Tusker ya Kenya yashinda Kagame Cup 2008

July 27, 2008
Tusker ya Kenya wakishangilia na Medali zao, Picha na Habari Leo

Tusker ya Kenya wakishangilia na Medali zao, Picha na Habari Leo

Na Habari Leo

Timu ya Tusker ya Kenya leo ilitawaza kuwa mabingwa wapya wa taji la michuano ya Kombe la Kagame baada ya kuichapa timu ya URA ya Uganda kwa mabao 2-1 kwenye mchezo wa fainali uliofanyika kwenye Uwanja Mpya wa Taifa jijini Dar es Salaam. Read the rest of this entry »


Yanga yaingia mitini…”Pa panga hapaingii kisu”

July 27, 2008
Wachezaji na Viongozi wa Simba, Picha na Muhidini Issa Muchuzi

Wachezaji na Viongozi wa Simba, Picha na Muhidini Issa Muchuzi

Ama kweli “pa panga hapaingii kisu”, Timu ya Simba ya Dar Es Salaam leo imetangazwa mshindi wa tatu wa mashindano ya Kagame Cup baada ya timu pinzani ya Yanga kuingia mitini kwenye mchezo wao wa kugombea nafasi ya tatu, Yanga ambayo hadi sasa haijajulikana sababu ya kuikacha mechihii inasemekana kuwa ilitaka ilipwe 35,000,000 kabla ya kuchezwa kwa mechi hii, Hizi ni habari toka kwa wadau wa soka ambazo mpaka sasa hazijathibitishwa ila tutawaletea habari zaidi kadri tukizipata, KWa habari na Picha zaidi mtembelee Michuzi.


Pashoka hapaingii kisu, Ni Simba na Yanga Leo

July 27, 2008
Yanga na Simba Leo

Yanga na Simba Leo

Leo ndio leo Uwanja mpya wa Taifa nyasi za bandia zitakapowaka moto wakati timu za Simba na Yanga zitakapokutana katika kugombea nafasi ya Tatu ya Kombe la Kagame. Mchezo huu utachezwa Uwanja mpya wa Taifa na utaanza saa nane juu ya alama mchana. Yanga wanasema walijifungisha ili wakutane na Simba kwao ndio muhimu kuliko Kombe teh teh teh teh.


Portmouth na Manchester wakutana Nigeria Leo

July 27, 2008
Nigeria Jana

Nigeria Jana

Mchezaji wa Portsmouth Mnigeria striker Kanu Nwankwo akiongea na mchezaji mwenzie Sol Campbell wakati wa mchezo wao wa jana wa kirafiki kati ya Portsmouth FC na Kano Pillars FC ya Nigeria mchezo uliofanyika huko Abuja, Nigeria, Jumamosi July 26 2008. Portsmouth walishinda 5-0. Leo hii Timu ya Portmouth inacheza na Manchester United kwenye mechi ya kirafiki huko Abuja Nigeria.


ING CUP kukutanisha timu nne za Taifa

July 27, 2008
China

USA Olympic Team - China

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya soka ya USA kwenye michezo ya Olympig ikiwa katika picha ya pamoja uwanja wa ndege wa Hong Kong international airport  July 26, 2008 tkwa ajili ya kujipasha moto kwa ajili ya Michuano hiyo ya Olympic kwa kucheza kwenye michuano midogo ya kuwania Kombe la kampuni ya Bima ya Kimataifa ya ING, Michuano hii itashirikisha timu nne ikiwemo mbili toka Africa, Timu hizo ni Marekani, the Netherlands, Ivory Coast na Cameroon, itaanza tarehe 30 na kumalizika tarehe 2 August. (Photo:STANLEY CHOU/AFP/Getty Images)