July 15, 2008

Ze Comedy wakiwa katika moja ya maonyesho yao jijini.
Waigizaji wachekeshaji maarufu Ze Comedy jana walivamia ukumbi wa Bunge na kufanya kila mmbunge kutaka kuongea ama kupiga nao picha ya kumbukumbu.
Ilikuwa ni kipindi cha asubuhi cha Bunge kama kawaida Naibu Spika Mheshimiwa Anne Makinda alikuwa akisoma majina ya wageni waliokuwemo ukumbini humo kama ilivyoada na ndipo aliposhtuliwa kuwa miongoni mwa majina aliyosoma ni wanachama wa kikundi cha Ze Comedy na kushtuka na wabunge kulipuka kwa kicheko.
Kwa mujibu wa Naibu Spika kundi hili lilihudhuria kwa mualiko maalum wa wabunge wa majimbo ya mkoa wa Dar Es Salaam.
Nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya kipindi cha Bunge cha Asubuhi wabunge na maofisa wengine wa Bunge waliungana kwa pamoja na wasanii hao kwa maongezi ya hapa na pale na kupata picha kadhaa za kumbukumbu, Akiongea na waandishi wa habari kiongozi wa kundi hilo Wakuvanga alisema wameamua kwenda Dodoma ili kujua ni jinsi gain Bunge linafanya Kazi zake.
Miongoni mwa waliokuwepo ni Masanja, Joti, Mpoki na Seki.
Hivi karibuni serikali kupitia Wizara ya habari ilitoa tamko la kuingilia mgogoro uliopo kati ya kikundi hicho na tajiri yao wa zamani EA Television na kuagiza asasi zinazohusika kukaa pamoja na kulitolea maamuzi suala hilo haraka inavyowezekana.
Akiongea bungeni Naibu waziri wa Habari Utamaduni na Michezo bwana Joel Bendera alisema suala hilo limekabidhiwa kwa Chama cha Haki Miliki (Cosota) na kuongeza kuwa mkataba kati ya Ze Comedy na EATV umekwisha na kundi hilo limeingia mkataba mpya na TBC1 lakini wameshindwa kuendelea kwa sababu ya SAGA hilo. Spoti Starehe inawatakia kila la heri.
Leave a Comment » |
Burudani | Tagged: Bungeni, Ze Comedy |
Permalink
Posted by piusmickys
July 15, 2008

Mwanamitindo Ally Remtullah
Mwanamitindo anayekuja juu kwa Afrika Mashariki Ally Remtullah atafanya onyesho la Mavazi kwenye Gala Night Dinner siku ya ijumaa tarehe 18 July katika hoteli ya Bwawani.
Katika usiku huo wa kukumbukwa Ally Remtullah atawatumia vijana mamodel toka Zanzibar ikiwa ni jitihada za kukuza vipaji vya wanamitindo toka visiwani. Hii ni moja ya shamra shamra za International Film Festival mwaka huu. Maudhui ya ZIFF mwaka huu ni “Culture Crossroad” ikiwa ni kutaka kuonyesha muingiliano wa kitamaduni katika jamii na Remtullah atathibitisha hilo kwa mavazi ambayo yatakuwa na radha ya kitamaduni zaidi. (Picha na Michuzi)
Leave a Comment » |
Urembo/Mitindo | Tagged: Add new tag, Ally Remtullah, Mavazi |
Permalink
Posted by piusmickys
July 15, 2008

.
Final Call for Artists
The final deadline for receiving applications from artists interested in performing at the next Sauti za Busara is 31 August 2008.
The sixth edition of Sauti za Busara [Sounds of Wisdom] music festival takes place in Zanzibar during 12 – 17 February 2009.
The main aim of the Festival is to bring people together in celebration of the wealth and diversity of Swahili music. Every year the festival features more than forty groups, including thirty from East Africa and ten from other parts of Africa and beyond.
This year, the festival is especially keen to encourage more applications from Ethiopia and Horn of Africa, Southern Africa as well as more traditional music groups from East Africa.
Please note that without receiving your application and at least one recent recording, the festival selection committee will not be able to consider your participation when it meets at beginning of September 2008.
You can apply online in English, Kiswahili and French.
Assuming your group is selected and that it is possible to find sponsors for international flights, the festival will cover costs for local travel, accommodation and meals in Zanzibar, a modest performance fee – and a magical and unforgettable experience is guaranteed!
Yusuf Mahmoud, Festival Director
Leave a Comment » |
Muziki | Tagged: Sauti za Busara |
Permalink
Posted by piusmickys
July 15, 2008

Emanuel Adebayor uwanjani
BARCELONA inajiandaa kutuma ofa ya kutaka kumchukua Emmanuel Adebayor wa Arsenal kwa kumbadilisha na mshambuliaji wake Samuel Eto’o na kutoa euro milioni 10, kwa mujibu wa gazeti la Sport.
Gazeti hilo la kila siku la Catalan linaamini kuwa ombi lake la kutaka kumchukua mshambuliaji huyo kutoka Emirates litapata nguvu wiki hii.
Eto’o thamani yake ni euro milioni 30, ina maana kuwa kwa kuongeza euro milioni 10 itakuwa imefikia dau linalotakiwa na Arsenal.
AC Milan ilikuwa ikimtaka mshmabuliaji huyo wa Arsenal, lakini imeonekana kusuasua baada ya timu yake kuonekana kushikilia dau la kuuzwa mchezaji huyo ni euro milioni 40.
Kocha Pep Guardiola wa Barcelona, amekuwa akitaka kumchukua mshambuliaji mwenye nguvu baada ya kutangaza kuwa Eto’o hayumo kwenye mipango yake na taarifa zinasema Adebayor ni kipaumbele cha kocha huyo.
Leave a Comment » |
Burudani | Tagged: adebayor, Arsenal |
Permalink
Posted by piusmickys