Werasson awakana wanamuziki wa Congo nchini

June 30, 2008
[image]

MWANAMUZIKI mkongwe wa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Kongo, Werasson amesema hamjui mwanamuziki hata mmoja kutoka Kongo anafanya muziki hapa Tanzania.

Hivi karibuni wanamuziki wengi kutoka Kongo waliokuja hapa nchini walijitangaza kuwa wengine ni ndugu wa Werrason huku wengine wakisema kuwa wenyewe ni watoto wa mkongwe wa Muziki nchini humo Pepe Kalle, na katika tukio la karibuni ni pale mwanamuziki ally Choki alipoonekana amepiga picha na Werason alipokwenda kutafuta wanamuziki huko na kusema kuwa Werasson alimsaidia kutafuta vijana.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam juzi Werasson alisema ’simfahamu mwanamuziki hata mmoja wa Tanzania wala mkongo ambaye anaimba muziki hapa huyo anayejiita mtoto wa Pepe Kalle pia hamfahamu.

“Mimi nipo na mtoto mmoja wa Pepe Kalle ambaye namfundisha muziki pale Kongo, lakini huyu wa Tanzania mimi simfahamu kwakuwa watoto wake wote nawajua na hivyo labda awe mwingine zaidi,” alisema Werassons.

Werrason alisema kwa kuwa hawajui wanamuziki wa Kongo walipo hapa nchini lakini yuko tayari kukutanao na kufanya mazungumzo ya kuendelea muziki Tanzania.
(Picha na Mpoki Bukuku)


Monday, June 30, 2008

June 30, 2008

Karibuni nyumbani mwayego….!

A German supporter waits on a traffic light for the arrival of the German football team with thousands of supporters who gathered at Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008 to greet their team upon their return from Vienna, where they lost by 0-1 to Spain in the final of the Euro 2008 Football Championships June 29. AFP PHOTO JOHN MACDOUGALL (Photo credit should read JOHN MACDOUGALL/AFP/Getty Images)
Shabiki wa Timu ya Ujerumani akiwa amesimama juu ya Taa za kuongozea magari wakati wachezaji na makocha wa Timu ya Taifa ya Ujerumani wakiwasili huko Ujerumani jana, Hebu pata picha hawa jaa wangeshinda mtiti ungekuwaje? Germany's striker Lukas Podolski sings to supporters of the German football team at the "Fanmeile" (fan zone) next to Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, the day after the Euro 2008 final Germany vs Spain in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO DDP/POOL/ GERO BRELOER  (Photo credit should read GERO BRELOER/AFP/Getty Images)
Mchezaji wa Ujerumani Lukas Podolski (Juu na chini pichani) akiimba mbele ya mashabiki waliokusanyika kuwapokea mashujaa wao.
Germany's striker Lukas Podolski appears on a giant screen as thousands of fans cheer the German national football team at the "Fanmeile" (fan zone) in front of Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, one day after the Euro 2008 final Germany vs Spain, held at Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria. Spain ended their 44-year wait for a major international title with a 1-0 victory over Germany at the Euro 2008 final.      AFP PHOTO  DDP/ MICHAEL GOTTSCHALK (Photo credit should read MICHAEL GOTTSCHALK/AFP/Getty Images)
Germany's head coach Joachim Loew (L) signs his name in the city's Golden Book next to Berlin's Mayor Klaus Wowereit as supporters of the German football team gather at the "Fanmeile" (fan zone) next to Berlin's Brandenburg Gate on June 30, 2008, the day after the Euro 2008 final Germany vs Spain in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO DDP/POOL/ GERO BRELOER  (Photo credit should read GERO BRELOER/AFP/Getty Images)
Kocha wa Ujerumani Joachim Loew (L) akitia mkono kwenye kitabu cha city’s Golden Book kulia kwake anayemkazia jicho ni Meya wa Berlin Klaus Wowereit pale mamia kwa maelfu ya washabiki wa Ujerumani walipokusanyika “Fanmeile” (fan zone) huko Berlin
Hii ni baada ya mchezo wao wa jana na Hispania kwenye fainali za Euro 2008 na Spain kushinda kwa 1-0. Picha zote na AFP

Serena na Venus hatarini kucheza Fainali wao kwa wao

Venus Williams
Venus na Serena, Ndugu wote wawili wameshinda mechi zao leo Jumatatu huko Wimbledon, Kama mambo yakienda hivi basi kuna hati hati ya Wawili hao ambao ni mtu na dada yake kucheza Fainali wao kwa wao. (Picha na AP)

Kili Music Award yafana

Wasanii mbali mbali wamefanikiwa kunyakua Tuzo mbali mbali kwenye tamasha la Kili Music Award usiku wa kuamkia leo, Kwa habari na picha zaidi bofya hapa kwa Haki Ngowi (Picha na Haki Ngowi)

Mchezaji Taifa Stars adaiwa “Jezi” baada ya kubadilishana na Eto’o wa Cameroon

Kipanya wa Leo na habari ndio hiyo hapo chini…

Na Phillip Nkini wa Mwananchi

UMILIKI wa jezi za timu ya Taifa Stars umezua balaa kwa baadhi ya wachezaji wa timu hiyo kujikuta wakikatwa fedha zao za posho kwa madai ya kufidia jezi ambazo ama walibadilishana na wenzao wa Cameroon au kupoteza.

Kwa upande wake, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) linasema: ”Jezi si mali ya wachezaji.”

Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries na Benki ya NMB, wadhamini wa Stars wamekuwa wakitoa vifaa kwa wachezaji wa timu hiyo kuanzia vile vya mazoezi hadi vya mechi mbalimbali ambazo timu hiyo imekuwa ikicheza.

Lakini, pamoja na hali hiyo kumezuka tatizo kwa baadhi yao (wachezaji) na uongozi wa timu hiyo kukosana baada ya baadhi yao kubadilishana jezi majuzi na wachezaji wa Cameroon, Indomitable Lions, jambo ambalo limewazulia mambo.

Mchezaji mmoja kinda wa timu hiyo (jina tunalo) alishindwa kumpa Geremi Njitap wa Cameroon jezi yake kwenye mchezo kati ya Stars na Cameroon mjini Yaounde baada ya mchezaji huyo kutaka wabadilishane.

Kinda huyo aliiambia Mwananchi kuwa alihofia kuja kurejea nchini na kudaiwa jezi.

Lakini, beki wa timu hiyo alibadilishana jezi na mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto’o Fils baada ya Mcameroon huyo kumfuata mwenyewe na kumtaka afanye hivyo.

Hata hivyo, pamoja na wachezaji hao kudaiwa jezi hizo Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage aliithibithishia Mwananchi kuwa jezi si mali ya wachezaji, bali ni mali ya shirikisho hilo na mchezaji atakapoipoteza, basi utaratibu wa malipo utafanywa.

”Jezi sio mali ya wachezaji ni mali ya Shirikisho la Soka, kila mchezaji anapewa jezi kwa kufuata utaratibu maalum ukipewa lazima urudishe usiporudisha unaandaliwa utaratibu wa kulipia.”

“Sisi bado tupo nyuma sana hatujafika huko walipo hao akina Senegal au Cameroon kuwa na wadhamini wakubwa, kiasi kwamba mchezaji mmoja kuwa na jezi zaidi ya kumi. Hapa kwetu, tunaweza kutumia jezi moja kwenye mechi mbili wenzetu kila mechi na jezi yake.

”Ukiangalia mchezaji kama Eto’o anandaliwa jezi zaidi ya 50 na Kampuni ya Puma ni tofauti sana na sisi, ingawa kubadilishana moja mbili siyo vibaya, lakini isiwe watu kumi na kuendelea,” alisema Kaijage.

Uchunguzi wa Mwananchi umeonyesha kuwa wachezaji hao wa Stars wamekuwa hata wakati mwingine wakipigiwa simu wakiwa majumbani kwao ili warudishe jezi ambazo wamekuwa wakiondoka nazo kwa bahati mbaya au ambazo zimekuwa zikipotea.

Ukweli ni kuwa kila mchezaji wa Stars anapopoteza jezi moja hukatwa posho yake kuanzia Sh20,000 na kuendelea.

Hali hiyo ndiyo inayosemekana kuwa itamkumba beki na nahodha msaidizi, Nadir Haroub Cannavaro aliyeamua kubadilisha jezi na Eto’o.

Eto’o, ambaye yuko katika ziara ya nchi kadhaa za Afrika, alionekana jijini Kampala, Uganda akiwa na jezi yenye nembo ya NMB huku akitoa mafunzo ya soka kwa watoto.

Werasson awakana wanamuziki wa Congo nchini

[image]

MWANAMUZIKI mkongwe wa Jamhuri wa Kidemokrasia ya Kongo, Werasson amesema hamjui mwanamuziki hata mmoja kutoka Kongo anafanya muziki hapa Tanzania.

Hivi karibuni wanamuziki wengi kutoka Kongo waliokuja hapa nchini walijitangaza kuwa wengine ni ndugu wa Werrason huku wengine wakisema kuwa wenyewe ni watoto wa mkongwe wa Muziki nchini humo Pepe Kalle, na katika tukio la karibuni ni pale mwanamuziki ally Choki alipoonekana amepiga picha na Werason alipokwenda kutafuta wanamuziki huko na kusema kuwa Werasson alimsaidia kutafuta vijana.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam juzi Werasson alisema ’simfahamu mwanamuziki hata mmoja wa Tanzania wala mkongo ambaye anaimba muziki hapa huyo anayejiita mtoto wa Pepe Kalle pia hamfahamu.

“Mimi nipo na mtoto mmoja wa Pepe Kalle ambaye namfundisha muziki pale Kongo, lakini huyu wa Tanzania mimi simfahamu kwakuwa watoto wake wote nawajua na hivyo labda awe mwingine zaidi,” alisema Werassons.

Werrason alisema kwa kuwa hawajui wanamuziki wa Kongo walipo hapa nchini lakini yuko tayari kukutanao na kufanya mazungumzo ya kuendelea muziki Tanzania.
(Picha na Mpoki Bukuku)

Wajerumani “Mbendembende” kwa Waspaniola

Germany 0-1 Spain
Spain's Iker Casillas celebrates with the trophy after the Euro 2008 final between Germany and Spain in the Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria, Sunday, June 29, 2008, the last day of the European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Spain defeated Germany 1-0.
Wachezaji wa Spain wakisheherekea baada ya kukabidhiwa “mwali ” wao
In this handout picture distributed by Spain's soccer Federation, Spain's King Juan Carlos, right, holds the Euro 2008 European Soccer Championship trophy with Spain's Prime Minister Jose Luis Rodriguez Zapatero, left, standing beside him.  Spain's soccer team won the trophy by beating Germany 0-1 in the final of Euro 2008 championship played Sunday in Vienna, Austria.
Pichani ni Mfalme wa Spain Juan Carlos, aliyeshika kombe walilokabidhiwa Spain jana na kushoto kwake ni Waziri Mkuu wa Spain Jose Luis Rodriguez Zapatero usiku wa kuamkia leo.
Some German supporters sit on the ground on a huge German flag in the Munich fan zone at the Olympic stadium after the Euro 2008 championships final football match Germany vs. Spain on June 29, 2008 at Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria. Spain won their first trophy in 44 years as they beat three-time champions Germany 1-0 in the Euro 2008 final.  AFP PHOTO   DDP / TIMM SCHAMBERGER   (Photo credit should read TIMM SCHAMBERGER/AFP/Getty Images)
Mashabiki wa Ujerumani wakiwa hawaamini kilichotokea wamebaki uwanjani hata baada ya mpira kumalizika.
Germany's Micheal Ballack reacts at the end of the Euro 2008 final between Germany and Spain in the Ernst-Happel stadium in Vienna, Austria, Sunday, June 29, 2008, the last day of the European Soccer Championships in Austria and Switzerland. Spain defeated Germany 1-0.
Kepteni wa Ujerumani Micheal Ballack akiwa haamini kama dakika 90 zimekwisha na wameshindwa kuchomoa goli moja la Spain katika mchezo uliofanyika Ernst-Happel stadium huko Vienna, Austria,
(Picha zote na AP)

Fernando Torres ndiye shujaa wa Spain baada ya kupachika bao dakika yaa 33 bao lililodumu hadi kipyenga cha mwisho na kuwafanya Spain kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa Mtanange wa Euro 2008 baada ya kuisaka nafasi hiyo kwa miaka 44.

Torres alipachika bao hilo swafi dakika ya 33 ya mchezo kipindi cha kwanza licha ya juhudi za Kapteni wa Ujerumani Ballack waspaniola walikaza na kulinda goli lao huku wakifanya mashambulizi ya hapa na pale.

Huku akisherehekea miaka 70 ya kuzaliwa , Kocha Luis Aragones alitanabaisha atang’atuka kuifunza timu ya Spain na inasemekana Kocha mwingine Vicente del Bosque ndiye anaweza kuchukua timu hiyo ambayo kwa bahati atarithi vijana wenye vipaji wadogo na wenye hari na mtazamo kwenye kombe la Dunia.
Mpaka dakika 90 bao likabaki 1-0, ama kwa hakika kanauma, kamonga tuu!!

Werason awasha moto Dar

June 29, 2008







Mwanamuziki Werasson Ngiama Makanda usiku wa leo amefanya balaa katika ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwapagawisha vilivyo mamia kwa maelfu ya mashabiki walifika katika onyesho hilo.
Werasson ambaye ameingia nchini majuzi aliingia jukwaani kama kawaida lilitangulia sebene na kisha yeye kuingia huku akiimba wimbo maarufu wa Kala Yi Boing Remix huku mashabiki lukuki nao wakimfatiisha kwa kuimba naye, kisha alifululizwa kwa vibao kama Sourire ambacho kinapatikana kwenye Albamu ya Zamani ya Volume I, Solo la bien,Kibuisa Mpipa, Kuna nyimbo inaitwa Simeone inapatikana kwenye single Album Soul Soul.
Mashabiki walipagawishwa na mauno ya mwandada mrembo aliyeumbika si kitoto Bibiciya Mfwengi kila mara alikuwa akijivuta mbele na kijana wa atalaku kama kawa anampa mapande mashaki wote wana lipuka kwa mayowe.Kwa ujumla shoo ilikuwa nzuri na kila mtu aliyeingia aliridhika na burudani ya haja aliyoipa.
Awali akizungumza na waandishi wa habari Werasson alisema kuwa amekaidi wito wa Rais wa Kongo Brazaville Denis Sasou Nguesso aliyemtaka kwenda kufanya shoo kadhaa kwa wiki nzima lakini alisema kuwa hawezi kuwaangusha mashabiki wake wa Dar Es Salaam ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakimngojea hasa baada ya onyesho la awali kutofanyika huku watu wakiwa wameshakata tiketi.
Werasson na kundi lake la wanamuziki 24 watapiga Arusha kesho.
Kama nakuona Big Producer Maghambo Philipo – Baba Martha, Collins na Fikire wazee wa USA, Mukubwa Ling’ande, Mwanangu Dulla nakati ya IFM, Abuu na Boss Chizenga!! Tuko pamoja.
Picha na Big Producer Magambo/Mpoki Bukuku

Saturday, June 28, 2008

June 28, 2008

Werason awasha moto Dar








Mwanamuziki Werasson Ngiama Makanda usiku wa leo amefanya balaa katika ukumbi wa Ubungo Plaza na kuwapagawisha vilivyo mamia kwa maelfu ya mashabiki walifika katika onyesho hilo.
Werasson ambaye ameingia nchini majuzi aliingia jukwaani kama kawaida lilitangulia sebene na kisha yeye kuingia huku akiimba wimbo maarufu wa Kala Yi Boing Remix huku mashabiki lukuki nao wakimfatiisha kwa kuimba naye, kisha alifululizwa kwa vibao kama Sourire ambacho kinapatikana kwenye Albamu ya Zamani ya Volume I, Solo la bien,Kibuisa Mpipa, Kuna nyimbo inaitwa Simeone inapatikana kwenye single Album Soul Soul.
Mashabiki walipagawishwa na mauno ya mwandada mrembo aliyeumbika si kitoto Bibiciya Mfwengi kila mara alikuwa akijivuta mbele na kijana wa atalaku kama kawa anampa mapande mashaki wote wana lipuka kwa mayowe.Kwa ujumla shoo ilikuwa nzuri na kila mtu aliyeingia aliridhika na burudani ya haja aliyoipa.
Awali akizungumza na waandishi wa habari Werasson alisema kuwa amekaidi wito wa Rais wa Kongo Brazaville Denis Sasou Nguesso aliyemtaka kwenda kufanya shoo kadhaa kwa wiki nzima lakini alisema kuwa hawezi kuwaangusha mashabiki wake wa Dar Es Salaam ambao kwa kiasi kikubwa walikuwa wakimngojea hasa baada ya onyesho la awali kutofanyika huku watu wakiwa wameshakata tiketi.
Werasson na kundi lake la wanamuziki 24 watapiga Arusha kesho.
Kama nakuona Big Producer Maghambo Philipo – Baba Martha, Collins na Fikire wazee wa USA, Mukubwa Ling’ande, Mwanangu Dulla nakati ya IFM, Abuu na Boss Chizenga!! Tuko pamoja.
Picha na Big Producer Magambo/Mpoki Bukuku

Sylvia Mashuda atwaa taji la Miss Ilala 2008

Kanda ya Ilala imekuwa ya kwanza kufungua pazia la mashindano ya Miss Tanzania ngazi ya Kanda kwa Mkoa wa Dar Esalaam hapo jana na mrembo Sylvia Mashuda katikati kunyakua taji hilo katika shindano lililofanyika usiku wa kuamkia leo pale Raiway Gerezani sasa ni City Garden Club. Kushoto ni mshindi wa pili, Nelly Kamwelu(kushoto) na mwingine ni Aneth John. Sylvia anamiaka 19 amemaliza, Form VI anangojea kujiunga na chuo kikuu.

mpira Maalum wa Fainali EURO 2008

Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas kwa kushirikiana na EURO2008 wametangaza aina ya mpira maalum utakao tumika kwa ajili ya Mtanange wa fainali kesho kati ya mabingwa mara tatu Ujerumani na mabingwa wa 1964 Hispania. Mpira huo umepewa jina la Euro Pass.
Mipira 30 yenye rangi ya Silver ambayo itakuwa na majina ya wababe hao wa timu mbili zinazokutana fainali.Pia imefahamika kuwa Kombe ambalo litanyakuliwa ama na Michael Balack wa Ujerumani au Casillas wa Hispania hapo kesho litakuwa na kilo mbili za uzito zaidi wa kombe la awali ambalo Theodoros Zagoraskis wa Ugiriki alilinyakua mwaka 2004.

Kombe jipya lina uzito wa kilo 8 na urefu wa sentimita 60 limepewa jina la Henri Delaunay, aliyekuwa Katibu wa zamani wa shirikisho la mchezo huu Mfaransa ambaye alitoa mchango mkubwa kwenye historia ya mashindano haya.

JB Mpiana alipofanya kweli Ufaransa

[image]

[image] [image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

Kama kawaida Ziara ya JB Mpiana ilihitimishwa Ndani ya Bataclan Paris, Ufaransa tarehe 22 mwezi huu na mambo yalikuwa moto, JB Mpiana anayetamba na Albamu yake Mpya Ya Quel Est Ton Probleme? Aliwaburudisha mashabiki walijaza ukumbi kwa nyimbo za zamani na zikichanganyika na mpya, Kama Zadio Congolo, Mtindo wa Lopele pia mashabiki walilipuka nao kinoma, Kali ni pale kibao matata cha Liberez kilipoanza kuimbwa, Wimbo huu umo kwenye Albamm yake mpya na umetokea kupendwa sana. Liberez ni utunzi wa mwanamuziki mpiga Bass gitaa wa Wenge BCBG Sunda Bass. Onyesho limesifiwa kwa kuwa na Sound System nzuri na Jb alitumia muda vizuri na muda wote mashabiki walifurahi.
Pata Kitu Liberez

Jiachie Kisela

Lebo zinazidi kutoka kila kukicha, ubunifu ndio unaotakiwa, Jiachie Kisela Kitu ndani ya Ulimwengu wa Lebo za nyumbani.

Friday, June 27, 2008

June 27, 2008

Werasson: Niko tayari kupiga na JB Mpiana Tanzania

Pichani ni Rais wa Kongo RDC Joseph Kabila akiwa na timu ya Wanamuziki akiwemo Marehemu Madilu System alipokutana nao na kuwapatanisha baadhi yao akiwemo JB Mpiana na Werasson mwaka juzi.
MWANAMUZIKI hodari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ngiama Makanda ‘Werrason’ amewasili Dar es Salaam na kusema yupo tayari kupiga pamoja na Jean Bedel Mpiana ‘JB Mpiana’ endapo atapatikana promota wa kuwaleta Tanzania kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania.Msanii huyo aliwasili juzi jioni akitokea Jamhuri ya Kongo ambapo na kundi la wanamuziki 24, anatarajiwa kutoa burudani kesho kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza kabla ya kupiga Arusha Jumapili kwenye Hoteli ya Naura Springs.

Endapo ‘Werrason’ atapiga pamoja na ‘JB’ Mpiana itakuwa ni historia baada ya nyota hao kuingia katika mzozo mkubwa ulioibua vita kati yao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Makanda alisema atafurahi kupiga pamoja na Mpiana ambaye inadaiwa ni wapinzani na chanzo cha kuvunjika kwa kundi maarufu la Wenge BCBG lililowahi kutamba Afrika.

“Sina matatizo na Mpiana ni rafiki yangu napenda siku moja nije naye hapa tufanye onesho la pamoja nipo tayari hata sasa cha msingi apatikane promota mwenye uwezo nitamwambia lakini naomba nipate uhakika kama mnatuhitaji kabla ya mwaka huu kumalizika,” alisema Makanda.

Makanda alisema anapenda kuona muziki wa Tanzania unapiga hatua kama ilivyo Jamhuri ya Kongo na kuongeza kuwa endapo atapata fursa ya kuzungumza nao atawashawishi watengeneze albamu ya pamoja.

Msanii huyo alisema alishindwa kutoa burudani mwaka jana kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake na alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi Watanzania kutokana na tukio hilo.

Alisema amejiandaa kuacha historia kwa kupiga nyimbo zake mfululizo ili kukata kiu ya mashabiki wa burudani ambao walikuwa na shauku kubwa ya kumuona nyota huyo akiwa jukwaani katika ardhi ya Tanzania.

Ziara ya mwanamuziki huyo imedhaminiwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya Embassy kwa kushirikiana na Club E.

Kipanya adhamini Miss Temeke

MSANII maarufu katika uchoraji wa katuni za siasa na sasa akiwa mbunifu maarufu wa mitindo nchini, Ali Masoud ‘Kipanya’ amejitosa kudhamini wa mashindano ya kumsaka Miss Temeke 2008.

Mratibu wa Miss Temeke, Benny Kisaka alisema Masoud, ambaye hutumia lebo ya KP, ambayo ni kifupi cha Kipanya, atawazawadia washindi watatu wa kwanza wa Miss Temeke nguo za watakazotumia katika fainali za Vodacom Miss Tanzania 2008, zitakazofanyika baadaye mwaka huu.

Alisema Temeke, ambayo inafunga dimba katika mashindano ya urembo ya kanda kwa mwaka huu, pia atatoa nguo maalum za shoo ya ufunguzi kwa warembo wote.

Alisema kwa sasa vimwana 12 wanaendelea kujifua chini ya Miss Temeke 2006, Jokate Mwegelo, ambaye anawafundisha mbinu za kutumia vyema jukwaa, unadhifu, kujengwa kisaikolojia na kuwapa uwezo wa kujiamini na hata kujibu maswali. Wasichana hao wanatoka katika vitongoji vya Kigamboni, Kurasini, Temeke Kusini na Chang’ombe.

Warembo hao ni Sheila Ally, Radhia Omary, Lilian Shayo, Zainabu Ally, Rona Swai, Nuru Hassan, Mwash Ramadhan, Angela Lubala, Caroline Sechuma, Glory Charles, Florence Josephat na Evelin Issack.

Werasson kuanzia Ubungo Plaza Leo

Mkurugenzi wa Clouds fm/Prime Time Promotions Joseph Kusaga akiteta jambo na Werrason mara baada ya kuwasili Dar. Werrason anatafanya onesho lake la kwanza leo Ijumaa usiku Ubungo Plaza ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni sh 20,000/= pamoja na msosi wa nguvu, Pia leo atafanya mahojiano ya moja kwa moja na kituo cha Radio cha Clouds FM kupitia kipindi cha African Bambataa kinachoongozwa na Bibi Sophia KEssy, Big Producer Maghambo, Boss Chizenga, Mukubwa Collins, Dulla Boy na kati ya IFM, Mama Irene Maggi, Fikiri Le Boss, Abuu na wapenzi wote wa Werasson kila la heri najua hamtakosa. Picha na Issa Michuzi.

Brazil yasherehekea miaka 50 tangu ichukue Kombe la Dunia

Brazilian President Luiz Inacio Lula da Silva (L) embraces Brazilian football legend Edson Arantes do Nacimento, known as Pele, as he decorates the winners of the 1958 World Cup, during the opening ceremony of an exposition celebrating the 50th anniversary of Brazil's first victory in this tournament, at Planalto palace in Brasilia on June 26, 2008.  AFP PHOTO/Joedson ALVES (Photo credit should read JOEDSON ALVES/AFP/Getty Images)
Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva shoto, akiwa amemkumbatia Mfalme wa soka la Brazil Edson Arantes do Nacimento, au Pele, Brasil inasherehekea miaka 50 tangu walipochukua Kombe la Dunia mwaka 1958 kwa shamra shamra za ina mbali mbali, sherehe hizi zilifanyika Planalto palace huko Brasilia jana tarehe June 26, 2008.

Spain yaigalagaza Russia 3-0….!

Russia 0 – 3 Spain

Spain's Xabi Alonso, Joan Capdevila, Xavi Hernandez and Fernando Navarro

Wachezaji wa Hispania, wakisherehekea ushindi wao mara baada ya kipyenga cha mwisho

Ama kweli ukitaka kumuua nyani usimuangalie usoni, ndivyo walivyofanya Waspaniola usiku huu walipomchapa Russia bila huruma mabao matatu bila kufurukuta.
Ikiwa ni fainali yao ya kwanza baada ya miaka 24 wamewafungisha virago Russia na sasa watautana na Ujerumani na Russia watacheza na Uturuki kutafuta mshindi wa tatu.

Ilikuwa ni siku ya furaha kwa vijana wa Luis Aragones kwani walikuwa wakishambulia muda wote bila kupumzika na kufanikiwa kupata goli la kuongoza kipindi cha pili kupitia kwa Xavi, ambaye baadaye alibadilishana na Xabi Aronso dakika ya 69. Pia aliingia Daniel Guiza dakika hiyo ya 69 na dakika 4 baada ya kuingia alipachika bao la pili kwa Hispaniola na goli la tatu lilifungwa na David Silva dakika ya 82 na kuwapa tiketi ya kukutana na Ujerumani siku ya Jumapili.

Russian football fans celebrate the success of the Russian national soccer team in Euro 2008 after watching the semi-final match between Russia Spain in Moscow early June 27, 2008. Despite Spain's 3-0 win, it has been more than 20 years since Russia has had such a serious presence on the international footabll stage and many citizens are proud of their team's performance. AFP PHOTO / NATALIA KOLESNIKOVA (Photo credit should read NATALIA KOLESNIKOVA/AFP/Getty Images)
Pamoja na kufungwa Mashabiki wa Russia walikuwa wakisherehekea kwa kile walichosema mafanikio ya timu yao kufika nusu fainali, si haba.

Matokeo haya yameinyima Russia nafasi ya kucheza Fainali kwa mara ya kwanza tangu kuunjika kwa muungano wa kisobvieti. Russia alichapwa 4-1 na Spain wakati wa mchezo wa ufunguzi.

Spain waliutawala mchezo kuanzia kipindi chwa kwanza lakini hawakuweza kupata goli lolote kwani Russia walikaza namna fulani, lakini marekebisho na mawaidha ya kocha kipindi cha mapumziko yalizaa matunda.


Werasson kuanzia Ubungo Plaza Leo

June 27, 2008
Mkurugenzi wa Clouds fm/Prime Time Promotions Joseph Kusaga akiteta jambo na Werrason mara baada ya kuwasili Dar. Werrason anatafanya onesho lake la kwanza leo Ijumaa usiku Ubungo Plaza ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni sh 20,000/= pamoja na msosi wa nguvu, Pia leo atafanya mahojiano ya moja kwa moja na kituo cha Radio cha Clouds FM kupitia kipindi cha African Bambataa kinachoongozwa na Bibi Sophia KEssy, Big Producer Maghambo, Boss Chizenga, Mukubwa Collins, Dulla Boy na kati ya IFM, Mama Irene Maggi, Fikiri Le Boss, Abuu na wapenzi wote wa Werasson kila la heri najua hamtakosa. Picha na Issa Michuzi.

Thursday, June 26, 2008

June 26, 2008

Ngoma Africa Band na Nyimbo za masimulizi!

*Ras Makunja kamrushia madongo Baba wa Kambo!?

Bendi maarufu ya mziki wa dansi the Ngoma Africa Band,inayoongozwa na mwanamziki

maarufu Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Ebby Makunja “Bw.Kichwa Ngumu”

Imeibua zogo la gumzo lingine kwa kufyatua wimbo wao uliobeba jina la “Baba wa kambo”

wimbo huo umefyatuliwa wakati CD yao “Apache wacha Pombe” inawasha moto mkali wa kimataifa !

wimbo wao huo wa “Baba wa Kambo” ulifyatuliwa katika kuadhimisha sikuu ya watoto dunian! wimbo huo unawakilisha kilio cha mamilion ya watoto wanao teseka katika utwala wa kidikteta wa kina “Baba wa Kambo” ni utunzi wake tena kiongozi na mwimbaji wa bendi

Ebrahim Makunja.

Katika wimbo huo Ras Makunja amemrushia lawama(madongo) “Baba wa kambo” na kikosi

cha Ngoma Africa kikimsindikiza kwa kumzomea !baba wa kambo tunakushikia bango!

Kindumbwe Ndumbwe Charia ! na Nguo! kaitia moto!

Bendi hiyo maarufu inayopeperusha bendera ya Tanzania katika majukwaa ya kimataifa,

imefanikiwa kuliachia song hilo ambalo linamshitaki “Baba wa kambo” Kwa Jamii!

na jamii pamoja na tahasisi zake zifanye kila njia kutupia jicho swala la maelezi ya watoto

ambao ulelewa na kina baba wa kufikia maarufu kwa jina la “Baba wa Kambo”

madongo hayo ya Ras Makunja na kikosi chake The Ngoma Africa hayakuishia hapo tu

bali lawama nazo zimerushiwa kwa kwa MAMA ALIYELEWA MAPENZI na kumshau mwanae akiteswa na “Baba wa Kambo”

Mzozo huo katika ya Baba wa kambo na The Ngoma Africa band utapelekwa kwa jamii hili

upatikane uhamuzi nani ?mwenye makosa Baba wa Kambo! au Mama Aliyelewa Mapenzi!

au Ngoma Africa Band waliomzomea baba wa kambo na kuweka mateso yake yote uwanjani yajadaliwe na jamii?

Baadhi ya Malalamiko ya ngoma africa kuwa “Baba wa Kambo” anamfanyishwa YATIMA kazi ya kutafuta kuni !wakati watoto wengine wapo shuleni! anamnyima ELimu yatima!

wakati Elimu ni ufunguo wa maisha,anampa KISAGO CHA MOTO yatima,anamlaza chumba cha Uwani karibu na chooni !kula na kulala kwa shida!

Baba wa Kambo naye labda atalalamika kuwa kiongozi wa bendi hiyo ni mwanamziki mwenye GUBU! kawashawishi wenziwe kumzomea wakati mila zinasema usimzomehe mkubwa!

hatujui Jamii itamuhua nini? au nani mwenye makosa


Werasson: Niko tayari kupiga na JB Mpiana Tanzania

June 26, 2008
Pichani ni Rais wa Kongo RDC Joseph Kabila akiwa na timu ya Wanamuziki akiwemo Marehemu Madilu System alipokutana nao na kuwapatanisha baadhi yao akiwemo JB Mpiana na Werasson mwaka juzi.
MWANAMUZIKI hodari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ngiama Makanda ‘Werrason’ amewasili Dar es Salaam na kusema yupo tayari kupiga pamoja na Jean Bedel Mpiana ‘JB Mpiana’ endapo atapatikana promota wa kuwaleta Tanzania kwa ajili ya kutoa burudani kwa Watanzania.Msanii huyo aliwasili juzi jioni akitokea Jamhuri ya Kongo ambapo na kundi la wanamuziki 24, anatarajiwa kutoa burudani kesho kwenye Ukumbi wa Ubungo Plaza kabla ya kupiga Arusha Jumapili kwenye Hoteli ya Naura Springs.

Endapo ‘Werrason’ atapiga pamoja na ‘JB’ Mpiana itakuwa ni historia baada ya nyota hao kuingia katika mzozo mkubwa ulioibua vita kati yao.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Makanda alisema atafurahi kupiga pamoja na Mpiana ambaye inadaiwa ni wapinzani na chanzo cha kuvunjika kwa kundi maarufu la Wenge BCBG lililowahi kutamba Afrika.

“Sina matatizo na Mpiana ni rafiki yangu napenda siku moja nije naye hapa tufanye onesho la pamoja nipo tayari hata sasa cha msingi apatikane promota mwenye uwezo nitamwambia lakini naomba nipate uhakika kama mnatuhitaji kabla ya mwaka huu kumalizika,” alisema Makanda.

Makanda alisema anapenda kuona muziki wa Tanzania unapiga hatua kama ilivyo Jamhuri ya Kongo na kuongeza kuwa endapo atapata fursa ya kuzungumza nao atawashawishi watengeneze albamu ya pamoja.

Msanii huyo alisema alishindwa kutoa burudani mwaka jana kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wake na alitumia nafasi hiyo kuwaomba radhi Watanzania kutokana na tukio hilo.

Alisema amejiandaa kuacha historia kwa kupiga nyimbo zake mfululizo ili kukata kiu ya mashabiki wa burudani ambao walikuwa na shauku kubwa ya kumuona nyota huyo akiwa jukwaani katika ardhi ya Tanzania.

Ziara ya mwanamuziki huyo imedhaminiwa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) kupitia chapa yake ya Embassy kwa kushirikiana na Club E.


JB Mpiana alipofanya kweli Ufaransa

June 26, 2008

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

[image]

Kama kawaida Ziara ya JB Mpiana ilihitimishwa Ndani ya Bataclan Paris, Ufaransa tarehe 22 mwezi huu na mambo yalikuwa moto, JB Mpiana anayetamba na Albamu yake Mpya Ya Quel Est Ton Probleme? Aliwaburudisha mashabiki walijaza ukumbi kwa nyimbo za zamani na zikichanganyika na mpya, Kama Zadio Congolo, Mtindo wa Lopele pia mashabiki walilipuka nao kinoma, Kali ni pale kibao matata cha Liberez kilipoanza kuimbwa, Wimbo huu umo kwenye Albamm yake mpya na umetokea kupendwa sana. Liberez ni utunzi wa mwanamuziki mpiga Bass gitaa wa Wenge BCBG Sunda Bass. Onyesho limesifiwa kwa kuwa na Sound System nzuri na Jb alitumia muda vizuri na muda wote mashabiki walifurahi.


Esther Nabaasa: Mshindi wa Tusker Project Fame mwaka huu

June 25, 2008

Esther Nabaasa Mugizi
Esther ana miaka 21 ni mwanafunzi wa Makerere University ambako anachukua Degree ya Telecommunication Engineering.

ESTHER Nabaasa kutoka Uganda, ametwaa kitita cha Sh85milioni baada ya kushinda shindano la Tusker Project Fame lililomalizika mwishoni mwa wiki jijini Nairobi.

Kwa ushindi huo, Esther alijipatia zawadi ya S milioni tano za Kenya na mkataba wa kutengenezewa albamu na kampuni kubwa ya kurekodi ya Galo iliyopo Afrika Kusini.

Nafasi ya pili ilitwaliwa na Wendy Kimani wa Kenya ambaye alijipatia shilingi milioni 2.5 za Kenya.

Katika hatua hiyo ya mwisho iliyokusanya maelfu ya mashabiki ukumbini, washiriki wanne waliobaki walipanda jukwaani na kuimba nyimbo tatu kila mmoja.

Washiriki wengine wawili wa kiume, David Ogola na Victor Asava walishindwa kuimba katika hatua hiyo.

Baada ya kila mshiriki kuimba wimbo mmoja, msanii kutoka Tanzania, Ambwene Yesaya ‘AY’ alipanda jukwaani na kutoa burudani kwa kuimba wimbo wake wa Usijaribu, ambao ulipokelewa kwa shangwe na mashabiki.

Kumalizika kwa zamu ya AY, washiriki walipanda tena jukwaani kuimba nyimbo zao za pili, David akiwa wa kwanza akifuatiwa na Esther, Victor na Wendy, kabla ya msanii nyota kutoka Uganda, Bobby Wine naye kupanda jukwaani.

Mbali na wasanii hao, msanii kutoka Kenya, Red Sun, naye alipanda jukwaani na kutoa burudani ambayo pia ilishangiliwa na mashabiki lukuki waliohudhuria.

Baadaye, MC wa shughuli hiyo, Gaitano Kagwa kutoka Uganda, aliwaonyesha mashabiki gari maalum lililoingia ukumbini likiwa na kitita hicho cha fedha za zawadi, ambao wanaume wanne waliokuwa wamevalia suti na miwani nyeusi, walipopanda jukwaani wakiwa na begi lenye fedha.

Esther amekuwa msichana wa pili kushinda mchuano huo baada ya Mkenya, Varerie Kimani kufanya hivyo mwaka jana

Tony Nyadundo, Mfalme wa Nyimbo za Ohangla

The Benga Maestro, Tony Nyadundo katika moja ya maonyesho yake

Tony Nyadundo ni mzaliwa wa Kanda ya Ziwa huko Kenya. Anatokea katika kabila la Wajaluo (Luo), Tony Nyadundo amejipatia umaarufu kwa aina ya mziki wake na ni jambo la kawaida kupita mitaani na kusikia nyimbo zake zikichezwa. Aina ya muziki wake inajulikana kama Ohangla (Muziki toka kanda ya Ziwa) na sasa yeye anajulikana kama Mfalme wa Ohangla. Tony ni mmoja wa wanamuziki walifaidika na muziki wake na kuufanya muziki huo kukubalika na rika lote. Tony pamoja na kaka yake anayejulikana kwa jina la Jack Nyadundo naye anapiga aina ya muziki kama wa Tony kama mdogo wake naye anakubalika sana kwenye Muziki na umaarufu wao ni mkubwa hasa Sehemu ambazo Wajaluo wanatoka.

Tony ambaye anatamba na nyimbo kama Dawa ya Mapenzi,Isanda Gi hera, Obama na nyinginezo nyingi ameshafanya matamasha ya muziki nchi mbali mbali ikiwemo Ujerumany na USA pia achilia mbali hizi za Afrika. Umaarufu huu unafuatia aina ya muziki wake ambao unajumuisha ala za asili, uchezaji pamoja na uimbaji ambao huvutia kwa taratiibu na kuupandisha toka Mziki wa Vilabu vya Pombe, Bar mpaka sasa zimbo zake zinapigwa hata kwenye Kumbi za Burudani zikichanganywa na Genge, muziki maarufu wa Kenya.

Mwaka 2006 alitoa albamu yake iliyoitwa Obama. Ikiwa ni kumuenzi Seneta Barak Obama wakati huo ambaye Baba yake ni Mzaliwa wa Kenya kama Nyadundo.

Wakati wa tamasha la Kisima Music Award mwaka 2007 alishinda kwenye kundi la Muziki wa kiasili. Tony ambaye binafsi anaweza kutumia ala zote za kiasili, muziki wake anatumia ala za kiasili tupu isipokuwa kinanda cha kupuliza tuu amefanikiwa kuweka utamaduni na muziki huo katika chati ya Muziki kitaifa na kimataifa.

Bonyeza Player upate Uhondo wa mwanamuziki Tony Nyadundo, Ukiangalia kwenye hii Video Utamuona Waziri Mkuu Raila Odinga, Prof Anyang Nyong, na wajaluo wengine ambao wapo kwenye nafsi za juu kichama(ODM) au kiserikali.

Serengeti Boys kufunzwa na Carlos Alberto Perreira Brazil


Pichani anaonekana Kocha Pereirra akiongea na Ronaldo

TIMU ya soka ya vijana walio chini ya umri wa miaka 17, Serengeti Boys, itaondoka nchini Juni 5 kuelekea Brazil , ambako itakuwa chini ya kocha aliyeiongoza Brazil kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1994, Carlos Alberto Perreira.

Mratibu wa mashindano ya Copa Coca-Cola, George Rwehimbiza alisema timu hiyo itafikia kwenye kituo cha michezo cha Brazil Football Academy, na itaondoka na viongozi wanne akiwemo kocha mkuu wa timu ya vijana, Marcus Tinocco.

“Timu itaondoka Juni 5 kuelekea Brazil itakaa huko kwa muda wa wiki moja,” alisema Rwehimbiza. “Timu itafikia kwenye kituo hicho kilicho chini ya Carlos Alberto Perreira.”

Perreira aliiongoza Afrika Kusini kwenye fainali za Mataifa ya Afrika mapema mwaka huu, lakini akajiondoa kwenye kazi hiyo hivi karibuni, akieleza kuwa mkewe alikuwa ni mgonjwa.

Vijana watakaokuwa kwenye safari hiyo watapatikana kutoka katika mashindano ya Copa Coca-Cola yanayoeelekea ukingoni jijini Dar es salaam baada ya kuendeshwa kwa takriban wiki mbili.

Mashindano hayo yanashirikisha timu za kombaini za mikoa yote ya Tanzania Bara na visiwani, zikiwemo wilaya za Ilaya, Kinondoni na Temeke zilizopewa hadhi ya mkoa.

Vijana wengi walioteuliwa kwa ubora katika mashindano ya kwanza yaliyofanyika jijini Dar es salaam kwa sasa wanasomeshwa na Shirikisho la Soka (TFF) kwenye shule ya sekondari ya Jitegemee, ambako huhudhuria vipindi vya masomo ya kawaida na yale ya soka.

Wakati huohuo, kocha Tinoco amesema kuwa hatapata kazi kubwa ya kuwanoa vijana 17 watakaopatikana katika michuano ya Copa Coca-Cola, anaripoti Sosthenes Nyoni.

Akizungumza baada ya mechi baina ya timu ya mkoa wa Kigoma na Kusini Pemba, Tinocco alisema kuwa hilo linatokana na wachezaji wengi kuonekana kuwa wamefundishika.

Alisema kuwa tofauti na mwaka jana mashindano ya mwaka huu yameonyesha baadhi walimu wa timu shiriki kuwa wana uwezo mkubwa wa kufundisha soka na ndio maana baadhi ya timu zinacheza soka lenye mpangilio.

Ally Kiba nakati ya Ujeruman

Ally Kiba akiwa na mashabiki wakisherehekea ushindi wa timu ya Ujerumani jana usiku

Ali Kiba akiwa na Wadau wa Ujeruman, wapili kushoto ni Bibie Nashe Mvungi mmoja wa waandazi wa Miss Tanzania EU.
Mwanamziki wa kizazi kipya Ali Kiba Amewasili Ujerumani 25.06.08 Tayari kabisa kwa show Miss Tanzania EU. Inayotegemewa kufanyika Jumamosi 28.06.08 mjini Essen Germany.
Ally ambaye aliwasili pamoja na promota wake Kassim wakitokea Oslo – Norway ambako waliwarusha mashabiki vilivyo.Pia imefahamika kwamba warembo washiriki wa Miss Tanzania EU wako kambini na tayari kabisa kwa mchujo wa round ya kwanza pre-selection utakaofanyika kesho ijumaa 27.06.08.

Ali kiba alipata nafasi ya kushangilia Mjini Essen na baadhi ya washabiki wa Ujerumani wa mpira wa miguu kwenye mtanange wa Ulaya kati ya Uturuki na Ujerumani ambapo Ujerumani Ilishinda 3-2.

Nani wa Kumfunga “Paka” Kengele Jumapili?

Germany 3 – 2 Turkey

Germany's Bastian Schweinsteiger and Miroslav Klose
Goli lililofungwa na Philip Lahm katika dakika ya 90 limewawezesha Ujerumani kufuzu kucheza Fainali za mtanange wa EURO 2008, na kuwafungisha virago waturuki katika mchezo uliochezwa usiku wa kuamkia leo huko St Jakob-Park in Basel.
Mpaka mapumziko timu zote mbili zilikuwa 1-1, huku Turkey wakiwa wakwanza kupata goli lililofungwa na Ugur Boral dakika ya 22 na dakika tano baadaye Ujerumani walisawazisha kupitia kwa Bastian Schweinsteiger.Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kushambuliana mashambulizi ya hapa na pale huku Ujerumani wakilisakama lango la Uturuki kama nyuki kwa mashambulizi ya kustukiza na dakika ya 79 wakapata goli Ujerumani lililofungwa na Miroslav Klose.
Huku mashabiki wa Ujerumani wakishangilia timu yao kuongoza kwa goli mbili walistukizwa na goli la kusawazisha toka kwa Semih Senturk dakika saba tuu baada ya goli lao, kiukweli mpira ulikuwa mtamu.
Timu zote zikawa zinahaha kupata walao cha “kuraria”, huku makocha viti vikiwa havikaliki na mashabiki wakiwahamasisha wachezaji wao kwa ushangiliaji non-stop, bahati haikuwa ua Waturuki na bahati hiyo ya Mtende iliwaangukia Wajerumani na kupachika bao dakika ya 90 ya mchezo kupitia kwa Philip Lahm . Mchezo wa jana ulikuwa na kufa mtu kwani kila timu ilikuwa inataka nafasi walao ya kucheza fainali kama sio kuchukua ubingwa.
Timu zote zilifanya mabadiliko ya hapa na pale walao kufufa hali ya mchezo kwa Wajerumani Torsten Frings aliingia badala ya Simon Rolfes dakika ya 46 na Marcell Jansen badala ya Miroslav Klose dakika ya 90.
Kwa upande wa waturuki walifanya mabadiliko mara tatu Mevlut Erding aliingia badala ya Ayhan Akman (81) na Gokdeniz Karadeniz alichukua nafasi ya Ugur Boral (84) na dakika ya 90 walimuingiza Tumer Metin na kutoka Colin Kazim-Richards.
Tanzania Dream naona kautabiri kako kanafikia kaka!!


Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri aja kivingine July

June 3, 2008

.

.

Solo thang akiwa na Mtoto wake Yassir nyumbani kwake, huko UK

Muziki ni safari, Kwa wanaokumbuka enzi hizo ukilitaja jina Solo Thang kila mtu mpenda Muziki anasisimuka, kwani ni mmoja wa wanamuziki wa Kizazi kipya ambao kwa kiasi kikubwa “walipigana vita ya msituni” kufanya muziki huu ukubalike kwa jamii. Kwa sasa Solo Thang AKA Traveller AKA Msafiri anaishi Uingereza akiwa ameoa na mtoto mmoja anayeitwa YASSIR na Mama yake anaitwa YASMIN.
Kwa muda sasa mwanamuziki Solo Thang amekuwa kimya kutaka kujua yuko wapi Spoti Starehe tumefanya mahojiano naye kutaka kujua machache toka kwake na maisha yake hasa ya kisanii kwenye sanaa nzima ya Muziki.

Spoti na Starehe (S na S): Mara ya mwisho nilisoma Interview yako Bongo5 ile Albamu uliyofanyia huku ughaibuni ilitoka kaka nataka mawili matatu kaka.

Solo: okee,bado ndo naiweka sawa kakakuna mambo mengi na shule ilinibana mkuu.

S na S: Jina ni bado lile lile la Albamu?

Solo: Yaa inaitwa TRAVELLER, ndio jina waliokuwa wananita enzi nasoma jitegemee….99

S na S: oooh poa sana, sasa unategemea kuimaliza lini, i mean itakuwa sokoni?

Solo: Kama nilivyo Kwambia kuna mambo namalizia ila Inshallah Hivi karibuni nitaanza na Single

Akiwa pamoja na Dj lee flex, na mdau baraka, DJ Lee ni mmoja wa Madj ambao wanaitangaza Bongo Flava Nje.

S na S: Vipi Maisha kwa ujumla nasikia ulikuwa unasoma, Je zaidi kumaliza Chuo cha Diplomasia pale Kurasini kuna chochote tena?

Solo : Shule kama kawa kaka haina mwisho,we learn new things daily ..nilishamaliza baadhi ya courses na nitaendelea na buku.kwa sasa napiga mzigo nakuiweka sawa family!


S na S: oooh safi sana mkuu kila la heri, Je unaionaje game kaka na ujio wa vijana wapya ukilinganisha na enzi zenu? nani mpya unamfeel sana?

Solo: Mmh well vijana wanatisha wanajitahidi ila FID Q yuko poa, CHIDI mwanangu yuko bomba

S na S: Je hufikirii kufanya kolabo na wanamuziki tofauti na wa nyumbani ili uende kimataifa zadi unalizungumziaje hili mkuu?

Solo: hicho ndio kilichonifanya niwe kimya kidogo,kunavitu vingi nilikuwa nafikiria jinsi kuviboresha ikiwa na kuliingilia soko la kimataifa babu, natarajia kutoa single mwezi july tarehe nitaitangaza baadae kaka

S na S: Single hiyo umemshirikisha nani babu? ni ya kiswahili au?

Solo: Nyimbo nitakazo toa kuanzia sasa zitakuwa na version mbili moja ya kiswahili na remix ambayo itakuwa ya kiingereza

S na S: Je mkubwa unazungumziaje wanamuziki wa Kenya ukilinganisha na wenzao wa Tanzania ambapo wengi wa Kenya wanapata shoo nyigi za nje, je hii ni kusema Genge inakubalika zaidi ya Bongo Flava kaka?

Solo hakuna babu,show ni connections na jinsi gani wasanii wanajiuza,inabidi wabongo tutumie sana mitandao katika kunadi kazi zetu…..kwa hiyo matumizi ya computer ni muhimu sana katika kujitangaza babu na nijukumu la wabongo walio nje ya nch kusupport vipaji vya home,kama Uk wapo baadhi ya maDj wakibongo wanajitahidi sana katika kuutangaza mziki wetu kuna jamaa wanajiita bongo flavour familly,Dj Jimmy blanks,kina Dj habib,Dj lee flex…..etc, ni jukumu la wabongo walio na michongo kumegeana babu

S na S: Kuna upande mwingine hata wewe uliupigia kelele sana kuhusu Wasambazaji kule nyumbani Bongo ambao bado ni hao hao kuna jinsi kweli ya kuepukana nao “wadosi” kama ipo kwa jinsi gani?

Solo: ipo dawa ni kuwa na umoja na kuwatosa,pia tunaweza kuuza kazi zetu kwa njia ya mtandao….kama itunes, beta record na store nyingine nyngi tu za muziki

S na S: Hapo utakuwa unalizungumzia soko la nje je kwa mikoani ambapo kazi zenu zinanunuliwa zaidi na jijini ambapo ndio kuna soko kubwa lakini ni rahisi kupata nyimbo za mwanamuziki kwa mtu ku burn CD tena toka kwa wanamuziki unasemaje kwa haya mawili?

Solo:ndo maana nikasema umoja muhimu!naamini wanamuziki sisi ndio waathirika wa hili,kama tutakuwa na msimamo kwa pamoja si kazi kupata suluhisho la hil, kama wadosi watakataa kubadilika ni kususia kuuza kazi zetu kwao naaamini watajitokeza tuwatu wa kununua kazi zetu,au tunaweza kuweka utaratibu wa kuuza wenyewe vyote inawezekana muhimu ni kujipanga….nakumbuka Mr Two alishawahi kukomaa na kusambaza mwenyewe na Kilimanjaro band kama sikusei

its all possible..pia wabongo waelimishwe umuhimu wa kununua nakala halisi na si zakukopy,ili kusupport vipaji vya nyumbani,la sivyo itabaki majina tu yanavuma mifuko imetoboka

.

.

“Traveller” Mitaani ughaibuni.

S na S: Je umewahi kuwaza kuwa na Chama chenu ili muwe na sauti moja? unafikiri hili linawezekana?

Solo: unajua tatizo njaa babu kwenye njaa hakuna msimamo…..vyama huwa vinaanzisha ila havidumu na huwa havina nguvu…..sababu mnaweza kupanga hili,baadhi wakazunguka! sauti moja ndo inatakiwa ya wasanii nchi nzima. Tukae chini na wadosi watueleze tatizo nini?kazi zinavuka mpaka mipaka hakuna mjadala wa hilo!, pia nimeanzisha blog yangu ili kuwapa latest mashabiki zangu pamoja na habari zingine za burudani ndani na nje ya bongo www.solothang.blogspot.com.

S na S: Elimu na usanii haviingiliani ila vinategemeana pia je kuna mabadiliko yeyote unayahisi kwa kipindi kile na sasa baada ya vidato kadhaa kimuziki?

Solo: makubwa kaka,am grown up now ha ha with wife and son,kuishi ngambo pia kunakupa experience kubwa kila ninachokiwaza na kwa faida yangu na family, which means siwazi kunyonywa tena.
S na S: Hongera sana kwa hilo!! Kila mtu anafikiria kuwekeza kwenye Studio na kwa sasa kila kona kuna Studio Dar hadi limekaa njema hili mkuu?
Solo: Studio kila kona poa muhimu kama zitakuwa na viwango tu babu,pia inaleta ushindani na ni mzuri kibiashara.

.

.

“when it comes to Mic,Rhyme!! man am baaad..”

S na S: Je una lolote la kuwaeleza MAshabiki, Wanamuziki wenzio, au hata wadau wa Muziki hata “wadosi”?

Solo; Mashabiki kwanza nawaomba msamaha kwa ukimya,pili wakae mkao wa kula soon tunaanzia July kwa washkaji ni muhimu kuwa na plan B,wasitegemee tu mziki kama kitega uchumi,wa Invest pesa wanayoipata ili kuwa na nyenzo nyingine ya kuingiza kipato,maisha mchakamchaka, fani yetu haina pension,so we need to work hard for the future,na nawatakia kila la kheri

S na S: Asante kaka kwa muda wako kila la heri kwenye shughuli zako

Solo: Asante sana kaka nawe pia.

Pata burudani ya Solo thang na Q Chilla kwa kubofya hapa