwwa hapangwei mara kwa mara kwenye kikosi cha kwanza cha Manchester kwani tangu aingie amecheza mechi 23 tuu na kufunga magoli mawili pekee dhidi ya Dynamo Kiev na Roma. Kocha wa Barcelona amesema anamjua Pique na combination ya mpira anayocheza ndio maana hakuweza kupata mafanikio Manchester na kusema ana hakika atafanya vizuri kwa combination aliyonayo Barcelona.
ESPN May 2008.
Liverpool yaichimbia mkwara Chelsea kuhusu Torres
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDzGZNQpQ9I/AAAAAAAAAo0/7YSMFlkWvKU/s400/Fernando_Torres_narrowweb__300x416,0.jpg)
Chelsea inasemekana kuweka nguvu nyingi sana katika kumuwania kumchukua Torres hasa baada ya mchezaji huyo kumaliza msimu huu kwa mafanikio makubwa.
Chelsea walikuwa wameahidi kutoa kitika cha paund milioni 50 kwa klabu ya Liverpool kwa ajili ya kumuchukua nyota huyo wa zamani wa Atletico Madrid lakini Liverpool imekataa ofa hiyo kwa kusema kuwa bado wanamuhitaji ila kama Chelsea wana mchezaji mwenye kiwango cha Toress wao Liverpool wangemtaka pia.alisema Rafa Benitez.
Ufaransa mbabe kwa Ecuado
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDzDBtQpQ8I/AAAAAAAAAos/ABYNSPLh2ZQ/s400/capt.a70777fc40664477a806bbeebbd50b41.france_soccer_ecuador_meu110.jpg)
Mchezaji wa Ufaransa Hatem Ben Arfa, shoto, akisakata goma kumtoka mchezaji wa Ecuado Isaac Mina, wakati wa mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu dhidi ya timu hizo mchezo uliofanyika huko Alps stadium, Grenoble Ufaransa, jana jumanne, May 27, 2008. Ufaransa ilishinda 2 – 0. Ufaransa ilitumia mechi hii ya mwisho ya majaribio ili kuchagua kikosi chake cha watu 23 kwa ajili ya michuano ya EURO 2008, kwa sasa kikosi kina wachezaji 30.
Austria 1-1 na Nigeria mechi ya kirafiki
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDzAndQpQ6I/AAAAAAAAAoc/xz3EIcED0Ao/s400/capt.cps.moa25.280508002800.photo00.photo.default-512x401.jpg)
Tuesday, May 27, 2008
Fally kuwasha moto Ufaransa
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDxeydQpQ5I/AAAAAAAAAoU/0PIPTgTOteI/s400/fally3.jpg)
Ferre Gora atimuliwa ulaya kwa kudanganya VISA!
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDxZ-tQpQ4I/AAAAAAAAAoM/hLaGDnd8yBE/s400/u1_ferre.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDxZa9QpQ2I/AAAAAAAAAn8/uBI6S2KMb1c/s400/f_110508m_e9981a2.jpg)
Pichani ni baadhi ya matangazo ya maonyesho ya Ferre
Nani kumrith Grant Chelsea?
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDwdt9QpQ1I/AAAAAAAAAn0/lhPtDEEsaDk/s400/grant.jpg)
Kutokana na hali hiyo magezeti ya Uingereza tangu Jumapili yalikuwa yamejaa tetesi mbalimbali juu ya atakayekabidhiwa funguo na mmiliki wa timu hiyo Roman Abramovich kitendawili ambacho bado kinasumbua vichwa mashabiki wa Ligi Kuu hadi utakapokuwa umefikiwa uamuzi.
Kocha anayepewa nafasi kubwa kuchukua mikoba hiyo ni Frank Rijkaard, ambaye naye alifungashiwa vilago na timu ya Barcelona mara tu baada ya Grant kutimuliwa.
Rijkaard alitimuliwa katika nafasi yake baada ya klabu hiyo ya Catalan kukosa ubingwa msimu huu ikiwa ni mara ya pili mfululizo, lakini hata hivyo kocha huyo bado anaaminika ndiye kocha bora katika klabu kubwa duniani, hali ambayo inamfanya apewe nafasi kubwa kuinoa Chelsea.
Kocha mwingine ambaye ametajwa na vyombo vya habari vya Uingereza ni Guus Hiddink, ambaye anapewa nafasi hiyo kutokana na kuonesha ni kocha mzuri kufuatia mafanikio aliyoyaonesha katika kazi yake ya sasa ya kuinoa timu ya taifa ya Urusi, ambayo mshahara wake analipwa na mmiliki wa Chelsea, Abramovich.
Mbali na hayo pia kocha huyo ni rafiki wa karibu wa Abramovich na hivi sasa Hiddink tayari amekubali kwa masharti kuinoa timu ya taifa ya Urusi.
Makocha wengine ambao wanapewa nafasi hiyo ni Roberto Mancini, ingawa kocha huyo anapewa nafasi kama Rijkaard na Hiddink wataikataa nafasi hiyo wao wenyewe.
Pia kyumo Sven-Goran Eriksson ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akimvutia Abramovich na mara mbili kocha huyo amewahi kukutaa kuifundisha Chelsea .
Kocha huyo aliwahi kunaswa na kamera akifanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Chelsea, Peter Kenyon wakati alipokuwa bado Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya England na hivi sasa anakaribia kuwa huru baada ya mmiliki wa Manchester City, Thaksin Shinawatra kumtema.
Mark Hughes naye pia ni miongoni mwa kundi hilo, ambapo Hughes anapewa nafasi hiyo, baada ya kuifanya Blackburn Rovers kuwa moja ya timu ngumu msimu huu, hali iliyoifanya kumaliza msimu huu ikiwa nyuma ya timu nne za mwanzo.
Hughes vilevile ana uzoefu na timu za taifa baada ya kuiongoza Wales kutinga katika michuano ya fainali za mataifa ya Ulaya mwaka 2004 na pia amewahi kuichezea Chelsea hadi alipotundika daruga.
Mwingine ni aliyekuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho, ambaye alikuwa kipenzi cha mashabiki wa timu hiyo ya Stamford Bridge na baada ya kuondoka mwezi Septemba mwaka jana uhusiano na Abramovich unaonekana kuwa mzuri.
Uhusiano huo ulidhihirika baada ya Mrusi huyo kumnunulia Mourinho gari aina ya Ferrari yenye thamani ya dola milioni 4 mwaka huu kama zawadi.
Na Majira
Picha zaidi za shoo ya BCBG
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtYSdQpQtI/AAAAAAAAAm0/bqvhhhupcrg/s400/m35.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtYStQpQuI/AAAAAAAAAm8/CuyXcclTI4I/s400/m41.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtYS9QpQwI/AAAAAAAAAnM/t8Y_JO2HckE/s400/m53.jpg)
Elodie Lipassa
Genta
Rio
JDL
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtXYdQpQqI/AAAAAAAAAmc/N9cl-5J-kRo/s400/m20.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtXINQpQpI/AAAAAAAAAmU/ggV9v9COGBk/s400/m13.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtaQ9QpQzI/AAAAAAAAAnk/tlHK52dHyow/s400/m56.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDtYY9QpQxI/AAAAAAAAAnU/UJNHAp-S7AQ/s400/m57.jpg)
Monday, May 26, 2008
Marina Bay: Mahali pa maraha Singapore
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDr_hNQpQlI/AAAAAAAAAl0/hiCb48p4LuM/s400/CliffordPier.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDr_h9QpQnI/AAAAAAAAAmE/y6VYgY63_i4/s400/singapore+flyer+1.jpg)
Reuters – Pictures of the Year 2007
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDr6KdQpQkI/AAAAAAAAAls/4U8YC53X1n8/s400/54_RTR1OKJS.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDr34NQpQiI/AAAAAAAAAlc/92Rn9JzIq4A/s400/28_RTR1MITG.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDr34dQpQjI/AAAAAAAAAlk/hl_T2pDC_GY/s400/93_RTR1T49L.jpg)
Miss Tanzania Europe 2008
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDrvdNQpQhI/AAAAAAAAAlU/DKod2PbIM6g/s400/chukua%252Bshengen.jpg)
“Schengen-Agreement”.
Na Haki Ngowi
Taifa Stars yatoka Sare ya 1-1 na Malawi
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDoSp9QpQgI/AAAAAAAAAlM/YZCjZ5x1lyc/s400/taifa_stars.jpg)
TIMU ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ na ile ya Malawi jana zilifungana bao 1-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika Uwanja Mkuu mpya wa Taifa, Dar es Salaam.
Maelfu ya mashabiki wa Taifa Stars iliwabidi wasubiri hadi dakika ya 79 kushangilia bao la kusawazisha lililofungwa na Salum Sued baada ya kutokea kizaazaa katika lango la Wamalawi.
Kabla ya bao hilo Stars ilifanya mashambulizi mengi langoni kwa Malawi, lakini umaliziaji haukuwa mzuri, huku washambuliaji Mrisho Ngassa, Danny Mrwanda, Emmanuel Gabriel kwa nyakati tofauti wakikosa nafasi nyingi za ushindi.
Iliwachukua dakika tano Stars tangu kuanza mchezo kwa kubisha hodi langoni mwa Malawi, baada ya Gabriel kukosa bao akiwa amebaki na kipa wa Malawi, kabla mpira haujaokolewa.
Stars ilizidisha mashambulizi, ambapo dakika ya 14 Mrisho Ngassa kidogo afunge, wakati shuti lake lilipookolewa na kipa Valence Kamzere.
Malawi nayo ilijipanga na kufanya mashambulizi ya kushtukiza, lakini nayo pia umaliziaji ulikuwa dhaifu, huku ngome ya Stars ikiondoa baadhi ya hatari.
Bao la Malawi lilifungwa dakika 54 na Essau Kanyenda aliyeunganisha vyema mpira kutoka wingi ya kushoto, huku mabeki wa Stars wakiwa wamezubaa.
Nafasi ambayo Stars itaijutia zaidi ni ile ya dakika ya 86 wakati shuti la Nadir Haroub ‘Cannavaro’ lilipogonga mwamba na mpira kurudi uwanjani, lakini mchezaji huyo alipigwa na butwaa huku akinyoosha mikono kushangilia, akijua tayari mpira ulitinga wavuni.
Wachezaji Nizar Khalfan na Godfry Bonny nao kwa nyakati tofauti walipiga mashuti langoni kwa Malawi na kutia matumaini.
Habari na Majira, picha na Global Publishers
Sunday, May 25, 2008
Photo Baraza na utani kwa picha.
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmW6NQpQcI/AAAAAAAAAks/oYPKHEObXeE/s400/kombelaluka.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmW6NQpQdI/AAAAAAAAAk0/oV9wtUfSZk0/s400/kuwamuhangalifu.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmW6NQpQeI/AAAAAAAAAk8/7KIeQAT676A/s400/mzeewautelezi.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmW6dQpQfI/AAAAAAAAAlE/dtF2pZmNm4I/s400/vidic.jpg)
Bwana wee, furaha haina mwisho atii
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmWhNQpQbI/AAAAAAAAAkk/SSUOT1QQZA4/s400/bingwa.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDmSI9QpQaI/AAAAAAAAAkc/qxpSeuXdRu4/s400/vikombetu.jpg)
BOB Wine-From Zero to Hero
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDkxPNQpQYI/AAAAAAAAAkM/MSWkyiAGuDY/s400/Untitled-12.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDkxPdQpQZI/AAAAAAAAAkU/q00z0hMrBMo/s400/Untitled-1.jpg)
Mr & Miss East Africa, ha ha haa Habari ndiyo hiyooo!
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDjWbNQpQTI/AAAAAAAAAjU/OBSRfo-C2x4/s400/flyer-2008c.jpg)
Kwa mengi zaidi Bofya hapa. Pia waweza tembelea gazeti lao linalopatikana online, pichani chini ni moja ya picha zilizomo kwenye Issue Mpya ya Gazeti hilo
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDjWOtQpQOI/AAAAAAAAAis/NKnxT300IF4/s400/4.jpg)
Blanchard De Plaizir Nyota mpya katika Muziki wa Congo
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDjPBNQpQMI/AAAAAAAAAic/-R8bBqaCXT4/s400/home.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDjQ89QpQNI/AAAAAAAAAik/8G-RgtcZksY/s400/deplaizir.jpg)
Blanchard anaishi Manchester Uingereza, alizaliwa Congo lakini alihamia Uingereza akiwa na umri mdogo ila anasema nia yake ni kuuendelez utamaduni wake hata kama yuko nje ya nchi yake. Katika albamu yake hii Blanchard amemshirikisha aliyekuwa mpiga Gitaa mahiri wa BCBG Burkina Faso Mboka lia. (utamsikia vizuri kwenye Albamu ya Pentagone)
Kwa sasa shughuli za kimuziki za Blanchard kwa East Africa zinaratibiwa na Meneja wake Mtanzania akiwa ni mtangazaji wa Radio ya Clouds FM Sophia Kessy ndiye anayeratibu shughuli za Blanchard na kwa sasa anamuandalia safari ya kuitambulisha Albamu yake ya kwanza nchini Tanzania.
Vichapo vya Man U vyaotesha nyasi “chibarua” cha Grant Chelsea.
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDjAw9QpQLI/AAAAAAAAAiU/dHfkFpxfU-4/s400/1211658545.jpg)
“Chelsea inathibitisha kwamba mkataba wa kocha Avram Grant umevunjwa rasmi toka leo, hii inafuatia majadiliano ya siku mbili ndani ya klabu. Kila mmoja katika klabu ya Chelsea FC anampongeza na kumshukuru Grant kwa kuwa Manager wa timu hii tangu mwezi Septermber mwaka jana.”
Kwa sasa tunaegemeza nguvu zetu katika kusaka kocha mpya, hakuna lolote litasemwa mpaka uamuzi ufanyike,
Grant aliichukua timu hiyo toka kwa Jose Mourinho mwezi September mwaka jana, Grant hakuwahi kuiongoza timu yeyote katika Uingereza alitakiwa kuchukua mikoba na baadaye angepewa mkataba wa miaka minne kama timu ingefanya vizuri.
Hebu fikiria kama wamefika Fainali na mambo ndio hayo, je sie tunatolewa hatua za awali wa kwetu si ndio wasingekaa kabisa!!!.
Lyon mabingwa wa Ufaransa
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDi9Q9QpQKI/AAAAAAAAAiM/mqB1-luL5Bk/s400/capt.6ece3ff88e194df696a9d6b34356efe4.france_soccer_french_cup_final_xtc104.jpg)
Stars, Malawi leo, Mtihani mwingine kwa Maximo
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDi7q9QpQJI/AAAAAAAAAiE/mDKQ4RxCGYg/s400/taifa-stars-01bc.jpg)
Ni wazi kuwa yeyote atakayepangwa kati ya wachezaji hawa Fredy Mbuna, Shadrack Nsajigwa, Amir Maftah, Stephano Mwasika, Juma Jabu, Salum Swed, Nadir Haroub na Kelvin Yondani atakuwa na uwezo mkubwa wa kuimarisha safu ya ulinzi ya timu hiyo.
Pia katika safu ya kiugo yeyote kati ya hawa watawaunganisha vyema wenzao, ambao ni Geofrey Bonny, Athuman Iddy, Adam Kingwande, Kigi Makassy, Shaaban Nditi na Nizar Khalfan.
Tumaini la ushambuliaji litakuwa kwa Ulimboka Mwakingwe, Jerson Tegete, Uhuru Seleman, Mrisho Ngasa na Emmnauel Gabriel.
Hadi sasa Taifa Stars imecheza michezo nane ya kimataifa ya kirafiki chini ya Marcio Maximo tangu aanze kibarua hicho karibu miezi 19 iliyopita.
Katika michezo hiyo Taifa Stars imeshinda mitatu dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Uganda na Zambia na kutoka sare mara nne dhidi ya Kenya, Angola, Zambia na Uganda na kufungwa na Yemen.
Source: Majira
Ilala bingwa Taifa Cup
Kwa ushindi huo Ilala licha ya kutwaa kombe pia ilizawadiwa sh. milioni 30 na medali kwa wachezaji wote, wakati Kinondoni ilizawadiwa medali na sh.milioni 15.
Dalili kwamba Ilala ingetwaa ubingwa zilianza kujionesha dakika ya 8 mfungaji akiwa Mussa Hassan ‘Mgosi’ akiunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Matangalu Anthony.
Bao la pili lilifungwa dakika ya 43 na Mohammed Kijuso akitumia vyema pasi ya Athumani Machupa aliyeingia badala ya Mgosi aliyeumia.
Kijuso alifunga bao la tatu dakika ya 50 akiunganisha krosi ya Mohammed Banka na kuongeza la nne dakika dakika kumi baadaye kwa pasi ya Salum Kanoni, kabla ya Ramadhani Chombo kufunga bao la tano dakika ya 85.
Kinondoni iliyoingia fainali kwa kuitoa Mbeya kwa mabao 2-0 katika nusu fainali, haikuonesha cheche zozote kiasi cha muda mwingi mpira kuchezwa langoni mwao na hivyo kumpa nafasi kipa Juma Kaseja kupumzika.
Katika michuano hiyo iliyoshirikisha mikoa 23 ya kimpira, Juma Kaseja alitangazwa kipa bora, wakati kocha bora ni Madaraka Bendera wa Arusha na timu yenye nidhamu pia ikiwa Arusha, huku Mussa Mgosi akiibuka mfungaji bora baada ya kupachika mabao 8 wavuni. Wote walizawadiwa sh. milioni 2 kila mmoja.
Katika mchezo wa mapema jana, timu ya Mbeya iliifunga Arusha mabao 4-3 katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu, hivyo Mbeya kuikwaa nafasi hiyo na kuzawadiwa sh. milioni 7.5 kutoka kwa wadhamini wa mashindano hayo Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Source:Majira
Tyson anakuja “Bongo”
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDi5HNQpQII/AAAAAAAAAh8/1zBDsC9grPM/s400/2774426_550_art_R0.jpg)
BINGWA wa zamani wa ndondi katika uzito wa juu duniani, Iron Mike Tyson, anatarajiwa kutua nchini Septemba mwaka huu akiambatana na bondia Laila Ali, ambaye ni binti wa nguli wa masumbwi duniani, Muhammed Ali.
Akizungumza katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), jijini Dar es Salaam jana, mratibu wa ujio huo, Zuwena Kibene, alisema mabondia hao wanakuja kwa mwaliko rasmi wa kutoa semina kwa mabondia wa Tanzania.
Alisema, kutokana na ujio huo, anatarajia kuanza ziara ya kuzunguka nchi nzima ili kuhamasisha mabondia kufika katika mikoa ya jirani ambako wageni hao wataifikia.
Kibene aliitaja mikoa ambayo mabondia hao wataifikia, ni Dar es Salaam, Arusha na Mwanza, hivyo amewataka mabondia wa jirani na mikoa hiyo, kufika katika mikoa hiyo kwa gharama zao.
Alisema, mabondia watakaokuwa wakitoka nje ya mikoa hiyo, watajigharamia usafiri, huku yeye (Kibena), akigharamia malazi, chakula na nauli za kurejea makwao.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDi4_tQpQHI/AAAAAAAAAh0/0c-9BR_oBd4/s400/lailaali.jpg)
Alipoulizwa kama mabondia hao watacheza pambano lolote, alisema hawatacheza pambano lolote kwani hakuna anayeweza kupambana nao.
Alisema, kitakachofanyika ni mabondia hao kutoa mafunzo kabla ya kushuhudia mapambano ya mabondia mbalimbali wa hapa nchini.
Tyson, mbabe aliyetamba vilivyo katika ulimwengu wa masumbwi duniani, ni miongoni mwa mabondia walio na mashabiki wengi kutokana na umahiri na vituko vyake.
Miongoni mwa kituko kinachokumbukwa, ni pale alipomng’ata sikio bondia mwenzake, Evander Hollyfield katika kuwania ubingwa wa dunia.
Source: Tanzania Daima
Saturday, May 24, 2008
Miss Tabata
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDhWMNQpQEI/AAAAAAAAAhc/xdHzc4ooevw/s400/3631.jpg)
soma zaidi kwa Haki
Lionel Messi
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDi0U9QpQFI/AAAAAAAAAhk/9zhsVVNULjQ/s400/messi-wallpapers.jpg)
Sweta la 50 Cent lilipoleta kizaazaa.
Kwa video zaidi za Msanii huyo ndani ya bongo Bongo5.com hapa
England Vs USA, Mtihani mwingine kwa Capello
![](https://i0.wp.com/njmg.typepad.com/photos/uncategorized/2007/12/14/fabio_capello_ap.jpg)
Kocha mpya Fabio Capello (pichani) anakibarua kigumu kuwahakikishia na kuwarudishia waingereza matumaini na timu yao hassa baada ya kuchapwa kwenye mchezo wao wa kirafiki na Ufaransa jambo ambalo lilileta kelele toka kwa mashabiki wa soka wa Uingereza na kuamsha hisia kuwa wachezaji wa kigeni wanachangia kuharibu soka la Uingereza kwa timu zinakuwa zinawategemea wao zaidi kuliko kukuza vijana kwa ajili ya Taifa lao. Hii ni nafasi nzuri kwa Capello kama watashinda itampa milege na kumjengea heshima kwa waingereza ambao wanaona timu yao ikifanya vibaya mfululizo. Mara ya mwisho mwaka 1994 walipokutana England waliichapa USA mabao 2-0 yaliyofungwa na Alan Shearer.
Pool hadi Mlimba!
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDfdadQpQCI/AAAAAAAAAhM/sUoVXg1MoVc/s400/SSL20802.jpg)
Laiti kamaaa……!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDfY4NQpP_I/AAAAAAAAAg0/KIhSxU1wnRs/s400/Pix%2B1.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDfY4dQpQAI/AAAAAAAAAg8/z-gyp1nWHJA/s400/sports3.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDfY4tQpQBI/AAAAAAAAAhE/CcgbeUolnmY/s400/spotistaa_2007091109311945574.jpg)
Serikali/TFF yaunda Kamati kusimamia Uwanja wa Taifa
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDfXUNQpP-I/AAAAAAAAAgs/FNE8xHM952U/s400/state-stadium_tanzania_fs.jpg)
Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela, alisema kamati hiyo itaongozwa na Mwenyekiti wake Kijazi Mtengwa ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo, chini ya Katibu Mkuu wake Lawrance Mkwaji ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa wizara hiyo.
Mwakalebela alisema kamati hiyo pia itakuwa na wajumbe ambao watakuwa wenyeviti katika kamati ndogo ndogo zitakazosimamia shughuli hiyo.
Aliwataja kuwa ni Tido Mhando (Habari, itifaki na uelimishaji), Leodger Tenga (Ufundi na matumizi ya uwanja), Aloyce Mushi (mtaalamu wa uwanja), Alfred Tibaigana (Ulinzi na usalama) na Laison Mwanjisi (fedha).
Na Majira
Tibaigana achimba mkwara Polisi kuingiza “Dezo” Taifa mechi za Stars
![](https://i0.wp.com/www.blog.co.tz/uploads/m/Mroki/2482.jpg)
Tibaigana ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Taifa ya kusimamia uwanja wa Taifa na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, alisema wanajeshi si masikini wa kutaka kila mara kuingia mpirani dezo, hivyo amewataka kuchangia timu yao ya Taifa kwa kulipa kiingilio.
Alisema mechi ya pili ambayo Stars itacheza na Maritius, Jumamosi ijayo pia kutakuwa na ulinzi wa kutosha na kuagiza kuwa magari yatakaoruhusiwa kuingia ni yale yaliyokatiwa tiketi za kuingia uwanjani.
Na Majira
Friday, May 23, 2008
Kung Fu Panda, Filamu ya Vikatuni iliyoshirikisha Magwiji wa Filamu
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbwINQpP9I/AAAAAAAAAgk/8k4nuTDsQaY/s400/kung_fu_panda.jpg)
Katika picha hii sauti za vinara wa Sinema zimetumika kama Jack Black, Seth Rogen, David Cross, Jackie Chan, Dustin Hoffman, Angelina Jolie na Lucy Liu. kama wanavyoonekana hapo chini. kwa habari zaidi Bofya hapa.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbvONQpP8I/AAAAAAAAAgc/GkOfJkyWqFk/s400/002509570046.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbuAtQpP3I/AAAAAAAAAf0/xkTGdvF0Vd8/s400/002508741571.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbuA9QpP4I/AAAAAAAAAf8/fXv_c9BB1NA/s400/002508741585.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbuBNQpP6I/AAAAAAAAAgM/kNQF3ez2wQo/s400/002508741669.jpg)
Wakutanapo Celebrities wa Sinema
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDboutQpPyI/AAAAAAAAAfM/tqlOTV5ONh4/s400/002509068090.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbou9QpPzI/AAAAAAAAAfU/89TOwPE9Scs/s400/002508239441.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbovdQpP0I/AAAAAAAAAfc/I9A9YpMVvAM/s400/002508239731.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbovdQpP1I/AAAAAAAAAfk/fctHLgr4Pc0/s400/002511990864.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDbovtQpP2I/AAAAAAAAAfs/kZu6JWk3IVA/s400/002508239815.jpg)
Marcio Maximo!
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDa20NQpPxI/AAAAAAAAAfE/SAOVXHCRf6w/s400/1306%5B1%5D.jpg)
Kuchaguliwa kwake kumefuatia ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Jakaya Kikwete kuhakikisha anaboresha sekta ya michezo kwa kuanzia na mpira wa miguu.
Amewahi kuifundindisha Livingston Football Club huko Scotland mwaka 2003/2004. Pia ni mwanachama wa Chama cha makocha cha Brazil’s .
Kwa mujibu wa wikipedia.
Yanga kuwakosa Chuji, Cannavaro
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/42775000/jpg/_42775921_chaabani.mouin203.jpg)
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa juma lililopita jijini Dar es Salaam, Cannavaro (pichani jezi kijani) alisema kuna mtu ambaye anashughulikia mipango yake ya kwenda kufanya majaribio nchini humo na kama mambo yatakamilika ataondoka hivi karibuni.
Alisema amefikia hatua hiyo kutokana na kuliangalia zaidi soka la kulipwa baada ya kwenda mara ya kwanza na Timu ya Taifa ya Zanzibar na kufanya majaribio na baadhi ya timu lakini kipindi hicho hakubahatika kupata soko kwa sababu hakuwa katika kiwango cha juu kama ilivyo sasa.
“Nategemea kwenda tena Ujerumani kufanya majaribio na nikifanikiwa nitacheza huko, kuna mtu anasimamia kila kitu na amefikia hatua nzuri kwa sasa, awali nilifanya lakini sikufikia kiwango kilichokuwa kinahitajika,” alisema Cannavaro.
Mlinzi huyo wa kati aliyeitumikia Yanga kwa misimu miwili sasa, amesema ana uhakika mkubwa wa kupata timu nchini Ujerumani kwani kiwango chake kimeimarika kuliko ilivyokuwa awali.
Aidha Cannavaro aliweka bayana kuwa, kwa sasa hana mkataba na Yanga baada ya ule wa awali kumalizika pindi Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ilipofikia ukingoni mwezi uliopita.
“Kama Yanga wakinihitaji kwa msimu ujao, nitasaini kuichezea, lakini mambo yangu yatakapokamilika muda wowote nitaondoka kwenda kusaka maisha mapya nchini Ujerumani,” alisema mlinzi huyo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa chanzo chetu kilichopo ndani ya uongozi wa Yanga, kilitueleza kwamba, piga ua lazima beki wa Simba Kelvin Yondan arithi mikoba ya Cannavaro endapo ataondoka.
“Ni kweli kuna uwezekano wa kumkosa Cannavaro endapo mipango yake itakamilika mapema, lakini hilo hatuna wasiwasi nalo kwani Yondan anatua Yanga kwa milioni 18, kwa ajili ya kuziba pengo hilo.
“Hata kama Cannavaro hataondoka, lazima tumnase Yondan ili aweze kusaidiana naye, kwani huyo ndiye chaguo la kwanza la kocha, kwa sasa mipango inaendelea vizuri,” kilieleza chanzo chetu huku kikitahadharisha kutotajwa jina gazetini.
Kiliongeza kuwa, uwezekano wa kumnasa kiungo ambaye ametupiwa virago na Timu yake ya Al Tadhamon ya Kuwait, Nizar Khalfan bado ni tata kutokana na mchezaji huyo kudai dau kubwa ambalo ni milioni 20 huku Meshack Abel anayeichezea Mujis ya Oman akitaka milioni 12.
Kadhalika Yanga imedaiwa pia kuwa mbioni kumnasa mlinzi machachari wa pembeni wa Klabu ya Tanzania Prisons ya Mbeya, Stephano Mwasika ambaye kwa sasa anakichezea kikosi cha Taifa Stars.
“Ukweli ni kwamba Klabu ya Yanga imenipa ofa ya nyumba pamoja na milioni kadhaa endapo nitakubali kuichezea msimu ujao, sitaweza kuikataa ofa hiyo,” Mwasika aliliambia Championi jana.
Wakati huo huo, Kondic anatarajia kurudi nchini kesho sambamba na wachezaji wawili kutoka Afrika Kusini alikoenda mapema wiki hii kufanya mazungumzo nao.
Kondic alimwambia mwandishi wetu kabla ya kuondoka kuelekea Afrika Kusini kuwa, tangu kumalizika kwa ziara yao alikuwa na mawasiliano ya karibu na wachezaji hao ambao walicheza mchezo wa kirafriki na Yanga ilipokuwa imeweka kambi nchini humo.
Alisema wachezaji hao ambao walikuwa wasumbufu katika mchezo wao wa majaribio nchini humo wanatokea katika Klabu ya Might Blues na kwamba wote ni washambuliaji.
“Wachezaji ambao naenda kukutana nao ni wazuri na kikubwa ambacho walinivutia ni kasi yao wawapo katika eneo la hatari, naamini wanaweza kuisaidia Yanga ambayo inakabiliwa na michuano migumu ya kitaifa na kimataifa,” alisema Kondic.
Habari na Global Publishers, Picha na BBC
Wanja la Liverpool likikamilika
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDZa2NQpPuI/AAAAAAAAAes/lqXiGu8TNG8/s400/LiverpoolStadium2PA_468x295.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDZa2dQpPvI/AAAAAAAAAe0/FxR3gZuQWUo/s400/LiverpoolStadium3PA_468x295.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDZa2tQpPwI/AAAAAAAAAe8/NJKorNlTX6M/s400/LiverpoolStadiumPA_468x295.jpg)
Soma habari za uhamisho wa Klabu hii hapa chini:-
![]() |
|
Liverpool
Latest News:
Udinese left-back Andrea Dossena is said to be close to a £9 million deal to join Liverpool, although Tottenham and Juventus have reportedly entered the fray. Liverpool are close to sealing a £9 million deal for Udinese left-back Andrea Dossena. Liverpool appear to be in pole position for the 26-year old after opening negotiations recently with Udinese sporting director Pietro Leonardi.
Rafa Benitez is lining up former France ‘keeper, and current Bordeaux number one Ulrich Rame to deputy for Pepe Reina. 20-year-old Napoli midfielder Marek Hamsik and Espanyol’s £6m-rated winger Albert Riera are other names being linked with the club. Riera could be a likely option as he has informed his club that he would like to leave this summer.
Liverpool have reportedly turned down a £25 million bid from Inter Milan for Steven Gerrard. The Italian giants want to make the 27-year-old their main signing as they begin their centenary celebrations.
Xabi Alonso is being linked with a £12 million move to Juventus.
Peter Crouch is up for sale and though a £15 million price tag has been hung around the striker’s neck there is still plenty of interest. Martin O’Neill and Roy Keane would be interested in buying Crouch and have the funds to pay the asking fee, as do Villareal, who, unlike Aston Villa and Sunderland, would be able to offer him Champions League football next season. At the same time the club have checked on Barcelona’s French left-back Frank Abidal, and are allegedly considering an £8 million offer.
Liverpool are preparing alternatives in case their bid to sign Gareth Barry falls through. Stewart Downingis one option that is currently being considered at Anfield, with Rafael Benitez ready to pay £12 million for the Middlesbrough winger.
Kwa habari zaidi za uhamisho wa klabs mbali mbali Gonga The Daily Mail Hapa
Ali Kiba kuanza makamuzi leo UK
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDYKD9QpPqI/AAAAAAAAAeM/nIrWYvE4QFA/s400/b.350.0.16777215.0.stories.springbreak_tour_backweb.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDYKENQpPrI/AAAAAAAAAeU/zlNiXz0uiuw/s400/b.350.0.16777215.0.stories.dscf0157.jpg)
SCOTLAND 23RD @ TIGER TIGER CLUB, GLASGOW
Kwa habari zaidi watembelee
http://www.bongouk.com
Thursday, May 22, 2008
David Cook ndiye American Idol Mpya!!
![](https://i0.wp.com/static.whatsontv.co.uk/images/08522_103547_47462441.jpg)
David Cook alisherehekea jana usiku baada ya kuibuka mshindi wa American Idol 2008 kwa kumshinda mpinzani wake David Archuleta , David mwenye miaka 25-alimshinda David (17) kwa kura Milioni 12 zaidi.
Na katika jambo la kushangaza jaji Simon Cowell aliomba msamaha kwa Cook kwa kile alichosema kumkosoa wakati akiimba wimbo wake wa mwisho.
Cowell alisema kuwa, maoni aliyotoa kwa Cook usiku mmoja kabla ya fainali hiyo hayakuwa ya busara na hayakumstahili David.
Alisema, nilipokwenda nyumbani na kuiangalia tena nilijiona nimemkosea kwa maoni ambayo niliyatoa. Hatimaye Cowell aliwapongeza wote wawili kwa ushujaa waliounyosha mpaka kufikia fainali hiyo, “kwa mara ya kwanza tangu nianze sitojali nani atashinda, kwangu wote mko sawa”
Kinyume na matarajio ya wengi ambao kwa kiasi kikubwa walimpa nafasi Archuleta ya ushindi wa mashindano haya, David Cook na David Archuleta kwa kiasi kikubwa waliwagawa mashabiki kiasi wasijue nani wa kumchagua kwani kila mmoja alikuwa na hisia na mvuto wa kipekee.
Rafiki yangu Tanzania Dream naona una kila sababu ya kufurahi.
RONALDO MFUNGAJI BORA UEFA CHAMPS LIGI
Msimamo wa wafungaji na timu zao ni kama ifuatavyo:-
2007/08 UEFA Champions League top scorers | ||
Player | Club | Goals |
Cristiano Ronaldo | Manchester United FC | 8 |
Lionel Messi | FC Barcelona | 6 |
Didier Drogba | Chelsea FC | 6 |
Steven Gerrard | Liverpool FC | 6 |
Fernando Torres | Liverpool FC | 6 |
Ryan Babel | Liverpool FC | 5 |
Dirk Kuyt | Liverpool FC | 5 |
Raúl González | Real Madrid CF | 5 |
Ni Manchester Kombe la UEFA Champions Ligi!
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDV3jNQpPiI/AAAAAAAAAdM/xTgVrTVD1xg/s400/man4.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDV3j9QpPkI/AAAAAAAAAdc/XmiaOu6gD6k/s400/man2.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDV3kNQpPmI/AAAAAAAAAds/oa0ZG9yx6ew/s400/drogba.jpg)
![](/Documents%20and%20Settings/INTEL/Desktop/New%20Folder/chelsea.jpg)
Ila pata yaliyojiri hasa kipindi cha Penalti kwa kubofya hapa.
Wednesday, May 21, 2008
Serge Mavili aka Celeo Scram kijana wa Wera anayekuja juu kwa kasi
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDNZysa2TYI/AAAAAAAAAcw/C-cnxfobpa8/s400/Celeo.bmp)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDNZy8a2TZI/AAAAAAAAAc4/sLzrm8vig_Y/s400/Celeo+Wera.jpg)
Tuesday, May 20, 2008
Rooney amkandia Drogba
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDKRE8a2TXI/AAAAAAAAAco/mOW1QLQU_uQ/s400/_42842431_did_rooney.jpg)
Nyota huyo wa Manchester United amempiga madongo mfungaji wa Blues muda mfupi kabla ya kufanyika kwa pambano la fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya litalozikutanisha timu zao.
Mchezaji huyo wa timu ya taifa ya England alisema: ” Wakati (Drogba) yuko katika kiwango cha juu, ni mchezaji asiyeaminika. ni mkubwa, imara, anafunga magoli kwa mguu wa kushoto, mguu wa kulia, kichwa na wakati wote si wa kumchezea,” alisema.
Hii si mara ya kwanza kwa Drogba kushutumiwa katika mashindano haya ambayo yanakutanisha timu za Uingereza tupu.
Kocha wa Liverpool, Rafa Benitez aliponda mchezaji huyo kutoka Kodivaa kwamba amekuwa akijiangusha kabla ya mechi ya pili ya nusu fainali mwezi uliopita.
Rooney na mchezaji mwenzie Nemanja Vidic pia wamemshutumu kuwa amekuwa akidanganya.
Rooney alisema kuwa alijisikia uchungu kuona Liverpool ikitwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya miaka mitatu iliyopita itamfanya yeye kujiamini zaidi mjini Moscow.
Alisema: Ni vigumu kuona mmoja wa wapinzani wako anafanikiwa vitu. Wakati Liverpool ilipotwaa ubingwa, ilitia uchungu sana. Ilitufanya sisi tutake kutwaa na hata zaidi,” alisema.
Mdau akiwa “Vakesheni”
Ni David Archulete ama David Cook American Idol
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDJdKca2TTI/AAAAAAAAAcI/MXu8tK2hACU/s400/20080519__idol19%7E1_Gallery.jpeg)
Bekham awatakia ushindi Manchester.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDI3O8a2TSI/AAAAAAAAAcA/CHECGr6SSG4/s400/1211191225.jpeg)
Monday, May 19, 2008
Bono amshawishi Bekham kupanda Mlima Kilimanjaro
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDHFQ8a2TRI/AAAAAAAAAb4/TfzhZKssCUM/s400/Bekham+mount+kilimanjaro.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDHDcca2TQI/AAAAAAAAAbw/aPJuBJlGW0c/s400/bono-american-idol-gives-back-1.jpeg)
ziara hiyo inaweza kumjumuisha pia golikipa wa West Ham Robert Green.
Bono amekuwa mstari wa mbele na kwa kipindi amekuwa nchini Tanzania kishiriki kwenye shughuli mbali mbali akisaidiana na Kampuni ya FOX/American Idol na Spoti na Starehe tuliwahi kumtoa habari zake bofya hapa humu.
Kujua zaidi ya Bekham angalia gazeti la The Sun hapa.
Portmouth alipochukua Ubingwa wa Kikombe cha FA
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDGofca2TMI/AAAAAAAAAbQ/kaFX3ucrTcM/s400/A1.jpg)
Mashabiki wa Portmount na Cardiff wakiingia uwanja wa Wembley kushuduhia mpambano kati ya Portmouth na Cardiff
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDGog8a2TOI/AAAAAAAAAbg/zf_vL6xvBjI/s400/celeb_g.jpg)
Jikumbushe yaliyojiri hapa.
Ujasiriamali wa Kitamaduni
Emillian na Irene
Ziara ya BCBG Ulaya
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDGmNsa2TLI/AAAAAAAAAbI/sXCXTnPi5yE/s400/jb4.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDGl0Ma2TKI/AAAAAAAAAbA/F2kVh158ovA/s400/jb3.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDGiTsa2TJI/AAAAAAAAAa4/tzGQqXibHvc/s400/jb.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDFc0ca2TCI/AAAAAAAAAaA/g47K3CxPXD4/s400/jb.jpg)
Ratiba ya kundi hilo iko kama ifuatavyo:-
Jikumbushe live hii ya Zenith (Audio Studio Version)
JB Mpiana :: 14 June 08 :: Liège Belgium
Kaunazi kwa mbaaaaaali!!
MIRIAM CHEMMOSS: muigizaji,mwimbaji,mtunzi wa nyimbo na pia mwanamitindo (model)
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2008/05/miriam1bc.jpg?w=392&h=531)
Miriam ni muigizaji,mwimbaji,mtunzi wa nyimbo na pia mwanamitindo (model) ambaye mpaka hivi leo ana haki ya kusimama na kujivunia rekodi yake katika ulimwengu changamani wa sanaa na maonyesho.Mwenyewe anasema safari yake ndio kwanza inaanza kwani bado ana ndoto na malengo chungu mbovu ya kutimiza.Hivi leo kazi zake nyingi anazifanyia kutokea jijini New York nchini Marekani anapoishi.
Bofya hapa upate mahojiano kamili na Bongo Celebrity
Inter Milan wachukua Ubingwa tena!!!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCr9sa2S_I/AAAAAAAAAZo/zqAb0znu7Q4/s400/1211122047.jpg)
Mechi ya leo ilikuwa ngumu na kila timu ilikuwa inataka ushindi, mashabiki waliipania na wachezaji walipania, jambo lililofanya mashabiki kadhaa kuumia vibaya ikiwa ni pamoja na polisi mmoja kwenye fujo zilizotokea nje ya uwanja mara baada ya mpira kumalizika.
Mc wa Uzinduzi wa Akudo wamuona atiii?
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCqV8a2S-I/AAAAAAAAAZg/fI8_KGQlefs/s320/1211015453_10.jpg)
Uzinduzi wa Akudo wawachengua mashabiki
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCpKsa2S6I/AAAAAAAAAZA/cYJeGYpUeKM/s320/1211019943_2.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCpK8a2S7I/AAAAAAAAAZI/jiOU-eRC0Xs/s320/1211018274_5.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCpK8a2S8I/AAAAAAAAAZQ/O0hniwN4b_M/s320/1211018274_3.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCpLMa2S9I/AAAAAAAAAZY/dBatVT2F3U4/s320/1211090639_simba_akudo.jpg)
Picha zote na habari na Global Publishers
Defao na Wazee wa Mujini!
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCn9ca2S4I/AAAAAAAAAYw/OztXD5aA-1c/s320/1211006766_img_0336.jpg)
Habari na picha na Global Publishers
Mbwembwe za wanasoka!!
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCmPMa2S3I/AAAAAAAAAYo/ZvCViIdDQ4w/s320/7984689bd672075c3051c9b0352413ba-getty-fbl-sesp-sevilla-athletic.jpg)
Furaha ya ushindi!!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDClKsa2S2I/AAAAAAAAAYg/rb1Skuf_-Cw/s320/18a7b3bd0621e33e4ed077d55eafed3f-getty-77414522jj016_real_madrid_v.jpg)
Raha ya Ubingwa Real Madrid
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SDCkh8a2S1I/AAAAAAAAAYY/9zabnO022uc/s320/SP0457%7EManchester-United-Cristiano-Ronaldo-Posters.jpg)
Saturday, May 17, 2008
Ronaldo: “Napenda kucheza La Liga Spain”
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC5H9sa2S0I/AAAAAAAAAYQ/h-kEcTEwui8/s320/SP0457%7EManchester-United-Cristiano-Ronaldo-Posters.jpg)
Ronaldo (23) amekuwa gumzo katika soko la wachezaji soka ulimwenguni kwa sasa hasa baada ya kuifungia timu yake jumla ya magoli 41 msimu huu,
Madrid wameonyesha nia ya kumtaka Ronaldo na kwa siku za karibuni harakati zinasemekana zimepamba moto na wamesema wako tayari kutoa kitita cha Pound £100million. Sijaamua lolote kwa sasa najisikia raha kucheza hapa, mawazo yapo kwenye mchezo na Chelsea kwa sasa ngoja tuangalie baada ya mchezo huo, alisema Ronaldo akihojiwa na Spanish TV network Antena 3.
‘Najua Real Madrid wanavutiwa na uchezaji wangu, najua pia kuna Timu Spain zinavutiwa na mimi pia, ni vizuri kujua kuwa kuna timu zinavutiwa na wewe, nimesema mara milioni kuwa ninapenda sana kucheza Spain, alimalizia Ronaldo.
Viera: Arsenal watampoteza Gallas wasipokuwa makini
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC5BP8a2SxI/AAAAAAAAAX4/Ow4nPFhuSHI/s320/gallas-412.jpg)
“Arsenal wanahitaji ubembeleza wachezaji wao, kwa mujibu wa malipo ya Arsenal kwa sasa ni rahisi kwa mchezaji kuondoka, tayari wamepata pigo kwa kuondokewa na Flamini aliyekwenda AC Milan alisema Viera, ni lazima watoe mikataba minono ili kuwafanya wachezaji wazuri wakae, vinginevyo timu haitakuwa wachezaji”.
Bayern Bango kuuuuuuubwa!!
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC45u8a2SwI/AAAAAAAAAXw/uCxg0PKKM5o/s320/09969b7908055106829a330d656ec5d1-getty-fbl-ger-bayern-munich-poster.jpg)
Oliver Kahn Kucheza mechi yake ya mwisho leo
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC43Vca2SvI/AAAAAAAAAXo/fOqRxitl9PQ/s320/1210920610.jpg)
Miss Chang’ombe Mazoezini
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC413sa2SuI/AAAAAAAAAXg/UaSIFIZjXdI/s320/1210941585_4w.jpg)
Philipp kuichezea Bayan Munich mpaka 2012.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SC40E8a2SsI/AAAAAAAAAXQ/fchHMkeEO9A/s320/capt.cps.nev63.160508194823.photo00.photo.default-396x492.jpg)
Thursday, May 15, 2008
Ngoma Inogile American Idol
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwYbca2SnI/AAAAAAAAAWo/QMOqA4Gd4BE/s320/2008_05_14t230155_450x309_us_americanidol.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwYbca2SoI/AAAAAAAAAWw/bxzWCbQbHN0/s320/capt.7bf7e6b392b34b9ba8f876ba38be9539.tv_american_idol_mercado_nyet183.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwYbsa2SpI/AAAAAAAAAW4/79boIRSGB1k/s320/capt.cc36cc2064ab43a0b3e0681975b5431c.neilsens_nyet226.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwYbsa2SqI/AAAAAAAAAXA/X_efG3MgM8I/s320/capt.4c3e4af890fa4e568d8bd2f3896ba235.archuleta_utah_utkc106.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwYb8a2SrI/AAAAAAAAAXI/XdKitfP_-0I/s320/capt.e855ab8bfa1d433e923e7cb1e5f29716.orioles_royals_baseball_moow109.jpg)
Video na Mchezaji wa Wiki: Didier Drogba
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwWTsa2SmI/AAAAAAAAAWg/AVuLFPOOwdg/s320/didie+drogba.jpg)
Urefu 6’2
Uzito 13st 3lbs
Club Chelsea
Nafasi Forward
Didier Drogba
Kwa mujibu wa gazete la Sports Gazzette la Italy, Dgrogba ni mmoja wa washambuliaji hatari sana katika bara la ulaya, linizungumzia sifa binafsi za Drogba gazeti hilo lilisema, “Drogba haogopi, ana mbio, ana nguvu na uwezo wa kumiliki mpira, misuli yake imeshika vyema, ni aina ya washambuliaji ambao mabeki wengi wanawaogopa”.
Akiongea na Televishen ya Chelsea kuhusu kucheza kwake mpira Uingereza Drogba alisema anafurahia sana kwani ligi ya uingereza inakutanisha wachezaji toka nchi mbali mbali duniani wenye vipaji lakini kitu pekee anacholalamikia ni ubaguzi, Drogba aliongelea hili alipoongea na Televisheni ya CFI (Chanal Franc Internationa) wakati wa kombe la mataifa ya Africa juu ya kitendo chake cha kumshika korodani mchezaji mwenziwe Van Bommel’s wakati timu yake alipocheza na Netherlands, Drogba alisema
“natamani ningekuwa na tape recorder ili niweze kuyarudia maneno ambayo wanasemaga hawa watu yenye ubaguzi, huwezi kuvumilia, wakati mwingine huoni adhabu anayofaa kupewa hivyo unaamua lolote lililoko kichwani kwa muda huo.
Bozi Boziana ndani ya Africa Bambataa
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwHgsa2SlI/AAAAAAAAAWY/sOldYVDxplg/s320/IMG_0713.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwGAsa2ShI/AAAAAAAAAV4/5yVejep6Q7Q/s320/IMG_0688.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwGAsa2SiI/AAAAAAAAAWA/qadqB_zn2wE/s320/IMG_0701.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwGBMa2SjI/AAAAAAAAAWI/DVLewmaZSgc/s320/IMG_0717.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCwGBMa2SkI/AAAAAAAAAWQ/0ezYz5V-wtM/s320/IMG_0719.jpg)
Mwanamuziki Bozi Boziana atawasindikiza Akudo sound kwenye uzinduzi wa albamu yao kesho.
Jikumbushe na wimbo huu wa Bozi Boziana
Wednesday, May 14, 2008
Bozi ndani ya Zizou Fashion
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrIS8a2SdI/AAAAAAAAAVY/d98pY2z3EKM/s320/bozi4.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrITMa2SeI/AAAAAAAAAVg/AcwqmYWubDg/s320/bozi5.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrITca2SfI/AAAAAAAAAVo/bV0LvlAY8Z8/s320/1210762000_1w.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrIUMa2SgI/AAAAAAAAAVw/hQ2ZHjbMkIg/s320/bozi.jpg)
Na Global Publishers
Uzinduzi wa Akudo Bozi atua Dar
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrDVsa2ScI/AAAAAAAAAVQ/dAkrMeXFWl4/s320/bozi3.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrBdMa2SaI/AAAAAAAAAVA/3Z7qFt0VRQw/s320/bozi+1.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCrBdca2SbI/AAAAAAAAAVI/7ZJJIOgWwDw/s320/bizi2.jpg)
Leo Bozi Boziana atakuwa na mahojiano na Kipindi cha Africa Bambataa kinachorushwa na Clouds Fm. Clouds ni mmoja wa wadhamini wa uzinduzi wa wanapekechapekecha Akudo Impact.
HAbari na picha na Father Kidevu
Kagera Yapeta kombe la TAIFA
Scolari: Nategemea Ronaldo kuwa kwenye kiwango hichohicho
![](https://i0.wp.com/img.dailymail.co.uk/i/pix/2007/04_01/ManUtdRonaldo2DM_468x394.jpg)
“Hakuna wasiwasi Ronaldo yuko fit na kwenye kiwango, ila siwezi kuahidi kuwa atacheza kwa kiwango mnachomuona nacho leo hii akiwa na klabu yake ya Manchester, alisema Scolari.
Hivi majuzi Chelsea wametangaza kumnyakuwa mchezaji mweingine machachari toka Urno mzaliwa wa Kongo Jose Bosingwa kwa kitita cha £16.2milioni.
Drogba, Terry kucheza na Man U.
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCpXPsa2SYI/AAAAAAAAAUw/8dHQo699r-U/s320/_44646109_terry_drogba_credit203.jpeg)
Terry na Drogba wote kwa pamoja waliumia wakati wa mchezo na Bolton jumapili iliyopita.
Drogba aliliambia gazeti la Ufaransa L’Equipe kuwa kuumia kwake si saaaana na aliongeza kuwa hakuna anayetaka kuikosa hii mechi, nitakuwepo.”
Thiery Hanry ndani ya Champion for Africa.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCpTr8a2SXI/AAAAAAAAAUo/UDNS-xSj2xc/s320/bc061ae5d5de35eb71bd93db64e9befb-getty-fbl-friendly-esp.jpeg)
Champions for Africa
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCpTMMa2SWI/AAAAAAAAAUg/vhyeQvmVK2E/s320/c475de13f2499ac4c285ba750a2069d4-getty-fbl-friendly-esp.jpeg)
Atlas na Boca leo
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCpSS8a2SVI/AAAAAAAAAUY/5g--RgOFhCI/s320/capt.c0070ca5982949c6b139f0627e63df34.argentina_soccer_copa_libertadores_edb101.jpeg)
Mashabiki wa Bekham
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCpQqca2SUI/AAAAAAAAAUQ/quYkTMeqm0o/s320/capt.3cd34bf318714962b8dccdb36540a645.galaxy_whitecaps_soccer_edm105.jpeg)
Tuesday, May 13, 2008
Mwana wa Rais Bush, Jenna Bush Afunga ndoa.
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkiMsa2SRI/AAAAAAAAAT4/qvZQa8HWwrs/s320/jenna_bush_wedding_1.jpeg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkiNMa2SSI/AAAAAAAAAUA/-vTN7iCx8mI/s320/jenna_bush_wedding_2.jpeg)
Jenna na Henry wakishikana mikono mbele ya Kiongozi wa Kanisa wakati wakifungishwa ndoa Jumamosi ya tarehe 10 May, 2007.
Rais Bush alitumia mwezi mzima kwa maandalizi ya harusi ya kipenzi binti yake Jenna. hatimaye Jumamosi yakatimia katika harusi iliyofanyika katika Ranchi ya Rais huyo.
“Mwanetu kipenzi Jenna amefunga ndoa na kijana mzuri kwa kweli, ni rafiki yake wa siku nyingi Henry Hagga, alisema Bush akiwa sambamba na na mkewe Laura wakati wakipanda ndege kurejea Ikulu kwa shughuli za ujenzi wa Taifa.
Ndoa hiyo ilifungwa huku kukiwa na ilinzi mkali eneo lote ikiwa ni tangu siku kadhaa kabla ya harusi eneo hilo lilikuwa kwenye ulinzi mkali, ndugu jamaa na marafiki wa familia zote mbili walijumuika kula na kunywa.
Tukio hili la kifamilia halikuonyeshwa moja kwa moja na Televisheni za Marekani kwani familia ya Bush haikupenda hilo.
Na southernledger.com
Mkongwe Suge Knight alambwa kichapo
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCke2Ma2SQI/AAAAAAAAATw/VkpwwulElXg/s320/dggsjksc_8459cv3fb3fj_b.jpeg)
Kapt. Komba Awakoromea Misambano,Hegga
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkdk8a2SPI/AAAAAAAAATo/49pkXHhLF4A/s320/Komba.jpeg)
Mkurugenzi wa T-RESPECT (T.O.T), Kapteni John Komba (pichani) ,mwishoni mwa wiki iliyopita aligeuka mbogo na kutaka kuwalamba vibao wanamuziki wake,Rogart Hegga na Abdul Missambano ambao walishindwa kusimamia vizuri mazoezi ya bendi yao, yaliyokuwa yakifanyika ndani ya Ukumbi wa Dar West Park, Tabata, Dar es Salaam.
“Nononooo, hebu njoooni hapa, bado sijaridhika na safu ya unenguaji, kuna sehemu wanakosea, nataka warudie kucheza na makosa kama hayo nisiyaone tena,” alisikika akifoka Kapteni Komba.Pamoja na makosa hayo madogo madogo, bendi hiyo kwa sasa inakuja juu katika sanaa ya dansi na tayari imeshaonesha kuwakuna mashabiki kibao wanajitokeza mazoezini.Habari hii kwa hisani kubwa ya Haki Ngowi
Bekham aitwa Kikosi cha Uingereza
![](https://i0.wp.com/i.l.cnn.net/cnn/2007/SPORT/football/07/10/anderson.beckham/art.david.beckham.gi.jpg)
Maradona uwanjani tena
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkWy8a2SNI/AAAAAAAAATY/ni-oD9w9PTw/s320/capt.2976442985f343cb80a39a9b37652a44.italy_soccer_maradona_gb102.jpeg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkWy8a2SOI/AAAAAAAAATg/211WrLmfjVs/s320/8a199105991d333cfbed0de8519a167b-getty-fbl-italy-maradona-charity.jpeg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkWAsa2SLI/AAAAAAAAATI/AS0zBgmPJlg/s320/6aa8b5d21ede64f0181615940bd8ce0c-getty-fbl-italy-maradona-charity.jpeg)
Maradona na Zico
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkWk8a2SMI/AAAAAAAAATQ/jQSj66kscqU/s320/de892ceb9772dd4a6c5ebfc2ee90f356-getty-fbl-italy-maradona-charity.jpeg)
Bekham wa makeke…
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkTbca2SJI/AAAAAAAAAS4/PBOLFbUR5is/s320/capt.530e3c2935e44065b7bac976d50b5edf.galaxy_beckham_soccer_edm101.jpeg)
Ferguson ahaidiwa Mshiko kuimarisha Kikosi
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkQ-8a2SII/AAAAAAAAASw/o361A2zv134/s320/_44648728_gill203b.jpeg)
Gill alisema: “Tuko kwenye nafasi ambayo tunahitaji kuiimarisha ili tuweze kubaki juu”.
“Mi ligi bora katika dunia, kama tunahitaji kuwa bora zaidi ni lazima kuangalia katika kikosi chetu, tuanzie hapa tulipo kuhakikisha kila udhaifu unafanyiwa kazi”
CHELSEA yamnyakuwa Mcongo toka Porto
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCkOt8a2SHI/AAAAAAAAASo/xPU8pt5gLUk/s320/_44647220_bosingwa203.jpeg)
Mchezaji huyo mwenye miaka 25 raia wa Ureno na mzaliwa wa Congo ataungana na timu yake mpya ya Chelesea mara baada ya michezo ya Euro 2008.
Bosingwa, ambaye pia alikuwa akiwaniwa na Manchester United, alizaliwa katika Jamhuri ya watu wa Kongo lakini alihamia Ureno akiwa bado mdogo.
FM V/s Akudo Ngoma inogile
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/10/akudo-impactbc.jpg?w=450)
Monday, May 12, 2008
Yaliyojiri Viwanjani Jana
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44645000/jpg/_44645985_giggs_ap.jpg)
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44645000/jpg/_44645791_celebration_getty.jpg)
Sunday, May 11, 2008
Ni Manchester United
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44645000/jpg/_44645941_cel_getty.jpg)
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44645000/jpg/_44645522_ronaldo_getty.jpg)
Timu ya Manchester United imefanikiwa kuchukua kombe la Ubingwa wa Premier League kwa pointi mbili zaidi ya Chelsea ambao walikuwa kwenye kinyang’anyiro kwa kuwa na pointi sawa mchezo ulikuwa mkali kwa upande wa Manchester na Wigan huku Wigan wakionyesha kuwabana na kutowapa nafasi Manchester kipindi cha kwanza ingawa kulikuwa na kosa kosa nyingi kwa kila upande, mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 1-o Manchester wakiongoza kwa bao moja lililofungwa na Cristian Ronaldo kwa njia ya Penati baada ya Rooney kuchezewa madhambi ndani ya boksi. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Manchester wakilishambulia lango la Wigan na Wigan kurudisha mashambulizi ingawa hayakuwatisha sana ManU kwani baada ya kubadilishwa Scholles na kuingia Gigs alileta changamoto kwa upande wa Manchester na alifanyikiwa kupachika bao la pili baada ya kupewa pasi akiwa karibu kabisa na kipa na ku press mpira ule na kuandika bao la pili, hadi mwisho ManU 2-0 Wigan.
Matokeo ya michezo ya leo yalikuwa kama ifuatavyo.
Mabingwa ni : Manchester United
Klabu zitakazo cheza Champions League ni: Manchester United, Chelsea, Arsenal, Liverpool
Uefa Cup ni: Everton
Intertoto Cup ni: Aston Villa
Walioshuka ni: Reading, Birmingham, Derby
PREMIER LEAGUE
FT Birmingham 4-1 Blackburn
FT Chelsea 1-1 Bolton
FT Derby 0-4 Reading
FT Everton 3-1 Newcastle
FT Middlesbrough 8-1 Man City
FT Portsmouth 0-1 Fulham
FT Sunderland 0-1 Arsenal
FT Tottenham 0-2 Liverpool
FT West Ham 2-2 Aston Villa
FT Wigan 0-2 Man Utd
Mashabiki matumbo moto
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44644000/jpg/_44644480_title466.jpg)
15:00 | Birmingham C. | ? – ? | Blackburn R. |
15:00 | Chelsea | ? – ? | Bolton W. |
15:00 | Derby County | ? – ? | Reading |
15:00 | Everton | ? – ? | Newcastle U. |
15:00 | Middlesbrough | ? – ? | Manchester C. |
15:00 | Portsmouth | ? – ? | Fulham |
15:00 | Sunderland | ? – ? | Arsenal |
15:00 | Tottenham H. | ? – ? | Liverpool |
15:00 | West Ham U. | ? – ? | Aston Villa |
15:00 | Wigan Athletic | ? – ? | Manchester U. |
Saturday, May 10, 2008
Mchizi wangu Remix
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCWoEZOUBLI/AAAAAAAAASg/MPBks9Umygg/s320/nako2nako.jpg)
Taboo Fatoo Top Model
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCWSH5OUBKI/AAAAAAAAASY/ZapwcIYC5uQ/s320/Tabou+Fatou.jpg)
Gonga hapo umsikie Jb Mpiana na Taboo Fatoo Top Modele”.
Ze Comedy wajitoa East Africa TV
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/08/ze-comedy.jpg?w=450)
Ukiondoa Ze Comedy, naye Mratibu wa kundi hilo Sekioni David amesitisha mkataba na kituo hicho na sasa anaelekeza nguvu zake ndani ya kundi hilo.
“Baada ya kuufahamisha uongozi nia yetu, nilipatwa na mtihani mgumu sana, maana niliambiwa nichague kuendelea kutangaza au kupumzika na Ze Comedy. Nimechagua kupumzika na kundi hili na sitajutia uamuzi huu hakika, mimi ni msanii msanii wa siku nyingi na nina uzoefu wa muda mrefu. Kama nilivyoweza mwazo kuiinua Ze Comedy, ndivyo nitakavyoweza kuiendeleza zaidi,’’ alisema Seki.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi hilo, Isaya Mwakilasa (Wakuvanga) alisema wameamua uamuzi huo ili kupata mapumziko kwa muda kabla ya kuendelea na sanaa hiyo.
Mwakilasa alisema wanasikitika kumaliza mkataba na EATV na hivyo wameamua kurudi nyumbani kujipanga upya lakini pia wanaweza kuingia mkataba mpya endapo watakubaliana.
“Mkataba wetu na EATV umeisha nasi tumeamua kurudi nyumbani kupumzika kwa nia njema, hasa kwa maslahi ya wengi zaidi na tulikuwa tukifanya kazi nao vizuri na huu si mwisho wetu,” alisema Mwakilasa.
Mwakilasa alikanusha taarifa kuwa Ze Comedy lina mpango wa kuingia mkataba mpya na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC 1) na kuongeza kuwa sanaa ni ajira yao hivyo kama watahitajika hawasita kuingia mkataba na kituo hicho.
Kamali ya Mpira yawanufaisha mashabiki
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCUoIpOUBJI/AAAAAAAAASQ/k8wz2SBbkKA/s320/genting_highland_2006.jpg)
Asia mpira ni biashara, toka kuuza jezi, sticker hadi matokeo kwani kunawaopoteza nyumba, magari na pesa taslimu kila siku, imekuwa ni sehemu ya utamaduni na ndio maana hizi timu kubwa haziishi kuja alisema Raj, Tax driver anayefanya shughuli zake Genting.
Kuna wanaotegemea mechi hizi kula na kulisha familia, nimekuwa nikicheza kamali ya mpira kwa mika nenda rudi, ni rahisi kupoteza na kupata pia kwani kwa mechi ndogo dau ni dogo kwa mechi kubwa ambayo matokeo hayatabiriki hapo ndio wengi hucheza na wengi hupoteza alisema Raj.
Binafsi nimenunua ticket za Ringit 800 (dola 250) nategemea ikishinda napata mara mara nne ya hapo, nasali Man washinde, siku ya Chelsea na Man nilipata Ringit 5000 (sawa na dola 1600). Nilifurahi mke wangu alikuwa na wasiwasi lakini Inshallah tukapata.
Ronaldo na Drogba, nani ataibeba timu yake?
![](https://i0.wp.com/img.thesun.co.uk/multimedia/archive/00033/ed_imgsnf17spdfx2_26_33590a.jpg)
Swali langu bado lipo pale pale kombe litawekwa wapi kusubiria mwenyewe apewe kwani timu zote zinacheza kwenye viwana tofauti na kipigo cha timu moja ni furaha ya ushindo kwa mwingine iwe atatoka sare au atashinda kwa idadi yeyote ya magoli.
Porto wapigwa faini kwa tuhuma za kupanga matokeo
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/us.yimg.com/p/ap/20080509/capt.66a1d60d5c914f95b8578c36c986bb09.portugal_soccer_xpd114.jpg)
Figo ana imani na Pep Guardiola
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/a/p/afp/20080509/capt.cps.ndc43.090508223524.photo00.photo.default-512x354.jpg)
Na BBC sports
Wenger asema Adebayo na Hleb bado ni wa kwao
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44641000/jpg/_44641941_adebayor_hleb203.jpg)
“Nina furaha na amani sana kwenye klabu yangu ya Arsenal,” alisema mshambuliaji Adebayor. “habari zinazosema nataka kuondoka ni uzushi mtupu.”
Hleb ana husishwa na kutaka kujiunga na klabu ya Inter Milan na agent wake amekuwa akiliongelea suala hilo la mchezaji huyo mwenye miaka 27 kuwa anataka kutoka Arsenal.
Habari za kuondoka wachezaji hawa ziliwatia matumbo joto mashabiki wa Arsenal hasa baada ya kuondoka mchezaji Flamini.
Na BBC Sports
Jose Mara: Akudo waache maneno tufanye kazi.
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCUUPJOUBII/AAAAAAAAASI/aq1TGmurprM/s320/Jose+Mara.jpg)
Mwanamuziki Jose Mara amemsihi mwenzake Christian Bella wa Akudo Impact kuacha maneno maneno na kufanya kazi, “mashabiki hawataki maneno, mashabiki wanataka kufurahishwa” alisema Jose Mara.
Hii yote ilitokana na suhindanishwaji wa wanamuziki hawa wawili kwenye kipindi cha kinachorushwa kwenye TV cha (Nyumbani ni Nyumbani) cha C2C na (Afro Beat) cha East Africa TV, Huwa wanashindanisha wanamuziki wawili au vikundi vinavyofanana, Kumetokea kushindanishwa zaidi ya mara mbili kati ya mwanamuziki Jose na Bella, na Jose amekuwa akishinda. Inasemekana hili lilimuuma sana Bella, na alipoongea na gazeti moja akasema mimi nashang’aa kushindanishwa na Jose, Kwanza Jose si wa rank yangu,Kwanza Mchafu Mchafu, yeye yupo sawa na kila Fally, Jose anasema yeye awezi kumjibu sababu majibu anayo yeye Bella, wakati wanatoka Congo, Jose alimlea Bella kwa kila kitu kula hadi Mavazi ni kama mdogo wake, anasikitishwa na kauli za Bella.
Ushindani wa bendi hizi umekuwa kwa kasi na hasa habari za hivi karibuni ambapo Akudo wanazindua albam yao na kumleta Mzee Bozi Boziana na FM wameandaa shoo usiku huo huo wa tarehe 16 ambapo walikuwa kwenye mipango ya kumleta Bozi Boziana, jambo linalotafsiriwa kuwa wanataka kuvuruga uzinduzi wa Akudo.
Friday, May 9, 2008
Ronaldo aomba msamaha.
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/ca.yimg.com/p/080408/afp/icpsmvq67080408124318photo00.jpg)
Ronaldo alituhumiwa kuchukua wanawake watatu ili akafanye nao mapenzi katika chumba chake cha hoteli lakini baada ya kufika aligundua kuw wale walikuwa si wanawake bali ni mashoga na kuwataka waondoke lakini wao walitaka mchezaji huyo awalipe jambo ambalo lilianzisha ugomvi mpaka polisi kuitwa.
Kesi ya R. Kelly yaanza kuunguruma
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/us.yimg.com/p/ap/20080509/capt.52f0a124779c4370ae98267669c93fbb.r_kelly_trial_ilca102.jpg)
Video na Mchezaji wa Wiki: Samuel Etoo’
Jina: Samuel Eto’o Fils
1998-1999 Real Madrid – Mechi 3 , bila goli
1999-2004 Real Mallorca – Mechi 133, magoli 54.
2004-mpaka sasa FC Barcelona
Eto’o baadaye alihamia FC Barcelona 2004 kwa donge nono la ada ya uhamisho jumla ya Pound Milioni £24.
2006 Eto’o alizawadiwa taji la “pichichi” (Mfungaji bora kwenye ligi ya La Liga) baada ya kuifungia Barcelona goli kwenye mechi ya mwisho ya msimu wa ligi dhidi ya Athletic de Bilbao.
Etoo alipata maswahibu kwani aliumia mwaka 2006 na tangu hapo imekuwa ikimletea matatizo mara kwa mara na kumfanya kuwa nje ya dimba, ingawa timu yake haikufanya vizuri kwa msimu huu lakini bado kijana huyu amerudi kwa kasi kwenye uwezo wake wa kawaida, ingawa kuna tetesi kuwa anawaniwa na timu za Uingereza, iwe ni Spain au Uingereza bado nyota ya Etoo inaashiria kuendelea kuwaka kwa muongo mwingine kwani bado umri unamruhusu.
Nani kuwa American Idol wa 7?
![](https://i0.wp.com/www.nationalledger.com/artman/uploads/american_idol_three.jpg)
Burudani ya Mpira na Muziki Giraffe Hotel
![](https://i0.wp.com/www.giraffeoceanviewhotel.com/makuti-bar.gif)
Allex Miller abwaga manyanga Liverpool
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/41346000/jpg/_41346233_benitezpic.jpg)
Katika mkataba mpya na timu hiyo kocha Miller atalipwa mshahara wa £500,000.
Ni habari njema kwa Alex, alisema Benitez jana, hii ni nafasi nzuri kwake kufanya kazi Japan, napenda kuchukua nafasi hii kumtakia mafanikio mema katika kibarua chake kipya, alimalizia Benitez.
Kombe litakuwa wapi?
![](https://i0.wp.com/www.goal.com/images/20357_news.jpg)
Manchester United: Tutajitahidi yasijirudie ya 1968
![](https://i0.wp.com/www.themartyrs.com/Images/stepney2.jpg)
ManU walikuwa na pointi 56 sawa na pointi 56 za mahasimu wao Manchester City, ManU walikuwa wakicheza dhidi ya Sunderland. Mashabiki walikuwa walikuwa akimpa Stepney maendeleo juu ya mchezo wa ManCity ambao kwa wakati huo huo walikuwa wakikipiga dhidi ya timu ya Newcastle. Mashabiki walikuwa wakiufatilia mchezo ule kwa njia ya redio na kutupa matokeo ili kutuhamasisha kwa ushindi, lakini mhhhh alisema Alex.
Kiukweli sikupenda nilichokuwa nakisikia wakati ule kwani kiukweli mpaka mwisho wa mchezo tulifungwa 2-1, City wakashinda 4-3 na kuchukua ubingwa, upinzani ule haujajirudia tena mpaka sasa ndio tunaona kwenye mtanange wa jumapili hii.
“Mashabiki walikuwa karibu kabisa na uwanja na walikuwa akipiga kelele kutwambia matokea ya City ambayo yalitutia tumbo joto na kutufanya kupanic na kushindwa mchezo ule” alisema Stepney, mwenye miaka 65 sasa.
Mtanange wa Premier League ndio unafikia ukingoni wiki end hii huku tukishuhudia timu mbili zikikabana makoo kwa point sawa mpaka sasa Manchester United na Chelsea, wote wana point 84. ManU wanamagoli mengi zaidi ya Chelsea kwani mpaka sasa wana magili 17 zaidi ya Chelsea , kwa hivo basi matokeo ya sare yeyote kati ya timu hizo nne zitakazo cheza yanawafanya Man kuchukua ubingwa la hasha ni kuwa Chelsea ashinde na Man ashindwe, au Chelsea atoe droo na Man ashindwe, Safari ya Man U wigan na huku Chelsea ikicheza uwanja wa nyumbani inaweza kuwapa faida Chelsea kwani hizi timu ndogo zikiwa kwao huwa zinadinda sana kwa timu kubwa.
Kimbembe hakitaishia hapo kwani kwa matokeo yeyote bado wawili hao wanakwenda kuumana tena kwenye mtanange wa fainali ya kufa mtu itakayofanyika Mei 21 jijini Moscow kwenye mtanange wa kwanza wa fainali kuzikutanisha timu zote toka Uingereza.
O’Neill: Ofa ya Liverpool inamshusha thamani Barry
![](https://i0.wp.com/soccernet-assets.espn.go.com/design05/images/PH2/BarryPA.jpg)
Ofa ya Liverpool ni kutoa mchezaji mmoja pamoja na donge hilo la Pound milioni 10 ambapo walitoa dau hilo hivi karibuni lakini O’Neill bado anaona kama dau ni dogo. Pia O’Neil alisema Liverpool hawajasema watatoa mchezaji gani kwani wanaweza wakakupatia mtu ambaye humuhitaji kwenye timu yako ndio maana tunakazia kwenye pesa zaidi au wangeweka wazi.
Mazungumzo yetu si kwamba hatumtaki Barry, kwani dhamira yetu si kuuza wachezaji, dhamira yetu ni kuwa na kikosi imara na kizuri ili na sisi tufike hapo juu na ndio nafasi tunayoitaka, sasa kama mtu kampenda mchezaji wetu basi ajichinje mwenyewe, tutafanya kila linalowekana Barry abaki kwetu la haiwezekani basi tukipata dau nono litatuwezesha kutafuta mbadala wake alisema O’Neil.
Marcio amfagilia Ivo Mapunda
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/10/ivo-mapundabc.jpg?w=450)
- Asema kwa Tanzania Hakuna kipa kama yeye.
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’, Marcio Maximo amesema atamtumia katika kikosi cha kwanza kwenye mchezo dhidi ya Mauritius kipa Ivo Mapunda (pichani) badala ya Farouk Ramadhani.
Mapunda aliitwa katika kikosi hicho hivi karibuni ikiwa ni miezi sita tangu awe benchi kutokana na kufungiwa na klabu yake ya Yanga kwa madai ya utovu wa nidhamu.
Kufungiwa kwa Mapunda aliyekuwa chaguo la kwanza la Maximo kulimfanya amuite kipa Farouk Ramadhani katika mchezo wa awali wa michuano mipya ya Afrika inayoshirikisha wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani tu, ambapo katika mchezo wa kwanza Stars iliitoa Kenya ‘Harambee Stars’ kwa jumla ya mabao 2-1. Mchezo wa kwanza uliofanyika Kenya, Harambee ilishinda bao 1-0, lakini ziliporudiana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Taifa Stars ilishinda mabao 2-0, kipa akiwa Farouk.
Pia katika mchezo wa kwanza hatua ya pili ya michuano hiyo dhidi ya Uganda ‘The Cranes’ uliofanyika Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Taifa Stars ilishinda mabao 2-0, kipa pia akiwa Farouk.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Maximo alisema analazimika kuanza kumtumia Mapunda kwa kuwa ni kipa mzuri zaidi ya Farouk na ana uwezo mkubwa kuliko kipa yeyote nchini, hivyo ana umuhimu kumtumia kwa mashindano makubwa.
Alisema tofauti na Farouk, Mapunda amecheza michezo mingi ya kimataifa ana uwezo mkubwa kumudu mashindano yeyote makubwa na kwamba tangu kipa huyo arudi kwenye kikosi chakr amesharudi kwenye chati.
Hata hivyo alisema katika mchezo wa marudiano dhidi ya Uganda wiki ijayo huenda akaanza Farouk, lakini mchezo wa kuwania kufuzu fainali za kombe la dunia 2010 dhidi ya Mauritius mwishoni mwa mwezi huu jijini Dar es Salaam atacheza Mapunda, ambapo Farouk atakuwa benchi.
Kuhusiana na mchezo dhidi ya Uganda, Maximo alisema kikosi chake kipo katika hali nzuri isipokuwa kuna majeruhi wachache, ambao ni Uhuru na Abdi Kassim aliosema huenda wasiwepo katika mchezo huo wa marudiano kwani watakuwa nje kwa muda mrefu.
Majeruhi wengine ni Ulimboka Mwakingwe na Henry Joseph, ambao hata hivyo watarejea uwanjani wakati wowote.
Mheshimiwa Pinda kuupamba Uzinduzi wa Akudo
Akizungumza Dar es Salaam jana Mratibu wa tamasha hilo, Bahati Singh alisema katika uzinduzi huo, bendi hiyo itasindikizwa na mwanamuziki kutoka Kongo, Bozi Boziana na Jahazi Morden Taarabu na utafanyika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Alisema Kamati ya Maandalizi ya uzinduzi huo imeahidi kutoa sh. milioni moja kwa ajili ya kusaidia kununua vitanda na magoro katika wodi ya wazazi ya hospitali ya mwananyamala.
“Wanamuziki wametamba kutoa burudani ya kukata na shoka, ambapo wapenzi wataulizwa kama ni funika bovu au la, kama burudani haitakonga nyoyo za mashabiki, hiyo ndio itakuwa mwisho wa bendi ya Akudo,” alisema Singh.
Singh alisema uzinduzi huo umedhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake Ndovu, Vodacom, QSSP Group LTD, Clouds FM Dotnata Decoration, C2C televisheni na CM LTD.
Tchasho Mbala
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCOwoXynJQI/AAAAAAAAASA/ederxmbZ5_g/s320/Tchato,+Mkewe+na+Wageni+Waalikwa.jpg)
Na Big Producer Maghambo
Celtel Idols
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCOvsnynJPI/AAAAAAAAAR4/nQoWkg8ZcmE/s320/Celtel-Idols.jpg)
Na Haki Ngowi
Thursday, May 8, 2008
Real Madrid walipomuua Barca 4-1
Real Madrid wamesherehekea ubingwa wa Ligi ya Spain kwa kuwachapa watani wao Barcelona mabao 4-1 kwenye kinyang’anyiro cha El Clasico derby.
Bonyeza Player upate uhondo
KIJIWE MAARIFA
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCKgVHynJOI/AAAAAAAAARw/qacYoXXhhEk/s320/Bila-kujali-Tofauti-1.jpg)
Karibuni kwa mara nyingine tena, husika na WAPI …tukio la kila mwezi. Kama kawaida”WAPI” inaendelea. safari hii tunajumuika na watu wa mataifa mbali mbali kwenye mada yetu BILA KUJALI TOFAUTI… kwenye KIJIWE MAARIFA tutakuwa na Kemi KALIKAWE, FATMA AMOUR WANAMITINDO/WABUNIFU mahiri. WASAMBAZIE huu waraka watu wengine kwenye orodha yako ya anuani
Yawaletea
Mboli -MC mahiri chipukizi, Rage- mwakilishi wa MC Afrika TZ, Enika
Mitindo na Kemi Kalikawe, Fatma Amour.
Wasanii wa sauti ya handaki(undeground), Katika harakati.
Madijei, ma emsii, machata, mabreka ,michoro mbali mbali, ushairi,ngoma, maigizo na usanifu mitindo.
(maelekezo: Samora na Ohio, mkabala na Steers kati kati ya jiji)
Mbali na kukutwa na Kichwa cha binadamu Rama ni msanii pia…
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCJbWHynJNI/AAAAAAAAARo/OVDyclgUdZM/s320/rama.jpg)
Sanaa ya uchoraji huwa inamuwezesha Mchoraji kutoa kilichomo mawazoni mwake na kukiweka katika muonekano, mara nyingi unaweza kuona picha tuu lakini akatokea mtu na kuitolea maana na maelezo lukuki picha hiyo hiyo moja, ama kuweza kutafsiriwa na watu tofauti pia.
Sijui huyu mtoto alikuwa akiwaza nini alipochora picha hii, lakini nafikiri wataalamu wa Saikolojia (Noel Kilonzo) wanaweza kuoanisha picha hii na tabia ya mtoto husika. Je wewe unafikiria nini?
FM wadaiwa kupanga kuvuruga uzinduzi wa AKUDO
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCJXPHynJMI/AAAAAAAAARg/hc4IF6yYUbk/s320/akudo.jpg)
Madai ya Defao kutiwa mbaroni yamekuja kutokana na kile kinachodaiwa kuwa alipofanya ziara ya mwisho hapa nchini alitoroka akiwa anadaiwa mamilioni ya hela za pango katika Hotel ya Sea Cliff pamoja na fedha ya matibabu katika Hospitali ya TMJ.
Kumekuwa na mashindano kati ya Bendi hizi nchini siku za karibuni na kwa sasa ushindani unatarajia kuwa mkubwa kwani ujio wa TOT Respect utanogesha burudani ukizingatia bado kuna Twanga Original na Twanga Chipolopolo, Patamu hapo mwanangu.
Source: Global Publishers
Taifa Stars wapongezwa
Pia inanikumbusha jinsi watanzania walipojitoa wakati timu yetu ikishiriki hatua za awali za kombe la Africa, natuma Taifa Stars itawapa raha watanzania na kuleta kombe nyumbani, inshallah kila kiti chawezekana.
Pichani Kocha wa Taifa Stars na msaidizi wake akikokokotwa na watoto wa kikundi cha sanaa ya Ngoma na Sarakasi kwenda kucheza Sindimba.
(picha zote na Sir Michuzi.)
Wednesday, May 7, 2008
Mbwembwe za Wanamuziki mazishi ya Madilu System
Wenger asikitishwa kuondoka Flamini
Kwa sababu alikuwa ni mchezaji huru tayari basi Flamini alionelea kuwa anaweza kupata “Handsome Package” mahala pengine zaidi ya hiyo. na habari ambazo hazijathibitishwa zinasema Inter Milan wamepania kumchukua mchezaji mwingine Alexander Hleb au hata Fabregas kabisa bado haijajulikana kama atakuwa bado kwa washika bunduki hao kwa msimu ujao ama la!!.
“I Am Because We Are” Makala ya Filamu ya Madona juu ya umasikini
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCHY2nynJII/AAAAAAAAARA/YCfnNzEihbA/s320/dd.jpg)
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/us.yimg.com/p/ap/20080506/capt.6223fb620b1c4652ae31c2b638564db8.people_madonna_malawi_joh101.jpg)
“I Am Because We Are,” ndio jina la makal ya filamu hiyo ambayo Madona ameitengeneza. Nia ni kuamsha uelewa wa watu kuhusu umasikini wa sehemu ya pili ya dunia, hatufanyi hivi kubeza, la hasha nia yetu ni kuwaonyesha watu kujua maisha halisi ya jamii nyingine na taabu wanazo pata ili kuamsha hari ya kujitolea kusaidia, alisema Madona.
Kati ya watu waliohudhuria uzinduzi huo walitaka kujua uguu uliopo katika kuchukua mtoto nchini malawi,
Madona alisema, “si kazi ndogo, inabidi ujitolee, inataka muda kwani ni suala geni kwenye utamaduni wao, halipo ama halijazoeleka”.
Filamu hii inaonyesha umasikini na maradhi yanavyochangia kugharimu maisha ya watu wa eneo husika. Madona ametaka watu kujitolea kusaidia, yeye alikutana na Banda alipokuwa katika harakati zake za kutoa misaada nchini Malawi.
Siku JB walipokutana na Koffi kwenye harusi ya Titina Alcapone.
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCGlMnynJEI/AAAAAAAAAQg/bweSqijF2M8/s320/kofi.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCGlM3ynJFI/AAAAAAAAAQo/wcS0TbMrzbE/s320/jb+mpiana.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCGlM3ynJGI/AAAAAAAAAQw/IhK2EIUl-d8/s320/jb.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCGm8nynJHI/AAAAAAAAAQ4/OV3cWfSd1V4/s320/titina+jb.jpg)
Lugha kuwabana wahamiaji ila si wachezaji waliopo.
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/a/p/afp/20080507/capt.cps.ncl72.070508121321.photo00.photo.default-342x512.jpg)
Chelsea wamuwania Sergio Ramos
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/a/p/afp/20080507/capt.cps.ncl75.070508121624.photo00.photo.default-411x512.jpg)
Tottenham wamtaka Etoo
![](https://i0.wp.com/d.yimg.com/a/p/afp/20080507/capt.cps.ncl84.070508124634.photo00.photo.default-512x417.jpg)
Inasemekana kuwa klabu ya Premier League ya Tottenham iko kwenye maongezi na klabu ya Barcelona kuhusu mchezaji huyu Mcamerun Samuel Etom limeripoti gazeti la michezo la Spain la sports daily Marca. Habari hazijafafanua kwambu ni wapi wamefikia kwenye maongezi hayo ila wanasema maongezi yanakwenda vizuri.
Schorali kumrith Ericson Manchester City?
![](https://i0.wp.com/www.4thegame.com/media/00/03/42/scolari_tantrum070706.jpg)
Kwa sasa mkataba unafanyiwa kazi kati ya Manchester City na Mwakilishi wa Kocha huyo Mreno Scolari ili aweze kuja Eastlands, Imefahamika kuwa Manchester City watavunja mkataba na kocha wa sasa Sven-Goran Eriksson baada ya msimu huu.
Thaksin kwa sasa anangojea jibu tu toka kwa Scolari, kama mkataba huo utakwenda kama ilivyopangwa basi kocha huyo ataondoka na donge nono la Paundi £3.2milioni kwa mwaka na mkataba unangoja jibu la mwisho ili upigwe muhuri. kwani kwa sasa kocha huyo yuko busy na kazi ya kuinoa timu Portugal kwa ajili ya Euro 2008.
Suala la kuondoshwa Ericson lilikuwa gumzo na hata katika mechi ya Manchester City na Chelsea majuzi mashabiki walionyesha kumuunga mkono kocha Ericson lakini ni suala la mmiliki na uongozi.
Kombe la Taifa na mfufuko wa soka letu
![](https://i0.wp.com/mwananchi.co.tz/image%5Ciringafunga.jpg)
Kwa kiasi kikubwa watanzania ni watu wanaopenda michezo sana hasa mchezo wa kandanda, itakumbukwa jinsi watanzania walivyojitolea kwa uzalendo mkubwa wakati Timu yetu ya Taifa ilipokuwa ikishiriki katika michuano ya Awali ya African Cup of Nations, kila mtu alionyesha uzalendo na watu wote walikuwa ama wanapeperusha bendeka iwe kwenye magari binafsi, daladala, Teksi, hata magari ya Serikali au ya Umma, iwe vibanda vya Chipsi au mabanda ya Mitumba, watu walinunua Jezi za timu ya Taifa lakini kama kamaida bahati haikiwa yetu.
Wengi walisema soka letu lingefanya vizuri kama michuano mbali mbali ingefufuliwa mbayo inachangia kupata wachezaji chipukizi kuchangia katika timu kubwa na Timu ya Taifa pia ili kuondoa utegemezi wa wachezaji wengi toka klabu kubwa za Simba na Yanga. Wengi wa wachezaji chipukizi jicho la TFF haliwafikii huko waliko, lakini kwa mpango kama huu wa Kombe la Taifa (TAIFA CUP) ni rahisi kuwaona wachezaji wenye moyo na chama cha makocha wakishirikiana na timu ya Ufundi ya TFF na Kocha mkuu pamoja na Msaidizi wanaweza kupata vijana wazuri kwa ajili ya timu yetu ya Taifa. Hongera Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na makampuni mengine pamoja na wadau bila kuwaacha TFF kwa kufanikisha hili.
Tunaimani kuwa kama michuano hiyo ikitumiwa vizuli inaweza kulisha timu kongwe na kuwa chachu ya kupata wachezaji wa Timu ya Taifa.
Tuesday, May 6, 2008
JB Mpiana: Tatizo lilo wapi?
Bonyeza Playa upate vitu:-
Msimamo wa Ligi Primier mpaka sasa.
2007/2008 English Premiership | |||||||||||||||||||||||
Kwa Ujumla |
Nyumbani | Ugenini | |||||||||||||||||||||
GP | W | D | L | GS | GA | W | D | L | GS | GA | W | D | L | GS | GA | GD | P | ||||||
1 | ![]() |
Man Utd | 37 | 26 | 6 | 5 | 78 | 22 | 17 | 1 | 1 | 47 | 7 | 9 | 5 | 4 | 31 | 15 | 56 | 84 | |||
2 | ![]() |
Chelsea | 37 | 25 | 9 | 3 | 64 | 25 | 12 | 6 | 0 | 35 | 12 | 13 | 3 | 3 | 29 | 13 | 39 | 84 | |||
3 | ![]() |
Arsenal | 37 | 23 | 11 | 3 | 73 | 31 | 14 | 5 | 0 | 37 | 11 | 9 | 6 | 3 | 36 | 20 | 42 | 80 | |||
4 | ![]() |
Liverpool | 37 | 20 | 13 | 4 | 65 | 28 | 12 | 6 | 1 | 43 | 13 | 8 | 7 | 3 | 22 | 15 | 37 | 73 | |||
5 | ![]() |
Everton | 37 | 18 | 8 | 11 | 52 | 32 | 10 | 4 | 4 | 31 | 16 | 8 | 4 | 7 | 21 | 16 | 20 | 62 | |||
6 | ![]() |
Aston Villa | 37 | 16 | 11 | 10 | 69 | 49 | 10 | 3 | 6 | 34 | 22 | 6 | 8 | 4 | 35 | 27 | 20 | 59 | |||
7 | ![]() |
Blackburn | 37 | 15 | 13 | 9 | 49 | 44 | 8 | 7 | 4 | 26 | 19 | 7 | 6 | 5 | 23 | 25 | 5 | 58 | |||
8 | ![]() |
Portsmouth | 37 | 16 | 9 | 12 | 48 | 39 | 7 | 8 | 3 | 24 | 13 | 9 | 1 | 9 | 24 | 26 | 9 | 57 | |||
9 | ![]() |
Man City | 37 | 15 | 10 | 12 | 44 | 45 | 11 | 4 | 4 | 28 | 20 | 4 | 6 | 8 | 16 | 25 | -1 | 55 | |||
10 | ![]() |
West Ham | 37 | 13 | 9 | 15 | 40 | 48 | 7 | 6 | 5 | 22 | 22 | 6 | 3 | 10 | 18 | 26 | -8 | 48 | |||
11 | ![]() |
Tottenham | 37 | 11 | 13 | 13 | 66 | 59 | 8 | 5 | 5 | 46 | 32 | 3 | 8 | 8 | 20 | 27 | 7 | 46 | |||
12 | ![]() |
Newcastle | 37 | 11 | 10 | 16 | 44 | 62 | 8 | 5 | 6 | 25 | 26 | 3 | 5 | 10 | 19 | 36 | -18 | 43 | |||
13 | ![]() |
Wigan | 37 | 10 | 10 | 17 | 34 | 49 | 8 | 5 | 5 | 21 | 15 | 2 | 5 | 12 | 13 | 34 | -15 | 40 | |||
14 | ![]() |
Middlesbrough | 37 | 9 | 12 | 16 | 35 | 52 | 6 | 5 | 7 | 19 | 22 | 3 | 7 | 9 | 16 | 30 | -17 | 39 | |||
15 | ![]() |
Sunderland | 37 | 11 | 6 | 20 | 36 | 58 | 9 | 3 | 6 | 23 | 20 | 2 | 3 | 14 | 13 | 38 | -22 | 39 | |||
16 | ![]() |
Bolton | 37 | 9 | 9 | 19 | 35 | 53 | 7 | 5 | 7 | 23 | 18 | 2 | 4 | 12 | 12 | 35 | -18 | 36 | |||
17 | ![]() |
Fulham | 37 | 7 | 12 | 18 | 37 | 60 | 5 | 5 | 9 | 22 | 31 | 2 | 7 | 9 | 15 | 29 | -23 | 33 | |||
18 | ![]() |
Reading | 37 | 9 | 6 | 22 | 37 | 66 | 8 | 2 | 9 | 19 | 25 | 1 | 4 | 13 | 18 | 41 | -29 | 33 | |||
19 | ![]() |
Birmingham | 37 | 7 | 11 | 19 | 42 | 61 | 5 | 8 | 5 | 26 | 22 | 2 | 3 | 14 | 16 | 39 | -19 | 32 | |||
20 | ![]() |
Derby | 37 | 1 | 8 | 28 | 20 | 85 | 1 | 5 | 12 | 12 | 39 | 0 | 3 | 16 | 8 | 46 | -65 | 11 |
Msimamo wa wafungaji hadi tarehe 5May na idadi ya magoli yao kwa ligi ya FA Primier
Rank | Mchezaji | Timu | Idadi ya magoli |
1 | Cristiano Ronaldo | Man Utd | 30 |
2 | Emmanuel Adebayor | Arsenal | 24 |
3 | Fernando Torres | Liverpool | 23 |
4 | Roque Santa Cruz | Blackburn | 19 |
5 | Robbie Keane | Tottenham | 15 |
Dimitar Berbatov | Tottenham | 15 | |
Benjani Mwaruwari | Man City | 15 | |
8 | Carlos Tevez | Man Utd | 14 |
9 | John Carew | Aston Villa | 13 |
Ayegbeni Yakubu | Everton | 13 | |
11 | Jermain Defoe | Portsmouth | 12 |
Wayne Rooney | Man Utd | 12 | |
13 | Steven Gerrard | Liverpool | 11 |
Nicolas Anelka | Chelsea | 11 | |
Gabriel Agbonlahor | Aston Villa | 11 | |
16 | Michael Owen | Newcastle | 10 |
Frank Lampard | Chelsea | 10 | |
18 | Dean Ashton | West Ham | 9 |
Dave Kitson | Reading | 9 | |
Mikael Forssell | Birmingham | 9 | |
Obafemi Martins | Newcastle | 9 | |
22 | Gareth Barry | Aston Villa | 8 |
Benedict McCarthy | Blackburn | 8 | |
Didier Drogba | Chelsea | 8 | |
Tuncay Sanli | Middlesbrough | 8 |
Kudwalika….
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SCAzqGNYU6I/AAAAAAAAAQY/pt29HtSTm0Y/s320/cam.jpg)
TBL yamwaga 140milioni kwa Kusaka mwanamuziki bora.
![](https://i0.wp.com/kilitimetz.com/images/jpg/kili_main.jpg)
Meneja Masoko wa Bia ya Kilimanjaro, Oscar Shelukindo alisema jana kuwa tayari TBL imetenga fedha hizo, zaidi ni kuenzi wasanii pamoja na kuibua vipaji vipya katika fani ya muziki.
” Nia yetu ya kudhamini mashindano hayo na kwa miaka saba sasa tumeibua na kukuza vipaji vya wasanii na kuwafanya watunge nyimbo ambazo zitaleta ushindani katika soko letu na kwa kiasi kikubwa tumefanikiwa,” alisema Shelukindo.
Alisema zoezi la kupendekeza wasanii ambao watashiriki katika tuzo hizo litaanza Mei 9 na Mei 28 utakuwa mwisho wa zoezi hilo na majaji wataangalia orodha ya asanii waliochaguliwa na kuakikisha kila aliyechaguliwa a akakaa kundi analostaili.
Shelukindo alisema Juni 2 watataja wasanii walioteuliwa na kila kundi litakuwa na wasanii watano Juni 4 watatangaza majina kwenye magazeti ili wananchi waweze kupiga kura kumchagua mshindi.
Alisema njia ya kutuma kupiga kura ni kwa ujumbe mfupi, kwa njia ya kuponi kwenye Magazeti na barua pepe.
Naye Mwenyekiti wa Tuzo hizo John Mhina alitaja vipengele vinavyoshindaniwa katika tuzo hizo kuwa ni Mwimbaji bora wa kike, Kiume, Albamu bora ya Taarab, Wimbo bora wa Taarab, Wimbo bora wa Mwaka.
Nyingine ni Wimbo bora wa Kiswahili, Albamu bora ya Kiswahili,, Albamu bora ya R’ n B’, Wimbo bora R’ n B, Wimbo bora wa Asili ya Kitanzania, Albamu Bora ya Asili ya Kitanzania.
Alisema Wimbo bora wa Hip Hop, Albamu Bora ya Hip Hop, Albamu bora ya Afrika mashariki, Mtunzi bora wa Muziki, Mtayarishaji bora, Mwandikaji nyimbo bora, Mtayarishaji bora wa Video, Mwanamziki aliyechangia mafanikio makubwa ya Muda, Wimbo bora wa Zouk na Mwanamziki au kikundi bora kinachochipukia.
Mwaka huu TBL haitaendesha mashindano ya Kanda kutokana na kukosa fungu la kuendesha mashindano kama ilivyokuwa mwaka jana.
Na Mwananchi
Kila Mtu alitaka kupiga picha na 50 Cent!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB_mpWNYU5I/AAAAAAAAAQQ/3CEjs_jvefo/s320/50c.bmp)
Kaseja Kutua Jangwani, Nsajigwa kwenda Simba!
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB_TPWNYU4I/AAAAAAAAAQI/tetPemIyi6I/s320/17898one.jpeg)
Golikipa wa Simba Juma Kaseja Juma, ambaye anasemekana anataka kuhamia Yanga.
Na Gobal Publishers
Happiness Magese aendelea kuchengua A.Kusini
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB-1cGNYU2I/AAAAAAAAAP4/nPsFDh2FyXc/s320/n668580395_483921_5962.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB-1cGNYU3I/AAAAAAAAAQA/DbtpjPECWDk/s320/n668580395_483925_6886.jpg)
Chelsea waunusa Ubingwa, waichapa Newcastle 2-0
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44628000/jpg/_44628359_ballack_big.jpg)
Magoli mawili yaliyopachikwa na Michael Ballack pamoja na Florent Malouda yalifanya mchezo wa jana jioni kuisha kwa ushindi wa 2-0 dhidi ya New CastleUnited na kuwafanya kuwa na point sawa na vinara wa Ligi hiyo Man U huku wakiwa na tofauti ya magoli.
Michael Owen kwa upande wa Newcastle alikuwa na nafasi mbili za wazi kipindi cha kwanza kuipa timu yake ushindi lakini nafasi hizo hazikuzaa matunda kwa kosa kosa ya kwanza dakika ya 18 baada ya kipa kutoka mpira uliokolewa na Mchezaji wa Chelsea akiwa yeye na goli pekee. na dakika ya 27 Ballack naye alikosa golo la wazi baada ya kupata pasi saaafi toka kwa Essien kwani Ballack hakuwa na haja ya kuwa na papara na mpira ule kwani tayari kulikuwa na watu wawili kwenye eneo la goli la Newcastle ambao Ballack angewachezea ule mpira walikuwa wanapata goli.
Mpaka mapumziko 0-0, baada ya mapumziko Chelsea waliumiliki mpira zaidi na kulishambulia lango la Newcastle na dakika ya 61 ya mchezo Ballack akatia kimiani gili mwanana kabla ya Malouda hajaongeza la pili.
Ushindi wa jana unaipa Chelsea nafasi nzuri kwani kwa sasa wamelingana point na Manchester wakiwa wote na Point 81 huku Manchester akiongoza kwa idadi ya magoli.
Manchester United, wanasafiri kwenda nyumbani kwa Wigan jumapili hii, wakiwa wanajua ushindi dhidi ya timu hii ndio utawahakikishia Kuchukua ubingwa tena msimu huu, na kuwaacha Chelsea ambao wanacheza na Bolton nyumbani kwao,
Timu hizi ndogo ndio huwa na upinzani mkubwa sana wanapocheza na timu kubwa kama Man U au Chelsea, Chelsea wananafasi kubwa ya kushinda kwani wanachezea nyumbani ilihali Man u wako ugenini.
Monday, May 5, 2008
Real Madrid Bingwa Primera La Liga
![](https://i0.wp.com/soccernet-assets.espn.go.com/design05/images/PH2/RMadrid.jpg)
Kwa ushindi huo basi Real Madrid wamefanikiwa kuongoza ligi hiyo na kuchukua ubingwa kwa msimu huu huku wakiwaacha wapinzani wao timu kubwa ya Barcelona ikiwa ya tatu na nyuma kwa point 35 dhidi ya 42 za Real Madrid.
Msimamo wa Ligi hiyo mpaka jana ulikuwa kama ifuatavyo:-
CLUB | GP | W | L | D | PTS | GD |
Real Madrid | 35 | 25 | 7 | 3 | 78 | 42 |
Villarreal | 35 | 21 | 9 | 5 | 68 | 17 |
Barcelona | 35 | 18 | 7 | 10 | 64 | 35 |
Atlético Madrid | 35 | 17 | 11 | 7 | 58 | 18 |
Racing Santander | 35 | 16 | 11 | 8 | 56 | 3 |
Sevilla FC | 35 | 17 | 14 | 4 | 55 | 18 |
Mallorca | 35 | 12 | 9 | 14 | 50 | 12 |
Deportivo La Coruña | 35 | 14 | 14 | 7 | 49 | 1 |
Almeria | 35 | 13 | 12 | 10 | 49 | -1 |
Espanyol | 35 | 13 | 13 | 9 | 48 | -4 |
Athletic Bilbao | 35 | 12 | 13 | 10 | 46 | -1 |
Real Betis | 35 | 12 | 14 | 9 | 45 | -4 |
Getafe | 35 | 11 | 15 | 9 | 42 | -6 |
Valladolid | 35 | 11 | 15 | 9 | 42 | -15 |
Valencia | 35 | 12 | 17 | 6 | 42 | -21 |
Real Zaragoza | 35 | 10 | 14 | 11 | 41 | -9 |
Osasuna | 35 | 11 | 17 | 7 | 40 | -6 |
Recreativo Huelva | 35 | 10 | 15 | 10 | 40 | -20 |
Murcia | 35 | 7 | 19 | 9 | 30 | -25 |
Levante | 35 | 7 | 23 | 5 | 26 | -34 |
Chelsea mtihani mzito leo
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB529mNYU1I/AAAAAAAAAPw/HoyAsxJZLb0/s320/drogba-celebrate.jpg)
Lakini juzi United ilishinda mechi yake nyingine dhidi ya West Ham United mabao 4-1 katika uwanja wa Old Trafford na kufikisha pointi 84 ikiwa imesaliwa na mechi moja dhidi ya Wigan.
Chelsea inayonolewa na Avram Grant leo italazimika kushinda ili kulingana pointi na Manchester na kisha kuiombea mabaya itoke sare au kufungwa na Wigan na yenyewe kushinda mechi yao ya mwisho dhidi Bolton na kutawazwa ubingwa.
Lakini United itatwaa ubingwa kama itashinda mechi yake ya mwisho dhidi ya Wigan hata kama Chelsea nayo itashinda mechi zake zote kutokana na kuwa na uwiano mkubwa wa mabao ya kufunga.
Liverpool yamchapa Manchester City Kimoja (1-0)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB50FmNYUzI/AAAAAAAAAPg/4QTo9YSbK3U/s320/liver.jpg)
Torres alimzunguka na kumuacha Richard Dunne na kuachia shuti kwenye angle na kuwafanya Liverpool kuongoza kwa goli 1-0, goli ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo.
Liverpool walikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa magoli mengi mchezo wa jana kwani kichwa cha Dirk Kuyt kiligonga mwamba na shuti la Ryan Babel kupaa juu.
Kijana Benjani kidogo awatoe nishai kwa mpira wa adhabu dakika za mwisho bahati ukaokolewa na Pepe Reina.
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB50FmNYU0I/AAAAAAAAAPo/DsqbKCOBIfQ/s320/man.jpg)
Kelele za mashabiki wakionyesha kumshangilia ni ishara kuwa bado wanaimani naye aendelee kuwepo katika timu yao.
Kapteni wa Liverpool Steve Gerald na Torres jana walicheza vizuri lakini umaliziaji haukuwa mzuri kwani kama nilivyosema Liverpool walitengeneza nafasi nyingi nzuri na za wazi lakini wao wenyewe walishindwa kuzitumia na kumalizia mipira kimiani. Mchezo ulikuwa mzuri na wa kasi huku kila timu ikijaribu kuonyesha uwezo wake huku Liverpool wakionyesha kubebwa na mashabiki wao wa nyumbani.
Hadi mwisho wa mchezo Liverpool 1-0 Man City, najua Michuzi unacheka tuu.
50 Cent achengua mashabiki Dar
Awali akiongea na waandishi wa habari baada ya kufika Dar, 50 alisema ana hamu sana kutembelea sehemu mbalimbali kila anakokwenda lakini ratiba ya waandaaji inamzuia kuona vitu vingine zaidi ya uwanja wa ndege, chumba cha hoteli na jukwaa la muziki.
ameeleza mipango ya kurejea bongo kama mtalii na kusema ana hamu sana kuona kwa macho yake mbuga ya serengeti na mlima kilimanjaro ambao amesema anatambua hauko kwa watani wa jadi.
amesema kwamba atalitilia maanani ombi la mwenyeji wake joseph kusaga kusaidia kunyanyua vipaji vya wasanii chipukizi wa bongo kwa kuomba propoza za afanye nini.
amesema kwa sasa anaelekea london, kisha los angeles ambako ana mradi wa filamu kubwa anayoshuti na mzee mzima al pacino. hakutaja jina lake ila itamalizika mwishoni mwa mwaka huu.
Kwa habari zaidi na picha zaidi Mtembelee Sir Issa Michuzi
Nani kuwa mshindi wa American Idol?
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB5q_mNYUvI/AAAAAAAAAPA/lVIDod8qeX8/s320/aidol.jpg)
Uchunguzi waonyesha American Idol yapungua Umaarufu
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB5oR2NYUuI/AAAAAAAAAO4/6c_aYJqPK1U/s320/idol.jpg)
Ingawaje American Idol bado ni show kubwa na ianyotazamwa na watu wengi zaidi, matokeo ya uchunguzi yanaonyesha umaarufu wa kipindi hiki unashuka kwa watazamani vijana wa umri wa kati hasa miaka kati ya 20 na 34. Mpaka kufikia mwisho wa msimu huu, Fox ndio watakuwa wanaongoza kwa kutazamwa na watu wengi zaidi kuliko kipindi kingine chochote.
Shoo hii imetazamwa na watazamaji takribani milioni 28.7 kwa mwaka huu, kwa mujibu wa kampuni ya Nielsen Media Research. hii ni chini kwa asilimia 7% ukilinganisha na jumla ya watazamaji milion 31 wa mwaka jana.
“Hatupingi kuwa idadi imepungua,” alisema ofisa wa juu wa Fox waandaaji wa American Idol Preston Beckman. “Kuna vitu unaweza kuvi control na vingine huwezi, hili liko nje ya uwezo wetu kwani kama ni ubora basi kipindi chetu kila mwaka kinazidi kuongezwa ubora ukilinganisha na kilichopita” alisema ofisa huyo.
Kuna vitu ambavyo viongezeka kwani waangaliaji walikuwa ni vijana hadi miaka ya mwanzoni ya 30 lakini kwa sasa hadi umri wa miaka 42 idadi ni kubwa.alisema Nielsen.
Kali kuliko yote ni wazee wa miaka hadi ya 50 ambao wengi waliohojiwa wameonyesha kuangalia zaidi vipindi vinavyoandaliwa na Fox Amerikan Idol ikiwa ni mojawapo.
Uchunguzi pia unaonyesha mashabiki kuchukia kitendo cha juma lililopita cha Paula Abdul, mmoja wa majaji wa AmeriCan Idol kuchemka kwa kutoa maoni ya wimbo wa pili wa mmoja wa washiriki ilihali wimbo huo ukiwa haujachezwa bado, hii iliwapa watu maswali mengi na kusema kuwa majaji wanakuwa na mtu wao kwani hata siku hiyo akiimba vipi uamuzi wanakuwa nao wao. Post ya kipindi hicho tuliitoa wiki iliyopita angalia chini au kwenye lebels gonga American Idol utaiona.
Sunday, May 4, 2008
Arsenal Yaichapa Everton 1-0
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB3Su2NYUsI/AAAAAAAAAOo/cHGkndnc2hg/s320/bendtner.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB3SvGNYUtI/AAAAAAAAAOw/lL52_AG_87w/s320/GaelClinchy.jpg)
Goli moja lililofungwa na Striker Nicklas Bendtner dakika ya 76 ya mchezo, limeihakikishia Arsenal nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi msimu huu.
Bendtner alifunga mpira huo kutoka krosi ya Armand Traore na kupachika kichwa maridhawa na kuupachika langoni mwa Everton.
Ingawaje mchezo wa leo Arsenal hawakuwa kwenye kiwango chao kwani kabla ya goli la Bendtner, Emmanuel Adebayor na Gilberto walikosa nafasi za wazi kufunga.
Andy Johnson na Joleon Lescott walicheza vizuri kwa upande wa Everton, ambao kwa kiasi fulani mechi hii ilikuwa muhimu kwao kwani wangeweza kujihakikishia nafasi ya tano ambayo ni muhimu kushiriki kombe la Uefa.
Kwa kichapo hicho cha kagolikamoja, Everton wamejipa mtihani mkubwa kwani katika mechi inayokuja wanakutana na Newcastle, wanahitajika kushinda ilikujihakikishia nafasi hiyo.
Kwa ushindi wa ManU jumamosi ya jana, Arsenal hawanan nafasi ya kuchukua ubingwa ila wanaweza kushindana na Chelsea kugombea nafasi ya pili.
Wenger akubali uamuzi wa kutonunua wachezaji unawagharimu
![](https://i0.wp.com/bp0.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SB0oOWNYUrI/AAAAAAAAAOg/at7_66Tu9WU/s320/939732895_c2d9a69930.jpg)
Wenger aliyasema hayo alipokuwa akiongelea ushindi wa Man U ambao kwa kiasi Arsena msimu huu ataondoka mikono mitupu, “ni wazi uamuzi wetu wa kutumia pesa kwa ajili ya uwanja mwaka 2004 ndio unaotutesa mpaka sasa, nina kikosi imara lakini ningekuwa na uwanja mpana zaidi wa mapendekezo ya kuimarisha timu kama tungekuwa na fungu la kutosha” alisema Wenger.
Ila bado matumaini yangu ni kwa kikosi cha vijana nilionao, naimani ni bora kutengeneza vijana nitakaa nao kwa muda mwingi kuliko kutumia pesa kumnunua mtu.
Arsenal waliamua kujenga uwanja mwaka 2004 uamuzi ambao ulisababisha Club kuingiza pesa nyingi, ni mkopo (Mortgage) wa muda mrefu wa Pound £300milioni ambao utailipwa kwa muda mrefu kwa hivyo pesa nyingi inatumika kulipa deni hilo.
“Kwa kipindi kile ndio ulikuwa uamuzi wetu sasa tulikubaliana kwenda na Policy mpya ambayo ni kutonunua wachezaji kwa gharama kubwa, najua kwenye mchezo huu hilo suala ni gumu kwani kila msimu ukiisha mashabiki wanataka kuona usajili mpya walao hata mmoja wa maana” alisema. Msimu huu tumepambana ingawa kombe si letu lakini tunajitahidi tusiwe mbali na washindi, tutajitahidi tufikie hizo point 83, zitatukea rekodi nzuri.
Emirates waliubadilisha jina uwanja huo wenye uwezo wa kukalisha watu 60,000, katika deal ya udhamini wa kiasi cha Pound 100m baada ya Klabu kukubali donge hilo, mkataba ambao utadumu kwa miaka 15 ikiwa ni pamoja miaka nane ya kuvaa jezi za shirika hilo la Ndege la Emirates.
Saturday, May 3, 2008
Taifa Stars yafanya kweli, yawanyuka waganda 2-0
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SByGQGNYUqI/AAAAAAAAAOY/DfiBbBbTz34/s320/tanzania.jpg)
Huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa Stars baada ya wiki chache zilizopita kufanikiwa kuitupa nje timu ya Taifa ya Kenya kwa jumla ya mabao 2-1 huku Uganda ikifanikiwa kuitoa Elitrea kwa jumla ya mabao 3-0.
Stars ikiwa na kikosi kile kile kilichoitoa Kenya isipokuwa kiungo Geofrey Bonny alichukua nafasi ya Athumani Idd aliyekuwa na kadi mbili za njano, ilianza mchezo wa jana kwa makeke makali na katika dakika ya 3 walikuwa wameshapiga hodi langoni mwa Uganda baada ya Uhuru Suleimani kupiga krosi lakini shuti la Amir Maftah likaokolewa na mabeki wa Uganda.
Bao la kwanza la Stars liliwekwa kimiani na Emanuel Gabriel katika dakika ya 12 baada ya kupata krosi safi toka kwa mshambuliaji machachari Mrisho Ngassa na kuunganisha mpira kimiani.
Shaabani Ndity aliyeingia kuchukua nafasi ya Henry Joseph mwanzoni mwa kipindi cha pili aliipatia Stars bao la pili katika dakika ya 60 baada ya kona safi iliyopigwa na Amir Maftah na kumkuta Nadil Haroub ‘Cannavaro’ ambaye alipiga kichwa kilichopanguliwa na kipa wa Uganda na kumkuta Nditi aliyepiga shuti kali na kutinga wavuni.
Katika dakika ya 15 Laurence Segawa alipewa kadi ya njano baada ya kumchezea madhambi Mrisho Ngassa ambaye alikuwa akiisumbua ngome ya Uganda kila mara.
Kipindi cha kwanza Stars walionyesha kiwango cha hali ya juu na kulisakama lango la Uganda muda mwingi wa mchezo.
Kipindi cha pili Stars walifanya mabadiliko baada ya Henry Joseph kutoka nje na nafasi yake kuchukuliwa na Shaaban Nditi, Uhuru Suleiman alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Ulimboka Mwakingwe Uganda alitoka Jeremiah Sebuyira na nafasi yake kuchukuliwa na Jonhson Bangole.
Dakika za mwanzo katika kipindi cha pili Uganda walitawala mchezo lakini Stars walitumia mwanya huo kufanya mashambulizi ya kushtukiza.
Katika dakika ya 63 Uganda walikosa bao baada ya kipa wa Stars Farouk Ramadhan kuupangua mpira ambao uliwahiwa na Nadil Haroub aliyeonyesha uwezo wa hali ya juu jana.
Na Mwananchi
Manchester YAUA, Yamtwanga mtu 4-1
![](https://i0.wp.com/soccernet-assets.espn.go.com/design05/images/JonMC/May2008/ronaldoo-412.jpg)
Ronaldo ambaye amefikisha magoli 40 sasa katika msimu huu wa ligi huku akisherehekea Tuzo ya Mwanamichezo bora aliyopewa na Chama cha waandishi wa habari wa Soka.
Goli la West Ham lilifungwa a Dean Ashton kupachika goli murua dakika ya 28 ya mchezo. Kabla ya M.Carick kupachika goli la nne na kuhitimisha karamu ya magoli kwa Manchester. Mchezo wa leo ulitawaliwa na rafu za hapa na pale kwani jumla ya kadi moja nyekundu aliyopewa Nani wa Manchester, na kadi nne za Njano moja ikiwa ya C.Ronaldo, na kwa upande wa West HAm walipewa kadi za njano ni L.Neil, G.McCatney, na B. Zamora.
Matokeo ya Mechi nyingine ni kama ifuatavyo
Bonyeza kwenye magoli upate Yaliyojiri pamoja na wafungaji wa magili hayo
FT | Aston Villa | 0 – 2 | Wigan Athletic |
FT | Blackburn R. | 3 – 1 | Derby County |
FT | Fulham | 2 – 0 | Birmingham C. |
FT | Middlesbrough | 2 – 0 | Portsmouth |
FT | Reading | 0 – 1 | Tottenham H |
Kalunde Band ndani ya Giraffe Ocean View Hotel
Halle Berry bado wamo.
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBwRxGNYUlI/AAAAAAAAANw/djkfe9nZDJs/s320/6758_701891816.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBwRxGNYUmI/AAAAAAAAAN4/LUA4Z_yiNxM/s320/2903_2153507070.jpg)
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBwRxWNYUnI/AAAAAAAAAOA/TrsBdEEGUs4/s320/8662_3853179023.jpg)
Kiingilio cha Taifa Stars na Uganda, Wananchi walia
![](https://i0.wp.com/bp3.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBvobmNYUgI/AAAAAAAAANI/1XhHs4FZx4o/s200/tanzania.jpg)
V/s
The Cranes
KIINGILIO cha mechi ya timu ya Tanzania,Taifa Stars na Uganda, The Cranes, itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba kimelalamikiwa na mashabiki wa soka hapa kuwa ni kikubwa.
Shirikisho la soka Tanzania, TFF limetangaza kuwa watakaotaka kuuona mchezo huo watalazimika kulipa sh,5,000 kwa mzunguko na sh,20,000 kwa jukwaa kuu.
Baadhi ya mashabiki wameanza kugwaya na kupanga kuusikiliza mchezo huo kupitia redio na kwa kile walichodai kuwa kiingilio ni kikubwa.
Taarifa mbalimbali zilizokuwa zikipatikana jijini humo kutoka kwa mashabiki na wapenzi wa soka tangu kutangazwa kwa kiingilio hicho zilikuwa zinasema kwamba kiingilio hicho ni kikubwa mno kiasi kwamba mashabiki wengi hawataweza kumudu hali ambayo inaweza kupunguza mapato kwa timu hizo.
Na Mwananchi
Leo ni Leo Taifa Stars Vs The Cranes
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/12/taifa-stars-01bc.jpg?w=448&h=336)
Tunataka kuwaonyesha Watanzania kuwa hatukubahatisha kuifunga Kenya tulipocheza nayo Dar es Salaam, leo tuna kila sababu ya ushindi pamoja na kuwa tunacheza na mmoja ya timu ngumu Afrika Mashariki.
Ushindi ni wetu tu tutafanya kila tuwezalo kuhakikisha tunashinda leo na kurudisha heshima ya Tanzania katika ramani ya soka Afrika.
Naye Jerry Tegete aliongezea kuwa wanatambua kuwa mechi ya marudiano itakuwa ngumu kwao watapokuwa nchini Uganda kwahiyo watacheza kwa moyo na kujituma wasiwaangushe mashabiki.
Kwenye mchezo lolote linaweza kutokea lakini sisi lengo letu ni kuhakikisha tunashinda na kujitegenezea mazingira mazuri ya kufuzu kwa hatua nyingine ya michuano hii.
Na Mwananchi
Shoo ya mavazi na vito vya madini yafana
Gattuso: Natamani kucheza Premier ligi UK
![](https://i0.wp.com/img.dailymail.co.uk/i/pix/2007/04_03/gattusoDM_468x328.jpg)
Timu za Uingereza zimekuwa katika heka heka za kutafuta wachezaji kwa msimu ujao wa ligi, wajuzi wa mambo wanasema Gattuso anaweza kuwa tumaini kwa vilabu vikubwa vya Uingereza na habari zinasema kumeonekana maajenti wa wachezaji toka Uingereza kwenye mechi za AC Milan bila kufafanua zaidi.
Video ya Wiki: Cristiano Ronaldo
Bonyeza Player ujue Ronaldo anakula nini, anaendesha nini, anapenda muziki gani, analala wapi anaendesha gari gani n.k, na hii ndio Video yetu ya wiki hii.
Ronaldo alamba Tuzo nyingine
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBwYzGNYUoI/AAAAAAAAAOI/6Gm1sepevkY/s320/MANU06-CR-03%7ECristiano-Ronaldo-Wallbangers-Posters.jpg)
Mchezaji wa Manchester United Cristiano Ronaldo (23) kwa mara nyingine tena amechaguliwa kuwa Mchezaji bora wa mwaka na Chama za Waandishi wa habari za Kandanda FWA (Football Writers’ Association) kwa mwaka wa pili mfululizo.
Winga huyo wa Ureno ndiye aliyechukua tuzo hiyo kwa mara ya pili baada ya Thiery Henry kuchukua tuzo hiyo mwaka 2004.
Zawadi hii inakuja baada ya wiki moja tuu kupata Tuzo nyingine kutoka kwenye chama kingine wakimtaja kama mchezaji bora wa mwaka.
Mshambuliaji wa Liverpool Fernando Torres na goilikipa wa Portsmouth David James waliambulia nafasi ya pili na tatu.
Kutokana na Tuzo hizi Ronaldo kwa sasa ndiye mchezaji pekee mwenye tuzo nyingi katika Ligi ya Uingereza.
“Kufunga magoli 38 katika msimu mpaka sasa si kitu cha mchezo, inaonyesha kipaji na kujituma kwa mchezaji husika, alisema mwenyekiti wa Chama hicho (FWA) Paul Hetherington.
“Hakupata asilimia 100% ya kura zote lakini tangu kura zianze kupigwa alikaa namba moja mpaka tunamaliza upiganji wa kura hizo alikuwa kileleni, hii inaonyesha ni jinsi gani watu pia wamemkubali”
“Kutokana na umri wake na namna ya uchezaji wake anayo nafasi ya kushikilia Tuzo hii kwa miaka, hiyo inategemeana na juhudi zake yeye mwenyewe kama ataendelea kujituma namna hii”
Furguson: “Hakuna wa kutuzuia Ubingwa”
![](https://i0.wp.com/newsimg.bbc.co.uk/media/images/44622000/jpg/_44622361_ferguson_203x152get.jpg)
Matokeo ya 2-1 na Chelsea yaliwafanya kuwa na pointi sawa kwenye msimamo wa ligi.
Lakini kocha Ferguson anasema ni lazima tukalie uongozi wa ligi, hata kama tuko na point sawa ila tumewazidi kwa magoli ya kufunga.
“Natarajia tutashinda mechi yetu na Westham jumamosi (leo) ambayo nauhakika itatuhakikishia kushinda ligi” alisema Furguson.
Wakati ManU wanakutana na Westham, Chelsea wao wanasafiri kwenda Newcastle jumatatu .
Defender Nemanja Vidic inawezekana asicheze kwenye mechi hiyo huku kukiwa na habari za matumaini kuwa Wayne Rooney hali yake imekuwa imeimarika hivyo anaweza akacheza pia, kwani aliukosa mtanange na Barcelona Manchester waliposhinda.
American Idol: Paula Hakulewa!
Kumekuwa na malalamiko toka kila upande wakishutumu kuwa Paula alikuwa na agenda ya siri na Jason kwamba anampenda na kutaka ashinde ndio maana alishindwa kuficha hisia zake.
Mariah Carey afunga ndoa na Cannon
![](https://i0.wp.com/blacknews.com/blackcelebritygossip/images/mariah_nick_engaged.jpg)
Carey na Cannon waliamua kwenda kufungia ndoa hiyo katika kisiwa moja ya visiwa vya Caribbean cha Eleuthera Jumatano hii, Henrietta White, ambaye anamiliki duka la maua kwenye kisiwa hicho cha Eleuthera, aliwaambia shirika la habari la E! News kuwa mwanaye ndiye aliyetengeneza maua kwa ajili ya harusi hiyo.
wawili hao wamefunga ndoa kwenye sherehe ndogo ambayo ilihudhuriwa na marafiki wa karibu na ndugu wachache sana.
Carey alimpenda sana Cannon, na hata katika video yake inayotarajiwa kutoka hivi karibuni , Carey amemtumia ameigiza kama mpenzi wa Cannon.
Mariah Carey amekuwa kwenye sekta ya muziki siku nyingi na kwa sasa Albam yake mpya ya E=MC2 ambayo aliitumbukiza sokoni tarehe 15 April inafanya vizuri sana na iko kwenye chati za juu ikiongoza, hivyo mafanikio bado anayo.
Carey amemuoa Cannon kwenye nyumba yake ambayo amenunua hivi karibuni kisiwani Eleuthera, habari kutoka kwa rafiki wa karibu wa mwanamuziki huyo maarufu ambaye alipata tuzo ya Grammy zilithibitisha.
“Wamekuwa pamoja kwa masiku sasa, mara nyingi wako pamoja, lakini mara nyingi wamekuwa na mikwaruzo ya hapa na pale, ni uhusiano ambao umedumu kwa mwezi mmoja kama mtu na rafiki wake wa kiume, sasa wameamua kuoana” alisema rafiki wa Carey.
PAmoja na suala la miaka kupishana sana lakini bado mapenzi ndio yaliyopelekea wawili hawa kufikia hapo, kwani Carey amemzidi mume wake kwa miaka 11.
Habari hii kwa msaada wa Ihano Kilonzo na FoxNews.
Friday, May 2, 2008
Je Unajua Ze Comedy ilipoanzia?
![](https://bongocelebrity.files.wordpress.com/2007/08/ze-comedy.jpg?w=450)
Nafasi imejaa Taifa Stars, walioikosa walie tuu.
![](https://i0.wp.com/bp1.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBqNdWNYUcI/AAAAAAAAAMo/U01ZI5uFV5g/s320/Taifa_Stars_026%5B1%5D.jpg)
KOCHA Msaidizi wa timu ya Taifa Stars, Ally Bushir amesema mfumo wa kubadilisha wachezaji timu ya Taifa sasa umekwisha na kama mchezaji hakupa nafasi hiyo huku nyuma sasa atafanya kazi ya ziada kuipata.
Stars ipo Mwanza ikijiandaa na mchezo wa kutafuta tiketi ya kucheza michuano mipya ya Mabingwa wa Afrika dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda mchezo utakaopigwa kesho jijini humo.
Bushir aliiambia Mwananchi juzi kuwa kocha mkuu wa Stars, Marcio Maximo amewaita wachezaji wale wale kwenye kikosi chake kwa kuwa ule muda wa kujaribu wachezaji kwenye kikosi hicho sasa haupo tena.
”Sisemi ya kwamba hawataitwa kwenye kikosi kama wakionyesha uwezo hapana, lakini watatakiwa kufanya kazi kubwa sana kwa kuwa wachezaji wengi kule wameiva na kuwatoa itawabidi waonyeshe uwezo sana,” alisema Bushir.
Mwananchi
Mkurugenzi wa Arsenal aachia ngazi.
![](https://i0.wp.com/soccernet-assets.espn.go.com/design05/images/domr/edelman205_g.jpg)
Mkurugenzi mtendaji wa klabu ya Arsenal Keith Edelman pichani, ametangaza kuacha kazi na klabu yake ya Arsenal imethibitisha habari hiyo.
Thursday, May 1, 2008
JB Mpiana alipompigia kampeni Kabila
Bonyeza player upate uhondo.
Siku 98 Zimebaki kwa Michezo ya Olympic ianze
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBnFD2NYUbI/AAAAAAAAAMg/uOkdUiR6Psw/s320/Img214331454.jpg)
Bird Nest: Uwanja wa Taifa wa Beijin China
![](https://i0.wp.com/bp2.blogger.com/_kW-lsRC7uYk/SBnCT2NYUWI/AAAAAAAAAL4/ybZWBE9pQ_4/s320/Img214247229_sss.jpg)
Uwanja huu una ukubwa wa Mita 330 kwa urefu, mita 220 upana, na una urefu wa mita 69.2, Uwanja umetumia jumla ya Mita za mraba 258,000. Umetumia jumla ya Kilomita 36 za chuma.
ambazo zina jumla ya Tani 45,000. kuna kilomita za mraba 11,000 za vyumba vya chini kwa chini (Underground rooms with waterproof walls.) Mpaka kukamilika uwanja unakadiriwa kutumia jumla ya USD 423 million USD.
Chelsea 3 – 2 Liverpool (4-3)
Didier Drogba ndiye aliyekuwa mwiba jana usiku kwenye mtanange wa kukata na mundu wa nusus fainali dhidi ya Liverpool
Mu Ivory Coast huyo ndiye aliyefungua kitabu cha magoli kwa shuti kali toka yadi 12 golini mwa Liverpool baada ya kipa kuutema mpira na kumfikia Drogba aliumalizia vizuri, lakini alikuwa Fernando Torres aliyeisawazishia Liverpool baada ya fowadi za Liverpool kuichambua ngome ya Chelsea na Tores kuutumbukiza mpira kwa shuti la chinichini, kwa vile mchezo wa jana ni lazima mshindi apatikane ikizingatiwa katika raund ya kwanza walitoka droo ya 1-1 ilibidi muda uongezwe baada ya kuwa sare ya 1-1 hadi daki 90 za mwanzo.
Magoli ya Lampard na Drogba dakika za nyongeza ndio yaliyoipeleka Chelsea fainali itakayo fanyika Moscoe mwezi ujao ambapo watakutana na Manchester.
Ikiwa ni mechi yake ya kwanza tangu afiwe na mama yake mzazi wiki iliyopita Lampard hakufanya ajizi kwani Kocha wa Chelsea alisema Lampard atamuenzi mama yake kwa kupachika goli huku akiwa bado kwenye majonzi, Baada ya kufunga goli hilo lililomchambua kipa kulia mpira kushoto Lampard alishangilia huku akishika kitambaa chake cheusi na alikwenda na kuinamisha kichwa chini mikono usoni akionyesha kumkumbuka mama yake mzazi.
Mchezo wa jana ulikuwa mkali sana na kosa kosa nyingi kwa kila upande, mpira ulikuwa mzuri Liverpool walicheza vizuri lakini bahati haikuwa yao.
Hali ya uwanja ilikuwa ya utelezi lakini Chelsea walionyesha kuimudu vilivyo labda ni kwa kuwa walikuwa wakichezea nyumbani na uwanja wao wameuzoea.
Hata hivyo goli moja la Essien lilikataliwa na msaidizi wa refa (L.man).
Chelsea wanakwenda kukutana na Manchester United katika Fainali zitakazofanyika mwezi ujao Moscow Urusi, mchezo ambao unatazamiwa kuwa mgumu, Pole Michuzi, Pole Balua, poleni Liverpool ndio ukubwa huo.
[…] Kumbukumbu mwezi MayMechi ya jana ilikuwa muhimu kwa Terry kupachika bao kwanza kama Kepteni kwa wakati mwingine chini ya kocha Capello na pili ni kufuta machungu ya kukosa penati siku saba zilizopita kwenye mechi ya Champions Ligi dhidi ya Manchester … […]
Trackback…
[…] … click here […]…
Tattoo Art Design Galleries…
[…]Kumbukumbu mwezi May « Spoti na Starehe[…]…
La Liga Fussball…
[…]Kumbukumbu mwezi May « Spoti na Starehe[…]…
kumbukumbu ya mwezi wa tano.
Vulli Sophie the Giraffe Teether…
[…]Kumbukumbu mwezi May « Spoti na Starehe[…]…
car rental business…
[…]Kumbukumbu mwezi May « Spoti na Starehe[…]…
best baby bath tub…
[…]Kumbukumbu mwezi May « Spoti na Starehe[…]…
It’s in point of fact a great and helpful piece of info. I’m glad that you just shared this helpful info with us.
Please keep us up to date like this. Thank you for sharing.