JB mpiana aendeleza mashambulizi Rotterdam

May 30, 2008

JB mpiana aendeleza mashambulizi Rotterdam

JB Mpiana na kundi zima la Wenge BCBG wikiend hii liliendelea na ziara yao ya Ulaya na usiku huu walipiga Rotterdam katika Concert iliyofana lakini kutonogeshwa na baadhi ya vijambo.

Ukiachilia mbali ufinyu wa stage ambao JB Mpiana aliulalamikia sana pia “hujma” na “fitna” ya kukatiwa umeme ilipunguza utamu wa onyesho hilo. Lakini wapenzi wa muziki waliofika mapema walifurahishwa na jinsi Mpangilio mzima wa onyesho ulivyokuwa kwani JB na kundi lake walipiga Non Stop nyimbo zaidi ya kumi na mbili jambo lililonogesha na kuwachengua zaidi mashabiki waliohudhuria onyesho hilo. Ukilinganisha na onyesho la Sweden au Bruxells kwa idadi ya mashabiki onyesha la jana halikuwa na mashabiki wengi ki viiile!! kwani palikuwepo na hati hati ya kutofanyika na wengi walisafiri kumuona JB Sweden na Bruxells kabla. Mdau Twaha Makau na kati ya IFM nafikiri tuko pamoja.
Papa Cherry JB Mpiana Sultan Bin adam akiwajibika jukwaani jana.
Baadhi ya wanamuziki wa Wenge BCBG wakishambulia Jukwaa ipasavyo
Mmoja wa wakongwe wa BCBG Chai Ngenge. Mashabiki wakijinafasi

JB Mpiana Papa Cherry akimtambulisha mmoja wa mashabiki mpiga solo wa zamani wa bendi ya Chock Stars SOS Matondo.
Wapenzi wa muziki wakiwa karibu kabisa na Stage ili kuweza kuwaona Wenge BCBG