-
Tresor Mputu amaliza adhabu ya mwaka mmoja na kurejea uwanjani kwa kishindo.
-
SAMATA azidi kung’aa
Mchezaji Tresor Mputu ambaye alikuwa kifungoni akitumikia adhabu ya mwaka mmoja baada ya kumfanyia fujo refa kwenye mechi ya TP Mazembe na APR ya Rwanda amerejea uwanjani kwa mbwembwe huku mashabiki wakimlaki kwa bashasha.
Tresor Mputu ni mchezaji ambaye amejinyakulia umaarufu si tu kwa Africa bali pale aliponyakua uchezaji bora kwa wachezaji wanaocheza ligi za huku Africa na pale alipofanikiwa kufanya majaribiribio na klabu ya Arsenal lakini bosi wa klabu yake ya TP Mazembe alipanda dau na kumbakiza.
Majuzi TP Mazembe walicheza na klabu ya TS Malekesa na klabu ya TP Mazembe ilishinda kwa bao moja, ikiwa ni katika ile ligi maarufu ya Vodacom Super League.
Leo jioni hiii Klabu ya TP Mazembe imeendeleza ushindi huku ilipocheza na Don Bosco katika mchezo wa Vodacom Super Ligi mchezo ambao uliisha kwa mabao 3-0 mabao hayo yalifungwa na SAMATA (15′), MPUTU (20′) na KIMWAKI (68′)
Pichani Mbwana Samata mbele na nyuma ni Tresor Mputu wakipambana na vijana wa TS Maleketa katika Super Ligi ya Congo.
Hii ilikuwa tarehe 19 Majuzi na leo TP Mazembe wameendeleza wimbi la ushindi walipocheza na Klabu ya Don Bosco na mpaka mapumziko TP Mazembe walikuwa wakiongoza kwa mabao 2-0 ambayo yamefungwa na Mbwana Samata na Tresor Mputu ambaye ametoka kwenye adhabu ya mwaka mzima.
Kikosi cha TP Mazembe ambacho kilicheza na TS Maleketa majuzi. Nyuma kushoto ni Mbwana Samata.
Mbwana Samata Hashikiki, Hapa jamaa akimshika bukta pamoja na hali ya hewa uwanja kujaa maji jamaa walikipiga na Mazembe walishinda.
Samata akikata Mbuga.
Pichani ni mchezaji Tresor Mputu akiwasili uwanjani chini ya ulinzi wa Polisi huku mashabiki wakimzonga.
Mashabiki wakifatilia mchezo wa TP Mazembe na TS Malekesa.
Kwa matokeo ya leo timu ya TP Mazembe imeshika nafasi ya pili na msimamo kamili ni kama ulivyo hapo chini.
Picha zote kwa hisani ya TP Mazembe
xxxx
@ Sergio
Sorry and Corrected
“mchezo ambao uliisha kwa mabao 3-0 mabao hayo yalifungwa na Tresor Mputu, Mbwana Samata na LUSADISU.”
Les buteurs sont SAMATA (15′), MPUTU (20′) et KIMWAKI (68′)
Merci Sergio, Merci Mingi
conglat’s Mbwana Samata for achievements you are get.ting.
conglat’s Mbwana Samata for achievements you are getting.
congalats SAMATHA.
naomba nipate list ya wachezaji wanaongoza kwa magoli katika ligi kuu ya kongo.
MAGAZETI
I want you to thank to your time of this amazing study!