Wapenzi wasomaji, nimehamisha Post zote toka anuani yangu ya zamani ya http://spotistarehe.blog.com kuja http://spotistarehe.wordpress.com. Hapa utaweza kuziona Post zote lakini hutoweza kusoma Comments kwa sababu zilizo nje ya uwezo. Pia kwa Post za Miezi iliyopita zinapatikana hapo Juu kwenye viungio vya Kuanzia May na June. Pius
Mpira si lelemama atii…
Simba yaanza vibaya Kagame lakini yaweka historia…
SIMBA imeanza vibaya michuano ya Kombe la Kagame baada ya kufungwa na Tusker ya Kenya mabao 3-2 katika mchezo wa ufunguzi ambao pia imeifanya michuano hiyo ianze kwa karamu ya mabao.
Kocha mpya wa Portugal

Friday, July 11, 2008
Miss Tanzania EU ajitoa kinyang’anyiro cha Miss Tanzania
Miss Tanzania EU 2008 – LUCY MWIZA FUNDIKIRA amejitoa katika kinyang’anyiro cha Miss Tanzania kinachotarajia kutifua baadaye mwezi ujao jijini Dar Es Salaam.
Hata hivyo habari zinasema Miss Lucy ni mmoja wa mamiss wanne ambao hawatoshiriki kwenye kinyang’anyiro hicho.
Mrembo namba mbili Kinondoni, Joan Faith pia amejitoa katika shindano na nafasi yake imechukuliwa na Miss Temeke namba nne Lilian Shayo baada ya warembo namba nne na tano wa kanda hiyo kushindwa kufika katika kambi hiyo,” alisema Lundenga.
Ze Comedy waenda Mahakamani
KUNDI la wasanii wa vichekesho la Ze Comedy limefungua kesi dhidi ya Televisheni ya EATV, Chama cha Hakimiliki Tanzania (COSOTA) pamoja na Msajili wa Nembo za biashara, likiomba Mahakama iwazuie kuingilia biashara zao na kuruhusu kutumia jina lao.
Kwa mujibu wa hati ya mashitaka iliyoko mahakamani hapo inaiomba Mahakama hiyo kutoa tamko kuwa walalamikaji hao ni wamiliki wa jina la Ze Comedy kabla na baada ya kuingia makubaliano na walalamikiwa.
Pamoja na maombi hayo pia wasanii hao wanaiomba Mahakama hiyo kuamuru walalamikiwa hao kulipa fidia ya Sh milioni 200 kama adhabu kwa usumbufu waliousababisha. Endelea kwa kusoma Habari Leo
Serikali yaruhusu Kagame Cup Wanja Jipya
SERIKALI imekubali kutumika kwa Uwanja Mkuu wa Taifa, Dar es Salaam kwa ajili ya mashindano ya Kombe la Kagame yanayotarajia kuanza kesho.
Akizungmza Dar es Salaam jana, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodeger Tenga, alisema serikali imekubali utumike kwa baadhi ya michezo, ambapo mingine itafanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam (uwanja wa zamani) na Jamhuri, Morogoro.
Alisema mchezo wa ufunguzi kesho kati ya Simba na Tusker kwa Kundi A na ule wa Jumapili Kundi C kati ya Yanga na APR itafanyika kwenye uwanja huo ambao ni mpya na wa kisasa, ambapo pia michezo ya robo fainali na nusu fainali itafanyika kwenye uwanja huo kama timu za Tanzania zitaingia hatua hiyo.
Pia alisema mchezo mwingine utakaofanyika kwenye uwanja huo mpya ni wa fainali na kuongeza kuwa timu za Tanzania zinapaswa kucheza kwa bidii kwani zimepata nafasi ya kuutumia. (Na Majira)
Wanasoka Gabriel, Nizar waelekea Ulaya kwa soka la kulipwa
WACHEZAJI wawili wa kimataifa wa Tanzania, Emanuel Gabriel na Nizar Khalfan wanatarajiwa kuondoka nchini kwenda barani Ulaya kusakata soka la kulipwa.
Katibu mkuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema Gabriel, ambaye anafunga ndoa Julai 14, ataondoka nchini Julai 19 kwenda Israel kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa, wakati Nizar anatakiwa Hungary.
”Kinachomchelewesha Gabriel ni harusi yake, anafunga ndoa mwezi huu tarehe 14. Isingekuwa harusi ungekuta ameshaondoka,” alisema Mwakalebela.
”Nizar pia yupo mbioni siku yoyote kuanzia sasa kwenda Hungary. Awali suala la viza ndilo lililomkwamisha, lakini kila kitu sasa hivi kinakwenda vizuri na ataondoka wakati wowote kuanzia sasa,” alisema.
Wachezaji wote wawili wana uzoefu wa kucheza nje ya nchi. Gabriel ameshakwenda Arabuni kucheza soka la kulipwa mara mbili na alirejea nchini mwishoni mwa msimu uliopita, wakati Nizar alikuwa nchini Kuwait kuchezea klabu ya Odlaham iliyomnasa wakati Stars ilipokwenda Uswisi kwa mazoezi.
Mwakaleleba pia alisema kuwa kiungo wa zamani wa Simba, Pius Kisambale na Erick Majaliwa wameondoka nchini juzi kwenda India na tayari wamesaini mkataba wa kuichezea klabu ya Dispot India ya nchini humo.
Alisema mbali na nyota hao pia beki wa Simba, Said Sued yupo kwenye hatua za mwisho za kukamilisha safari yake ya kwenda barani Ulaya kusaka soka la kulipwa. Sued aligoma kusaini Simba msimu huu.
Mbali na wachezaji hao kutimkia nje, beki aliyeachwa na Yanga, Lulanga Mapunda na Uhuru Selemani, ambaye klabu yake ya Coastal Union imeshuka daraja, wamemwaga wino kuichezea Miembeni ya Zanzibar.
Mwakalebela alisema wachezaji hao wapo kwenye orodha ya kikosi cha Miembeni kitakachoshiriki Kombe la Kagame inayoanza kesho jijini Dar es salam na Morogoro.
Wakati huo huo Mwakalebela amesema Cheti cha Uhamisho wa Kimataifa (ITC) cha kipa mpya Mserbia wa Yanga, Obren Curkovic kimewasili. (Na Na Mwananchi)
Blatter yuko sawa: Ronaldo
Soka ya wanawake si lelemama atii

Liverpool yaongeza nguvu
Warembo washawasili Bagamoyo
Wednesday, July 9, 2008
Chama cha riadha na TOC wavutana kuhusu wadhamini

Li-Ning
Kumekuwa na mvutano kati ya makampuni mawili ya Vifaa vya michezo kuhusu Ni vifaa vya kampuni gani Timu ya Taifa inayokwenda kwenye michezo ya Olympic itumie. Kampouni hizo ni Puma na Li-Ning ya China ambayo inakuja kwa kasi katika lebo ya vifaa vya michezo. Mvutano huu ni kati ya Chama cha Riadha Tanzania na Kamati ya Olimpiki Tanzania TOC.
Kauli hiyo ya TOC inafuatia ile ya AT kuwa wanaridha wake watatumia vifaa vya Kampuni ya Li- ning ambayo ndiyo iliyoingia nayo mkataba wa kutumia vifaa vyake wakati wa michezo ya Olimpiki.
Kambi Miss Tanzania iyooo
Mshindi wa nne, Sh2 .7 milioni na mshindi wa tano atajipatia Sh2.2milioni na washindi wa sita hadi wa 10 wataondoka na Sh1.3milioni kila mmoja.
Miss Temeke 2007 kwa Jicho la Michuzi
Tano bora Miss Temeke 2008 (Picha/Habari: Muhidini Michuzi)
Emperor Orlando na Saida Karoli katika na kitu Nsonyiwa
Afrika Kusini huenda Ikapokwa uandazi Kombe la Dunia 2010

Nchi ya Africa ya Kusini huenda ikanyang’anywa nafasi ya kuandaa mashindano ya Kombe la Dunia kwa kile kinachosemwa suala la usalama, akizungumza na idhaa ya kiswahili ya BBC Mjumbe wa kudumu wa CAF Said El Maamry alisema ni kweli minong’ono hiyo ipo na siku za karibuni imezidi, pia aliongeza Africa Kusini wamejiimarisha kwa maandalizi yote ikiwemo viwanja na mahoteli lakini tatizo ambalo watu wanaliona kwa sasa ni la kiusalama zaidi ambapo hivi karibuni kumeshuhudiwa watu wakiuana kwa ajili ya sababu za kimaisha jambo linalotishia usalama kwa wageni katika kipindi cha mashindano hayo. Lakini Elmaamry alionyesha wasiwasi wake juu ya jambo hilo na kusema kama watatumia hiyo ndio sababu basi mbona hata nchi ya Uingereza kila kukicha mnapigana visu? alihoji Elmaamry
Akijibu swali la mtangazaji Salum Kikeke juu ya Sitaki nataka ya FIFA kuhusu kufanyika kwa mashindano haya Afrika, Bw. El Maamry alisema kuwa Blatter ni kati ya watu ambao walitaka mashindano haya yafanyike Africa kwa nguvu zote na hii ni kutokana na ile Block Vote aliyoipata toka Afrika ikiwa ni jitihada zake za kuipigania Afrika na vile vile angependa kuweka historia kwa kuleta mashindano haya Afrika, na katika jitihada zake si tu kutaka yaje Africa bali kuja nchi ambayo ni ya Waafrica Weusi ukiziondoa nchi kama Tunisia, Morroco, Misri na nyingine ambazo zina waafrica Waarabu.
Elmaamry alisema kuwa ni kweli kulikuwa na bado kuna upinzani mkubwa toka kwa Executive members wa FIFA baadhi ambao hawakutaka mashindano haya yaje Afrika ya Kusini, sasa linapotokea hili la kiusalama wao wanapata sababu ya kukandamiazia na El Maamry alionyesha wasiwasi wake kuwa jambo hili linakuzwa zaidi na zile nchi ambazo zinataka kunyakua nafasi hii.
Baadhi ya viwanja vya Africa ya Kusini kwa ajili ya mtanange huo:-
King Senzangakhona Stadium, Durban, South Africa

King Senzangakhona Stadium usiku.

Port Elizabeth Stadium, Port Elizabeth, South Africa

Peter Mokaba Stadium, Polokwane, South Africa

Tuesday, July 8, 2008
Maboss wa Manchster na Liverpool

Newly elected ECA member of the board, CEO of FC Liverpool, Rick Parry, left, talks to Manchester United CEO, David Gill, right, after the first general assembly of the new European Club Association, ECA, at the UEFA Headquarters in Nyon, Switzerland, Monday, July 7, 2008. The European Club Association (ECA) is an new organization representing football clubs in Europe. Formed on the dissolution of the G-14 group in January 2008, it has 103 members, with at least one from each of the 53 national associations.
Ronaldo afanyiwa operesheni ya Ankle
Yanga yamshangilia Kaseja, Simba Yamzomea
Baada ya purukushani kuhusu usajili wake baina ya watani wa jadi Simba na Yanga na hatimaye Klabu ya Jangwani ya Yanga kufanikiwa kumchukua golikipa Juma Kasea Juma, jana klabu ya Yanga ilimtumia Kaseja pamoja na wachezaji wengine wapya iliyowachukua kwa msimu huu wa Ligi katika mchezo wake na Express ya Uganda.
Alipotoka tu mashabiki wa Yanga walimshangilia kwa nguvu na kuwabeza mashabiki wa Simba.
Mashabiki wa Simba, ambao pengine walikuwa hawaamini macho yao, mara walipomwona akiingia na wachezaji wenzake wa Yanga, walianza kumzomea na kumrushia matusi akiwa na wenzake, Mkenya George Owino na Nurdin Bakari, ambao pia walikuwa Simba msimu uliopita.
Kaseja, ambaye hata hivyo, hakupata purukushani kubwa katika mchezo wa jana, alikuwa na taabu , ambapo kila alipogusa mpira alikuwa akizomewa na mashabiki wa Simba wakati wale wa Yanga walikuwa wakimpa moyo.
Nurdin, ambaye alikuwa akicheza soka ya hali ya juu, naye alijikuta mara kwa mara akitukanwa na mashabiki wa timu yake ya zamani.
Pamoja na wachezaji hao waliokuwa na wakati mgumu, Yanga pia kwa nyakati tofauti iliwatumia wachezaji wake wapya, Godfrey Bonny, Kigi Makassy, Ally Shamte na Iddi Ally. Wachezaji wa zamani waliocheza walikuwa ni pamoja na Shadrack Nsajigwa, Athumani Iddi, Fred Mbuna, Ben Mwalala, Laurent Kabanda na Gaudence Mwaikimba.
AC Milan yakaza msuli kumnyakua Adebayo, Drogba

Mkurugenzi wa ufundi wa Klabu ya AC Milan Mbrazil Leonardo amesema kuwa Klabu yake ya Italy bado haijakata tamaa na iko kwenye mazungumzo ya maamuzi ya majaliwa ya wachezaji Didier Drogba wa Chelsea na Emmanuel Adebayor wa Arsenal, pictured in April 2008.
Lampard atabaki Chelsea: Scolari

Mapaparazi kazini

Bado naweza kuisaidia Lone Star: George Weah
Kepteni wa zamani wa Liberia na mchezaji bora wa FIFA kwa mwaka 2005 George Opong Weah amesema bado anajiona anajukumu la kufanya juu ya timu yake ya Taifa ya Liberia Lone Star.
Weah ambaye kwa sasa yuko USA kwa masomo amesema kwa sasa hawezi kuwa na nafasi ya kudumu kuifunza timu hiyo ya Lone Star.
Weah alikiambia kipindi cha BBC Fast Track kwamba kocha wa Liberia Antoine Hey hatumii ujuzi wake kwa ajili ya timu ya Liberia.
“Naweza kuwapa ushauri wa kiufundi, ninachoweza kwa sasa ni kufanya kazi na kocha pamoja na wachezaji, kuongea nao kuwafanya waone umuhimu wao kwa Taifa na kwa maisha yao pia, hicho ni kitu wanahitaji sana” alisema Weah.
“Nilimtaarifu [Hey] kuwa kuna wachezaji nimewavumbua vipaji vyao na wangemfaa kwa ajili ya kikosi cha Taifa, lakini alisema hapana anataka kutumia watu anaowajua yeye” alisema Weah kwa masikitiko.
Liberia ilicheza kombe la mataifa huru ya Africa mwaka 1996 na 2002, wakati huo Weah akiwa kepteni.
Prof Jay achana live Miss Vyuo vikuu
Dunga awaitwa Ronaldinho na Robinho kikosi cha Olympic
SAO PAULO, Brazil (AP)—Ronaldinho na Robinho (Pichani) ndio watakao ongoza kikosi cha Brazil kwa ajili ya mashindano ya Olympic kuwania medali ya dhahabu kwa michezo ya mwaka huu.
Nyota huyo wa Barcelona, Robinho pamoja na kikosi kingine cha wachezaji wengine 16 pia wameitwa na kocha Dunga kukamilisha kikosi hicho zikiwa zimebakia siku 15 kabla ya kuanza kwa mazoezi kwa ajili ya mashindano hayo.
Olympic ndio mashindano pekee ambayo mabingwa hao wa Kombe la dunia kwa mara tano wameshindwa kutamba nayo. Tangia mashindano hayo yaanze Brazili imefanikiwa kuchukua medali ya Silver mara mbili mwaka 1984 huko Los Angeles na 1988 huko Seoul Korea. Brazil pia walishinda medali ya bronze mwaka 1996 huko Atlanta ambapo Nigeria walishinda Dhahabu.
Dunga pia amemchukua defender wa Fluminense Thiago Silva ambaye ana miaka zaidi ya 23 pamoja na Ronaldinho and Robinho ukilinganisha na kikosi hicho cha Olympic ambacho nia yake ni kuchukua dhahabu, Dunga alisema wachezaji wengi walichaguliwa wamezaliwa 1885, pamoja na udogo wao wengi wao wana uzoefu wa kimataifa.
Kati ya hao wenye uzoefu ni pamoja na Diego, Mchezaji wa Manchester United Anderson, Lucas wa Liverpool na Alexandre Pato wa AC Milan.
Kaseja, Bonny, Owino waing’arisha Yanga
TIMU ya Yanga jana iliifunga Express ya Uganda bao 1-0 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa, uliofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku ikiwatumia wachezaji wake wengi wapya waliosajiliwa katika msimu huu.
Bao pekee la Yanga lilifungwa na Gaudence Mwaikimba aliyeingia kipindi cha pili akichukua nafasi ya Laurent Kabanda, dakika ya 69 kwa kichwa akiunganisha krosi ya Fred Mbuna ambaye alichukua nafasi ya Shadrack Nsajigwa.
Wachezaji wapya wa Yanga waliocheza jana na kuonesha kiwango cha kuridhisha ni kipa Juma Kaseja, Nurudin Bakari na George Owino waliotokea Simba, Kigi Makasi wa Mtibwa, Shamte Ally kutoka Kagera Sugar Godfrey Boniface wa Prisons na Idd Ali aliyepandishwa kutoka Yanga B.
Yanga ilianza mchezo huo kwa kushambulia lango la Express, huku mshambuliaji wake Bernard Mwalala akikosa nafasi nyingi za wazi hasa dakika za 19, 21 na 24, ambapo mashuti yake yalitoka nje na mengine kudakwa na Wahabu Geofrey.
Katika mchezo huo beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Canavaro’ ililazimika kukimbizwa hospitali kwa matibabu zaidi baada ya kuchezwa rafu mbaya na Lubwana Richard ambaye alitolea nje kwa kadi nyekunndu.
Dakika ya 40 Express waligoma kuendelea na mchezo kwa dakika tano, baada ya mchezaji wao kutolewa kwa kadi nyekundu wakidaia haikuwa rafu ya kutolewa nje, lakini viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) waliingilia kati na kuendelea na mpira.
Yanga: Juma Kaseja, Shadrack Nsajigwa/ Fred Mbuna, Nurudin Bakari, George Owino, Nadir Haroub ‘Canavaro’/ Wisdom Ndhlovu, Godfrey Boniface, Sahamte Ali/ Vicent Barnabas, Athumani Idd, Ben Mwalala/ Idd Ali, Lurent Kabanda/ Gaudence Mwaikimba na Kigi Makassy/ Amir Maftar. (Na Erasto Stanslaus wa Majira)
Richard kutoka na Filamu ya kukemea Mauaji ya Maalbino
Richard ambaye alikuwa Jijini Mwanza hivi karibuni katika kampeni zake za kupinga vitendo hivyo wanavyofanyiwa Maalbino hao aliyasema hayo akiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Maalbino wa kanda hiyo Alfred Kapore
Alisema, kwa kuthamini maisha ya Watanzania na majukumu yake kwa jamii, ameona analo jukumu la kuwaelimisha wananchi kwa kupitia filamu ili waondokane na imani za kishirikina na hivyo wasijihusishe na vitendo vya kuwaua albino ambao wanastahili kuishi katika jamii kama walivyo wengine. (Na Dar 411)
Wanazi wa mbio za magari
Niko na wanazi wa Mbio za Magari hii baada ya kuzifata Tanga ingawa mtu wetu hakushinda lakini si haba, asubuhi watu wakaamkia Mombasa maisha yakaendelea. Toka shoto Six, Tameem, Cathy, Mimi na Berty.Temeke yahitimisha kwa Angela kunyakua taji
Monday, July 7, 2008
Torres: Benitez ndiye mchawi wangu!!

Raha inapogeuka karaha michezoni

“Operesheni Vikombe” ya Chelsea yamtaka KAKA

Wanachama wamcharukia Rais Barcelona FC

Akina mama wa Afrika Kusini na Soka

LIMPOPO, SOUTH AFRICA – JULY 6: Wakinamama wa wakicheza soka huko kwenye mji wa Nkowankowa nchini Africa ya Kusini jana. Akina mama hawa hucheza mara mbili kwa wiki kujiweka fit na pia kuonyesha support yao kwa nchi yao kuandaa mtanange wa Kombe la Dunia 2010. Akina mama wa Tanzania mpoo? (Na Get Image).
Je Kitaeleweka leo?

Saturday, July 5, 2008
Fay Antony ashinda Miss Kinondoni 2008
Pichani Kati ni mshindi wa kwanza aliyelinyakua taji la miss Kinondoni 2008, Fay Antony yaliyofanyika jana usiku katika ukumbi wa Msasani Club,kushoto ni mshindi wa pili Joonfaith John na kulia ni mshindi wa tatu Amata Chryspin,aidha katika walimbwende hao kila mmoja aliibuka na kitita cha laki nane taslim
Pichani ni Miss Tanzania 2007 Richa Adhia akimvisha taji miss kinondoni 2008 Fay Antony usiku wa jana baada ya kulinyakua taji hilo. Giraffe Ocean View Hotel walidhamini wa shindano hili. (Picha/Habari Michuzi Jr)
Venus amshinda dadake kwenye fainali

(Picha na Yahoo Sport)

Hughes: Nipeni Ronaldinho nimrudishe kwenye nafasi yake

Man City ambayo imetoka kumsajili Mbrazil Jo kwa kitita cha Pound 19 milion akitokea CSKA Moscow imeonyesha nia ya kumtaka Ronaldinho.”watu wanahoji uwezo na nafasi ya Ronaldinho kwa sasa, mi namuona bado ananafasi kubwa ya kung’aa na anaweza kuvutiwa na program yetu ya mazoezi na kutengenezea ya kwake rasmi kuliko atakapo kwenda kwenye klabu kubwa ambapo wao watataka afanye kutokana na ukubwa wa jina lake” alisema Hughes.
Kwa sasa Ronaldinho yuko ziara ya Asia akitangaza bidhaa za Nike.
Man City wako tayari utoa Pound Milion 10 kama ada ya uhamisho kwa Barcelona ambayo itakuwa ni kwa mkataba wa miaka mitatu ambayo inathamani ya zaidi ya Pound 100,000 kwa wiki.
uwepo wakeBarcelona warned Friday that it would not sell its Brazilian striker Ronaldinho, who has been deemed surplus by the Spanish side’s new coach Pep Guardiola, at a discount.
Kura yako lwa Amanda tafadhali

Wakati shindano la kumtafuta Miss Universe 2008 liko kwenye mchakato mbali mbali shime watanzania tunapewa changamoto ya kumpigia kura Mrembo wetu Amanda, Shindano hilo litafanyika July 13 Jijini Nha Trang Vietnam nje kidogo ya mji wa Hanoi. Amanda Ole Sululu mnyange wa Kimasai ndio muwakilishi wetu kwenye mtanange huo. Pichani anaonekana Amanda akiwa ndani ya Vazi la Taifa, Hili ndilo Vazi ambalo mnaombwa kumpigia Kura ili ashinde kipengele hiki ambapo mchakato mzima wa kupiga kura unaanza Jumatatu tarehe 7, Kwa kupiga kura Bofra hapa kubonyeza hapa. Kumbuka kura nyingi ndio zinaweza kumpa nafasi Amanda. Kwa mapicha zaidi Gonga hapa
(Na Maria Sarungi)
Friday, July 4, 2008
Bushoke awarudishia Kili Music award tuzo yao
Bushoke alitwaa tuzo hiyo kupitia wimbo wa ‘Mbali Nami’ lakini amesema wimbo huo si wa kwake na unaitwa ‘Usiende.’
Akizungumza na gazeti la Mwanaspoti Bushoke alisema ameamua kurejesha tuzo hiyo kwa kuwa wimbo pamoja kwamba ameutunga yeye, lakini ni mali ya Juliana Kanyomozi wa Uganda.
“Mimi sielewi hawa mabwana wanafanya kazi vipi, kama ni nyimbo zangu zipo nyingi tu lakini kwa wimbo huo walipaswa kuwasiliana na mimi hata kunieleza nimeteuliwa badala ya kukurupuka na kunipa tuzo ambayo si yangu,” alilalamika.
“Ingekuwa tuzo ya uandishi wa wimbo ingekuwa yangu, lakini tuzo ya wimbo inatakiwa kwenda kwa Juliana kwa Juliana. Kwenye redio nyingi sana wimbo huo upo kwenye ‘tip 10’ na unatangazwa kuwa ni wa Juliana Kanyomozi akiwa ameshirikiana na Bushoke sasa wenyewe lipi hapo ambalo hawakujua,” alihoji msanii huyo. (Spoti & Starehe iliwahi kuandika kuhusu wimbo huo)
Meneja wa Bushoke, Athuman Tippo naye alisema wamechukua uamuzi huo wakiamini ni wa busara kwa kuwa isingekuwa vema Bushoke kujivunia kitu ambacho si chake.
“Bushoke ni kati ya wasanii bora na ana uwezo wa kufanya vitu vikubwa hivyo si vema akachukua tuzo ya mtu hata kama amepewa. Ipo siku atafanya hivyo kwa uwezo wake mwenyewe sababu anao,” alisema.
Bushoke, ambaye ni mtoto wa mkongwe katika miondoko ya dansi Maximilian Bushoke sasa anatamba na wimbo wa ‘Dunia Mapito’ ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya albamu yake mpya. Msimamo huo wa Bushoke umezidi kuonyesha namna utoaji wa tuzo za Kilimanjaro unavyoyumba na kusababisha lawama kwa wasanii mbalimbali. Waandaaji wa Kili Music Award wamezidi kulalamikiwa kutokana na mchakato mzima wa kuwapata washiriki na ugawaji wa Tuzo, Hivi majuzi muaandaaji wa muziki Bw. Said Comorein naye alilalamika kuwa yeye ndiye aliyetengeneza nyimbo nyingi zaidi ya nusiu zilizoshinda lakini yeye kama Prodyuza hakuambulia kitu
Gonga Player usikie wimbo wenyewe:
MAsikini Ngwea
Hivi karibuni Mangwea ameripotiwa kuwa anaishi nyumba ya kulala wageni (Guest House) na alisababisha kufungiwa na wenye Guest hiyo (Jina Kapuni) baada ya kushindwa kulipa pango (Bofya hapa). Kwa wanaomjua Ngwea wanasema bwana huyu kimziki alikuja wakati mzuri ambapo Bongo Flava imeshakubalika na wanamuziki walikuwa wakilipwa vizuri na kipindo hicho alishaingiza Albamu sokoni na kupata mshiko wa haja, Pia Ngwea ambaye alishiriki kwenye matamasha kadha wa kadha ikiwa ni pamoja na yanayodhaminiwa na makampuni makubwa kama TBL, Coca Cola, Celtel, Tigo na mengineyo ambayo hutoa mshiko mzuri kwa wanamuziki.
Wadau mbali mbali waliozungumza na dawati hili wanasema kimsingi hawaoni sababu ya Mwanamuziki huyu kuishi maisha hayo anayoishi kwa sasa kwani hata wanamuziki wenzie wanamkimbia kwani akikuona lazima akupige mzinga.
Mtangazaji wa kipindi cha Planet Bongo Salama Jabri aliwahi kuliongelea suala la wanamuziki kujisahau kwa kina na mapana na hata juzi kwenye mahojiano ya SS na mwanamuziki mkongwe wa Bongo Flava Solo Thang aliongelea kitu hicho (Bofya hapa uone).
Wanamuziki wengi wa ujio wa Ngwea wametoka kimaisha ingawa wengine sio sana lakini wanacho cha kuonyesha kidole, Sio nia ya safu hii kusema kuwa lazima Ngwea afike mahala fulani kimaisha la hasha ila kimsingi hakupaswa kuwa hapo alipo na bado ana nafasi ya kufanya mambo makubwa kwani ni mwanamuziki mzuri na anakubalika, “Ups and downs” ni sehemu ya maisha.
Ngwea ambaye awali alifahamika kama mkali wa Free Style alijizolea sifa nyingi na mashabiki wengi hasa kwa vibao vyake na wengi walipenda kumshirikisha katika nyimbo zao kwani kwa mujibu wa wanamuziki wenyewe wanasema Ngwea aukimpa maudhui ya nyimbo hata mkiwa Studio basi ndani ya dakika chache anaweza kukupa Mistari ya kutosha na mkaingiza sauti kwenye beat na mambo yakawa mswano na usipoangalia hata akakufunika wewe mwenye nyimbo. Nwea ameshirikiswa na wanamuziki kibao kama Jay Moe, Sarah Kaisi, John Mtembezi, Mchizi Mox, Feruz, Rah Pee, Daz Mwalimu, na wengineo wengi.
Pata Burudani toka kwake kibao Kimya Kimya toka kwa Jay More akimshirikisha Ngwea
(Picha na GPL)
Wazee wa Ngwasuma kazini
Wanamuziki wa bendi ya FM Academia a.k.a Waze wa ngwasuma, wakitumbiza wakati wa utoaji wa tuzo za muziki za Kili 2007 katika ukumbi wa hoteli ya Kempinski,jini Dar hivi karibuni.
Thursday, July 3, 2008
Mfungwa Schapelle Corby aruhusiwa kwenda Salon/Shopping

Mshtakiwa Mrembo Schapelle Corby akijaribu kufunika uso mbele ya wapiga picha jana alipokuwa akitoka Gardenia Salon kutengeneza nywele salon huko Denpasar, Bali.
Picha: AFP
Schapelle Corby ambaye anatumikia kifungo cha miaka 20 jela kwa kukuttwa na madawa ya kulevywa jana aliruhusiwa kwenda Saloon na kutengeneza nywele huko kwa muda wa masaa matatu na ushehe huko katika kisiwa cha Bali anakotumikia kifungo chake.
Corby anatumikia kifungo hicho tangu mwaka 2005 alipokamatwa na maofisa wa Polisi wa Indonesia huko Bali na kuhukumiwa kifungo hicho, kwa sasa ana miaka 30. Corby alipatikana na kilo 4.5 za Bangi siku alipokamatwa huko Indonesia mwaka 2005 ambapo aliziingiza akitokea Australia.
Ikumbukwe Indonesia ni nchi yenye waislamu wengi zaidi duniani na katika kisiwa cha Bali ni maarufu kwa watalii wa kila aina na huko kuna beach na mahoteli mazuri ya kitalii na ndio maana kuna matukio mengi ya Ugaidi katika kisiwa cha Bali ambayo yanaaminika kutoka kwenye vikundi vya Waislamu wenye siasa kali ambao wanapinga utamaduni wa magharibi unaingizwa huko na watalii na wenyeji wa maeneo hayo.
Corby ambaye kesi yake toka kukamatwa kwake imekuwa ni gumzo kipande hiki cha Mashariki ya Mbali ya Asia ameonekana mchangamfu na mwenye afya njema alikubaliwa kununua nguo kwenye shopping mall na pia alinunua viburudisho kama Ice Cream na kushiriki na ndugu zake.
Huku akisindikizwa na Polisi wawili wenye silaha za moto na Pingu hawakuruhusu mtu yeyote kumsogelea Corby ambaye siku za karibuni magazeti yaliandika alikuwa na mpango wa kujiua.
Kwa sheria za nchi nyingi za Asia ukikutwa na madawa ya kulevya na ikathibitishwa ni yako basi unanyongwatena kwa nchi kama Malaysia ninayoishi mimi au Singapore niliyopata kuishi kabla sijahamia Malaysia, Kukutwa na madawa ya kulevya yapaswa huku yako iwe imekamilishwa ndani ya masaa 48.
Corby alikuwa nchini Indonesia akijishughulisha na urembo ambapo alijipatia umaarufu sana kwa Indonesia, Malaysia, Singapore, Thailand na hata Hong Kong na Uchina.

Pichani ni Corby akiwa ameshikiliwa na wanausalama akirudishwa Jela baada ya rufani yake kutupiliwa mbali, hapa alionekana mdhoofu sana.
Mwezi uliopita Corby alilazwa kwa kuwa na Msongo wa Mawazo (depression) alilalamika kuwa angependa kwenda kutumikia hukumu hiyo ambayo kama atamaliza atatoka akiwa na miaka 50, Nchini kwake Australia makundi mbali mbali yanajitahidi kufanya kampeni za kutaka serikali imhurumie na kumfutia adhabu Corby kama sio kumpunguzia muda wa kuitumikia adhabu hiyo.

Mkalimani Eka Sulistiowati (shoto) akimshika Corby baada ya Jaji kusoma hukumu ya miaka 20 dhidi yake mwaka 2005
MISSTemeke 2008 wametangaziwa zawadi
MISSTemeke 2008 wametangaziwa zawadi zao na waandaaji wa Shindano hilo litakalofanyika jumapili ijayo TCC Chang’ombe Dar es Salaam
Akizungumza na waandishi wa Habari leo Mratibu wa Onyesho hilo Benny Kisaka alisema wanasababu kuu mbili za kutoa zawadi za kulingana, kwanza warembo watakuwa na siku mbili za kujiandaa na fainali za taifa ambapo watatakiwa kuingia kambini julai 9, hivyo kiwango cha pesa kutawawezesha kufanya maandalizi kuliko kuwapa vitu.
“Warembo watatu wa kwanza katika fainali hiyo watapata Sh 800,000 kila mmoja sanjari na kujipatia tiketi ya kuiwakilisha wilaya ya Temeke katika fainali za Vodacom Miss Tanzania 2008″ alisema Kisaka
Aidha, alisema washindi wa wanne na watano kila mmoja atapata Sh 300,000 na waliobaki watapata kifutajasho cha Sh 100,000 kila mmoja.
Kiingilio cha Shindano hilo ni Sh. 50,000 kwa viti maalumu itakayoenda sambamba na chakula kamili cha jioni na Sh. 10,000 kwa viti vya kawaida.
Pia litaenda sambamba na burudani kutoka kwa Bushoke na Bendi ya B band ikongozwa na Banana Zoro na baba yake Zahir Zorro.
Warembo watakaochuana katika shindano hilo kutoka kitongoji cha Kigamboni ni Rona Swai, Florence Josephat, Kitongoji cha Kurasini ni Caroline Sechuma, Evanuru Isaac na Glory Charles.
Soma Zaidi Kwa Msimbe Lukwangule
FIFA nayo yamchinja Rage
Ismail Aden Rage
*Mwenyewe hatambui, adai TFF imemfitini Na Sophia AShery wa Majira SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), limemtolea nje aliyekuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania Ismail Aden Rage kurudi katika nafasi yake na kumtaka kusubiri Uchaguzi MKuu kama anahitaji kuwa kiongozi wa TFF. Hatua hiyo imetokana na majibu ya barua aliyoandika Rage kwenda FIFA akipinga uamuzi wa kutorudishwa katika nafasi yake uliotolewa na Kamati ya Nidhamu ya TFF iliyokutana Aprili 26 mwaka huu. Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu MKuu wa TFF, Fredrick Mwakalebela alisema TFF ilipokea barua kutoka FIFA iliyoandikwa Juni 24 mwaka huu na kusainiwa na Katibu Mkuu Jerome Valcke. Mwakalebela alisema katika barua hiyo FIFA imesema uamuzi uliotolewa na Mkutano MKuu wa TFF kumuondoa Rage katika nafasi hiyo ni sahihi kwa kuwa katiba ya TFF inafanya kazi, hivyo uamuzi huo umezingatia katiba. Kwa Habari Zaidi Bofya Hapa |
|||||||||||||
Samaki mkunje angali mbichi

Ronaldinho akiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kutoa mafunzo kwa vitendo kwa watoto wa Shule maalum ya michezo, Wenzetu wanaanzia mbali
- Sie tunang’ang’ana na wazee!! -
Ni usajili kwa kwenda mbele…

Mchezaji mpya wa timu ya Barcelona Daniel Alves toka Brazil, kati, Rais wa Klabu ya Barcelona Joan Laporta, kulia, na Kocha wa Barcelona Pep Guardiola, wakiwa katika picha ya pamoja walipokamilisha usajili wa Mbrazili huyo hapo jana.
Karibuni Nyumbani vijana wangu…

Rais wa Russia Dmitry Medevedev akiongea wakati alipokutana na timu ya Taifa ya Russia katika makazi yake huko Meindorf nje kidogo ya jiji la Moscow, Jana July 2, 2008. Russia walipoteza mchezo wa nusu fainali dhidi ya Waispaniola.
Jo ajiunga na Man City

Wednesday, July 2, 2008
Mambo ya Bongotyube.com
Mdau Issa Michuzi anawaambia hivi:-
Habari na Issa Michuzi
Tuesday, July 1, 2008
Kaijage wajibu Wazalendo hawa…
“Habari yako,
pole na shughuli nzito ya kuwakilisha jamii.Sisi Vijana wa Tanzanite fc Ya Atlanta Ga tunasikitika na habari tuliyosoma juu ya mchezaji wetu aliyewakilisha timu yetu ya taifa huko Cameroon kwa kuadhibiwa kwa kulipia jezi ya timu ya taifa aliyobadilishana na mchezaji mwenzie wa Cameroon(Etoo) tumeona kwamba ni swala la aibu kwa chama cha soka cha Tanzania kumdai mchezeji huyo hasa ukizingitia mchango wake kwa Taifa.
Sisi Tanzanite fc tungependa kujitolea kulipa deni hilo la huyo mchezaji. Je ni utaratibu gani tuutumie kuwakilisha mchango huo, na je ni kiasi gani?Tunatanguliza shukrani zetu kwa msaada wako kutufanikishia swala hili.
Wako
Tanzanite fcAtlanta,GA.
USA”
HAYA KAKA KAIJAGE
Majaji wanakazi bwana…
Tenga: Jezi mali ya mchezaji Taifa Stars

Raisi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Leodgar Chilla Tenga(pichani).
*Ampa tano Cannavaro kumvulia jezi Eto’o.
Na Erasto Stanslaus wa Majira
RAIS wa Shiriksho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amempongeza beki wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Nadir Haroub ‘Canavaro’ kubadilishana jezi na mchezaji wa kimataifa wa Kameruni, Samuel Eto’o katika mchezo wa marudiano wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika 2010 uliofanyika mjini Younde, Kameruni.
Baada ya mchezo huo kumalizika ‘Cannavaro’ alifuatwa na Eto’o anayecheza klabu ya Barcelona ya Hispania akitaka wabadilishane jezi baada ya pambano hilo kumalizika ambapo Stars ilichapwa mabao 2-1 yaliyofungwa na mchezaji huyo.
Tukio hilo limeibua mjadala baada ya Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage akikaririwa na vyombo vya habari akisema ‘Cannavaro’ atakatwa sh. 20,000 kwa kitendo cha kubadilishana jezi na Eto’o.
Mchezaji mwingine iliyeingia katika mzozo huo ni Jerry Tegete ambaye alibadilishana jezi na mchezaji Jean Makoun wa Kameruni anayevaa 11. Tegete alivaa jezi nambari 10 katika mchezo huo.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Tenga alikata mzizi wa fitina na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusiana na sakata hilo na alimpongeza beki huyo akisema amefanya kitendo cha kishujaa kutoa jezi ya Taifa bila kujali kama atadaiwa au la.
“Canavaro amefanya kitendo cha kishujaa kwani sasa tunakwenda na wakati kwani angekataa kutoa jezi kwa kuhofia kudaiwa ulimwengu usingetuelewa na kutoa jezi ni kuitangaza nchi,” alisema Tenga.
Nahodha huyo wa zamani wa timu ya Taifa, alisema kuanzia sasa TFF imepitisha uamuzi kila mchezaji wa Stars ataondoka na jezi aliyovaa siku ya mchezo bila kujali alicheza uwanjani au la baada ya pambano kumalizika na itakuwa mali yake.
Tenga alisema kimsingi waliokuwa wakimdai ‘Cannavaro’ jezi hiyo walikuwa wakitimiza wajibu waliojipangia kati ya uongozi wa Stars na wachezaji lakini alionya kuwa walishindwa kuangalia mazingira halisi ya tukio husika.
Baadhi ya wadau wa mpira wa miguu wameuponda uongozi wa TFF kutokana na kitendo hicho hicho na walikuwa tayari kuwalipia gharama za jezi hizo ‘Cannavaro’ na Tegete
S.S – Inampongeza Bwana Tenga kwa kutoa ufafanuzi huo.
Tunaomba na vingine vyenye utata mjitokeze mapema kutoa ufafanuzi kabla mambo hayajaaharibika au kuwafanya mashabiki na wapenzi kuwa na fikra mbadala.
Spoti na Starehe
Lucy Fundikira ndiye Miss Tanzania EU.
Mgeni rasmi Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mheshimiwa Ngemera akimvisha Taji la ushindi, Bi Lucy Fundikira baada ya kutangazwa mshindi wa Miss Tanzania EU, Lucy atashiriki kwenye Miss Tanzania huko Dar Es Salaam.
Miss Tanzania EU 2008 – LUCY MWIZA FUNDIKIRA (holland), 1st Runner up – SABRINA BASHIR (Germany), 2nd Runner up – JACQUILINE SABANYA (Germany)
Washiriki wakitupa karata ya mwisho mbele ya mashabiki na majaji.
Mkurugenzi wa Ethiopian Airlines kanda ya Ujerumani na Central Europe Mr. Esayas Hailu Akimkabidhi mshindi tiketi ya ndege ya kwenda na Kurudi Dar Es Salaam.
Miss Tanzania EU 2008 – LUCY MWIZA FUNDIKIRA akipita mbele ya washabiki baada ya kutangazwa mshindi jana usiku.

Mwanamuziki Ali Kiba akipagawisha mashabiki wakati wa shindano la Miss Tanzania EU.
Godlove Muliahela mwenye kofia ndiye aliye aliye imba wimbo wa Taifa wakati wa mashindano hayo akiwa na washindi wa pili na watatu na wadau.
Lucy akionyesha Ticket aliyopewa na wadhamini wa shindano hilo ambayo itamuwezesha kwenda Tanzania na kurudi kushiriki kwenye shindano la Miss Tanzania mwezi August. Tiketi hii imetolewa na Ethiopian Air Lines na kampuni ya EAS logistic ya Köln imetoa 20kg cargo ya kwenda Dar, ikiwa ni mizigo ya yake na vifaa vya maandalizi.(Picha zote na Nashe Mvungi wa Ujerumani)
Pata kionjo cha mwanamuziki Ali Kiba wakati wa mashindano hayo:-
Ballack ana “gundu” na dhahabu!

Baada ya kupoteza Ubingwa mwezi may kwenye Champions League akiwa na Chelsea, Michael Ballack juzi alikuwa looser tena baada ya timu yake ya Ujerumani kulikosa Kombe la EURO2008 na kuambulia medali ya Silver.
Ballack alikuwa kikosi kilicho chapwa na Manchester United na kuchukua Kombe katika mchezo uliochezwa Moscow Urusi na juzi ameshuhudia Fernando Tores wa Liverpool akipachika kagoli kamoja na hivyo kuwanyima ushindi.
Hii sio mara ya kwanza kwa Ballack, mwaka 202 alipokuwa akichezea Bayer Leverkusen walichapwa 2-1 na Ral Madrid kwenye fainali ya Champions Ligi. wakati Kepteni wa Spain Iker Casillas ambaye alikuwa Real Madrid walishinda kwa upande wao.
Ballack ambaye aliumia siku ya ijumaa kabla ya mtanange wa juzi na hivyo alikuwa na hati hati ya kucheza hadi dakika za mwisho Daktari wake aliposema anaweza kucheza.
Aliwahi kukaa miezi saba bila kucheza baada ya kuumia mguu pia mwaka 2007, na kurudi dimbani mwezi wa pili walipocheza mechi ya kirafiki na Austria na kuwatwanga 3-0.
Ballack alikosa mechi 10 kwa timu yake ya Taifa, na ndio ilikuwa ya kwanza kupata tiketi ya michuano hii.
Ballack mkataba wake na Chelsea unamaliziaka 2009 na 2010 itakuwa nafasi pekee kwake na timu ya Taifa kupigania kikombe kikubwa kwenye mtanange wa Kombe la Dunia nchini Afrika ya Kusini.
David Villa, Mfungaji bora EURO 2008

Jina la David Villa (pichani juu) bado ni mwiba kwa baadhi ya Timu kwani aliwatungua bila huruma, Pamoja na kutokucheza Fainali dhidi ya Ujerumani bado Bado Villa amechukua nafasi ya ufungaji bora baada ya kupachika kimiani mabao manne katika michuano hiyo.
Villa alifunga jumla ya mabao hayo manne kwenye mechi mbili pekee za mwanzo za Spain , ikiwa ni matatu walipocheza na Russia na goli moja walipocheza na Sweden.
Ufungaji wake wa magoli matatu kwenye mechi yao na Russia ilimfanya kuwa ndiye mfungaji aliyefunga magoli matatu katika mechoi moja tangu mwaka 2000 ambapo Mholanzi Patric Kluvert alifanya hivyo.
Villa mwenye miaka 26 hivi sasa anasakamwa na Vilabu vikubwa ili kumchukua kwa msimu ujao wa ligi zao, inasemwa Chelsea, Arsenal, Real Madrid na Liverpool ni moja ya vilabu ambavyo vinamhitaji mchezaji huyo.
Villa aliwaongoza Lukas Podolski wa Ujerumani, Roman Pavlyuchenko wa Russia, Hakan Yakin wa Switzerland na Semih Senturk wa Turkey walipata jumla ya magoli matatu kila mmoja.
Pia wachezaji 12 walifanikiwa kufunga magoli 2 kila mmoja kwenye michuano hii, Daniel Guiza na muuaji wa wajerumani Fernando Torres, wote toka Hispania. Mjerumani Michael Ballack, Miroslav Klose na Bastian Schweinsteiger wao pia walifunga magoli mawili kila mmoja.
(Picha na GI)
Posted by piusmickys 










Kampuni ya Uniliver imedhamini Sh milioni 10 kwa michuano ya kikapu ya Miji Mikuu ya Afrika Mashariki kati na kusini









Gonga player hapo chini Kupata Sebene la Werason na vijana wake, Muangalie kwa makini stage show wa Wera anaitwa Bibiceya Mufwengi. Selamat Datang…




mambo yameshaiva na tayari warembo takriban 10 wako tayari kugombea taji la miss morocco, kitongoji kinachosifika kwa walimbwende wilaya ya kinondoni. mambo yatakuwa pale new msasani club nyuma ya ubalozi wa marekani kuanzia saa mbili usiku ambapo fm academia wana wa ngwasuma wanaotamba na kibao cha ’si kila mwanamke aendaye baa ni malaya’ watakuwepo kusindikiza usiku huo unaosimamiwa na mama wa mitindo aisa idarous, Habari hii na Muhidini Issa Michuzi ambaye ni mmoja wa wadhamini wa shindano hilo. Hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania wameamka na kuanza kuzipa nafasi Blog kama sehemu ya Media na mchango wake kuthaminiwa katika jamii.





Timu za Manchester United (Pichani) na Portsmouth zote za Uingereza zinatarajiwa kucheza mechi ya Kirafiki nchini Nigeria mwishoni mwa mwezi ujao wa July. Mpaka Sasa Timu ya Manchester United imekwisha thibitisha habari hizo na kusema itacheza mchezo mmoja tuu, ilihali timu ya Portsmouth wao watacheza na timu ya Taifa Super Eagle. Tayari Uingereza imekwisha tuma maofisa wake nchini Nigeria kufanya maandalizi ya timu zake ikiwa ni pamoja na kuukagua Uwanja kwa ajili ya mechi hiyo.
Polisi jijini Dar Es Salaam wamethibitisha habari zinazohusu Kukamatwa kwa wachezaji wa Timu ya Taifa ya Ndondi ambayo ilikuwa nchini Mauritius.
























BENDI maarufu ya muziki wa dansi nchini ya Akudo Impact ‘Wazee wa Masauti’ wataongoza burudani katika mashindano ya kumsaka mrembo wa kitongoji cha Sinza Ijumaa kwenye Ukumbi wa Vatican City, Sinza.

Selamat Datang Ke Malaysia, Hikli tangazo limo ndani ya Train ya Umeme sasa OLE wako!! Hii ndio Malaysia!. Hahaha Denda maana yake ni Adhabu!!, (USd 1=3.2 RM-Malaysian Ringit)



Anaitwa Klynn, Miss, Mwanamitindo na Mwanamuziki, mtembelee kwenye wavuti wake kwa kubofya hapa au waweza Tembelee 8020 uone Wadrobe yake na Mamaa Zeze.








Wiki iliyopita niliandika habari ya Vijana wa Ifakara wanaoburudisha watu na kuelimisha kuhusu janga la Ukimwi (Bofya hapa usome tena) , kutokana na vifaa duni wanavyo tumia nashukuru Mdau mmoja msomaji wa Blog hii toka Japan anafanya mipango ya kuwapatia vyombo vya muziki vijana hao na mambo yakikamilika tutawaletea habari kamili, Wiki hii tunakutana na vijana wa Mitaani ambao waliamua kuanzisha Bendi yao katika kujitafutia lizki na kutumbuiza mitaani jijini Dar es SalaamVijana hawa walinaswa na Kamera ya Global Publishers hivi karibuni maeneo ya Soko kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakiburudisha watu kwa kuwapigia muziki ili kujipatia chochote. Vijana kama hawa wanatakiwa wapewe msaada na kuendelezwa.










Mashabiki wa Holland wakiwa mitaani wakisherehekea ushindi dhidi ya Ufaransa, Mashabiki wa Holland ambao wanaongoza kwa staili yao ya ushangiliaji na mavazi ya rangi ya chungwa wamejaa na wanazidi kumiminika mjini Bern ambapo ndio kituo cha Timu yao, mji mzima umekuwa rangi ya Chungwa.


Kundi la ucheshi la Ze Comedy leo mchana limekilalamikia kituo cha Televisheni cha East Africa kwa kuwawekea pingamizi la kutumia staili za ucheshi walizokuwa wakitumia walipokuwa kituo hicho kama wataamua kuendelea kufanya shughuli hiyo iliyolipatia kundi hilo umaarufu mkubwa.
Klabu ya Chelsea imethibitisha kumchukua kocha wa timu ya Taifa ya Portugal Mbrazir Luiz Felipe Scolari kama Manager na Kocha mkuu wa timu hiyo. Mbrazir huyu ndiye aliyeonekana kuweza kurithi mikoba ya Grant darajani Stamford.
Baada ya kuonyesha maajabu kwenye mchezo wa juzi mchezaji wa Spain David Villa ameanza kusakamwa na madalali wa wachezaji wakimtamanisha kwa donge nono ili afikirie kusajili na timu zinazowakilishwa na Maajenti hao. Habari zinapasha kuwa maajenti wa Vilabu vikubwa vywa Uingereza ndio wanaongoza kwa kutaka kufanya mazungumzo na Villa.
Wachezaji wa Italy toka shoto Daniele De Rossi, walinzi Andrea Barzagli, Marco Materazzi na Fabio Grosso, striker Luca Toni na forward Marco Borriello wakipiga jalamba wakati wa mazoezi ya timu yao kwa ajili ya michuano ya Euro 2008 huko Maria Enzersdorf karibu na jiji la Vienna leo June 11, 2008. Italy watacheza na Romania katika mchezo wao wa kundi C tarehe 13 keshokutwa.
Aliyekuwa muigizaji maarufu Husna Shabani ‘Dotnata’ na mumewe Mohamedi Poshi wakivishana pete mara baada ya kutambulishana katika sherehe iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Msasani Beach ambako kulikuwa na hafla ya ya kuitambulisha ndoa yao kwa ndugu, jamaa na marafiki iliyofanyika usiku wa kuamkia leo.
Mmoja wa Ma-Mc kati ya Ma-Mc 10 waliokuwepo ukumbini humo msanii wa fani ya maigizo Muhsin Awadh ‘Dk Cheni’ akimwaga sera zake kwa maharusi Dotnata na mumewe Mohamedi Poshi.
Mashabiki wa Czech na Portugal wakishangilia kabla ya mechi kati ya timu zao leo, Mpambano huu unatazamiwa kuwa mkali kwani kila timu ina kiwango kizuri cha mchezo.
Siku ya Kuoa au kuolewa ni siku pekee ambayo mtu anatakiwa asiisahau kwani kwa wengi wanaoamini siku hii huja mara moja ila kama tuu kutakuwa na ndoa ya mitala. Inaitwa Under water Wedding, ni maarufu kwa kipande hii ya Asia (Malaysia na Thailand) kwa Malaysia Chama cha Waogeleaji ndio mtaji wao mkubwa wakishirikiani na Hotel kubwa ambapo utapenda Harusi yako ifanyike. Package ya harusi hii ni Malaysian Ringit 160 (55,000 Tsh) kwa kila kichwa na idadi ya chini ni watu 60. Hii inakuwa ni pamoja na Vinywaji na Vilaji kwa waalikwa wako,
Keki kwa ajili ya maharusi, Champagne 5, Mitungi ya Gas kwa ajili ya maharusi na yeyote atakaye hitaji kuzamia, Albamu ya Picha pamoja na DVD moja ya kumbukumbu ya tukio zima, Fataki 10Kg, pamoja na gharama za kuiandikisha ndoa na Cheti cha Ndoa kwa anayetaka anakaribishwa kuja Malaysia hakuhitaji VISA kwa Mtanzania.
Pichani Kushoto (Khadija Mwanamboka na Mama Asia Idarous wa FABAK Fashions) ambao ni moja ya viongozi wa shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Mitindo house wakizunguza na waandishi wa habari hivi karibuni jijini Dar kuhusu onesho lao la mavazi watakaloliita KIMASO MASO litakalofanyika ukumbi wa Waterfront juni 13/08,Kuanzia saa Moja Usiku,Kwa Kiingilio cha 12000/= Tu.













Mchezaji wa Los Angeles Galaxy David Beckham akiwa na mwanaye Brooklyn akipozi kabla ya mchezo wa Ligi ya kikapu kati ya Boston Celtics na Los Angeles Lakers jana jumanne, Bekham amekuwa gumzo tangia aingie USA na kila anapokwenda watu hujitokeza ku chill naye.






Timu ya Taifa ya
Ushindi wa magoli 3-0 walioupata wa Dtch dhidi ya waitaliano umeinua nderemo si tu kwa kushinda mechi hiyo bali kusherehekea ushindi wa kwanza dhidi ya Italy tangu mwaka 1978, Pichani mchezaji wa Netherlands Ruud van Nistelrooy (R) akifunga goli la kwanza wakati wa Mchezo wa kundi C wa Euro 2008 didi ya Italy. Netherlands waliwabugiza mabingwa wa Kombe la Dunia mabao 3-0. Katika mchezo ulikuwa mkali na wa kusisimua, goli la pili la Netherlands lilifungwa na Wesley Sneijder dakika ya 31 na kufanya Netherlands waende mapumziko kwa kuongoza 2-0. Kipindi cha pili kilianza kwa piga nikupige huku Italy wakuionyesha matumaini kidogo lakini ushambuliaji na Ngome ya Netherlands vilikatisha tamaa waitaliano na dakika kumi kabla ya mchezo kumalizika Giovanni Van Bronckhorst akaipatia timu yake bao la tatu na kuhitimisha karamu hiyo ya magoli, Rafiki yangu Tanzania Dreams wa India alitabiria kuwa hawa jamaa wamo katika watu wanaweza kuondoka na kikombe mwaka huu na dalili zinaonekana.
Angeline Jolie akiwa na Jack Black walipokutana kwenye tamasha la filamu la Canes, Inasemwa Angeline amejifungua mapacha na Mashuirika makubwa ya Habari yametangaza dau kubwa kwa ajili ya picha ya kwanza ya Watoto/Mtoto wa Jolie. Kazi kwenye mapapa na mamamarazi.
Anaitwa Kim Kardashian, Mwanadada huyu huwaacha “Wakware” mate yakiwatoka kila apitapo kwa shepu yake hutoa Tips za urembo kwa akina dada kwenye Blog yake, picha hii ilipigwa wakati yeye pamoja na wifi yake wakifanya Shoping ya Furniture. Gonga hapa utapata vitu vyake

Magoli mawili yaliyofungwa na
Jana, pale MovenPick Hotel, MultiChoice Tanzania ilitangaza rasmi kuonesha michuano ya UEFA kwenye mtandao wake wa DSTV iliyoanza rasmi jana. Pichani ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Lucy Kiwhele, akinadi mpira katika bahati nasibu iliyochezeshwa hotelini hapo kwa wageni waalikwa!











Mshindi wa Taji la Miss Dar Indian Ocean Joan Fast (katikati) akionesha tabasamu mara baada ya kutwaa Taji hilo katika ukumbi wa Cine Club Mikocheni Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.Kushoto kwake ni mshindi wa pili wa Taji hilo Grace na kulia ni mshindi watatu Groly. Picha na 
Je unapenda Logo, Wallpaper, Ring Tones na Video Ipod za Euro 2008?
Mchezaji wa timu ya Taifa tya Ufaransa Claude Makelele amesema Ufaransa inawezakushinda bila Kepteni wao Patrick Vieira ambaye ataukosa mpambano wa ufunguzi kutokana na maumivu ya kwenye mguu sehemu ya paja.
Zimebaki siku chache kabla mkataba wa kocha Mbrazili Marcio Maximo (pichani) umalizike, Mengi yamesemwa kuhusu kocha huyu mgeni ambaye jukumu lake ilikuwa ni kutupeleka CAN, tunaiangalia leo Stars kwa macho mawili , Tujaribu kujiuliza je dhumuni lilifikiwa na tuangalie tulikotoka na tulipo sasa na nini kifanyike.
Fikiria jinsi watu walivyohamasika kwa timu yao ya Taifa kipindi tunagombea kucheza CAN Ghana!! Nafikiri kwa kiasi kikubwa tumeona mabadiliko ingawa ni kweli mabadiliko hayawezi kuja mara moja. kwa mfumo wetu wa Soka wa kukusanya wachezaji dakika za mwisho hatuwezi kuona mabadiliko kwa muda mfupi kamwe. Ni lazima tuwe na Program ya muda mrefu na muda mfupi, muda mrefu ni kwa Serikali kuimarisha michezo kuanzia ngazi ya shule za msingi, na kuimarisha mashindano kama ya Taifa Cup.

Picha na 


Miss Tanga2007, Miss Tanzania Kanda ya Kaskazini, Redds fashion Ambassador Victoria MartinAmbaye amepata mikataba na kampuni za Modelling za South Afika. Hivi karibuni alikwenda South Afica kuangalia soko la uanamitindo na tayari kampuni mbili zimevutiwa naye na kumpa mapendekezo yao. Kampuni hizo ni O Model na EXTRA. Soma hapa zaidi

TIMU ya taifa ya soka, Taifa Stars inaondoka leo alfajiri bila ya mchezaji wake nyota, Mrisho Ngassa na kiungo Abdi Kassim, huku kocha, Marcio Maximo akiahidi kwenda Cape Verde kupambana, na Naibu Waziri wa Habari, Michezo na Utamaduni, Joel Bendera akigeuka mbogo kwa wachezaji.
Sanamu kubwa zilizotengenezwa kwa sura na maumbo ya wachezaji kutoka Timu za Nchi tofauti duniani zanazoshiriki Kombe la EURO 2008 wakiwa ni pamoja na Michael Ballack na Philipp Lahm toka Germany, Karim Benzema na Patrick Vieira toka France, Angelos Charisteas toka Greece, Petr Cech wa the Czech Republic, Cristain Chivu wa Romania, David Villa toka Spain, Tanquillo Barnetta toka Switzerland, Andreas Ivanschitz wa Austria and Robin van Persie wa Netherlands.
Cristiano Ronaldo wa Ureno akipozwa baada ya kulia sana wakati wa mchezo wa Fainali ya EURO 2004 kati ya Ureno na Ugiriki (Portugal na Greece), Baada ya Ureno kupoteza mchezo huo kwa goli 1-0. hii ilikuwa Euro 2004, Je mwaka huu atalia au atacheka?
NEW YORK – “Entertainment Tonight” walitangaza jana habari za kujifungua mcheza Sinema maaruf Angelina Julie ila kila wakati walikuwa wakisisitiza kuwa habari hizi ni kwa mujibu wa chanzo chao. Hata Shirika kubwa la habari la Associated Press katika taarifa yake limesema kuwa wao walipokea e-mail iliyotoka kwa mtu aliyejitambulisha kama mtu wa karibu na mcheza Sinema huyo. Kumekuwa usiri mkubwa kuhusu kujifungua kwa Angelina Julie tangu ijumaa ya wiki iliyopita, habari hizo zinasema mwanadada huyo amejifungua Mapacha.
Tambara kuuubwa likipitishwa kwenye jukwaa la mashabiki katika Kupigia debe jiji la Rio De Janeiro kuwa muandaaji wa michezo ya Olympic 2016, Hii ilikuwa ni kwenye mchezo wa Mzunguko wa pili wa mchezo wa nusu fainali ya kombe la Libertadores Cup kati ya Fluminense ya Brazil na Boca Junior ya Argentina, Mchezo ulichezwa Rio de Janeiro, June 4, 2008. Fluminense alishinda 3-1
Miss universe tz 2008 Amanda katika Pose, Mdau wangu Jimmy Mlay anasema wanakuwaga wapi hawa mbona mitaani hatuwaoni?





Nahodha wa Italy Fabio Cannavaro akiwa ameshikilia Kombe la Dunia wakati timu yake iliponyakua kombe hilo mwaka 2006. Nahodha huyo na mchezaji wa timu ya Real Madrid hatokuwemo kwenye kikosi cha Italy cha sasa kitakachoshiriki mtanange wa kombe la UEFA – EURO 2008 baada ya kuumia mguu wakati wa mazoezi na daktari wake kuthibitisha kuwa hatoweza kucheza michuano hiyo.


Kocha wa timu ya Manchester United Mkongwe Sir Alex Ferguson amesema kuwa atastaafu kazi ya ukocha rasmi akifikisha miaka 70, kwa sasa umri wa Ferguson ni miaka 66 hivyo basi ni wa “misimu” mitatu toka sasa.
Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ufaransa Thierry Henry (R), akielekeza jambo kwa Mwanamuziki maarufu wa Ufaransa Grand Corps Malade, wakati wa kipindi cha mazoezi kwa klabu hiyo June 4 mwaka huu, kwenye kambi ya timu hiyo Clairefontaine, kusini Magharibi mwa Paris, mwanamuziki huyo aliitembelea timu hiyo kuipa moyo kwani Ufaransa wanacheza na Romania June 9, 2008 kwenye mechi yao ya kwanza ya mashindano ya UEFA – EURO 2008.
HUYO WA KATI NI MADAM RITA AKIWA NA WASICHANA WAREMBO KWENYE MOJA YA EVENT HAO WASICHANA KITAALUM NAAMBIWA WANAITWA ‘ASHIERS’ SINA UHAKIKA NA SPELLING WAJUZI WATATUJUZA…ANAKUWA WANAWAPOKEA WAGENI N.K NAONA NI KAMRADI BONGO SIKU HIZI KWA WADADA HUSUSAN WENYE SHEPU ZA KIMISS,
Kuta kuwa na mpambanao wa marapa wa muziki wa dance Tanzania kutoka bendi mbali mbali ingawa hii haita husisha bendi bali mtu mmoja mmoja
Anaitwa Zadio Kongolo ukipenda muite ZK wengine humuita Sir Joe Kongolo, ni mfanyabiashara wa Kongo anayeishi Uingereza, Huyu ni mpenzi mkubwa wa JB Mpiana na Wenge BCBG kwa ujumla, ni maarufu kwa kutunza pesa, kwenye onyesho moja la JB alimtunza mwanzo hadi mwisho wa nyimbo (kwa nini asiimbwe!!!) kwenye kila onyesho la JB Mpiana Ulaya humkosi huyu bwana, kama anavyoonekana pichani alisafiri kwenda Belgium hii ilikuwa kwenye onyesho la JB Mpiana mwezi uliopita tarehe 3 May Bruxelles. JB Mpiana humuimba karibia katika kila wimbo lazima atamtaja ni kama vile unavyosikia PDG Ndama, Abdul Tall Omary Tall, Andrew Traders wanavyotajwa kwenye nyimbo za nyumbani, lakini Zadio amekwenda mbali zaidi kwani kwenye Albamu ya JB Mpiana ambayo inatamba sasa ya “Quel est ton probleme” akimaanisha Nini Tatizo lako?. Jb amemtungia wimbo kabisa Zadio unaoitwa Zadio Kongolo – ZK. Angalia na usikilize hapo chini, pia wimbo huu uwaburudishe wadau wangu PDG Mukubwa Ling’ande, Big Producer Magambo, Papaa Masabo, Mukulu Biloko Zadio wa Darisalama, Papaa Kasapila, Mukubwa Shabani, Ally Tandika – Tajiri mtoto, Batty William Mwafrica na wengine wengi, Mna nini bwanaaa. Pata burudani.
Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba (Babake Januari) akisakata sebene la T- Respect akiwa na Mbunge wa Kuteuliwa Mh. Al-Shymaa Kwegyir, kwenye ukumbi wa Travertine Magomeni Jumamosi.
Rais wa Real Madrid Ramon Calderon jana amesisitiza kuwa Timyake inayopesa ya kutosha kumnunua mchezaji machachari wa Manchester United Christian Ronaldo (pichani).
Wafanyakazi wa huduma ya kwanza wakimbeba mmoja wa mashabiki walipoteza fahamu kwa kukosa hewa kutokana na mrundikano wa mashabiki kwenye mchezo wa kuwania tiketi ya kombe la Dunia kati ya Liberia na Gambia, uliochezwa kwenye uwanja wa Samuel K. Doe . Uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 33,000 ulijaa kupita uwezo wake kwani inakisiwa zaidi ya watu 40,000 waliingia kuona mchezo huo uliochezwa jumapili ya juzi.
Jose Mourinho (pichani) jana alilamba dume baada ya kuapishwa rasmi kuwa kocha wa timu ya Inter Milan, ambayo imemfukuza kocha wake Roberto Mancini.
Gari likipita mbele ya bango kuuuubwa likiwa na mchezaji mpira likiwakaribisha wageni kwa ajili ya Michuano ya Euro inayotarajiwa kuanza hivi karibuni. Bango hili limewekwa Airport Schwechat, kilomita 25 mashariki mwa jiji la Vienna, Mamia kwa maelfu ya wageni wanamiminika kwa ajili ya ichuano hii inayotarajia kuanza wiki ijayo.
Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini, Mzee Nelson Mandela akiwa ameshikilia Kombe la Dunia, Afrika Kusini ndio waandazi wa Mtanange ujao wa Kombe la Dunia. Mandela atasherehekea miaka 90 ya kuzaliwa kwake mnamo tarehe 27 Mwezi huu katika Concert iliyoandaliwa Hyde Park mjini London ikiwa ni kuchangisha fedha kwa ajili ya Charity.
Mchezaji wa England Dean Ashton (L) na Jerman Defoe wakipongezana baada ya timu ya kupata goli la pili dhidi ya Trinidad and Tobago wakati wa mechi yao ya kirafiki huko Hasley Crawford stadium nchini Spain. England alishinda 3-0.
Mchezaji wa Manchester United na Portugal Christiano Ronaldo akiwapungia mashabiki wakati wa mazoezi ya timu yake ya Taifa inayojiandaa kwa michezo ya EURO 2008, Ronaldo anatazamiwa kuwa na mkutana na waandishi wa habari siku ya jumatano kuzungumzia hatma yake kisoka ikiwa ni pamoja na tetesi za uhamisho wake kwenda Real Madrid.
Wachezaji wa timu ya Santos wakiwa wameshikilia Kombe la Ubingwa Juu mwisho mwa mchezo wa fainali wa Ligi ya Mexico dhidi ya Cruz Azul Torreon, Mexico, Sunday, June 1, 2008. Santos walishinda kwa agregate ya 3-2.
Binti wa kitanzania mwenye ndoto ya kuwa super model, bado yuko gado na anaonekana kufanya vizuri ndani mji wa Knoxville, Tennessee hapa Marekani. Kwa habari na picha zaidi mtembelee Teddy Kalonga kwenye Total Knock Out
Hii ni kwa wadau wote waishio pande hizi za dunia, USA, UK, Canada, na sehemu zote ughaibuni.
Laurent alikuwa na mlolongo wa bidhaa za fasheni chini ya lebo yake (pichani) kuanzia viatu, nguo, manukato, mikoba ya akina baba na akina mama, kwa ujumla amejijenga kwa ulimwengu wa fasheni, Mwenyezi Mungu Amrehemu.



Mshindi wa taji la Miss Chang’ombe 2008 Angela Deo Lubala (katikati) mshindi wa pili Lilian Shayo (kulia) na mshindi watatu Shadia Ally (kushoto) katika picha ya pamoja mara baada ya kutangazwa washindi kwenye shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa TCC Club Chang’ombe Temeke Jijini Dar es Salaam likishirikisha vimwana 10.
Waliokuwa washiriki wa shindano la Bongo Star Search (BSS) 2008, Maangaza Nyange (kushoto) na Rogers Lucas wakikonga nyoyo za mashabiki wakati wa fainali za kumsaka mrembo wa kitongoji cha Chang’ombe usiku wa kuamkia leo.
Jaji wa shindano la Bongo Star Search (BSS) John Kitine shoto akiwa na mpiga gita la Bass Majuto Jr wa Bendi ya Kalunde inayoongozwa na Deo Mwanambilimbi, Majuto ni mtoto wa muigizaji na mchekeshaji maarufu wa kwenye TV Majuto. Kalunde Band kila ijumaa na Jumamosi wanapiga Giraffe Ocean View Hotel
SEATTLE – MAY 31: Robinho #11 wa Brazil akimrukia Diego #10 baada ya Diego kufunga goli katika kipindi cha kwanza cha mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Canada jana may 31 kwenye uwanja wa Qwest huko Seattle, Washington. Brazil walishinda Canada 3-2.
Brasili utawataka kwa kushangilia, Samba uwanjani mpaka kieleweke. Hii ilikuwa jana kwenye mchezo dhidi ya CANADA ilibidi wacanada wenyewe kuwakodolea macho hawa jamaa.
Kwa mara ya kwanza tangu fainali za kombe la dunia 2006 mchezaji David Bekham amepewa jukumu la kuiongoza timu yake leo watakapo kuwa wakipambana na Trinidad and Tobago.



JB Mpiana na kundi zima la Wenge BCBG wikiend hii liliendelea na ziara yao ya Ulaya na usiku huu walipiga Rotterdam katika Concert iliyofana lakini kutonogeshwa na baadhi ya vijambo.







Posted by piusmickys
Usiku wa kuamkia leo kundi la Jahazi Modern Taarabu kama kawaida yake lilipagawisha ile kinona na vibao vyake mbalimbali kikiwemo kile cha Msumali katika Ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam na kufanya Mademu na Mabrazaneni waliofika kuwasarandia mademu hao kushindwa kukaa vitini mpaka majogoo.





Jumba la kifahari la mwanamuziki 50 Cents limeungua moto jana ijumaa majira ya saa saa kumi na moja alfajiri, Watu wote sita waliokuwemo ndani ya nyumba hiyo walikimbizwa hospitali na kupatiwa matibabu na bado walikuwa chini ya uangalizi wa madaktari lakini hali zao zinasemwa kuendelea vizuri. Rafiki wa kike wa zamani wa mwanamuziki huyo alikuwepo pamoja na Marquise mtoto wa kiume wa 50 Cent mwenye miaka 10.






Mdau akiwa amepozi na Genta, mmoja wa wanamuziki wa kundi la Wenge BCBG, Picha hii imepigwa na Ronald mnazi hasa wa Wenge. Kundi la Wenge BGBG waliwasili Rotterdam majuzi kwa ajili ya onyesho lao ambalo limefanyika usiku wa kuamkia leo. hapa ni kwenye duka maarufu la Muziki wa Kiafrika la 



KUNDI la vichekesho la Ze Comedy jana lilitangaza kuingia mkataba wa mwaka mmoja na kituo cha televisheni la TBC 1.

Msanii DePlaizer ameweka wazi kuhusiana na hisia zake za kutaka kufaya kazi na wanamuziki wa barani afrika ikiwa ni moja katika malengo yake katika kuunyanyua muziki wa kifrika duniani.



KAMPUNI ya simu za mkononi ya Celtel imejitosa kudhamini kwa miaka mitatu mashindano ya kimataifa ya gofu yanayotarajia kuanza Dar es Salaam kesho kwa sh.milioni 120.

Kelly Rowland toka kundi la Destiny’s Child akiimba wimbo wa taifa wa USA kabla ya kuanza kwa mechi ya mpira wa miguu kati ya USA na England iliyofanyika Wembley Stadium hapo jana, England ilishinda kwa magoli 2-0.
Mchezaji wa England David Beckham akiwa na Kofia yake ya Dhahabu aliyopewa na Mkongwe Boby Charlton, ikiwa ni kuthamini mchango wake wa 100 kwa timu ya Taifa ya England kabla ya kuanza kwa mchezo wa jana dhidi ya USA.



Kocha wa timu ya England Fabio Capello amemtaja John Terry (pichani) kuwa ndiye captain katika mchezo wa kirafiki dhidi ya USA utakao fanyika leo.
Timu ya soka ya Barcelona imemsajili mchezaji wa Manchester United Gerard Pique katika mkataba wa miaka minne kwa gharama ya paund milion 5.
Timu ya mpira ya Liverpool imechimba mkwara kwa klabu ya Chelsea na kuwaambia mchezaji wao mwenye uraia wa Spain
Mchezaji wa timu ya taifa ya Ufaransa Bafetimbi Gomis akishangilia mara baada ya kupachika kimiani goli la pili kwenye mechi ya kirafiki kati ya Ufaransa na Ecuado.
Mchezaji wa Ufaransa Hatem Ben Arfa, shoto, akisakata goma kumtoka mchezaji wa Ecuado Isaac Mina, wakati wa mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu dhidi ya timu hizo mchezo uliofanyika huko Alps stadium, Grenoble Ufaransa, jana jumanne, May 27, 2008. Ufaransa ilishinda 2 – 0. Ufaransa ilitumia mechi hii ya mwisho ya majaribio ili kuchagua kikosi chake cha watu 23 kwa ajili ya michuano ya EURO 2008, kwa sasa kikosi kina wachezaji 30.
Mchezaji wa Austria Emanuel Pogatetz (L) akiwania mpira na Ikechukwo Uche wa Nigeria wakati wa mchezo wa kirafiki wa soka huko Graz, Austria wanajiandaa na mtanange wa kombe la EURO, mechi hii ilimalizika droo ya 1-1.



BAADA ya aliyekuwa Mocha Mkuu wa timu ya Chelsea Avram Grant (pichani) kufungashiwa virago mwishoni mwa wiki, tetesi zimeanza kusambaa juu ya makocha ambao watarithi mikoba yake.


Papa Cherry
Zadio Congolo akimtunza JB Mpiana, Jamaa huyu ni mpenzi mkubwa wa JB Mpiana husafiri kila mara JB anapokuwa na Onyesho nchi yeyote ya Ulaya.![[image]](http://i223.photobucket.com/albums/dd10/ronaldcc/m22.jpg)
![[image]](http://i223.photobucket.com/albums/dd10/ronaldcc/m25.jpg)
![[image]](http://i223.photobucket.com/albums/dd10/ronaldcc/m27.jpg)



Watu wakitawanyika hasubuhi saa moja kasoro baada ya shoo kuisha
Pamoja na njia mbali mbali za kufika Marina Bay ukitumia njia ya Boat maalum unapata mandhali nzuri zaidi na picha mwanana kama hii.
Singapore Flyer ina urefu wa mita 165, ndio flyer kubwa zaidi duniani na ya kwanza kwa Asia imejengwa kwenye muinuko katika eneo maarufu la Marina Bay, Ndani ya hii flyer unaweza kuona mandhari ya mji mzima wa Singapore na nchi jirani kama Malaysia na Indonesia. ilizinduliwa tarehe 15 April na tiketi kwa ajili ya uzinduzi zilikwisha kwa siku tatu mfululizo zikiwa zinauzwa USD 8000, Booking ya Flyer inabidi ifanywe mapema kwani huwa imejaa kwa miezi miwili hadi mitatu kabla ila nafasi maalumu huwekwa kwa ajili ya wageni (watalii). soma hapa zaidi
Kalbfleisch (anayechungulia) akijiandaa kumkabili mshindani wake katika michezo ya wazi ya Sumo huko Los Angeles, April 7, 2007. REUTERS/Lucy Nicholson.
Wakati huo akiichezea timu yake ya Arsenal, Thierry Henry akionyesha kuumiliki mpira kwa style ya aina yake huku David Bentley wa Blackburn Rovers akimuangalia wakati wa mchezo baina yao uliofanyika uwanja wa Emirates London February 17, 2007. Picha na Eddie Keogh.
Mchezaji wa Manchester United Nani (aliyeruka juu) akishangilia baada ya kufunga goli dhidi ya timu ya Tottenham Hotspur huko Manchester, Kaskazini mwa England, August 26, 2007. REUTERS/Phil Noble, Picha hizi ni baadhi ya picha zilizomo kwenye mkusanyiko wa Picha bora za mwaka jana za shirika la habari la REUTERS, kwa picha zaidi za Mwaka 2007 bofya hapa
Jioni hii Taifa Stars ya Tanzania ilikuwa ikipimana ubavu na timu kutoka Malawi, The Flames, ambapo timu zilitoka sare ya bao moja kwa moja. Pichani ni mchezaji wa Taifa Stars Mrisho Ngasa(kulia) akijaribu kumtoka beki wa Malawi, Wisdom Ndlovu.



Aaaah!! Bwana wee, kila mmoja ana jicho lake anavyouangalia mpira huo huo tulio uangalia mimi na wewe, tembelea Photo Baraza uone hizi na nyinginezo!!
Bwana wee furaha haina mwisho mtu waweza sherehekea hata mwaka mzima Rukhsa!!!!
Mhh wapo wengi waliwabeza wanamuziki wa kizazi kipya si Tanzania tuu hata Mwanamuziki kutoka Uganda Bob Wine hakutarajia kufika na kufanikiwa kama alivyosasa, pichani ni “mjengo” wa mwanamuziki huyo. Kwa mahojiano kamoli tembelea gazeti tando la Miss East Africa.
Mashindano ya Mr & Miss East Africa Uk yanatazamiwa kufanyika tarehe 26 July 2008 na kushirikisha walimwende na vijana watanashati toka pembe hiyo ya Africa. Mshindi wa mashindano haya pamoja na mambo mengine husaidia kwenye shughuli za kujitolea kwa ajili ya watoto waliona shida huko nyumbani Africa ya Mashariki kwa ujumla. Kwa mwaka huu pamoja na burudani kadha wa kadha zilizoandaliwa usiku huo utapambwa na Mwanamuziki Ali Kiba




Wimbo huu umeandikwwa na Muimbaji kijana anayekuja kwa kasi kwenye fani ya Muziki wa Congo kwa jina ni Blanchard de Plaizir, Homme Plus inaongelea hadithi ya mdada mmoja mdogo mrembo ambaye aliangukia kwenye penzi la kijana mtanashati na maarufu ambaye binafsi alimuona kwenye Tv na magazeti ya watu maarudu (celebrity magazines) na kuamini kuwa hatoweza kukutana na kijana huyu kamwe katika maisha yake ya kawaida mdada analalamika na kuona kuwa dunia haimtendei haki katika ulimwengu wa mapenzi, kijana anajitahidi na muziki wake ni mzuri kwa kweli.
Pamoja na kumaliza wakiwa nafasi ya pili kwa mashindano yote mawili la ligi na na la UEFA, bado sio kigezo kwa uongozi wa klabu ya Chelsea kumpa mkataba kocha Avram Grant.
Kepteni wa timu ya soka ya Lyon’s , Antonio Ribeiro Reis, shoto, Gregory Coupet, kati, na Sidney Govou wakiwa wameshikilia Kombea na kushangilia baada ya timu yao kuwachapa Paris Saint Germain 1-0 katika mtanange wa fainali ya soka Kombe la Ufaransa. Mchezo huu ulifanyija jana tarehe 24 May katika uwanja wa Stade de France stadium nje ya jiji la Paris.
TIMU ya soka ya Taifa ‘Taifa Stars’ leo inashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuumana na Malawi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.



Lionel Messi alizaliwa 24 June 1987 huko Rosario – Argentina. kwa sasa anachezea timu ya FC Barcelona. alionyesha uwezo mkubwa akiwa na umri mdogo sana na medi zilimpachika kuw ndiye “Diego Maradona Mpya”. Messi alikaraishwa sana na timu yake kutochukua Kombe lolote kwa mwaka wa pili mfululizo na alitajwa kuwaniwa na vilabu vya Uingereza lakini timu yake ya Barcelona inasema itafanya kila linalowezekana kuendelea kuwa naye Messi. na huyu ndiye mchezaji wetu wa wiki hii na hii chini ni moja ya Video zake.
Baada ya kukosa fainali za michuano ya Euro 2008, timu ya soka ya England kwa sasa inajiandaa na mechi za kirafiki ikiwa imeegemeza nguvu kwenye michuano ya kombe la Dunia mwaka 2010. Tarehe 28 mwezi huu England wanawakaribisha USA katika mechi ya kirafiki ambayo itafanyika katika uwanja wa Wembley.
Mchezo wa Pool umekuwa maarufu sana Tanzania kila kona si jambo la ajabu kukuta meza na watu wamerundikana, Hii ilikuwa Mlimba Ifakara Morogo nilikuwa na kijana wangu Robert Mwafrica akaomba game moja duh dogo alimtoa nishai katika michezo minne alishinda mmoja tuu, Batty ndiye mwalimu wangu wa Pool na vijana wake wengi kwa sasa wanatisha. Ama kweli jogoo wa mjini hawiki shamba pia.
Hebu pata picha ndio Tanzania ingefanikiwa kufika Fainali tuu za Ghana ingekuwaje, Pichani ni watanzania wakiongozwa na Rais Kikwete (picha katikati) kipindi tunajongea kwenye mashindano ya Kombe la Mataifa ya Africa. Watanzania wanapenda sana Mpira basi tuu.
Serikali kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeunda kamati itakayosimamia Uwanja mkuu wa Taifa na timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’.
JESHI la Polisi limesema limeimarisha ulinzi na kuwataka askari wa majeshi yote nchini kuingia uwanjani kwa kulipa kiingilio katika mechi mbili za kimataifa kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Malawi na ile ya Maritius zitakazochezwa Uwanja mpya wa Dar es Salaam.







Angelina Jolie & Brad Pitt
Aishwarya Rai Kulia toka Bollywood
Jean-Claude Van Damme
Madonna
Star Jones
Marcio Maximo, Kocha mwenye uraia wa Brazili, aliteuliwa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama kocha mkuu wa Taifa Stars .
Hivi karibuni Chuji aliweka wazi kwamba hategemei kuwepo ndani ya kikosi cha Yanga msimu ujao kutokana na kuitwa na mjomba wake nchini Hispania kwa lengo la kutafutiwa timu ya kufanya majaribio na baadaye kucheza soka huko.

Wanja la Liverpool likikamilika, Katika picha hizo zilizotolewa na The Daily Mail zinaonyesha jinsi wanja likikamilika litavyokuwa, Wanja hili litakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 60,000 wakiwa wamekaa “Konfotabo” na uwezo wa kuegesha magari mengi kwa wakati mmoja, utakamilika mwaka 2010. Gharama yake inakadiriwa kufikia Paund Milioni 300.
Nyote mnakaribishwa












MSHAMBULIAJI wa Manchester United Wayne Rooney amemwambiamshambuliaji wa Chelsea, Didier Drogba kwamba hana lolote.
Kindumbwendumbwe cha mashindano ya American Idol ndio kinafikia ukingoni wiki hii huku mashabiki wakishuhudia mpambano mkali kati ya wawili hao pichani David Archulete (shoto) na David Cook ambao kwa kiasi kikubwa wamewagawa mashabiki hasa baada ya kutoka msichana pekee Syesha wiki iliyopita. Kila mmoja anapewa nafasi ya kushinda na kila mmoja ana mashabiki wake, wakati wa mwanzo wa mpambano wawili hawa walikuwa wakishabikiwa na watu wote lakini imefika mahala ni lazima kuchagua mmoja hilo ni jukumu gumu sana hata siwezi kusema nani ni zaidi ya mwingine, binafsi nawaona wote wana vipaji, kwangu huu ni mtihani kila mmoja na mvuto wa kipekee na wote wana kipaji alisema Simon, Jaji maarufu wa shindano hilo alipokuwa akiongea na Television ya FOX.
Fainali zilizopita Bekham aliisaidia Manchester kuchukua Kombe.

Goli moja lililofungwa na Kanu lilifanya timu ya Portmouth kunyakua ubingwa wa Kikombe cha FA. Kulikuwa na kila sababu kwa klabu ya Portmouth kusherehekea ubingwa huu baada ya kuichapa Cardiff kwa goli moja bola (1-0) katika mchezo wa Fainali wa kombe la FA uliochezwa hivi karibuni. kwani Portmouth wameshinda kikombe hicho baada ya miaka 69 kwani mara ya mwisho ilikuwa mwaka 1939 walipowachapa Wolves. baada ya hapo wamekuwa wakijitahidi bila mafanikio, Hata hivo Portmouth walikuwa na nafasi nzuri ya kushinda kwa magoli zaidi mchezo wa jana, baada washambuliajia wake akiwembo Kanu kukosa magoli ya wazi tangu dakika za awali za mchezo.
Mashabiki wa Portmount na Cardiff wakiingia uwanja wa Wembley kushuduhia mpambano kati ya Portmouth na Cardiff
Kanu akishangilia na mwenzie kwa Style ya chamukwale baada ya kuwatandika Cardiff bao 1-0.

Mwanamuziki JB Mpiana na kundi zima la Wenge Muzika BCBG bado wanaendelea kukonga nyoyo za mashabiki na wapenzi wa Muziki wa lingala katika ziara ambayo inampitisha nchi za mbali mbali za Ulaya, katika onyesho lililofanyika wiki mbili zilizopita inasemekana palitokea fujo ambazo ziliwazidi nguvu walinzi, katika siku za karibuni kumekuwa na hati hati ya onyesho ambalo limepangwa kufanyika nchini Uingereza kutokana na masuala ya kiusalama kutokana na mashabiki kusababisha fujo kwenye onyesho la mwisho la mwanamuziki Koffi Olomide.
MILAN, May 18 (Reuters) – Zlatan Ibrahimovic akiwa ameifungia timu yake mabao mawili na kuihakikishia ushindi na kuchukua kikombe tena, katika mchezo uliochezwa leo dhidi ya Palma na kushinda magoli 2-0 na kuwafanya kuchukua kombe kwa miaka mitatu mfululizo.
Maimatha Jesse, mtangazaji wa Channel 5 ndiye alikuwa MC katika uzinduzi wa Akudo Impact Diamond Jubilee.

Mwanamuziki kutoka DRC, Bozi Boziana, ‘Benz’ akiwa katika jukwaa la Akudo Impact alfajiri ya jana wakati akiwasindiza ‘wazee wa masuati’ katika uzinduzi wao. Bozi alikonga nyoyo za mashabiki wa vibao vyake vya zamani ambavyo wabongo wanavikumbuka.


Mchezaji wa Sevilla Dragutinovic akishangilia baada ya timu yake ya Sevilla kushinda 4-1 dhidi ya Athletic wakati wa mchezo wa ligi ya Spain taree 18 May 2008.
MADRID, SPAIN – MAY 18: Marcelo (kati) wa Real Madrid akiwa amelishikilia kombe la ubingwa wa Ligi ya La Loga akiwa na wenzake Sergio Ramos (L) na Ruud van Nistelrooy (R) mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao na Levante huko Santiago uwanja wa Bernabeu.

Kapteni wa zamani wa timu ya Arsenal Patrick Vieira anasema anahofia matokea kama kocha Arsene Wenger ataamua “kumvua” nafasi ya kepten mchezaji William Gallas.
Mafundi wakimalizia kuweka bango kubwa likiwa na wachezaji wa timu ya Bayern Munich katika eneola “Alte Boerse” (Soko la zamani la Hisa) katikati ya jiji la Munich. Bango hilo lina ujumbe usemao “Sisi ni FC Bayern ! Tuna rekodi ya ubingwa!, Tunarekodi ya Vikombe vya ushindi!, Tuna rekodi ya bango kubwa!, Twashukuru wapenzi wetu!, Bango hilo lina ukubwa wa Mita za mraba 180.
Golikipa wa Bayern Munich Oliver Kahn, Jumamosi ya leo anacheza mechi yake ya mwisho kabla ya kustaafu mchezo wa soka rasmi baada ya kutumikia mchezo huo kwa miaka 21, Mchezo wa leo ni mgumu kwani timu inayocheza na Bayern ni nzuri pia na Oliver Kahn atataka kustaafu vizuri kwa ushindi kwa timu yake na bila yeye kufungwa, Bayern Munich wanawakaribisha Hertha Berlin leo kwenye ligi ya Bundesliga.
Pilika pilika za kumsaka Miss Tanzania zimeanza hivo pichani baadhi ya wanyange wanaowania Taji la Miss Chang’ombe 2008 wakijifua katika Ukumbi wa Sigara (TTC), Chang’ombe Jijini Dar es Salaam.
Beki wa Ujerumani Philipp Lahm, ameamua kuongeza mkataba na timu yake ya Bayan Munich baada ya kuwa na maongezi na kocha wake Jugen Klinsmann, katika mkataba mpya Philipp atakaa na timu hiyo mpaka mwaka 2012.












Mwanamuziki Bozi Boziana akifanya shopping kwenye dula la Zizzou Fashion Sinza leo asubuhi, akiwa ameongozana na stage shoo wake, pichani Bozi Boziana akichagua kiatu kutokea huku mnenguaji wake Blaisesse Ayembe akimsistiza kutokiacha kibuti hicho ambacho mabrazameni wamekipa jina la Ngwasuma.
Mkongwe wa DRC – Congo Bozi Boziana (kushoto) akisalimina na King Kikii na Kassim Mapili (katikati) alipowasili jana jijini Dar es Salaam.
Mwanamuziki mkongwe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Mbezu Bokili maarufu kama Bozi Boziana akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kuwasili nchini jana katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwal Nyerere Dar es Salaam. Atasindikiza uzinduzi wa albam ya Akudo.
Ronaldo ameifungia klabu yake ya Manchester magoli 41 kwa msimu huu.
Boss wa Chelsea Avram Grant anategemea wachezaji wake John Terry (shoto) na Didier Drogba (kulia) wanatarajia kupona na kuwemo kwenye kikosi cha Chelsea kitakachocheza kwenye fainali Moscow.
‘Kanoute’s friends’ team player Thierry Henry (R) shakes hands with International Team’s goalkeeper Casillas before thier friendly football match “Champions for Africa” at the Sanchez Pizjuan stadium in Sevilla, southern Spain, on May 13, 2008.
Kanoute’s friends team and International Team players are pictured before their friendly football match “Champions for Africa” at the Sanchez Pizjuan stadium in Sevilla, southern Spain, on May 13, 2008
Kocha wa timu ya Atlas ya Mexico Miguel Brindisi, wa tatu toka kulia, akiongea na wachezaji wake wakati wa mazoezi kwenye uwanja wa Amalfitani Stadium huko Buenos Aires, jana, Timu hii itacheza na Boca Junior ya Argentina leo tarehe 14, katika mtanange wa kinyang’anyiro cha Copa Libertadores.
Mashabiki waliofika kwenye uwanja wa Commonwealth Stadium, Edmonton huko Alberta kuangalia mpambano wa soka wa kirafiki kati ya Los Angeles Galaxy na Vancouver Whitecaps, jana May 13, 2008.Timu ya Los Angels Galaxy ndiyo timu anayochezea David Bekham kwa sasa.
Rais Bush akila Pose la Picha muda mfupi kabla ya kufungwa ndoa kati ya Mwanaye Jenna na Henry Hager Jumamosi tarehe 10 May, 2008
Familia ya Rais Bush toka shoto Barbara ambaye ni pacha mwenzie Jenna, Laura na George
Jenna na Henry wakishikana mikono mbele ya Kiongozi wa Kanisa wakati wakifungishwa ndoa Jumamosi ya tarehe 10 May, 2007.
Mkongwe Suge Knight alilambwa kichapo katika ugomvi ambao ulihusisha kundi la watu wakiwa Club.

NYOTA wa zamani wa Manchester United, David Beckham ametajwa katika kikosi cha England kitakachocheza mechi za kirafiki na Marekani, Trinidad na Tobago. Kocha Mkuu wa England, Fabio Capello amemtaja kiungo huyo ambaye hivi sasa anakipiga katika klabu ya Los Angeles Galaxy kuwa ni miongoni mwa wachezaji 3, ambao wataivaa Marekani kwenye Uwanja wa Wembley Mei 28 na katika mechi nyingine dhidi ya Trinidad itakayofanyika Juni mosi.
Mchezaji wa Argentinean Mkongwe Diego Armando Maradona akionyesha mbwembwe katika mchezo wa Hisani jana.
Wakongwe wa soka Diego Armando Maradona, kushoto, na Mchezaji wa zamani wa Brazili ace Zico wakati wa mchezo wa Maalum wa hisani wa Soka kwenye uwanja wa Rome Olympic stadium, jana jumatatu May 12, 2008.
Mchezaji wa Los Angeles Galaxy’s David Beckham akipita kwenye uwanja wa ndege wa Edmonton International Airport akiwa na timu yake Jumatatu May 12, 2008 huko Edmonton, Alberta. The Galaxy wako Edmonton kucheza na timu ya Vancouver Whitecaps leo jumanne, May 13. Tangu mchezaji huyo ahamie Ligi ya Amerika kumekuwa na ongezeko kubwa la wapenzi wa mchezo huo ikilinganishwa na awali na amekuwa kivutio kila anapopita.
Mkurugenzi Mtendaji wa Manchester David Gill
Vita ya Akudo ya Akudo na FM inaendelea na FM kusisitiza uwepo wa onyesho lao, likiwa na kila kitu kimeshabihiana na maandalizi ya Uzinduzi wa Akudo “wazee wa masauti”, Katika Onyesho la FM ambalo linatazamamiwa kuwa katika ukumbi wao wa nyumbani wa Msasani Fm wapepanga kumleta General Def Defao akiwa na Montana ambaye alijitoa kipindi fulani na kuwa na Koffi pia wameweka kikundi cha Taarabu cha zanzibara star ambapo katika uzinduzi wa Akudo wao wanamleta Nguli Bozi Boziana na watasindikizwa na Mzee Yusuph na Jahazi Morden Taarab.














Huku zikiwa yakiwa yamebaki masaa kadhaa kabla ya mitanange ya fainali mechi za mwisho kuamua mshindi, mashabiki wako roho juu kila mmoja akijaribu kutetea upande wake kuwa utashinda kikombe hicho. Hakuna mechi inayotabirika leo kwani kwa droo yeyote Man anabeba “chikombe” kwani Man U wanatofauti kubwa ya magoli, kwa Upande wa Chelsea wanatarajiwa kubebwa na mashabiki 62,000 walioshakata tiketi kwa ajili ya kuuona mtanange huu, ambapo inakadiriwa 90% ni mashabiki wa Chelsea, kwani Chelsea wanacheza nyumbani leo na Man U wanacheza ugenini.
Wimbo wa wasanii Nako 2 Nako ‘We ndo mchizi wangu’ hivi karibuni umerudiwa na kufanyiwa remix ambayo imewakutanisha wasanii kibao na wakali akiwemo, Jay Moe, Fid Q, Mansu-Li, Geez Mabovu, Dr K wa Mapacha, Adili Chapakazi, Chidi Benz, Mwanafalsafah, Mheshimiwa Temba, Babuu wa King’oko na wenye ngoma yao ambao ni Nako 2 Nako Souldierz. 
KUNDI maarufu la sanaa za maigizo The Comedy (pichani) limemaliza mkataba wake na kituo cha televisheni cha East Afrika (EATV) kinachorushwa kila siku ya Alhamis.
Kilomita 50 toka mji wa Kuala Lumpur Malaysia, Genting (pichani) ni maarufu kwa starehe za aina zote kuna kasino kubwa ambayo hukutanisha mataikun wa kila sehemu ikiwa ni pamoja na Singapore, Malaysia, Thailand na hata Indonesia, ukifika usiku ni milio ya Helcopter kila mmoja akiingia na kutoka kwenye jumba la Casino la sehemu hii changamfu.
Ni wazi kuwa mtanange huu wa kesho unawategeme hawa watu wawili kufanya maajabu, thamani ya magoli kwa ushindi wowote utaibeba timu husika, na nani atabaki na Kombe muamuzi ni dakika 90, kwani Machester anacheza ugenini na Chelsea anacheza nyumbani, Chelsea ana historia nzuri ya kuutumia uwanja wa Nyumbani lakini pia Manchester bado ana rekodi ya kushinda mechi nyingi hata za ugenini, hii inawapa matumbo joto mashabiki kwani kuna uwezekano mkubwa mtanange huu ukaamuliwa kwa idadi ya magoli ambayo mpaka sasa Man wako mbele kwa tofauti ya magoli 17.
Raisi wa FC Porto Jorge Nuno Pinto da Costa, katikati na maofisa wa klabu hiyo Adelino Caldeira, right, naFernando Gomes wakiinuka kumaliza mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye uwanja wa Dragao Porto, Portugal, ijumaa May 9, 2008. Kamati ya nidhamu ya chama cha mpira wa miguu nchini humo kimewanyang’anya point Porto na Uniao Leiria kwa madai ya kupanga matokeo katika kashfa kubwa ya mchezo wa soka ambayo haijawahi kutokea. Kamati hiyo iliamua kwamba Porto walimhonga Refarii kwenye mechi mbili katika msimu wa 2003-04 na kuamua kuwanyang’anya pointi 6 na kuwapiga faini ya Euro150,000 (US$230,000) na kumzuia Mwenyekiti Jorge Pinto da Costa kwenye kuonekana kwenye benchi la akiba kwa miaka miwili.
Midfielder wa Inter Milan Luis Figo, ambaye amechezea klabu ya Barcelona kwa misimu mitano mfululizo amesema, Kocha mpya wa klabu hiyo ambaye alikuwa Kepteni ya timu hiyo zamani Pep Guardiola anauwezo mkubwa na anaweza kuleta matumaini mapya kwenye klabu hiyo. Barcelona ambayo haijafanya vizuri kwenye ligi ya na hasa mechi zake za kribuni pia imeongeza nguvu kwa kumpa timu mchezaji huyu wa zamani nafasi ya kuifunza timu hiyo.
Mchezaji mahiri wa klabu ya Arsenal Emmanuel Adebayor amekanusha uvumi kuwa anataka kuondoka klabu yake ya Arsenal na kukimbilia Italy.

SAO PAULO, Brazil – Kufuatia kesi ya kugombana na
Mwanamuziki R. Kelly, lakiwasili mahakamani ya Cook County Criminal Courthouse, Chicago leo hii (ijumaa) akiwa ameongozana na mlinzi wake katika siku ya kwanza ya kusikilizwa kesi inayomkabili, Mwanamuziki huyu anashtakiwa kwa kujihusisha na udhalilishaji watoto kijinsia kutokana na makanda wa Video ambao unadaiwa kuwa unaonyesha akifanya mapenzi na mtoto wa miaka 13.
Baada ya matokeo ya wiki hatimaye walibari watatu David Cook, David Archuleta & Syesha Mercado, mchuano bado ni mkali hasa katika ya David wawili ingawa Syesha anatoa upinzani kwa wa aina yake, ila mvuto wa akina David unamfanya awe kwenye wakati mgumu. Nani ataibuka mshindi? swali juu yako msomaji.
Kwa wapenzi wa mpira, 
Alex Stepney (Pichani) aliyekuwa golikipa wa Manchester United Mwaka 1968 anakumbuka sikuiku ya fainali huku wakipewa shinikizo na mashabiki kutokana na habari za mchezo uliokuwa unaendelea uwanja mwingine huku timu zote mbili zikigombea ushindi ili kuchukua kombe.
Martin O’Neill amesisistiza kuwa kitendo cha Liverpool cha kusema kumtolea mchezaji wao Gereth Barry kiasi cha Pound 10milion ni kumshusha thamani.



Kundi la Muziki la FM Academia linatarajia kumleta mwanamuziki General Defao kuja kutumbuiza nao siku ya May 16 katika onyesho lililoitwa “Uchwara” ambalo dhamira yake ni kuvuruga uzinduzi wa Akudo Wazee wa Masauti, ambapo siku hiyo pia watakuwa na Uzinduzi wa Albamu yao mpya, Ikumbukwe pia Akudo walishatangaza kumleta Mwananamuziki Bozi Boziana ili kuwasindikiza kwenye uzinduzi huo ambao unasemekana kuwa wa aina yake. Lakini habari zinasema endapo Defao akitia timu hapa Tanzania, huenda akalakiwa na pingu kutokana na tuhuma mbalimbali zinazomkabili.



Meza ya wageni waalikwa anaonekana JB Mpiana, Alain Mpela (aliyevaa kiarabu), Dadé Mpoko, Papito Mbala, Thitsho Lembe
JB Mpiana na tajiri mtoto PDG Patrick Bolognia, aliyesimama nyuma yao suti nyeusi ni Titina Alcapone. Majina haya wengi wa wapenzi wa Lingala watakuwa wamezoea kuyasikia kwenye kila wimbo na leo kubahatika kuwaona katika picha hizi.
Mchezaji wa Manchester United mwenye uraia wa Argentina Carlos Tevez akishangilia ushindi baada ya kuwachapa Barcelona katika mechi ya kombe la UEFA Champions League mzunguko wa pili, April 2008. Idara ya uhamiaji ya Uingereza imesema hakuna raia mchezaji ambaye si raia wa European ambaye hawezi kuzungumza “kidhungu” atafukuzwa chini ya sheria mpya ngumu za uhamiaji ambazo zitaanza kutumika mwaka huu ambapo lugha ni suala muhimu.
Mchezaji wa Real Madrid Sergio Ramos akishangilia ushindi baada ya kushinda mechi ya fainali ya ligi ya Spain dhidi ya Osasuna katika uwanja wa Reyno de Navarra stadium, Pamplona, tarehe 4 May. Imesemekana kwamba Chelsea wametoa ofa ya dau nono kwa Real Madrid jumla ya 70 million euros (108 million dollars) kwa ajili ya mchezaji huyu na kama mambo yakienda kama ilivyopangwa basi atahamia kucheza ligi ya UK, kwani Real Madrid wameonyesha kuridhia ofa hiyo. imeripotiwa na gazeti la michezo la El Mundo.
Mchezaji machachari wa Barcelona’s Samuel Eto akishangilia wakati wa mchezo wa ligi wao ya Spanish dhidi ya Valencia huko Camp Nou stadium Barcelona, May 4.
Timu ya Manchester City wamefanya uamuzi wao na kuamua kumpendekeza Luiz Felipe Scolari kuwa kocha wao ajaye.
Michuano ya Kombe la Taifa imeanza kwa kasi na msisimko wa ajabu huku mikoa yote 23 ikishiriki kwenye kinyang’anyiro hicho, pichani Wachezaji wa Timu ya Manyara kushoto Zawadiel Stephen na Marwa Gabriel wakiwania mpira mshambuliaji wa timu ya Iringa Bunda Oden. Iringa ilishinda 4-1 katika mashindano ya Taifa Cup yanayodhaminia na Safari Lager.
Watu wakidwalika kwenye Usiku wa Black and White, unataka kujua kulikoni na Black and White mtembelee dada 
KAMPUNI ya Bia Tanzania, TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro imetangaza kutumia zaidi ya Sh140milioni kuandaa Tuzo za Kilimanjaro zitakazotolewa kwa wasanii mbalimbali baadaye mwezi ujao.
Mara nyingi ikitokea super star fulani akatokea mahali,mashabiki au wapenzi wa chochote anachokifanya(iwe sinema,muziki nk) hupenda kujipatia japo nafasi ya kupiga naye picha kwa minajili ya kuweka kumbukumbu na mambo kama hayo.Kama inavyoonekana pichani,mashabiki na wapenzi wa 50 Cent waliopata nafasi ya kuwa karibu naye hivi majuzi jijini Dar,walikuwa na shauku ya kupiga naye picha!Go 50!

Happiness Magesa ambaye alishanyakua Taji la Miss Temeke na baadaye Miss Tanzania 2001 anaendelea kutesa vyema nchini South Africa kwenye Fashion Show Mbalimbali nchini humo kama muonavyo Pichani, Happiness kwa sasa anaishi Africa ya Kunisi akijishughulisha na shughuli za U model huko.

Kwa mara nyingine tena Real Madrid walifanikiwa kukalia kiti cha Ubingwa wa ligi ya Spain ya La Liga jumapili hii baada ya kushinda magoli 2-1 huko Osasuna ikiwaacha Real Madrid wakiwa na pointi 10 zaidi ya wenzao Villarreal kwenye msimamo wa Ligi hiyo ya Primera Liga, huku wakiwa na mechi tatu mkononi ambazo wanatakiwa kucheza kukamilisha ratiba. Real Madrid walicheza wakiwa 10 uwanjani ilibidi wafanye kazi ya ziada kwani Osasuna walikuwa wakiongoza kwa goli lililofungwa na Patxi Punal kwa mkwaju wa penati baada ya mchezaji wa Real Madrid Gabriel Heinze kuunawa mpira katika eneo la hatari. Na Fabio Canavaro kutolewa nje kwa kadi nyekundu na hivyo kuwafanya Real Madril kucheza wakiwa kumi uwanjani.
CHELSEA iko katika mbio za kuwania ubingwa na Manchester United leo itakuwa ugenini Uwanja wa St. James Park kupambana na Newcastle.