Soyons Serieux ya BCBG yaendelea kutesa Kinshasa

September 30, 2012

Tangu kutoka albamu ya Wenge BCBG ya Soyons Serieux imeendelea kutesa mitaa ya Kinshasa.

Kwa mujibu wa mtandao maarufu na unaoaminika wa Digital Congo albamu hiyo bado inatesa kwenye mauzo, kupigwa mitaani kwenye radio na hata kwenye sherehe. “albamu hii inanyimbo nyingi nzuri na zenye mvuto na kupigwa kifundi ambazo yeyote mpenda muziki hawezi kuacha kuzisikiliza hivi karibuni…” ilisema sehemu ya habari hiyo.

Hayo pia yamedhihirika hata upande wa pili wa Mto Congo yaani Brazaville ambako JB na kundi lake la Wenge wanapendwa zaidi, amekuwa akipata mialiko mingi ya huko na kila mara kupata interview za magazeti ama radio na hata kwenye vituo vya luninga. hii ni kuthibitisha jinsi gani kazi ya Binadamu Mukullu Papaa Cherie inavyokubalika.

Habari hiyo imemalizikia kwa kuwakaribisha wapenda muziki kwenye show ya BCBG kwenye kiota chao cha Crystal Club leo jumapili kilicho kwenye barabara ya June 30 kupata burudani mwanana. Nakuacha na kibao Bologna ambacho binafsi nakipenda sana ambacho kiko kwenye albamu hiyo ya Soyons Sirieux. Jumapili njema waungwana


Heritier Watanabehuenda akatimuliwa Wenge Musica Maison Merre

September 30, 2012

Mwanamuziki Heritier Watanabe wa WMMM

Mwanamuziki nguli na mwenye sauti ya Radi Heritier Watanabe toka kundi la Wenge Musica Maison Merre WMMM linaloongozwa na Grand Tata Werasson Ngiama Makanda anaweza kutimuliwa kundini.

Watanabe ambaye siku za karibuni amekuwa akigonga vichwa vya habari hasa baada ya kurejea kundini mwanamuziki wa siku nyingi wa kundi hilo Japonaise na kupewa uongozi. kumekuwa na vita ya kugombea madaraka kati ya Japonaise na Watanabe na kwa kiasi fulani Watanabe ambaye tangu awali anatabia ya utukutu amekuwa haheshimu ratiba za mazoezi, anagombana na wenzake kwenye kundi na hata kiongozi mkuu Werasson amekuwa hamsikilizi kilisema chanzo cha habari hizi.

Watanabe ambaye wiki mbili zilizopita aliachwa na bendi yake ilipokwenda kutumbuiza Muanda huko jimbo la Bas- Congo ikiwa nai adhabu baada ya kupayuka kwenye vyombo vya habari kuwa kuna upendeleo kwenye kundi lake na ye kuona kama hatendewi haki. Habari pia zimesema mwanamuziki Mwingine Papii Kakol aliwahi kupata adhabu kama hiyo pale alipoonyesha utovu na nidhamu wakati wa mazoezi ya “Zamba Playa” ni baada ya kukwaruzana na Wata, Wajuzi wa mambo wanasema kutoonekana kwenye show ile na hata juzi jumapili kwenye Show ya Kisenso hakuwepo inawezekana ndio byebye.

Mgogoro wa uongozi ambao washabiki wanauhusisha na matajiri ambao wanauhusiano na hasimu mwingine Koffi Olomide ambaye awali alikuwa rafiki mkubwa wa Werasson na sasa yuko kambi ya Jb Mpiana, habari zinasema kuwa Watanabe anachochewa na watu wa nje asikubali kuwa chini ya Japonaise  ambaye tangu arejee kwenye bendi baada ya kuwa nje kwa zaidi ya miaka kumi amekuwa gumzo kila bendi inapopiga.